Wachezaji hao Wawili waliumia Jumanne iliyopita kwenye Mechi ya Raundi ya 4 ya Capital One waliyofungwa 3-0 na Sheffield Wednesday.
Oxlade-Chamberlain aliumia Dakika ya 5 tu ya Mechi hiyo alipopata tatizo la Musuli za Pajani na kubadilishwa na Walcott ambae nae ilibidi atolewe Dakika ya 19 baada kuumia Musuli za Mguuni.
Ingawa bado haijathibitika watakuwa nje kwa muda gani, Wenger amethibitisha Wawili hao kuikosa Mechi ya Ligi Kuu England ya Jumamosi Ugenini na Swansea City na pia ile ya Kundi lao la UEFA CHAMPIONS LIGI huko Munich watakaporudiana na Bayern Munich.
0 maoni:
Post a Comment