Wakati huo Liverpool walikuwa tayari washafunga Bao lao pekee na la ushindi kupitia Christian Benteke aliefunga Dakika ya 53.
Klopp aliamini Sakho ameumia vibaya na Lens alipaswa kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu lakini Refa alimpa Kadi ya Njano.
Hapo ndipo Klopp alipoanza kumbatukia Sam Allardyce, maarufu kama Big Sam, na munkari ulipopanda Polisi waliingia kati kumtuliza Klopp.
Hata hivyo, bifu halikuendelea kwani mwishoni Mameneja hao walipeana mikono kama ilivyo desturi Mechi ikimalizika.
Wednesday, December 30, 2015
LA LIGA: ..FC BARCELONA 4 v 0 REAL BETIS
Barcelona, wakicheza kwao Nou Camp, waliitwanga Real Bertis 4-0 na kuongoza La Liga wakiwa na Pointi 38 kwa Mechi 16 wakifuata Atletico wenye Pointi 38 kwa Mechi 17 na Real wakiwa wa 3 na Pointi zao 36 kwa Mechi 17.
Mapema Leo, Real Madrid iliichapa Real Sociedad 3-1 na kutwaa uongozi.
0 maoni:
Post a Comment