Friday, March 31, 2017


VPL, LIGI KUU VODACOM, inarejea tena kwa kishindo Jumamosi hii Aprili Mosi kwa Mechi 3 na kubwa kabisa ni ile itayopigwa Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam kati ya Mabingwa Watetezi Yanga na Timu ngumu Azam FC.
Hakika Mechi hii ni Bigi Mechi na itatoa mwanga mkubwa kama kweli Yanga wanaweza kutetea Ubingwa wao hasa kwa vile wapo Nafasi ya Pili wakiwa Pointi 2 nyuma ya Vinara Simba huku wote wakiwa wamecheza Mechi 24 kila mmoja na kubakiza Mechi 6 tu kila mmoja.

Azam FC wao wapo Nafasi ya 3 wakiwa Pointi 9 nyuma ya Yanga wakiwa bado wana matumaini finyu ya Ubingwa.

Mechi nyingine za hiyo Jumamosi, ambazo hasa nyingi ni vita za kutoshuka Daraja, ni huko Songea kati ya Maji Maji FC na Toto Africans wakati nyingine ni Mjini Mbeya kati Mbeya City na Ruvu Shooting.

Jumapili zipo Mechi 4 na Macho Kodo ni huko Uwanja wa Kaitaba Mjini Bukoba kati ya Kagera Sugar, walio Nafasi ya 4, wakiwavaa Vinara Simba.

Nyingine za Jumapili ni Jijini Dar es Salaam kati ya African Lyon na Stand United, Mjini Mbeya ni Tanzania Prisons na Mtibwa Sugar na huko Mwadui Complex, Shinyanga ni Mwadui FC na JKT Ruvu.

VPL – LIGI KUU VODACOM
Jumamosi Aprili 1

Yanga v Azam FC
Maji Maji FC v Toto Africans
Mbeya City v Ruvu Shooting

Jumapili Aprili 2

Kagera Sugar v Simba
African Lyon v Stand United
Tanzania Prisons v Mtibwa Sugar
Mwadui FC v JKT Ruvu

Jumamosi Aprili 8
Stand United v Tanzania Prisons
Kagera Sugar v JKT Ruvu
Yanga v Toto Africans
Mtibwa Sugar v Azam FC

Jumapili Aprili 9
Mbeya City v Ndanda FC
Maji Maji FC v African Lyon

Jumatatu Aprili 10
Mbao FC v Simba

Kiungo wa kimataifa wa Hispania anayeichezea Man United ya England Juan Mata jina lake limerudi kwenye headlines baada ya kufanyiwa upasuaji wa groin, Mata ambaye mwanzoni mwa wiki hii alikuwa akilalamika mazoezini kuwa anasumbuliwa na groin amefanyiwa upasuaji.
Taarifa zilizotoka usiku wa March 31 2017 kuhusu kiungo huyo ni kuwa upasuaji wake umeenda salama lakini kutokana na tatizo lake, kuna uwezekano mkubwa wa kukosa mechi zote za kumalizika za Man United tofauti na awali alivyotazamiwa kuwa anaweza kukosa mechi tatu tu.

Juan Mata ambaye alijiunga na Man United akitokea Chelsea mwaka 2014 , hajawahi kukosa mechi za Man United katika kipindi cha miaka yote mitatu aliyokuwepo klabuni hapo pasipokuwa na majeruhi, mara zote amekuwa akikosekana kwa sababu za msingi ikiwemo majeruhi.

Wednesday, March 22, 2017


Sir Alex Ferguson atarudi tena Old Trafford kwenye Benchi wakati wa Mechi ya Kumtukuza Kiungo wa Manchester United Michael Carrick kwa Utumishi Ulitukuka wa muda mrefu Klabuni hapo.
Ferguson, aliestaafu Umeneja Mwaka 2013 baada ya kuitumikia Man United kwa Miaka 27, ataongoza moja ya Timu katika Mechi hiyo Maalum.
Timu atakayoongoza Sir Alex Ferguson itaitwa Manchester United 2008 XI na itaundwa na Wachezaji waliotwaa Ubingwa wa England na UEFA CHAMPIONS LIGI Mwaka 2008 wakiwa chini yake.
Timu hiyo itacheza na Timu itakayoitwa Michael Carrick All-Star XI ikiongozwa na aliewahi kuwa mmoja wa Mameneja wa Michael Carrick, Harry Redknapp.

Carrick, mwenye Miaka 35 na ambae amedumu Man United kwa Miaka 11 hadi sasa, ameelezea kurejea kwa Sir Alex Ferguson: “Ni heshima kubwa kurejea kwake na kuwa sehemu ya hiyo Gemu. Yeye pengine ndio sababu pekee nilijiunga na Man United, sina uwezo kumshukuru inavyostahili!”

Miongoni mwa Majina makubwa ya Wachezaji Soka watakaoshiriki Mechi hiyo maalum ni Edwin van der Sar, Gary Neville, Rio Ferdinand, Paul Scholes na Ryan Giggs wakiichezea Man United na upande wa Michael Carrick All-Star XI watakuwemo Steven Gerrard, Frank Lampard na Michael Owen.
Ferguson was manager at United for 27 years between 1986 and 2013Ferguson amekuwa Meneja wa United kwa miaka 27 kwenye miaka ya 1986 na 2013

Friday, March 17, 2017


Juan Mata(kushoto) akipongezwa na wenzake kwa bao lake la pekee katika mchezo huo wa marudiano.Juan Mata helped Manchester United move into the last eight of the Europa League.cha pili dakika ya 70 Juan Mata aliwafungia Man United bao na kubadilisha matokeo ya awali na kuwa (2-1 kwenye Agg.) Hku katika Mchezo huo wa raundi ya 16 Man United wakimbadilisha Paul Pogba dakika ya 48 aliyeumia na kuondolewa na nafasi yake kuchukuliwa na Fellaini. Manchester United pia walimbadilisha Beki Blind dakika ya 64 na kumuingiza Jones. Pia katika mchezo huo Zlatan alicheza vyema kipindi cha kwanza na kidogo afunge aligonga mwamba.Hadi dakika 45 za kipindi cha kwanza zinamalizika Man Unied 0 Rostov 0.

Monday, March 6, 2017


Gwiji wa soka duniani kutoka klabu ya Liverpool nchini Uingereza, John Barnes jana amewanoa wachezaji wa timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 15 (Serengeti Boys) katika siku yake ya kwanza nchini katika kuadhimisha miaka 100 ya benki ya standard Chartered tangu kuanzishwa kwake.
“Ni muhimu sana kwa kuwafundisha vijana wadogo soka katika umri huo ni wito kwa viongozi wa soka hapa Tanzania na wadau wote wa michezo kuweka nguvu zao za kutosha kwa vijana maana ni tegemeo la siku za usoni,
“Ni muhimu kama taifa kuwekeza kwa vijana kuwaweka mazingira na miundombinu ya kutosha kabisa ili kuweza kuinua vipaji vyao vya soka na ndio staili inayotumiwa na mataifa yaliopiga hatua kubwa kwenye maendeleo ya mpira wa miguu,” amesema Barnes.

Gwiji wa soka duniani kutoka klabu ya Liverpool nchini Uingereza, John Barnes akizungumza jambo na walimu wa viwanja vya JK Youth Park mara baada ya kuwasili uwanjani hapo kwa ajili ya kuifunda timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 15 (Serengeti Boys) akiwa kwenye ziara ya siku tatu nchini. Katika siku yake ya tatu (leo) nchini gwiji huyo wa soka atashuhudia fainali ya timu tatu kutoka nchini za Tanzania, Uganda na Kenya ambao watapambana vikali kuwania kombe la Standard Chartered 2017 safari ya kuelekea Anfield mjini Liverpool nchini Uingereza.
Barnes amesistiza muhimu wa kuwafunda vijana wadogo wakiwa katika umri mdogo kabisa kama njia bora ya kuwaandaa kuwa wachezaji bora siku za usoni na kuwa tegemeo katika nchini yao.
Mkuu wa kitengo cha Mahusiano na Masoko wa Benki hiyo, Bi Juanita Mramba amesema kwamba Azania Group of Companies kutoka Tanzania, Capital Fm-Kenya na Coca Cola ya Uganda watamenyana vikali kwenye fainali hizo kesho kwenye viwanja vya Jk Youth Park, Kidongo Chekundu jijini Dar es Salaam.
“Tumeweza kumleta John Barnes kushiriki kwenye mazoezi ya vijana chini ya miaka 15 kwa ajili ya kuwaanda kwenye mashindano ya AFCON ya vijana mwakani, lakini pia amekuja kwa ajili ya tukio la benki hiyo kutimiza miaka 100 tangu kuanza shughuli zake mwaka 1917 za kibenki nchini,” amesema Mramba.
 

Gwiji wa soka kutoka klabu ya Liverpool, John Barnes akizungumza machache na timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 15 (Serengeti Boys) kabla ya kuelekea uwanjani kuwafunda kwa vitendo katika viwanja vya JK Youth Park, Gerezani, jijini Dar es Salaam. Aliongeza kwamba takribani timu 32 zilishiriki kwenye mashindano ya awali ya kutafuta mwakilishi wa Tanzania katika fainali zitakazofanyika kesho na timu mbili kutoka Uganda na Kenya.
Mramba alifafanua kwamba gwiji huyo wa soka aliyetamba miaka ya 1990 atakuwa nchini kwa siku tatu na kushiriki kwenye program ya kuwafundisha vijana wa umri chini ya miaka 15 kuwapa mbinu za soka tangu wakiwa vijana wadogo.
Kwa upande wake, Msemaji wa Shirikisho la soka nchini (TFF) Bw Alfred Lucas amesema kwamba hii ni fursa adimu kwa vijana kupata nafasi ya kufundishwa soka na mmoja wa magwiji wa soka wa dunia.
“Hii ni nafasi yao muhimu sana katika kujifunza mambo ya soka na kupanua uelewa wao kuhusu mpira wa miguu wakiwa bado vijana wadogo kabisa maana ni mastaa wa taifa wa baadaye,” alisema.

Aidha, kocha wa timu ya Serengeti Boys, Kim Poulsen aliwashukuru benki ya Standard Chartered kwa kufanikisha ujio wa gwiji hilo la soka kuja kushiriki kwenye mazoezi na kutoa mchango wa mafunzo kwa vijana wake.
Aliongeza kwamba ni muhimu kwa wadau wengine wa michezo kuiga mfano wa benki hiyo na kuweza kuwaleta magwiji wa soka duniani kama chachu ya maendeleo ya soka kwa nchini zinazoendelea kama Tanzania.
Gwiji hilo la soka kutoka klabu ya Liverpool anatarajiwa kuondoka leo jioni baada ya fainali hizo kwenye viwanja vya JK Youth Park mjini Dar es Salaam.

Gwiji wa soka kutoka klabu ya Liverpool, John Barnes akizungumza na wanahabari (hawapo pichani) kuhusu umuhimu wa kuwawekea mazingira na miundombinu ya kutosha watoto ili kuweza kuinua maendeleo ya soka nchini.

Kocha Mkuu wa Serengeti Boys, Kim Poulsen akifafanua jambo kwa wanahabari (hawapo pichani) juu ya umuhimu wa kuendelea kuweka mazingira mazuri kwenye soka la watoto chini ya umri wa miaka 15 kama njia bora ya kukuza vipaji nchini wakati wa kliniki fupi iliyoendeshwa na Gwiji wa Soka wa timu ya Liverpool, John Barnes katika viwanja vya JK Youth Park vilivyopo Kidongo Chekundu, jijini Dar es Salaam.
Afisa Habari wa TFF, Alfred Lucas akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ujio wa John Barnes na umuhimu wa kuinua vipaji kwa watoto chini ya miaka 15.

Pichani juu na chini ni John Barnes akiwapa mbinu mbalimbali wakati wa mazoezi kwa watoto chini ya umri wa miaka 15 (Serengeti Boys) baada ya kupata fursa ya kuwepo nchini kushuhudia fainali za mashindano ya Kombe la Standard Chartered 2017 safari ya kuelekea Anfield katika kuadhimisha miaka 100 tangu benki ya hiyo kuanzishwa nchini yatakayofanyika leo katika viwanja vya JK Youth Park jijini Dar es Salaam.

Timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 15 (Serengeti Boys) wakitoana jasho baada ya kliniki fupi iliyoendeshwa na Gwiji wa soka wa timu ya Liverpool, John Barnes (hayupo pichani) katika viwanja vya JK Youth Park, jijini Dar es Salaam.
Gwiji wa soka kutoka klabu ya Liverpool, John Barnes katika picha ya pamoja na baadhi ya watoto wa wateja wa benki ya Standard Chartered waliopata nafasi ya kukutana na gwiji huyo katika viwanja vya JK Youth Park.

Saturday, February 25, 2017


Image may contain: 2 people, stadium and outdoorDabi ya Kariakoo uliochezwa Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam, Leo ulishuhudia Mtu Simba ikitoka nyuma kwa Bao 1-0 na kuichapa Yanga 2-1.
Yanga walifunga Bao lao Dakika ya 5 kwa Penati ya Simon Msuva iliyotolewa baa Fowadi wao Obrey Chirwa kuangushwa na Beki Novatus Lufunga.

Image may contain: 8 people, people standing, stadium, grass and outdoorDakika ya 55 Simba walibaki Mtu 10 baada ya Mchezaji wao Janvier Besala Bokungu kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu baada ya kulambwa Kadi za Njano 2.
Simba wakasawazisha Bao Dakika ya 66 kupitia Laudit Mavugo aleingizwa Kipindi cha Pili na kufunga Bao la Pili na la ushindi Dakika ya 81 Mfungaji akiwa Shiza Kichuya.
VPL, inayoshirikisha Timu 16, sasa inaongozwa na Simba wenye Pointi 54 kwa Mechi 23 na Yanga ni wa Pili wakiwa na Pointi 49 kwa Mechi 22 huku Azam FC ni wa 3 wakiwa na Pointi 41 kwa Mechi 23.
VIKOSI:
SIMBA:
Daniel Agyei, Janvier Bokungu, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Novaty Lufunga [Shiza Kichuya, 51’], Abdi Banda, James Kotei, Ibrahim Hajib, Muzamil Yassin, Juma Luizio [Said Ndemla, 27’], Laudit Mavugo, Mohammed ‘Mo’ Ibrahim [Jonas Mkude, 57’].

YANGA:
Deogratius Munishi ‘Dida’, Juma Abdul, Mwinyi Haji, Andrew Vincent, Kevin Yondan, Justine Zulu [Juma Mahadhi, 78’], Simoni Msuva, Thabani Kamusoko [Said Juma ‘Makapu’, 45’], Amisi Tambwe [Deus Kaseke, 70’], Obrey Chirwa, Haruna Niyonzima.

REFA:
Mathew Akrama [Mwanza]
WASAIDIZI: Mohammed Mkono [Tanga] na Hassan Zani [Arusha]

Tuesday, February 21, 2017



Kocha wa Man United Jose Mourinho kuelekea mchezo wao wa marudiano wa Europa League dhidi ya St Etienne ya Ufaransa, ameulizwa maswali kuhusu hatma ya nahodha wa Man United Wayne Rooney kama ataondoka katika timu hiyo au atabaki.
Jose Mourinho ambaye inaaminika ndio anaweza akafanya Rooney aondoke mwisho wa msimu kama inavyoripotiwa au akabaki, ameshindwa kuweka wazi kama ataondoka staa huyo au atabaki, lakini amekiri kuwa hawezi kumlazimisha mchezaji kuhama.
“Kuhusu kuondoka unaweza kumuuliza mwenyewe kwa sababu hata mimi siwezi kukuhakikishia kama nitakuwa hapa wiki ijayo, sasa nawezaje kukuhakikishia kuwa mchezaji ataendelea kuwepo msimu ujao, kama Rooney ataamua kuondoka sio kwa sababu mimi nataka aondoke”

“Hicho ndio ninachoweza kukuhakikishia sitaweza kulazimisha legend wa Club hii kwenda sehemu nyingine, hivyo unaweza kumuuliza Rooney mwenyewe kama angependa kumaliza soka lake katika timu hii? lakini mimi nina furaha kuwa nae katika timu”

waliotembelea blog