Jesus amekuwa Kambini na City kwa Wiki 3 sasa lakini ukiritimba umekwamisha Uhamisho wake kukamilika rasmi na hivyo kusitisha kuichezea rasmi City.
Jesus alianza kukichezea Kikosi cha Kwanza cha Timu ya Taifa ya Brazil Mwezi Septemba Mwaka Jana na kufunga Bao 4 katika Mechi zake 6.
Hivi sasa Man City wapo Nafasi ya 5 kwenye EPL, wakiwa Pointi 10, nyuma ya Vinara Chelsea baada ya kufungwa Mechi 2 kati ya 3 walizocheza mwisho.
JE WAJUA?
-Jesus alijilukana kama Gabriel Fernando alipoanza kuichezea Palmeiras akiwa na Miaka 17.
-Akiwa huko alipewa Jezi Namba 33 [Umri wa Yesu Kristu] na mmoja wa Maafisa Habari wa Klabu hiyo akammwambia atumie Jina la Gabriel Jesus.
-Akiwa na Man City, Jesus pia atavaa Jezi Namba 33 ambayo awali ilivaliwa na Nahodha wa City Vincent Kompany.
0 maoni:
Post a Comment