Usiku wa February 5 ndio siku ambayo mchezo wa fainali ya mataifa ya Afrika maarufu kama
AFCON 2017 ulichezwa, mchezo wa fainali ya
AFCON 2017 ulikuwa unazikutanisha timu za
Misri dhidi ya
Cameroon, lakini
Cameroon wamefanikiwa kufuta uteja kwa kufungwa fainali mbili na
Misri.
Cameroon wamefanikiwa kupata ushindi wa goli 2-1,
Nicolas N’koulou alifunga goli la kusawazishia
Cameroon dakika ya 58 baada ya
Mohamed Elneny kuifungia
Misri goli la uongozi dakika ya 22,
Vincent Aboubakar ndio alizima ndoto za
Misri baada ya dakika ya 88 kufunga goli la ushindi.

Ushindi huo unakuja baada ya
Cameroon kufumgwa fainali mbili za
AFCON na
Misri, alifungwa fainali ya AFCON 2008 goli 1-0
Mohamed Aboutrika akifunga goli hilo, lakini walipoteza fainali ya AFCON 1986,
Cameroon wanakuwa wamechukua taji lao la tano la
AFCON wakati
Misri wanabakia na rekodi yao ya kuchukua mataji nane ya
AFCON.

Rekodi nyingine zilizowekwa katika
AFCON na
Cameroon ni kuwa inakuwa timu ya kwanza kuwahi kuifunga
Misri goli katika fainali za
AFCON baada ya
Ethiopia, huku kocha wa
Misri Hector Raul Cuper akiendeleza rekodi yake mbovu kwa kupoteza fainali yake ya sita katika soka akiwa kama kocha wa timu tofauti.