JUMATANO
Klabu za Liverpool na Barcelona zilifanya mazungumzo kuhusu Uhamisho wa
Luis Suarez ambae kwa sasa yuko kwenye Kifungo cha Miezi Minne
alichopewa na FIFA kwa kumuuma Meno Beki wa Italy Giorgio Chiellini
wakati wa Mechi ya Kombe la Dunia kati ya Uruguay na Italy huko Brazil. Mtendaji Mkuu wa Liverpool, Ian Ayre, alikutana na Maafisa kutoka Barcelona na mazungumzo zaidi yamepangwa....