Thursday, April 6, 2017



Premier League
PosLogo &TeamPWDLGDPts
1ChelseaChelsea3023343872
2Tottenham HotspurTottenham Hotspur3019833865
3LiverpoolLiverpool3117952760
4Manchester CityManchester City3017762358
5ArsenalArsenal2916672554
6Manchester UnitedManchester United29141231954
7EvertonEverton3114981951
8West Bromwich AlbionWest Bromwich Albion3112811-144
9SouthamptonSouthampton2910712-137
10WatfordWatford3010713-1237
11Leicester CityLeicester City3010614-1036
12Stoke CityStoke City319913-1236
13BournemouthBournemouth319814-1235
14BurnleyBurnley3110516-1235
15West Ham UnitedWest Ham United319616-1633
16Crystal PalaceCrystal Palace309417-1131
17Hull CityHull City318617-2930
18Swansea CitySwansea City318419-2928
19MiddlesbroughMiddlesbrough3041115-1523
20SunderlandSunderland305520-2920

Wednesday, April 5, 2017



Mchezaji anayetaka kuondoka Yanga Ruksa, Mlango wazi
Uongozi wa Yanga umeweka bayana kwamba hauna mpango wa kumzuia mchezaji yeyote kuondoka iwapo atahitaji kuihama klabu hiyo
Mabingwa watetezi Ligi Kuu Bara, Yanga SC ambao ndio wanaoongoza kwenye msimamo wa ligi msimu huu kwa tofauti ya pointi moja dhidi ya mahasimu wao Simba huku kila timu ikibakiwa na mechi tano kumalizika, wamtamka kuwa mchezaji yeyote anayetaka kuondoka mwisho wa msimu mlango uko wazi.
Kuelekea mwisho wa msimu Uongozi wa Yanga umetoa ruhusa kwa mchezaji yoyote kuondoka Yanga iwapo tu atafuata taratibu, Katibu wa Yanga Boniface Mkwasa alisema.
“Kama kuna Mchezaji anataka kuondoka basi awe muungwana, atueleze mapema na taratibu zifuatwe, Pia kama kutakuwa na mchezaji ambaye Mwalimu anona hamuhitaji sisi tutafuata taratibu na kumueleza mapema kabisa.” Alisema katibu huyo wa Yanga kwa mujibu wa Shaffih Dauda Blog.
Wakati akiyasema hayo Mkwasa kuna hatari timu ya Yanga ikawakosa wachezaji wengi muhimu ambao mikataba yao inaelekea kuisha ndani ya Yanga, Wazimbambwe wawili Donald Ngoma na Thabani Kamusoko wanaelekea kumaliza mikataba yao mwishoni mwa msimu huu na uongozi wa klabu hiyo haujaweka bayana kuhusu kuwaongezea mikataba mipya.
Pia mabeki wa kati wazawa Kelvin Yondani na nahodha Nadir Haroub ‘Cannavaro’ mikataba yao inafikia tamati mwisho wa msimu, kadhalika kwa mshambuliaji Anthony Mateo na beki wa kimataifa wa Togo Vicent Bossou.
Kwa sasa wapo katika maandalizi kwa ajili ya mechi ya kombe la shirikisho Afrika dhidi ya MC Alger katika uwanja wa Taifa na watarudiana wiki moja baadaye huko Algeria.

Tuesday, April 4, 2017


EPL RATIBA
Jumanne Aprili 4

2145 Burnley v Stoke City
2145 Leicester City v Sunderland
2145 Watford v West Bromwich Albion
2200 Manchester United v Everton


MANCHESTER UNITED Jumanne Usiku wako kwao Old Trafford kucheza na Everton kwenye Mechi ya EPL, Ligi Kuu England, ambayo hiyo na ile inayufuatia Wikiendi inayokuja dhidi ya Sunderland ndiyo itatoa mwelekeo wa Timu hiyo kuwemo 4 Bora au la kwa mujibu wa Meneja wao Jose Mourinho.

Akiongelea kuelekea Mechi hii na Everton, Mourinho alisema atashusha Kikosi kikali dhidi ya Everton na Sunderland na matokeo ya Mechi hizo ndio yataamua nini hatima yao kwenye Ligi na kwani baada ya hapo watacheza Robo Fainali ya UEFA EUROPA LIGI na mkazo utakuwa huko.
Kufuzu 4 Bora ya Ligi kutawawezesha Man United kucheza UCL, UEFA CHAMPIONS LIGI Msimu ujao lakini pia kutwaa EUROPA LIGI kutawapa nafasi hiyo pia.

Hivi sasa kwenye EPL Man United wapo Nafasi ya 5 wakiwa na Pointi 53 kwa Mechi 28 wakati Man City wapo Nafasi ya 4 wakiwa na Pointi 58 kwa Mechi 29.
Uso kwa Uso
-Man United hawajafungwa katika Mechi 4 zilizopita na Everton.
-Katika Mechi 49 za EPL, Man United Ushindi 33 Sare 8 Everton Ushindi 8
Man United wataingia Mechi hii wakitoka Sare ya 0-0 na West Bromwich wakati Everton walichapwa 3-1 na Liverpool Mechi zote zikichezwa Juzi Jumamosi.
Sare hiyo kwa Man United imeendeleza wimbi lao la Mechi 19 kutofungwa kwenye Ligi.

Hali za Vikosi:
Man United inategemewa kuwa nao tena Mfungaji wao Bora Zlatan Ibrahimovic na Kiungo Ander Herrera baada ya kumaliza Vifungo vyao vya Mechi 3 na 2 lakini itawakosa Majeruhi Juan Mata, Chris Smalling na Phil Jones huku pia kukiwepo uwezekano wa Paul Pogba kucheza baada ya kupona maumivu yake na kuanza mazoezi.
Everton inakabiliwa na Majeruhi 6 wakiwemo Seamus Coleman, alievunjwa Mguu akiichezea Nchi yake Republic of Ireland dhidi ya Wales Wiki ilyopita na pia Sentahafu wao wa Argentina Ramiro Funes Mori alieumia vibaya Goti.

Pia Mchezaji wa zamani wa Man United Kiungo Morgan Schneiderlin na Winga Aaron Lennon watakosekana kwa kuwa na maumivu.

Mechi ya Kwanza Msimu huu
Mapema Mwezi Desemba Zlatan Ibrahimovic aliifungia Bao Man United na Everton kusawazisha Dakika za lala salama kwa Penalti tata iliyotolewa kwa Rafu iliyofanywa na Mchezaji wa zamani wa Everton Marouane Fellaini na Adhabu hiyo kufungwa na Leighton Baines na kuifanya Gemu iishe 1-1.



Wanasayansi wa Chuo Kikuu cha Ghent nchini Ubelgiji wamegundua njia mpya ya kutengeneza mafuta ya kuendeshea gari kwa kutumia majani ‘Biofuel’ ambapo kwa mujibu wa wanasayansi hao, majani yana uwezo wa kutengeneza kiwango kikubwa cha ‘decane’ ambacho hutumika katika kuzalisha mafuta.
Akizungumza na Science Daily, Professa Way Cern Khor alisema: >>> “Majani yamekuwa yakitumika kulisha wanyama lakini pia yanaweza kuzalisha mafuta ‘Biofuel’ kwa kiasi kikubwa. Hii inaweza kuja kusaidia kupunguza bei ya mafuta. Tunafurahi kuweza kubadilisha kitu kisichotumika na kuwa nishati muhimu.”
Prof. alielezea jinsi atakavyoweza kuyabadilisha majani na kuwa mafuta ya gari akisema kuwa majani hayo yatawekwa bakteria maalum watakaoweza kuondoa sukari iliyopo ndani yake na kubadilika kuwa katika asidi ya lactic na caproic ambayo inatumika kutengeneza mafuta.
Hadi sasa wanasayansi hao wameweza kutengeneza kiasi kidogo cha mafuta kinachotokana na majani lakini jitihada zinaendelea kuweza kubadilisha majani kuwa katika hali ya kimiminika.

Monday, April 3, 2017



Moja kati ya majina yaliojipatia umaarufu na heshima kubwa katika soka ni Zinedine Zidane na Ronaldinho ambao uwezo wao umeifanya dunia ya soka kutokusahau mchango wao, Zidane ni mahiri katika kucheza mpira na kufanyia mbwembwe kama ilivyo kwa Ronaldinho.
Naomba nikusogezee video yao kila mmoja akionesha uwezo wake katika soka, mtu wangu wa nguvu naomba jikumbushe halafu usisahau kuacha comment yako nani unamkubali zaidi katika umahiri wa kuuchezea mpira.



Leo April 3 kupitia kipindi cha XXL cha Clouds FM mtangazaji Soudy Brown katuletea U-heard inayomhusu msanii Nay wa Mitego kudaiwa kuvunja uchumba wa shabiki yake kutokana na shabiki huyo kuchora tatoo ya Nay wa Mitego. Ndugu wa mchumba aliyekuwa akitarajia kumuoa dada huyo walikataa baada ya kuona tatoo ya Nay wa Mitego kwake.

Soudy Brown alipiga story na Nay wa mitego na majibu yake yalikuwa haya.…..>>>“Mimi simfahamu na mimi napendwa na watu wengi sana wengine siwajui so inawezekana ni shabiki tu japo nashukuru maana amechora tatoo mpaka kufikia hatua ya kuachika lakini mimi simfahamu”:- Nay wa mitego

Friday, March 31, 2017


TANGU wafungwe 4-0 na Chelsea huko Stamford Bridge hapo Oktoba 23, Manchester United imekuwa Timu pekee ‘Isiyofungika’ kwenye EPL, Ligi Kuu England, ikimaliza zaidi ya Miezi 5 bila kufungwa zikiwa ni mbio za Mechi 18.

Licha kusakamwa na Mechi kedekede wakiwa Timu pekee wenye Mechi nyingi kupita yeyote huko England, Jose Mourinho ameongoza Kikosi hicho kwa ufanisi mkubwa na kuwawezesha Mwezi Februari kutwa Taji kubwa walipobeba Kombe la Ligi, EFL CUP.
Mwezi Aprili wanakabiliwa na Mechi 9 na ingawa Mourinho amelalamikia ugumu wa Ratiba yao lakini hilo ni dalili tosha ya mafanikio yao Msimu huu wao wa kwanza chini ya Jose Mourinho ambao walikuwemo kwenye mbio za Mashindano Manne na kutolewa tu Wiki 2 zilizopita kwenye FA CUP.

Hilo limempa Mourinho nafasi ya kubadili Kikosi chake katika kila Mashindano na kumwezesha kupata Kikosi imara cha kucheza EPL bila kufungwa.

Related imageMtizame Mchezaji wa Kimataifa wa Armenia, Henrikh Mkhitaryan, ambae kwenye Mechi yake ya kwanza tu Klabuni hapo, walipofungwa na Man City Mwezi Septemba, alitolewa nje lakini hilo halikumkatisha tamaa kwani aliibukia kwenye UEFA EUROPA LIGI na kung’ara na kurudi tena Kikosi cha Kwanza.

Kushiriki Mashindano mengi kumemfanya Mourinho azungushe Wachezaji kwenye kila Mechi ya EUROPA LIGI, EFL CUP na FA CUP lakini kwenye Ligi panga pangua wapo David de Gea; Antonio Valencia, Phil Jones, Marcos Rojo, Matteo Damian; Ander Herrera, Michael Carrick; Henrikh Mkhitaryan/Juan Mata, Paul Pogba, Marcus Rashford; Zlatan Ibrahimovic.

Wafutiliaji wa hizo Mechi zao 18 ambazo hawakufungwa kwenye Ligi wamebaini Man United hufungwa Goli chache, 11 tu, lakini pia kufunga chache, Bao 29 tu.

Hiyo ndiyo sababu kubwa Man United wako Nafasi ya 5 kwenye Ligi wakiwa Pointi 17 nyuma ya Vinara Chelsea.

Kwa ujumla Man United wamefunga Bao 42 katika Mechi 27 za Ligi tofauti na wenzao kama Liverpool waliofunga 62, Chelsea 59, Tottenham Hotspur 55, City 54, Arsenal 56 na Everton 51.

Kitu muhimu kwa Kikosi cha Mourinho kutofungwa Mechi 18 za Ligi ni Difensi yake hasa ule upacha wa Sentahafu ya Marcos Rojo na Phil Jones huku Ander Herrera akiwa nguzo kubwa kwenye Kiungo.

Walipofungwa Mechi yao ya mwisho ya Ligi na Chelsea, upacha wa Sentahafu ulikuwa ni wa Eric Bailly na Chris Smalling na kuumia kwao kukatoa mwanya kwa Rojo-Jones kucheza pamoja na wao ni kati ya Wachezaji 6 waliocheza Mechi nyingi kwenye hizo 18 ambazo hawakufungwa wakifuatia Herrera, Ibrahimovic, Pogba na Kipa De Gea anaeongoza.

Lakini tatizo kubwa ni ufungaji ambao umebaki kwa Zlatan Ibrahimovic pekee aliefunga Jumla ya Mabao 26 Msimu huu na 11 kati ya Mechi 16 za Ligi zilizopita.

Sasa Mwezi Aprili Man United wanakabiliwa na Mechi 9 wakianzia Jumamosi Old Trafford kucheza na West Brom na kisha Jumanne Everton watatua Uwanja huo huo wakati Jumamosi inayofuatia watakuwa safarini Stadium of Light kuivaa Timu ya Mkiani Sunderland inayoongozwa na Meneja wa zamani wa Man United David Moyes.

Mbio hizi za kutofungwa za Mechi 18 za Ligi ndio bora kabisa kwenye Ligi Kuu England tangu Machi 2013 pale Kikosi chini ya Sir Alex Ferguson kilivyofanya hivyo.

waliotembelea blog