Alonso, Miaka 32, amekuwa mmoja wa kiini cha mafaniko ya Spain iliyotwaa EURO 2008 na EURO 2012 pamoja na Kombe la Dunia huko Afrika Kusini Mwaka 2010.
Juzi Alonso aliichezea Spain Mechi yake ya 112 ilipofungwa 2-0 na Chile kwenye Mechi Kundi B na kutupwa nje ya Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil.
Kwenye Mechi hiyo, Alonso alibadilishwa wakati wa Mapumziko baada kupwaya na kupokonywa Mpira uliozaa Bao la Kwanza la Chile.
Lakini Alonso ndie Mchezaji pekee aliewafungia Spain Bao pekee kwenye Mashindano haya huko Brazil alipofunga kwa Penati kwenye Mechi ya Kwanza ya Kundi B waliponyukwa Bao 5-1 na Netherlands.
Mara baada ya Spain kutupwa nje ya Fainali ya Kombe la Dunia, Alonso alisema: “Vitu vinabadilika. Zama zinaisha kwa kufungwa…na hiki kilikuwa kipigo kichungu. Hatukutegemea lakini ndio mchezo. Hivi vitu vinatokea. Hatukutegemea lakini ni lazima tuyakabili majonzi yetu vile vile kama tunavyofurahia, kama Wanaume.”
Aliongeza: “Tumecheza dhidi ya Timu zilizojitayarisha vyema na sasa tunarudi nyumbani. Inauma lakini huu ndio mpira. Kama nilivyosema, tulijua namna ya kushinda, sasa inabidi tujue namna ya kushindwa!”
Mbali ya Alonso kutangaza kustaafu pia kuna wasiwasi kuwa Kiungo Xavi na Kipa Iker Casillas, ambao wote wamecheza ovyo huko Brazil, wanaweza kufuata nyayo zake.
Zipo habari kuwa Kocha wa Spain, Vicente del Bosque, hasa kwa vile Shirikisho la Soccer la Spain, RFEF, linaunga mkono aendelee na kazi yake.
KUHUSU REKODI YA XABI ALONSO
BORN: Tolosa, Spain, November 25, 1981
1999-2000: Real Sociedad B (39 apps, 2 gls)
1999-2004: Real Sociedad (114 apps, 9 gls)
2000-2001: Eibar (loan) (14 apps, 0 gls)
2004-2009: Liverpool (143 apps, 15 gls)
2009-NOW: Real Madrid (158 apps, 4 gls)
2003-NOW: Spain (112 caps, 16 gls)
CLUB HONOURS:
LIVERPOOL - FA Cup (2006), FA Community Shield (2006), Champions League (2005), UEFA Super Cup (2005)
REAL MADRID - La Liga (2012), Copa del Rey (2011, 2014), Supercopa de Espana (2012), Champions League (2014)
SPAIN - World Cup (2010), European Championship (2008, 2012)
RSS Feed
Twitter
2:59 AM
Unknown
Warembo
wanaowania taji la mkoa wa Tanga, Nice & Lovely Miss Tanga 2014
wakijiaandaa kufanya usafi katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga, ikiwa
ni moja ya kampeni ya kuendelea kulifanya jiji hilo liwe safi muda wote.
Washiriki
wa Nice & Lovely Miss Tanga 2014 wakitupa takataka katika gari
maalum la kubeba taka. Mshindi wa kwanza katika shindano hilo atapata
zawadi ya gari dogo aina ya Toyota Vitz.
Zoezi
la usafi limepamba moto na kuliacha eneo hilo safi kabisa. Mgeni rasmi
katika shindano hilo atakuwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mheshimiwa Chiki
Gallawa. 


Rais Kenyatta akiongea na Wachezaji wa Timu hiyo.
Hapa Akigawa tiketi huku akishuhudiwa na mkewe Bi. Margaret Kenyatta na seneta wa Nairobi Mike Sonko (kushoto).
Picha ya Pamoja.