Saturday, October 31, 2015


LIGI KUU ENGLAND
RATIBA:
Jumamosi Oktoba 31

15:45 Chelsea v Liverpool
18:00 Crystal Palace v Man United
18:00 Man City v Norwich
18:00 Newcastle v Stoke
18:00 Swansea v Arsenal
18:00 Watford v West Ham
18:00 West Brom v Leicester

Jumapili Novemba 1
16:30 Everton v Sunderland
19:00 Southampton v Bournemouth

Jumatatu Novemba 2

23:00 Tottenham v Aston Villa


Theo Walcott na Alex Oxlade-Chamberlain watazikosa Mechi kadhaa za Arsenal kama ilivyothibitishwa na Meneja wa Klabu hiyo Arsene Wenger.
Wachezaji hao Wawili waliumia Jumanne iliyopita kwenye Mechi ya Raundi ya 4 ya Capital One waliyofungwa 3-0 na Sheffield Wednesday.
Oxlade-Chamberlain aliumia Dakika ya 5 tu ya Mechi hiyo alipopata tatizo la Musuli za Pajani na kubadilishwa na Walcott ambae nae ilibidi atolewe Dakika ya 19 baada kuumia Musuli za Mguuni.
Ingawa bado haijathibitika watakuwa nje kwa muda gani, Wenger amethibitisha Wawili hao kuikosa Mechi ya Ligi Kuu England ya Jumamosi Ugenini na Swansea City na pia ile ya Kundi lao la UEFA CHAMPIONS LIGI huko Munich watakaporudiana na Bayern Munich.

Mechi nyingine ambayo Wachezaji hao wataikosa ni ile Dabi ya London ya Kaskazini na Mahasimu Tottenham.



Chelsea wana kibarua tena wikendi hii watakapowakaribisha nyumbani Liverpool kwenye Ligi ya Premia Jumamosi.
Vijana wa Jose Mourinho wamekuwa wakiandikisha matokeo mabaya msimu huu, meneja huyo anakabilisha na shinikizo la kubadili mambo.
Chelsea wameshinda mechi moja pekee kati ya sita walizocheza karibuni zaidi katika mashindano yote.

The Blues wamefungwa mabao 19 Ligi ya Premia na ni Norwich (21), Bournemouth na Newcastle (wote wakiwa na 22) ambao wamefungwa mabao mengi zaidi msimu huu.
Ingawa huenda mshambuliaji wao Diego Costa akacheza, bado kuna shaka kumhusu Pedro ambaye anafuatiliwa kwa karibu baada yake kurejelea mazoezi.
Hata hivyo watakuwa bila Branislav Ivanovic na Thibaut Courtois. Nemanja Matic, aliyepigwa marufuku mechi moja atarejea uwanjani baada ya kutimikia marufuku hiyo mechi dhidi ya Stoke katika League Cup.
Upande wa Liverpool, meneja wao mpya Jurgen Klopp ataweza kumtumia Christian Benteke lakini Daniel Sturridge bado anauguza jeraha, Kolo Toure vilevile.
Akizungumza na wanahabari leo Mourinho amesema: “Matokeo sasa yamekuwa kila kitu (hasa kwenu wanahabari). Ni jambo la kushangaza kwamba miezi michache iliyopita nilishinda mechi nyingi na nikawa bingwa wa Uingereza, watu walikuwa wakisema kuna mambo muhimu zaidi kushinda matokeo.”
Kwa upande wake, Klopp amesema Chelsea bado ni hatari.
“Sina uhakika kwamba ni rahisi kucheza dhidi ya Chelsea leo kuliko mwaka jana. Mbona iwe hivyo?”

Liverpool walishinda mechi tatu mfululizo Stamford Bridge mwaka 2011 lakini hawajashinda hata mechi moja tangu wakati huo.

11218903_963430877028605_2270729444866256425_n
Wafanyakazi wa kampuni ya Screen Masters Limited ya jijini Dar wakiendelea kulipamba basi la Mbeya City. 
12079536_963430803695279_6917505578594463550_n
Basi la klabu ya Mbeya City FC baada ya kupambwa na kampuni ya Screen Masters Limited ya Dar es Salaam tayari kuanza shughuli ya kusafirisha wachezaji wa timu hiyo kwa safari za ndani na nje ya Mbeya kwenye mechi mbalimbali za Ligi Kuu Bara.

12196214_1667951416755226_8732075203516045367_n

Hatua kubwa sana hongera kwa uongozi wa timu,baada ya basi nini kinafuata usichoke kuwa nasubira kikubwa tuendelee kuisapoti timu yetu.
Posted by Mbeya City Fans on Thursday, October 29, 2015



Kocha wa klabu ya Manchester United Louis van Gaal ambaye wengi wamekuwa wakihoji juu ya mahusiano yake na wachezaji wa timu yake pamoja na aina ya mbinu anazotumia kuifundisha timu hiyo, October 30 amejibu kauli za kiungo wa zamani wa timu hiyo Paul Scholes ambaye October 29 aliponda mbinu za kocha huyo.
October 30 Louis van Gaal amejibu juu ya kauli ya Scholes ambaye alilenga kukosoa mfumo wa kocha huyo, Scholes alisema kwa sasa mfumo wa Man United sio mzuri na asingeweza kufurahia kucheza kikosi hicho akiwa chini ya Van Gaal. October 30 Louis van Gaal amemjibu Scholes ambaye ni mchezaji wa zamani wa Man United mwenye heshima klabuni hapo.
2DA584D700000578-3296538-Former_Manchester_United_midfielder_Paul_Scholes_has_criticised_-a-1_1446205312799
Paul Scholes
“Hana mamlaka yoyote hivyo anaweza kusema kila kitu kwa ajili ya faida yake au klabu, sitaki kujitetea kwa sababu siwezi kujitetea, nafikiria Scholes kama nguli wa klabu alipaswa kuongea na kocha au rafiki yake Ryan Giggs au Ed Woodward lakini sio kwa njia aliyoichagua kwa sababu atakuwa akilipwa na BBC au SKY, siku zote huwa na kauli ya kidachi fimbo na mawe ndio inaweza kuvunja mifupa lakini sio maneno”>>> Louis van Gaal
Tukiwa bado katika muendelezo au mfululizo wa mechi mbalimbali za soka, naomba nikusogezee ratiba ya mechi za Ligi Kuu Tanzania bara, Uingereza na Hispania zitakazochezwa weekend hii, Ligi Kuu Tanzania bara October 31 na November 1 kutakuwa na jumla ya mechi nane, baada ya hapo Ligi Kuu Tanzania bara itasimama hadi December 12 hii inatokana na kupisha maandalizi ya mechi ya Algeria na michuano ya Kombe la Chalenji. Hii ni ratiba ya mechi za Ligi Kuu Tanzania, Uingereza na Hispania kwa mechi za October 31 na November 1.
vpl
Ratiba ya mechi za Ligi Kuu Tanzania bara weekend hii zitachezwa saa 16:00
epl
Ratiba ya Ligi Kuu Uingereza kwa saa za Afrika Mashariki October 31
  • Chelsea Vs Liverpool  Saa 15:45
  • Crystal Palace Vs Man Utd  Saa 18:00
  • Man City Vs Norwich Saa 18:00
  • Newcastle Vs Stoke Saa 18:00
  • Swansea Vs Arsenal Saa 18:00
  • Watford Vs West Ham Saa 18:00
  • West Brom Vs Leicester Saa 18:00
Jumapili ya November 1
  • Everton Vs Sunderland Saa 16:30
  • Southampton Vs Bournemouth Saa 19:00
Laliga
Ratiba ya Ligi Kuu Hispania kwa saa za Afrika Mashariki Jumamosi ya October 31
  • Real Madrid Vs Las Palmas Saa 18:00
  • Valencia Vs Levante Saa 20:15
  • Villarreal Vs Sevilla Saa 20:15
  • Getafe Vs Barcelona Saa 22:30
  • Real Sociedad Vs Celta de Vigo  Saa 00:05
Jumapili ya November 1
  • Eibar Vs Rayo Vallecano Saa 14:00
  • Espanyol Vs Granada CF Saa 18:00
  • Sporting de Gijón Vs Málaga Saa 20:15
  • Real Betis Vs Ath Bilbao Saa 22:30

Wakiingia katika basi tayari kwa msafara
Watumiaji mbalimbali wa vyombo vya muziki wa msanii Wizkid wakiwasili katika Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere tayari kwa shoo yao ya leo katika Viwanja vya Leaders.
Huyo mwenye fulana nyeusi anaitwa  Snipes ndio kiongozi wa bendi ya msanii Wizkid.

waliotembelea blog