Hii Leo FIFA imetoa taarifa kwamba Kamati ya Dharura imeamua kuisimamisha Nigeria mara moja baada Mahakama Kuu ya Jos, Plateau State, kusimamisha shughuli za NFF na kumtaka Waziri wa Michezo wa Nigeria kumteua Mtu kuendesha shughuli za NFF.
FIFA imesema maamuzi hayo ni kinyume na Kanuni ya 13, Aya ya 1 na Kanuni ya 17, Aya ya 1 ya Sheria za FIFA ambazo zinataka Vyama vya Wanachama wake kuendeshwa huru na kutoingiliwa na upande mwingine wowote.
Barua ya Valcke iliikumbusha Nigeria wajibu wake wa kuiruhusu NFF kuendesha shughuli zake bila kuingiliwa na Mtu yeyote kwa mujibu wa Kanuni ya 13 ya Sheria za FIFA.
Uamuzi huu wa Leo utaifaya Nigeria isiweze kushiriki Mashindano yeyote ya Kimataifa.
RSS Feed
Twitter
2:57 AM
Unknown
0 maoni:
Post a Comment