Wednesday, December 30, 2015


www.bukobasports.comLA LIGA
RATIBA
Jumatano Desemba 30

18:00 Real Madrid CF v Real Sociedad
18:00 Levante v Malaga CF
20:15 Rayo Vallecano v Atletico de Madrid
20:15 Sevilla FC v RCD Espanyol
20:30 SD Eibar v Sporting Gijon
22:30 FC Barcelona v Real Betis
22:30 Celta de Vigo v Athletic de Bilbao
22:30 Getafe CF v Deportivo La Coruna
23:00 Las Palmas v Granada CF
Alhamisi Desemba 31
18:00 Villarreal CF v Valencia C.F


Barclays Premier League
PosLogo &TeamPWDLGDPts
1ArsenalArsenal1912341539
2Leicester CityLeicester City1911621239
3Manchester CityManchester City1911351736
4Tottenham HotspurTottenham Hotspur199821835
5Crystal PalaceCrystal Palace19946731
6Manchester UnitedManchester United19865630
7West Ham UnitedWest Ham United19784529
8WatfordWatford19856429
9Stoke CityStoke City19856129
10LiverpoolLiverpool18765-127
11EvertonEverton19685726
12SouthamptonSouthampton19667324
13West Bromwich AlbionWest Bromwich Albion19658-623
14ChelseaChelsea19559-620
15Norwich CityNorwich City19559-1020
16BournemouthBournemouth19559-1220
17Swansea CitySwansea City19478-819
18Newcastle UnitedNewcastle United194510-1517
19SunderlandSunderland183312-1812
20Aston VillaAston Villa191513-198


MARA baada ya Jumatatu Usiku kutoka Sare 0-0 na Mabingwa Watetezi Chelsea Uwanjani Old Trafford na kusitisha wimbi la kufungwa Mechi 4 mfululizo, Meneja wa Manchester United Louis van Gaal aliibuka na kutamba hana mipango ya kujiuzulu.
Baada ya kuchapwa 2-0 na Stoke City Siku ya Boksing Dei, Man United waliibuka na kusakata Soka safi na kustahili kuifunga Chelsea lakini, kama kawaida, umaliziaji uliwaangusha.
Hali hiyo ilimfanya Louis van Gaal apige ‘abauti tani’ na kudai Wachezaji wake wamempa sababu ya kutojiuzulu tofauti na alivyodokeza huko Britannia Stadium mara baada ya kufungwa na Stoke. Jana Van Gaal alisema: “Wachezaji wakicheza namna ile hasa wakati huu wa presha kubwa, hamna sababu ya mimi kujiuzulu. Labda Vyombo vya Habari wanataka hivyo, ila sitafanya.”
Wakati huo huo, Mchambuzi wa Soka anaeaminika huko England, Andy Gray, Mchezaji wa zamani wa Scotland aliechezea Klabu kadhaa huko England, amedai Man United hawana uchu wa kumwajiri Jose Mourinho kama Meneja.
Mourinho, ambae alitimuliwa na Chelsea Wiki iliyokwisha, amekuwa akitajwa na wengi kuwa atachukua wadhifa wa Van Gaal.

Jumatatu, nje ya Old Trafford, kwenye Mechi na Chelsea, Wachuuzi walikuwa wakitembeza bidhaa kadhaa zikiwa na Nembo ya Man United na Jina la Jose Mourinho wakimpigia debe kuwa Meneja wa Man United.
Lakini Andy Gray anaamini Bodi ya Man United bado inamsapoti Van Gaal na haimtaki Mourinho ambae wanaona hulka yake haiendani na utamaduni wa Man United.
Patashika za Ligi Kuu England kuendelea tena leo, Kuna Mechi moja pekee ambayo itaamua nani anamaliza 2015 akiwa anaongoza Ligi.
Jana, Arsenal iliichapa Bournemouth 2-0 na kutwaa uongozi wa Ligi wakiwa na Pointi 39 kwa Mechi 19 wakifuata Leicester wenye Pointi 38 kwa Mechi 18, Tottenham ni wa 3 na wana Pointi 35 kwa Mechi 19 na wa 4 ni Man City wenye Pointi 35 kwa Mechi 18.
Leo huko King Power Stadium, Leicester wanacheza na Man City na wakishinda watarudi kileleni na wakitoka Sare watabaki Nafasi ya Pili.
Ikiwa City itashinda basi watapanda hadi Nafasi ya Pili.
Leicester wanatinga kwenye Mechi hii wakitoka kufungwa 1-0 na Liverpool na kupoteza wimbi lao la kutofungwa katika Mechi 10 wakati City ikiichapa Sunderland 4-1.
Wakati Leicester wana Kikosi kamili bila Majeruhi ingawa mapema walipatwa na wasiwasi wa Staa wao Jamie Vardy, ambae ndie Mfungaji Bora wa Ligi, kutocheza kutokana na kuugua, City watamkosa Nahodha wao Vincent Kompany ambae ni Majeruhi pamoja na majeruhi wengine Pablo Zabaleta, Fernando na Samir Nasri.
Yaya Toure kendeleza tena wimbi la magoli!



Tukiwa tunaelekea kuumaliza mwaka 2015 na kuingia mwaka mpya 2016 moja kati ya mitandao inayoandika stori za michezo duniani imeandika TOP ya wachezaji bora wakali wa Ligi Kuu Uingereza. Mtandao wa bleacherreport.com umeandika list ya wachezaji 20 wakali wa Ligi Kuu Uingereza kwa mwaka 2015.
Hii ndio list ya majina yote 20 mtu wangu.
  1. David De Gea (Man United/Hispania)
  2. Mesut Ozil (Arsenal/Ujerumani)
  3. Alexis Sanchez ( Arsenal/Chile)
  4. David Silva (Man City/Hispania)
  5. Sergio Aguero (Man City/Argentina)
  6. Chris Smalling (Man United/Uingereza)
  7. Santi Cazorla (Arsenal/Hispania)
  8. Harry Kane (Tottenham/Uingereza)
  9. Toby Alderweireld (Tottenham/Ubelgiji)
  10. Francis Coquelin (Arsenal/Ufaransa)
  11. Willian (Chelsea/Brazil)
  12. Riyad Mahrez (Leicester City/Algeria)
  13. Jamie Vardy (Leicester City/Uingereza)
  14. Philippe Coutinho (Liverpool/Brazil)
  15. Hector Bellerin (Arsenal/Hispania)
  16. Hugo Lloris (Tottenham/Ufaransa)
  17. Morgan Schneiderlin (Man United/Ufaransa)
  18. Scott Dann (Crystal Palace/ Uingereza)
  19. Sadio Mane (Southampton/Senegal)
  20. John Stones (Everton/Uingereza)


Monday, December 28, 2015

 
Waziri Wizara ya Maliasili na Utalii Mhe. Prof. Jumanne Maghembe (mbele kulia) akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Selestine Gesimba wakati wa mapokezi yake leo tarehe 28 Desemba 2015 katika ofisi yake mpya Mpingo House mara baada ya kuapishwa Ikulu mapema asubuhi ya leo. Nyuma yake kulia ni naibu Waziri wa Wizara hiyo Mhe. Eng. Ramo Makani na anaeongoza utambulisho katikati yao ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Adelhelm Meru.
 Waziri Wizara ya Maliasili na Utalii Mhe. Prof. Jumanne Maghembe akisaini kitabu cha wageni mara tu baada ya kuingia katika ofisi yake mpya iliyopo Mpingo House mapema leo tarehe 28 Desemba 2015 baada ya kuapishwa Ikulu na Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli. Wanaoshuhudia kulia ni Naibu Wazari wa Wizara hiyo Mhe. Eng. Ramo Makani na Katibu Mkuu Dkt. Adelhelm Meru (kushoto).
Waziri Wizara ya Maliasili na Utalii Mhe. Prof. Jumanne Maghembe akiongea na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Adelhelm Meru (kushoto) na Naibu Waziri Mhe. Eng. Ramo Makani (kulia) mara baada ya kusaini kitabu cha wageni ofisini kwake mapema leo tarehe 28 Desemba 2015.
Picha ya pamoja kati ya Mhe. Waziri wa Maliasili na Utalii Prof. Jumanne Maghembe (wa pili kulia) na Naibu Waziri wake Mhe. Eng. Ramo Makani (wa pili kushoto), Katibu Mkuu wa Wziara hiyo Dkt. Adelhelm Meru (wa kwanza kulia) na Naibu Katibu Mkuu Ndugu Selestine Gesimba(kushoto). 
Sehemu ya wafanyakazi wa Wizara ya Maliasili na Utalii wakiwa tayari kwa mapokezi ya Waziri wao mpya Mhe. Prof. Jumanne Maghembe aliyeapishwa Ikulu leo na Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tazania Mhe. John Pombe Magufuli.(Picha na Hamza Temba - Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Maliasili na Utalii)

Siku chache baada ya kuachia video ya wimbo wake - ‘NINGEFANYAJE’, muimbaji wa R&B kutoka Tanzania, Bernard Paul  maarufu kama Ben Pol ameeleza sababu zilizopelekea muimbaji  Avril kutoka Kenya aliyeshirikishwa kwenye wimbo huo,  kutoonekana kwenye video hiyo anayoitaja kuwa kubwa kuliko video zote alizowahi kufanya.

Katika video hiyo iliyoongozwa na Justin Campos wa Afrika Kusini, Ben Pol anaonekana akiimba na Rossie M  ambaye pia ameshirikishwa kwenye wimbo huo huku mashabiki wakiisikia sauti ya Avril bila kumuona mwimbaji huyo mrembo.

Ben Pol amewaomba radhi mashabiki wake kwa kuwapa video ambayo haijakamilisha wahusika wote hususan kutokuonekana kwa Avril,  na kwamba sababu zilizopelekea hivyo zilikuwa nje ya uwezo wa pande zote katika utayarishaji wa video hiyo.

​​​Ben amesema kuwa baada ya yeye na Rossie M kuwasili Afrika Kusini ilikoshutiwa video hiyo, zilijitokeza changamoto muda mfupi kabla ya kuanza zoezi hilo. Ben Pol ameeleza kuwa pamoja na kuwa na maandalizi makubwa, video ya ‘Ningefanyaje’ ilikumbwa na changamoto nyingi tangu awali zilizopelekea kuahirishwa mara tatu.

“Kwa kweli hii video tokea mwanzo ilikuwa na changamoto, kwanza tuliisogeza mbele karibu mara tatu tena tukiwa tayari tumeshafika Afrika Kusini mimi na Rossie,” alisema Ben Pol. “Mara ya kwanza ni kutokana na ‘delay’ ya viza upande wa Avril. Si unajua Wakenya wao wanaenda South kwa viza tofauti na sisi Tanzania hatuendi kwa viza so kwetu ni rahisi zaidi muda wowote tu ukiamua fasta unaenda,” aliongeza.

Mkali huyo alieleza kuwa baada ya terehe mpya kupangwa na muongozaji aliyeshuti video hiyo, Justin Campos, siku moja kabla ya kushuti, AVRIL alipata tatizo lingine ambalo lilimzuia kusafiri kwa siku iliyofata kwenda Afrika Kusini.

Wakati huo huo, Campos naye alimueleza Ben Pol kuwa  kwa jinsi ratiba yake ilivyo endapo ataahirisha tena kushuti video hiyo, ratiba yake isingemruhusu kushuti video hiyo hadi Januari au Februari 2016,  kitu ambacho Ben Pol amesema  kisingewezekana kwasababu ingeendelea kumgharimu zaidi kifedha na kuvuruga ‘timing’ yake.

“Kutokana na hali hiyo, sikuwa na jinsi nyingine zaidi ya kukubali matokeo kwasababu  mwisho wa siku si mimi wala Avril wala director aliyekwamisha bali ni ‘situation’ ambayo ilikuwa nje ya uwezo wa kibinadamu.” Ben Pol anaeleza.

Ameongezea kuwa pamoja na kwamba angeweza kuamua kushuti video kwa kutumia version nyingine ya wimbo huo isiyokuwa na sauti ya Avril ili video isionekane na upungufu wake, lakini hakupenda kufanya hivyo kwa kuwa lengo kuu la wimbo lilikuwa kumshirikisha mwimbaji huyo. Pia, mashabiki wangekosa ladha nzuri na kazi nzuri aliyoifanya Avril.  Hivyo, aliamua kufanya video hiyo bila Avril na kukusudia kuwaeleza mashabiki wake kilichosababisha hali hiyo kwa kuwa aliamini mashabiki wataelewa magumu aliyopitia katika kuwapa video hiyo waliyokuwa wakiisubiri.

“Namshukuru sana Avril kwa kukubali kufanya kazi na mimi kwasababu imetimiza moja kati ya malengo yangu ya 2015, ambayo ilikuwa kuanza kufanya kazi na wasanii wa nje ya Tanzania na yeye ndiye alikuwa chaguo langu la kwanza. Ni imani yangu tutafanya tena project nyingine ya pamoja na kuikamilisha kama tulivyoikusudia,” alimaliza Ben Pol na kuwashukuru  mashabiki wake kwa kuupokea kwa mtazamo chanya wimbo na video yake.

waliotembelea blog