Saturday, June 13, 2015
6:16 AM
Unknown
1:28 AM
Unknown

Winga Memphis Depay amekamilisha Uhamishi wake wa Pauni Milioni 31 kujiunga na Manchester United kutoka PSV Eindhoven ya Holland.
Depay, mwenye Miaka 21, amesaini Mkataba wa Miaka Minne ukiwa na nyongeza ya Mwaka Mmoja.
Wakiongea baada ya kusaini Mkataba, Depay alisema hii ni ndoto yake iliyotimia wakati Meneja wa Man United, Louis van Gaal, alisema Mchezaji huyo ana nafasi kubwa kuwa mmoja wa Wachezaji bora kwenye Klabu hiyo.
Mwezi uliopita, Depay alifuzu upimwaji afya yake na kusubiri kusainiwa Mkataba.
Katika Msimu ulioisha Mwezi Mei, Depay ndie aliibuka akiwa Mfungaji Bora wa Ligi Kuu ya Holland, Eredivisie, alipofunga bao 22 na kuibeba PSV Eindhoven kubeba Ubingwa wao wa kwanza wa Holland tangu 2008.
1:25 AM
Unknown
Mayweather ameingiza kiasi cha dola milioni 300 katika kipindi cha miezi hiyo na fedha nyingi ikiwa imepatikana kutoka na pambano lake na bondia Manny Pacquiao.
Manny ameshika nafasi ya pili katika orodha hiyo huku nyota wa kandanda Cristiano Ronaldo akiwa katika nafasi ya tatu kwa wanamichezo waliotengeneza pesa nyingi.
Orodha kamili ipitie katika tovuti ya bbcswahili.com
1. Floyd Mayweather, US, US$300m (£194m).
2. Manny Pacquiao, Philippines, $160m (£103.4m)
3. Cristiano Ronaldo, Portugal, $79.6m (£51.4m)
4. Lionel Messi, Argentina, $73.8m (£47.7m)
5. Roger Federer, Switzerland, $67m (£43.3m)
6. LeBron James, US, $64.8m (£41.9m)
7. Kevin Durant, US, $54.1m (£35m)
8. Phil Mickelson, US$50.8m (£32.8m)
9. Tiger Woods, US, $50.6m (£32.7m)
10. Kobe Bryant, US, = $49.5m (£32m)
Subscribe to:
Comments (Atom)
RSS Feed
Twitter







