Wednesday, February 15, 2017


Jana huko Parc des Princes Jijini Paris Nchini France Mabingwa wa huko Paris St Germain waliifumua Barcelona 4-0 katika Mechi ya Kwanza ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UCL, UEFA CHAMPIONS LIGI.
Kwenye Mechi nyingine ya Raundi hiyo Benfica iliichapa Borussian Dortmund 1-0.
Katika Mechi ya PSG na Barca, Bao za PSG zilipigwa na Angel Di Maria, Dakika za 18 na 55, Julian Draxler, 40', na Edinson Cavani, 71'.
PSG walitawala Mechi hii na Barca kupooza mno huku Mastaa wao Lionel Messi, Luis Suarez na Neymar 'wakijificha'.
Kipigo hiki kinaiweka Barca pagumu kufuzu kwenda Robo Fainali na wakishindwa hilo hii itakuwa mara ya kwanza kwao kutotinga Robo Fainali katika Miaka 10.


Jana huko Parc des Princes Jijini Paris Nchini France Mabingwa wa huko Paris St Germain waliifumua Barcelona 4-0 katika Mechi ya Kwanza ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UCL, UEFA CHAMPIONS LIGI.
Kwenye Mechi nyingine ya Raundi hiyo Benfica iliichapa Borussian Dortmund 1-0.
Katika Mechi ya PSG na Barca, Bao za PSG zilipigwa na Angel Di Maria, Dakika za 18 na 55, Julian Draxler, 40', na Edinson Cavani, 71'.
PSG walitawala Mechi hii na Barca kupooza mno huku Mastaa wao Lionel Messi, Luis Suarez na Neymar 'wakijificha'.
Kipigo hiki kinaiweka Barca pagumu kufuzu kwenda Robo Fainali na wakishindwa hilo hii itakuwa mara ya kwanza kwao kutotinga Robo Fainali katika Miaka 10.

Monday, February 13, 2017


UEFA CHAMPIONS LIGI
Raundi ya Mtoano ya Timu 16 

Mechi zote kuanza Saa 4 Dakika 45 Usiku
Mechi za Kwanza
Jumanne 14 Februari 2017

Benfica v Borussia Dortmund
Paris Saint Germain v Barcelona

Jumatano 15 Februari 2017
Bayern Munich v Arsenal
Real Madrid v Napoli

Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UEFA CHAMPIONS LIGI, UCL, inaanza Jumanne Usiku kwa Mechi mbili na Jumatano pia zipo Mechi mbili na kuendelea Wiki ijayo, zote zikiwa ni Mechi za Kwanza za Raundi hiyo.
Jumanne ni huko Portugal wakati Benfica wakiikaribisha BVB Borussia Dortmund na nyingine ni huko Jijini Paris, Paris pale Paris Saint Germain wakicheza na Barcelona.
Jumatano pia zipo Mechi 2 za Raundi hii ambapo huko Germany ni Bayern Munich na Arsenal na nyingine ni kule Santiago Bernabeu Jijini Madrid Nchini Spain kati ya Real Madrid na Napoli ya Italy.

Mechi za Kwanza za Raundi ya Mtoano ya Timu 16 za UCL zitakamilika Wiki ijayo, Jumanne na Jumatano kwa Mechi 4.

Dondoo Muhimu:
Benfica v Borussia Dortmund

Mechi hii itachezwa huko Estádio do Sport Lisboa e Benfica, Lisbon na kuchezeshwa na Refa mzoefu kutoka Italy Nicola Rizzoli.
Timu hizi zimekutana mara 2 Ulaya na kila moja kushinda mara moja.
Benfica watatinga kwenye Mechi hii wakiwakosa Andrija Zivkovic, alie Kifungoni, na Majeruhi Lisandro Lopez huku Jonas akiwa kwenye hatihati kucheza kutokana na maumivu.
Nao BVB watawakosa Majeruhi Mario Götze na Sven Bender huku hatihati ikiwa kwenye maumivu Nuri Şahin na Sebastian Rode.

Paris Saint Germain v Barcelona
Mechi hii ipo ndani ya Parc des Princes Jijini Paris Nchini France na itachezeshwa na Refa Szymon Marciniak kutoka Poland.

Katika Mechi zilizopita, PSG ilishinda mara 2, Sare 3 na Barca kushinda 4 kati yao.

PSG kwenye Mechi hii itamkosa Thiago Motta ambaye yupo Kifungoni wakati Barca watawakosa Majeruhi Arda Turan, Javier Mascherano na Aleix Vidal.

UEFA CHAMPIONS LIGI
Raundi ya Mtoano ya Timu 16

Mechi zote kuanza Saa 4 Dakika 45 Usiku 
Mechi za Kwanza
Jumanne 21 Februari 2017

Bayer 04 Leverkusen v Atlético Madrid
Manchester City v Monaco

Jumatano 22 Februari 2017
FC Porto v Juventus
Sevilla v Leicester City
 

Mechi za Pili
Jumanne 7 Machi 2017

Arsenal v Bayern Munich
Napoli v Real Madrid

Jumatano 8 Machi 2017

Barcelona v Paris Saint Germain
Borussia Dortmund v Benfica


Jumanne 14 Machi 2017
Juventus v FC Porto
Leicester City v Sevilla

Jumatano 15 Machi 2017
Atlético Madrid v Bayer 04 Leverkusen
Monaco v Manchester City


Antonio Conte amesema hapendi 'mzaha'wa Jose Mourinho baada ya Meneja huyo wa Manchester United kudai Chelsea ambao ni Vinara wa EPL, Ligi Kuu England, hawawezi kukamatika kileleni kwa sababu ni Timu 'inayojihami mno!'.
Hivi sasa Chelsea wapo Pointi 10 mbele ya Timu ya Pili Tottenham baada Jana kutoka 1-1 na Burnley huko Turf Moor.
Mourinho, ambae anasifika kwa kuchota akili za Mameneja wapinzani na kuwavuruga, Juzi alidai Chelsea haiwezi kuteleza kutoka kileleni kwa vile 'wanajihami mno' na kushinda kwa kutumia 'kaunta ataki'.
Jana Meneja wa Chelsea Antonio Conte alijibu mapigo kwa kusema: "Hiyo ni hadaa yake. Nina uzoefu kuelewa hilo!"
Mara nyingi Mourinho amekuwa akikwaruzana na Mameneja wenzake kutokana na vijembe vyake vya kuwapandisha munkari ili kushinda vita ya kisaikolojia na muhanga mkuu wa mashambulizi hayo huko nyuma akiwa Arsene Wenger wa Arsenal.

Hata hivyo Conte amegoma kuburutwa kwenye vita hiyo na kujibu: "Sipendi kujibu kuhusu Makocha wengine!" 

EPL – Ligi Kuu England
RATIBA:
Jumatatu Februari 13

2300 Bournemouth v Manchester City
Jumamosi Februari 25
1800 Chelsea v Swansea City
1800 Crystal Palace v Middlesbrough
1800 Everton v Sunderland
1800 Hull City v Burnley
Southampton v Arsenal [IMEAHIRISHWA]
1800 West Bromwich Albion v Bournemouth
2030 Watford v West Ham United
Jumapili Februari 26
1630 Tottenham Hotspur v Stoke City
Manchester City v Manchester United[IMEAHIRISHWA]
Jumatatu Februari 27
2300 Leicester City v Liverpool
Jumamosi Machi 4
1530 Manchester United v Bournemouth
1800 Leicester City v Hull City
1800 Stoke City v Middlesbrough
1800 Swansea City v Burnley
1800 Watford v Southampton
1800 West Bromwich Albion v Crystal Palace
2030 Liverpool v Arsenal
Jumapili Machi 5
1630 Tottenham Hotspur v Everton
1900 Sunderland v Manchester City
Jumatatu Machi 6
2300 West Ham United v Chelsea


Chelsea Leo wameikosa nafasi ya kwenda Pointi 12 mbele baada ya kutoka Sare na Burnley huko Turf Moor.
Chelsea sasa wako Pointi 10 mbele ya Timu ya Pili Tottenham lakini Jumatatu Usiku Manchester City wanaweza kutwaa Nafasi ya Pili na pengo lao na Chelsea kuwa Pointi 8 ikiwa wataifunga Bournemouth Ugenini.

Hii Leo Chelsea walitangulia kufunga Dakika ya 7 kwa Bao la Pedro lakini Robbie Brady akaisawazishia Burnley Dakika ya 24 kwa Frikiki kali.

Matokeo haya yanawaweka Burnley Nafasi ya 12 na kudumisha rekodi yao ya kuwa wagumu mno wakiwa kwao Turf Moor.

Sunday, February 5, 2017



Usiku wa February 5 ndio siku ambayo mchezo wa fainali ya mataifa ya Afrika maarufu kama AFCON 2017 ulichezwa,  mchezo wa fainali ya AFCON 2017 ulikuwa unazikutanisha timu za Misri dhidi ya Cameroon, lakini Cameroon wamefanikiwa kufuta uteja kwa kufungwa fainali mbili na Misri.

Cameroon wamefanikiwa kupata ushindi wa goli 2-1, Nicolas N’koulou alifunga goli la kusawazishia Cameroon dakika ya 58 baada ya Mohamed Elneny kuifungia Misri goli la uongozi dakika ya 22, Vincent Aboubakar ndio alizima ndoto za Misri baada ya dakika ya 88 kufunga goli la ushindi.

Ushindi huo unakuja baada ya Cameroon kufumgwa fainali mbili za AFCON na Misri, alifungwa fainali ya AFCON 2008 goli 1-0 Mohamed Aboutrika akifunga goli hilo, lakini walipoteza fainali ya AFCON 1986, Cameroon wanakuwa wamechukua taji lao la tano la AFCON wakati Misri wanabakia na rekodi yao ya kuchukua mataji nane ya AFCON.

Rekodi nyingine zilizowekwa katika AFCON na Cameroon ni kuwa inakuwa timu ya kwanza kuwahi kuifunga Misri goli katika fainali za AFCON baada ya Ethiopia, huku kocha wa Misri Hector Raul  Cuper akiendeleza rekodi yake mbovu kwa kupoteza fainali yake ya sita katika soka akiwa kama kocha wa timu tofauti.


Ibra akishangilia bao lake MANCHESTER UNITED imewatandika Mabingwa wa England Leicester City 3-0 wakiwa kwao King Power Stadium kwenye Mechi ya EPL, Ligi Kuu England.
Ushindi huu umewabakiza Man United Nafasi ya 6 lakini sasa wapo Pointi 1 nyuma ya Timu ya 5 Liverpool, Pointi 2 nyuma ya Timu ya 4 Arsenal, Pointi 4 nyuma ya Timu ya 3 Man City na Pointi 5 nyuma ya Timu ya Pili Spurs huku Chelsea wakiwa kileleni Pointi 14 mbele ya Man United.

Man United walipata Bao lao la kwanza Dakika ya 41 baada ya Kichwa cha Chris Smalling kuwahiwa na Mkhitaryan kabla Beki wa Leicester Huth kuukuta Mpira na kumtoka Beki mwingine wa Leicester Morgan na kumchambua Kipa Schmeichel.

Sekunde 87 baada ya Bao hilo Man United walikuwa 2-0 mbele kwa Bao la Zlatan Ibrahimovic alieunganisha Krosi ya Valencia.
Hadi Mapumziko Leicester 0 Man United 2.

Kipindi cha Pili kuanza Timu zote zilifanya mabadiliko kwa Leicester kuwaingiza King na Gray kuwabadili Musa na Okazakina huku Man United wakimtoa Marcos Rojo na kumwingiza Daley Blind.
Man United walifunga Bao la 3 Dakika ya 49 kufuatia ushirikiano mwema wa Ibrahimovic na Mkhitaryan kumfungulia Juan Mata kupiga Bao.

waliotembelea blog