Friday, June 26, 2015

KOCHA mpya wa Simba, Muingereza Dylan Kerr amesema ataendeleza wachezaji chipukizi ili kuwa na timu bora kwa sasa na baadae.Kerr aliyasema hayo baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere na kulakiwa na wajumbe wa Kamati ya Simba, Collin Frisch na Said Tully.“Nimefurahi kuja Tanzania na nawaahidi viongozi na mashabiki kuwa nitahakikisha naendeleza wachezaji...
Morgan Schneiderlin Manchester United wanajiandaa kutoa kitita cha £24million kumnasa Mchezaji wa Southampton Morgan Schneiderlin. Mchezaji huyo alikuwa akiwaniwa na Arsenal na Tottenham lakini vyanzo vinaonesha Man United Pekee ndio yenye nafasi nzuri kumnunua mchezaji huyo na taratibu zitakamilia wiki ijayo...
Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) leo limefungua kozi ya makocha wa mpira wa miguu kwa watoto na vijana kwa nchi nzima kwa lengo la kuhakikisha vijana wengi wanapata nafasi ya kufundishwa mpira na kuucheza mpira kuanzia katika umri mdogo. Akifungua kozi hiyo, Katibu Mkuu wa TFF Mwesigwa Selestine amesema ili nchi/Taifa lifanikiwe katika soka ni lazima kuwekeza katika mpira wa...
West Ham leo Ijumaa wamemsajili Payet kwa kitita cha £10.7m na hapa akiwa anapimwa AfyaAkisaini mkataba wa miaka 5 leo hii IjumaaWest Ham tayari wanae Winga ambaye walikuwa wanamfukuzia siku nyingi Dimitri Payet kutoka Klabu ya Marseille ya Ufaran...
Manchester United imeionya Real Madrid kwamba wanapaswa kulipa zaidi ya ile Ada ya Uhamisho inayoshika Rekodi ya Dunia kwa Kipa ikiwa wanamtaka Kipa wao David De Gea. Habari zimedai ili kumng'oa Kipa huyo kutoka Spain huko Man United lazima Wanunuzi wavunje Rekodi ya ununuzi wa Kipa wa Italy Gianluigi Buffon iliyowekwa 2001 kwa kulipwa Pauni Milioni 32.6 aliponunuliwa kutoka Parma na...
  Saa zisizopungua 48 baada ya klabu ya Manchester United kuripotiwa kutuma ofa ya kumsajili beki wa kimataifa wa Spain, Sergio Ramos, klabu yake ya Real Madrid imepokea ofa hiyo na imetoa uamuzi.   Manchester United, juzi walituma ofa ya £35million kwa ajili ya kupata saini ya Ramos na klabu ya Madrid wameipiga chini ofa hiyo. Madrid walimpa...

waliotembelea blog