Thursday, August 13, 2015

LIGI KUU ENGLAND RATIBA: Ijumaa Agosti 14 21:45 Aston Villa vs Man United Jumamosi Agosti 15 14:45 Southampton vs Everton 17:00 Sunderland vs Norwich 17:00 Swansea vs Newcastle 17:00 Tottenham vs Stoke 17:00 Watford vs West Brom 17:00 West Ham vs Leicester Jumapili Agosti 16 15:30 Crystal Palace vs Arsenal ...
MENEJA wa Arsenal Arsene Wenger amesema Jack Wilshere atarejea Uwanjani baada ya Wiki 2 baada ya kujiuguza Enka yake lakini Kiungo wao mwingine Tomas Rosicky atakuwa nje kwa Miezi Miwili baada ya kupasuliwa Goti lake. Wilshere, mwenye Umri wa Miaka 23, aliumia Enka ambayo ilipata ufa kwenye mfupa wake Mazoezini hapo Agosti 1 na ilidhaniwa atakuwa nje kwa kipindi cha hadi Miezi Miwili....
FIFA Leo imetoa tamko la kumzodoa Meneja wa Chelsea Jose Mourinho baada kumtupa nje kusimamia Timu ya Kwanza Dokta wao Mwanama Eva Carneiro kwa kuingia Uwanjani kumtibu Mchezaji alieumia. Profesa Jiri Dvorak, Daktari Mkuu wa FIFA, ametamka kuwa Mameneja hawana haki yeyote kuwaambia Matabibu wao waingie Uwanjani au la kumtibu Mchezaji alieumia kwani jukumu hilo ni la Dokta aliepo Uwanjani....
Rais wa Simba Sport Club Evans Aveva wa tatu kutoka kushoto akiwa na Washindi wa bahati nasibu Pamoja na Afisa Mtendaji Mkuu wa Eaggroup ImanKajula kushoto na Msemaji wa Timu hiyo Manara Rais wa Simba Evans Aveva Akikabidhi Zawadi kwa Mmoja wa Washindi. Uongozi wa klabu ya Simba leo umetoa zawadi kwa washindi wa bahati na sibu iliyochezeshwa siku ya Simba Day Aosti 8 mwaka huu wakati...
David De Gea hatarudi kwenye Kikosi cha Manchester United dhidi ya Aston Villa hapo Ijumaa huko Villa Park kwa mujibu wa Meneja Louis Van Gaal. Kipa wa Kimataifa wa Argentina Sergio Romero ataendelea kuwa Golini kama alivyofanya Jumamosi iliyopita huko Old Trafford Man United ilipoifunga Tottenham 1-0 katika Mechi yao ya kwanza ya Ligi Kuu England kwa Msimu mpya wa 2015/16. Hivi sasa...
Kukiwa na kila dalili kuwa Fowadi wa Barcelona Pedro yuko njiani kwenda Manchester United, Kocha wa Mabingwa hao wa Spain Luis Enrique amesisitiza ni juu ya Mchezaji huyo mwenyewe kuamua nini hatima yake. Pedro, mwenye Miaka 28, aliijulisha rasmi Barcelona Juzi Jumanne nia yake kuhama ikiwa ni Masaa kadha kabla hajaifungia Klabu hiyo Bao la ushindi walipotwaa UEFA Super Cup kwa kuibwaga...
Kwa sababu za kiusalama Gemu ya Ligi Kuu England kati ya Aston Villa na Manchester United imewekwa Ijumaa Usiku kutokana na Mji wa Birmingham kuwa na Maandamano badala ya kuchezwa Wikiendi. Mechi hii, ambayo itachezwa Villa Park, inazikutanisha Timu ambazo zilishinda Mechi zao za kwanza za Msimu mpya Wikiendi iliyopita kwa zote kushinda kwa Bao 1-0. Man United walishinda kwao Old Trafford...
...
Mshambuliaji wa klabu ya Manchester City Edin Dzeko amejiunga na kilabu ya ligi ya Seria A Roma kwa mkopo.Kilabu hiyo imetoa kitita cha pauni milioni 2.9, na nyengine pauni 7.9 zikitarajiwa kulipwa iwapo uhamisho huo utabadilika na kuwa wa kudumu.''Nimekuja hapa kushinda mataji'',alisema Dzeko.''Ninaweza kuahidi kitu kimoja kwamba nitajitahidi vilivyo katika kilabu hii''.Mchezaji huyo mwenye...
Kutoka makao makuu ya shirikisho la soka ulimwenguni FIFA, Rais wa FIFA Sepp Blatter ametoa ushauri kwa nia njema kwa nchi za Ulaya Magharibi kuiga na kujifunza kitu kutoka katika nchi ya Urusi ambayo sheria ya soka ya nchi hiyo ina ruhusu idadi maalumu ya wachezaji wa kigeni kucheza katika mechi moja. Kupitia katika Magazine ya FIFA Blatter alishauri kujali vipaji...

waliotembelea blog