Tuesday, August 13, 2013


NIANZE kwa kumshukuru Mungu kwa kuweza kutupa uhai na tumuombe atuzidishie moyo wa upendo ili tuwe na amani katika nchi zote hasa za  Afrika Mashariki.
Hakuna shaka yoyote nikisema kwamba uhai na ustawi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) upo mashakani kutokana na viongozi wa nchi hizo kuonesha kutoshikamana.
Inanikumbusha mwaka 1977, EAC iliposambaratika na kutokana na itikadi za kisiasa licha ya kuasisiwa na Marais, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (Tanzania), Jomo Kenyatta (Kenya) na Dk. Milton Obote (Uganda)  ingawa safari hii suala la itikadi zinazokinzana haliwezi tena kuwa sababu au chanzo cha kuparaganyika kwa jumuiya.
Kwa waliokuwa vijana au watu wazima zama hizo, wanakumbuka jinsi EAC ya wakati ule ilivyovunjika na kuiacha kila nchi kati ya Tanzania, Kenya na Uganda ikichukua mali, madeni ya jumuiya hiyo na kila moja na msimamo wake, ikiendesha pia mambo yake kwa mgawanyo wa mali ambao haukuwa wa haki.
Lakini baadaye marais wa nchi hizo, Benjamin Mkapa (Tanzania), Daniel arap Moi (Kenya) na Yoweri Museveni (Uganda) wakaanzisha juhudi mpya zikawezesha kurejea na kuzaliwa upya kwa EAC  yenye makazi yake Arusha, mahali ambako zimewekezwa fedha lukuki kujenga makao makuu mapya, ingawa kwa sasa jumuiya hiyo inayumba.
EAC ya sasa inayumba licha ya kuongezwa nguvu kwa kuzijumuisha nchi za Rwanda na Burundi kama wanachama wake wapya, jumuiya ina nyufa kubwa ambazo kwa mtazamo wangu zinaashiria kuanguka au kuporomoka siku si nyingi zijazo.
Baadhi ya watu walidhani kwamba EAC yetu ya sasa ingekuwa jumuiya moja kubwa yenye nguvu kibiashara, kisiasa, lakini ndoto hizo zimekwisha na tayari (EAC) imegawanyika katika makundi.
Hakuna shaka kwamba makundi hayo yanatokana na mitazamo ya kimasilahi zaidi ya viongozi wakuu wa nchi tatu,  hasa Rwanda, Kenya na Uganda, kwa kweli yanaiacha EAC ya sasa katika hatari ya kufa kabla ya kutimiza malengo yake.
Ni bahati nzuri kwamba Burundi, nchi ambayo imekuwa katika mizozo mingi ya ndani, vita ya wenyewe kwa wenyewe, haina upande katika mzozo huu wa sasa wa EAC.
Kwa mtazamo wa kawaida mgogoro unaweza kuonekana kuwa ni kati ya Rais Jakaya Kikwete na Rais wa Rwanda, Paul Kagame huku wengine wakiwa ni mashabiki na huenda hata Kenya ya Rais Uhuru Kenyatta na Uganda ya Yoweri Museveni zinaiona Tanzania kama tishio kwa masilahi yao.
 Hakuna shaka kwamba matarajio ya wengi katika jumuiya hiyo ni kuifikiria Tanzania kama eneo la kuingia kiholela, kujichotea mali, ardhi, ajira kama wapendavyo kupitia EAC lakini sasa wanaona kuna ugumu, hivyo kuanzisha chokochoko.
Uganda kwa mfano, ni nchi  ambayo siku zote imekuwa ikifumbia macho magendo ya kahawa, maharage, ndizi kutoka Kagera kupitia njia za panya  mpakani.
Huenda nayo inaona kwamba biashara hii kuwa si endelevu kama ilivyo pengine kwa kufanya biashara au ushirikiano  mzuri zaidi na Kenya kwa njia ya barabara na reli.
Tuliwahi kushuhudia Museveni akimualika Kenyatta na Kagame nchini mwake na Kikwete hawakumualika, tena walisema walikuwa wanazungumzia maendeleo ya Afrika Mashariki!
Hii yote inatokana na Rais Kikwete, katika kikao cha mwaka cha Umoja wa Afrika (AU), kilichofanyika mwanzoni mwa Juni, mwaka huu, mjini Addis Ababa Ethiopia kutoa ushauri kwenye Kamisheni ya Ulinzi na Usalama ya umoja huo, kwamba ili kutafuta suluhisho la kudumu la hali ya kiusalama katika nchi za Maziwa Makuu, upo umuhimu kwa Marais Kagame, Museveni na Joseph Kabila wa DRC kuzungumza na makundi ya waasi wanayopambana nayo katika nchi zao.
Makundi hayo ya waasi ni pamoja na Democratic Forces for the Liberation of Rwanda (FDLR), kundi ambalo Rais Kagame amekuwa akisisitiza linaundwa na Wanyarwanda waliokimbilia DRC mwaka 1994, baada ya kutekeleza mauaji ya kimbari, wanaojulikana kwa jina la Interahamwe. Mengine ni Allied Democratic Force (ADF) kwa upande wa Uganda na M23 kwa Rais Kabila wa DRC.
Ushauri huo haikuwa amri, kinyume chake, Rais Kagame aliukataa kwa kutoa matusi na kejeli kwa mwenzake!
Marais hao hawatakuwa viongozi wa kwanza kupewa ushauri na Rais Kikwete kwani itakumbukwa alikuwa mmoja wa viongozi walioshiriki kumshauri Rais Mwai Kibaki wa Kenya akubali kuzungumza na mpinzani wake, Raila Odinga baada ya Uchaguzi Mkuu wa 2007 uliomalizika kwa vurugu na uvunjifu wa amani na akakubali.
Inawezekana Kagame ana chuki ya muda mrefu dhidi ya Tanzania kwani hakufurahishwa hata kidogo na hatua ya Tanzania kushirikiana na nchi za Afrika Kusini, Malawi na Msumbiji, kupeleka majeshi ya kulinda amani nchini DRC, eneo lenye madini mengi na Rwanda wapo huko kwa kisingizio cha kuwasaka FDLR.
Nimwambie Rais Kagame kwamba hakuwa na sababu ya kumtukana Rais Kikwete kwani angeweza kutofuata ushauri aliopewa na kila kitu kikaishia hapo.




Chuo kilichopo mji wa Nsuka kimeshuhudia tena mauaji ya kikatili ya dereva wa tipa ambae amewapa mimba mjane na mtoto wake. Ripoti inasema dereva huyo amechomwa moto na mtoto wa kiume wa mjane huyo,Sunday Ugwoke.

 Kutokana na habari zilizokusanywa  Sylvester Ezema alikuwa amejishikiza kwenye kampuni ya Ferguso Nig. Limited huko Akpa Edem na alikokuwa anaishi  alikuwa anashea fensi ya kawaida tu na mpenzi wake mjane. Taarifa zinasema kuwa alikuwa pia na mahusiano ya kimapenzi na mtoto wa kike wa mjane huyo ambaye alikuwa hajui mpaka alipofariki siku chache zilizopita ndipo alipokuja kujua.

Sylvester alichomwa moto mpaka akafa na Sunday ambaye alishamwonya aachane na mama yake na aache kufanya nae mapenzi kwenye chumba cha marehemu baba yake,ambacho kimepakana na chumba chake,Onyo ambalo marehemu Sylvester hakulizingatia na kuendelea na tendo hilo baya.
Sylvester aliyapa kisogo maonyo ya Sunday akisema kuwa huyo mjane ni 'family friend' so hakuna atakayewashitukia. Kwa kutofuata maonyo,siku moja Sunday,alijikoki na pilipili ya kusagwa na petrol akamvamia yule 'lover boy'. Sylvester alipotoka tu mlangoni kwake, Sunday alimmwagia pilipili na petrol kisha akamuwasha  moto.
PICHA ya staa wa filamu, Hisani Muya ‘Tino’ na msichana aliyetajwa kwa jina moja la Hellen mkazi wa Arusha imezua utata ikidaiwa kuwa wawili hao huenda wakawa na uhusiano. 
Hisani Muya ‘Tino’ katika pozi tata na msichana aliyetajwa kwa jina moja la Hellen.
Chanzo kilichoipenyeza picha hiyo kimeitonya Stori 3 kuwa, Hellen aishiye jijini Arusha amekuwa akiwatambulisha mashosti zake kuwa wana uhusiano wa karibu sana na staa huyo ndiyo maana amekuwa akihifadhi picha nyingi walizopiga naye kimahaba.
Alipotafutwa Tino kuhusiana na picha hiyo, alidai hakumbuki kama ana mchumba aitwaye Hellen isipokuwa alikiri kupiga picha nyingi za kimalovee na wanawake tofauti.

Wednesday, August 7, 2013


Diamond ni miongoni mwa waliokwama Nairobi, picha alizopost na za mlipuko ziko hapa
2
1
2
Diamond Platnums akiwa ni miongoni wa abiria waliokwama kutokana na uwanja huo kulipuliwa, ameiambia millardayo.com kwamba imebidi abiria wapelekwe hotelini na kuambiwa inawezekana ndege zikaanza kuruka saa moja au saa mbili usiku leo ambapo taarifa walizozisikia ni kwamba ni shambulio la bomu.
Bado tunaendelea kuwa karibu na vyanzo ili kupata info zaidi lakini kwa sasa ni kwamba imetangazwa abiria wako salama ambapo ndege zote zilizokua zinatua Nairobi zimeelekezwa kutua Mombasa.



Reports are coming in through the Kenya Red Cross, the country’s foremost emergency response organization, that a major fire is raging at Jomo Kenyatta International Airport. Courtesy of twitter picture via this tweet: ‘FIRE reported at Jomo Kenyatta International Airport #Nairobi via #iVolunteer @decibyte ^PO’ this is the first available image of the raging inferno, which seems to have fully engulfed one of the main buildings.

Stand by for more reports and updates in due course.

The latest update at 06.17 hrs speaks of the main arrival building, at least the upper floors, being completely engulfed in a major fire and the arrival hall and immigration area has been cleared of passengers while those outside the main arrival hall, beyond customs check points, too has been cleared of people and cars normally waiting there. Parked cars should be removed to make way for fire brigade units coming from the city too.

UPDATE: 0617 hours EAT
The latest update at 0617 hours speaks of the main arrival building, at least the upper floors, being completely engulfed in a major fire and the arrival hall and immigration area has been cleared of passengers while those outside the main arrival call, beyond customs, has also been cleared of people and cars normally waiting there. Parked cars should be removed to make way for fire brigade units coming from the city, too.
UPDATE: 0634 hours EAT
Kenya Airport Authority Statement:

We confirm reports of a fire at JKIA affecting part of the International Arrivals building and Unit 1 departures. The KAA Fire and Rescue Team is on the ground being assisted by G4S and the Nairobi Fire Brigade. Passengers have been evacuated to safety.

This correspondent also urges to refrain from any speculation over the cause of the fire, which will no doubt be fully investigated.
At present there is NO information about any injuries or loss of life.

UPDATE: 0648 hours EAT
Reliable sources from JKIA now speak of a development just taking place at JKIA, that access to the airport has been closed for passengers trying to depart on morning flights, domestic, regional and international, to allow additional firefighting services from the Kenya Army, the National Youth Service, and other government organizations priority access to the arrival/departure buildings as the sheer size of the blaze requires additional resources.

Unit One departures according to some reports is also affected.

Still no reports of injuries or loss of life.

Passengers should be aware that their departure may be delayed considerably until the blaze has been brought under full control and no more danger exists for travelers and staff working at JKIA.

And just in, news that inbound flights may have to be diverted to avoid passengers piling up at JKIA and authorities being unable to process them into the country.


UPDATE: 0725 hours EAT
It has now been confirmed that parked aircraft near the terminal have been towed away to a safe distance and that equipment like high loaders, movable stairs, and vehicles have also been taken away from the apron area just outside Terminal 3, 2, and 1.

Incoming flights are being diverted to Mombasa, Eldoret, Entebbe, Kilimanjaro International, and Dar es Salaam.

Due to the major airline offices located in the affected area, there is no landline communication possible right now, and unless mobile numbers of airline staff at the JKIA station are available, authoritative statements about where respective flights have been diverted to can only be obtained through the airline city offices in due course.

Katibu mkuu wa Baraza la wazee Ibrahim Akilimali (katikati) akiongea na waandishi wa habari le makao makuu ya klabu, kushoto kwake ni mzee Bilal Chakupewa na kulia kwake ni mzee Jabir Katundu
Uongozi wa klabu ya Young Africans umetangaza mkutano mkuu wa dharura wa wanachama wote utakaofanyika tarehe 18.08.2013 katika ukumbi wa PTA sabasaba eneo la mtoni jijini Dar es salaam.
Akiongea na waandishi wa habari leo makao makuu ya klabu hiyo, katibu mkuu wa Yanga Lawrence Mwalusako amesema mwenyekiti wa klabu ameamua kuitisha mkutano mkuu huo wa dharula  kwa ajili ya kupata maoni ya wanachama juu ya mustakabali wa TPL kuingia makubaliano na TV ya Azam kuonyesha michezo ya Ligi Kuu.
Mwalusako amesema kwa mfumo wa klabu ya Yanga, wanachama ndio wana maamuzi ya mwisho juu ya mustakabali wa timu yao kuhusiana na masuala ya klabu yao, hivyo tumeona ni bora kurirudisha suala hili kwa wanachama ili waweze kutoa mchango wao.
Katibu wa baraza la wazee wa klabu ya Yanga mzee Ibrahim Akilimali akiongea kwa niaba ya wazee wa klab hyo, amesema wao wanaungana na kamati ya utendaji  juu ya msimamo wao wa kutotaka Azam Tv kurusha michezo yake yote watakayocheza.
Sisi wazee wa Yanga tunaunagana na mwenyekiti, Kamati Kuu ya Utendaji na viongozi wa matawi kuwa hatupo tayari kuona kampuni ya Azam Media kupitia kupitia kituo chake cha Azam TV inaonyesha mchezo wetu wowote wa Ligi Kuu.
Ifuatayo ni  Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari,
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI.
1. Hivi karibuni tumepata uhakika kuwa Tanzania Premier League (TPL) na Azam Media wanayo nia ya kuingia mkataba wa kuonyesha mechi za Ligi Kuu (Premier League) kwa msimu wa 2013/2014, 2014/2015 na 2015/2016
2. Baada ya Kamati ya Utendaji ya YANGA kufanya uchambuzi wa kina juu ya taarifa ya makubaliano ya kibiashara ya TPL / Azam Media ilihitimisha kuwa mkataba huu hauna maslahi kwa YANGA, na kwa hivyo Kamati ya Utendaji ya YANGA ilifikia uamuzi kuwa mechi za YANGA zisirushwe hewani na Azam Media.
Kwa kuwa wawazi, Kamati ya Utendaji ya YANGA ilitoa taarifa kwa wanachama wa YANGA kupitia vyombo vya habari tarehe 29 Julai, 2013 ambapo iliweka bayana sababu zake na kueleza kuwa YANGA haina tatizo na vilabu vingine vya mpira wa miguu ikiruhusu mechi zao kurushwa na Azam Television ila haifurahii kuwa TPL inalazimisha YANGA kuonyesha mechi zake za Vodacom Premier League katika Azam Television.
3. Sote tumeona baada ya hapo kuwa “nguvu ya ziada” inatumika kupotosha msimamo wa Kamati ya Utendaji ya YANGA na kuidhalilisha Klabu ya YANGA hadharani.
Juu ya hayo na kwa kushangaza sana, baadhi ya vilabu vya mpira wa miguu ambavyo vina sifa kuwa havijawahi kushinda Ligi Kuu, vimeundwa hivi juzi tu, havina uzoefu wowote wa kucheza soka kimataifa n.k. vina kuja kuyapinga Kamati ya Utendaji ya YANGA jinsi ya kuendesha shughuli za klabu ya Yanga, vikiwa vinasahau vilabu vyao wenyewe na badala yake kuiingilia YANGA kwa sababu zinazojionyesha wazi.
Inadhihirika wazi kwamba kuna ushirikiano usio mzuri unaoashiria kula njama kuilazimisha YANGA iruhusu mechi zake zirushwe na Azam Television.
Kwa kuwa YANGA ni Klabu ya Wanachama yenye kupata nguvu kutokana na misingi yake ya kidemokrasia iliyojijengea na uamuzi wake wa mwisho unatokana na Wanachama wake mwenyewe, umeamua kuliweka suala hili zima kwa Wanachama wa Yanga ili waamue ni njia gani ya kufuata kwa maslahi ya Klabu yetu.
Kwa kuzingatia hali hiyo basi, na kulingana na mamlaka niliyonayo kama Mwenyekiti wa YANGA, natangaza mkutano wa dharura wa Wanachama wa YANGA tarehe 18 Agosti, 2013 utakaofanyika uwanja wa Sabasaba kwenye ukumbi wa PTA saa 3.30 asubuhi waje tujadiliane na kuamua suala la Azam Television kurusha mechi za YANGA.


 Ni mwili wa marehemu Tumaini mzibua mitaro ya maji machafu kashai amekutwa kafariki katika mtaro wa kashai maeneo ya kiwanda cha pepsi zamani,chanzo cha kifo chake hakijafahamika
                                              umati wa watu waliokuja kushuhudia tukio la kusikitisha
                                    mwili wa marehemu kabla ya kutolewa kwenye mtaro
                                                  mwili wa marehemu ukitolewa mtaroni
                                                        mwili ukitolewa kwenye maji
                                        mwili ukipakiwa kupelekwa hospital kwa uchunguzi
eneo yalipomkuta mauti marehemu Tumain mzibua mitaro maarufu kashai,PICHA KWA HISANI YA DJ ANAS

waliotembelea blog