Terry, alivishwa Unahodha na kucheza Mechi yake kama Kepteni wa Chelsea Desemba 5, Mwaka 2001 walipofungwa kwao Stamford Bridge Bao 1-0 na Charlton Athletica na Jumamosi, akicheza Mechi yake ya 500 tangu Siku hiyo, aliiongoza Chelsea kuichapa Crystal Palace Bao 2-1 kwenye Mechi ya Ligi Kuu England na kendelea kutamba kileleni.
Mchezaji ambae alikuwa anashikilia Rekodi ya kuwa Nahodha kwa Mechi nyingi hapo Chelsea ni Lejendari Ron 'Chopper' Harris alieiongoza kwa Mechi 324.
Alieleza: “Nakumbuka nilipopata Unahodha, Marcel alikuwa ndie Kepteni na akaitisha Mkutano na Menejimenti na Dennis. Walisema wakati wangu umefika. Nilikuwa bado Kijana lakini walinipa utepe na kuniongoza. Sitasahau hilo. Bila yao nisingeweza kufanya haya!”
RSS Feed
Twitter
10:34 PM
Unknown
0 maoni:
Post a Comment