Tuesday, September 16, 2014



Warembo wanaoshiriki shindano la Redd’s Miss Tanzania 2014 leo wameingia siku ya pili ya kambi yao jijini Dar es Salaam na baada ya semina asubuhi na mapumziko ya mchana jioni hii wamefanya mazoezi katika chumba maalum cha mazoezi ‘Gym’, ungana na mpigapicha wa Father Kidevu Blog katika picha mbalimbali za warembo hao katika kambi yao.









Kikosi cha Timu ya Wakata Miwa Kagera Sugar wameanza leo hii safari kuelekea jijini Tanga kwa ajili ya mchezo wa ufunguzi wa Ligi kuu soka Tanzania bara katika uwanja wa CCM Mkwakwani dhidi ya wenyeji Mgambo JKT, septemba 20 mwaka huu.
Kocha msaidizi wa Kagera Sugar, Murage Kabange amesema klabu hiyo ina jumla ya wachezaji 25 na hii leo tayari wapo safari na viongozi watano kwenda kusaka pointi tatu muhimu.
Kabange aliongeza kuwa wameamua kuanza safari mapema kwasababu kutoka Kagera kwenda Tanga ni mbali sana.
Viongozi wa Kagera Sugar
Ubutu wa safu ya ushambuliaji lilikuwa tatizo la kudumu kwa Kagera Sugar lakini kwa sasa limepata marekebisho kwani wamesajili Vijana wa nguvu msimu huu.
WAKATA miwa wa Kaitaba, `Wanankulukumbi` Kagera Sugar wakijifua kwenye Uwanja wa Kagera Sugar hivi karibuni tayari kwa Ligi kuu Vodacom sep 20 mwaka huu. Kagera Sugar wataanza ufunguzi wa Ligi kuu Vodacom Ugenini na timu ya Mgambo JKT mkwakwani Mjini Tanga wikiendi hii.
Kocha huyo alisema: “Tuna imani na vijana wetu kuwa wanaweza kutufikisha tunapotaka, japokuwa ligi ya msimu huu inaonekana itakuwa ngumu, lakini tutajitahidi kupigana ili kuweza kushika nafasi za juu”.



Wachezaji wa Kagera Sugar wakifaya mazoezi yao kwenye Uwanja wa Kaitaba Hivi karibuni.

Baadhi ya Viongozi wa Timu ya Kagera Sugar wakiwa Uwanjani Kaitaba wakishuhudia mazoezi ya Vijana wao. Wakijifua kujiandaa na Ligi Kuu Vodacom msimu mpya 2014/15 inayotarajia kuanza hivi Karibuni sep.20 mwaka huu.


Murage Kabange, kocha msaidizi wa Kagera Sugar (kulia) tayari amebainisha kuwa mapungufu waliyokuwa nayo katika kikosi chao kuwa wameishayafanyia marekebisho na wako tayari kupambana na Mgambo JKT ya Mjini Tanga.
Kocha Mkuu wa Kagera Sugar (kulia) Bw. Jackson Mayanja akiangalia vijana wake wakati w mazoezi yao kwenye Uwanja wao wa Nyumbani Kaitaba hivi karibuni


Msanii mwingine anaekuja vyema kwenye anga ya muziki wa Bongofleva aitwaye Kadja ambaye anatamba na wimbo wake wa Maumivu niache akiimba pamoja na Linah.

Mkali wa Bongo Hip Hop Farid Kubanda a.k.a Fid Q akikamua vilivyo juu ya jukwaa na la Fiesta.

Msanii wa Bongofleva,Kadja akiimba wimbo wake wa Maumivu niache mbele ya maelfu ya wakazi wa Tabora (hawapo pichani) waliofika kwenye tamasha la Fiesta usiku wa kuamkia leo.

Ilikuwa buruuudani ya kusambaza upendo wa kweli kwa wakazi wa Tabora ndani ya tamasha la Fiesta

Palikuwa hapatoshi usiku wa kuamkia leo ndani ya uwanja wa Al-Hassan Mwinyi mjini Tabora,ambapo tamasha la Fiesta lilirindima.

Wasanii chipukizi kutoka Tabora nao walionesha umahiri wao jukwaani

Sehemu ya umati mkubwa wa watu waliofika kulishuhudia tamasha la Fiesta lililofanyika usiku wa kuamkia leo ndani ya uwanja wa Al-Hassan Mwinyi mjini Tabora.


Aaron Ramsey and Mesut Ozil celebrate the Welshman's goal away at Dortmund last November, in a game the Gunners won 1-0

EUROPE: Champions League - Group Stage
11:45 Benfica-Zenit Petersburg


11:45 Dortmund-Arsenal


11:45 Galatasaray-Anderlecht


11:45 Juventus-Malmo FF


11:45 Liverpool-Ludogorets


11:45 Monaco-Bayer Leverkusen


11:45 Olympiakos Piraeus-Atl. Madrid


11:45 Real Madrid-Basel

Monday, September 15, 2014



Manchester United  wameshinda Mechi yao ya kwanza Msimu huu kwenye Ligi Kuu England wakati Kikosi chao kipya kikiisambaratisha QPR kwa Bao 4-0 ndani ya Old Trafford huku Angel De Maria aking’ara na Wachezaji wapya Marcos Rojo na Daley Blind wakicheza Mechi yao ya kwanza na kuleta uhai mkubwa.Manchester United v QPRJuan Mata akifanya yake..Manchester United v QPR
Bao 3 kabla ya Mapumziko, zilizofungwa na Di Maria, Ander Herrera na Wayne Rooney ziliwaua QPR na kuwamaliza kabisa pale Kipindi cha Pili Juan Mata alipofunga Bao la 4.Manchester United v QPRRadamel Falcao akikimbiza mpira mwishoni kipindi cha pili..Manchester United v QPRRadamel Falcao chupuchupu afunge! Kipa wa QPR aliutema mpira..
Manchester United v QPR
Straika mpya, Radamel Falcao, alikuwa Benchi na kuingizwa Dakika ya 67 na alionyesha matumaini na nusura afunge Bao kama si uhodari wa Kipa wa Robert Green. Bao la nne lilifungwa na Juan Mata katika dakika ya 58 kipindi cha pili baada ya kupata pasi kutoka kwa Ángel Di María.
Ander Herrera akishangilia bao lake la pili kwa United.Angel Di Maria alifunga Bao la Kwanza kwa frikiki murua na ni yeye alietengeneza Bao la Pili kwa kukokota ngoma Mita 60 na kumpasia Rooney aliepiga Shuti lililookolewa na kumrudia Herrera na kufunga.Manchester United v QPRDakika ya 24 Di Maria anaipachikia bao la kwanza Manchester United..1-0 dhidi ya QPR. Ni Frii kiki ya Di Maria ya umbali wa  yadi  30 na kutinga moja kwa moja hadi langoni mwa QPR.Ander Herrera  alitupia la pili na kufanya 2-0 dhidi ya QPR katika dakika ya 36 kipindi cha kwanza baada ya kupata mpira kutoka kwa Wayne Rooney. Bao la tatu lilifungwa na Wayne Rooney katika dakika ya 44 kwa shuti kali lililomzidi kipa wa QPR Green na kuzama langoni moja kwa moja na ni kwa ushirikiano wa Ander Herrera aliyetoa pasi kwa Rooney.Manchester United v QPRFalcao alichukua nafasi ya Juani Mata kipindi cja pili dakika ya 67Manchester United v QPRRojo kwenye patashika na Matt Philips wa QPRManchester United v QPRFer wa QPR akichuana na Angel Di MariaRio Ferdinand kwenye wasiwasi kutoka kwa timu yake ya zamani UnitedRadamel Falcao kaanzia benchiManchester United v QPRRio Ferdinand akipewa zawadi yake mapema kabla ya mtanange..Louis van GaalVan Gaal kati..Radamel FalcaoTayari kwa kipute...
Daley Blind na Radomel Falcao wakiingia Old Trafford...yasemekana Falcao kuingia kipindi cha pili..dhidi ya QPR.Wachezaji wa Man United wakiwa tayari kwa kipute na QPR jioni hii kwenye uwanja wa Old Trafford. United wanatarajia kuchezesha wachezaji wao wapya katika mtanange huu.
Daley Blind na Radomel Falcao wa  Manchester United wakiwasili kwenye Uwanja wa Old Trafford, Tayari kwa mtanange huo.
Luke Shawna  Ander Herrera wakishuka kwenye basi kuingia Uwanjani Old Trafford.
Meneja wa Man United Louis van Gaal akiwsiliWachezaji wa QPR wakiwa kwenye Uwanja wa  Old Trafford
Mashabiki nao ndio kwanza wanaanza kuingia kuchukua nafasi zao Uwanjani Old Trafford.
VIKOSI:

waliotembelea blog