
Ferguson, aliestaafu Umeneja Mwaka 2013 baada ya kuitumikia Man United kwa Miaka 27, ataongoza moja ya Timu katika Mechi hiyo Maalum.
Timu atakayoongoza Sir Alex Ferguson itaitwa Manchester United 2008 XI na itaundwa na Wachezaji waliotwaa Ubingwa wa England na UEFA CHAMPIONS LIGI Mwaka 2008 wakiwa chini yake.
Timu hiyo itacheza na Timu itakayoitwa Michael Carrick All-Star XI ikiongozwa na aliewahi kuwa mmoja wa Mameneja wa Michael Carrick, Harry Redknapp.

Miongoni mwa Majina makubwa ya Wachezaji Soka watakaoshiriki Mechi hiyo maalum ni Edwin van der Sar, Gary Neville, Rio Ferdinand, Paul Scholes na Ryan Giggs wakiichezea Man United na upande wa Michael Carrick All-Star XI watakuwemo Steven Gerrard, Frank Lampard na Michael Owen.

0 maoni:
Post a Comment