Wednesday, January 29, 2014

Justin Bieber mashakani
Mwanamziki mashuhuri wa muziki wa 'pop' kutoka Canada Justin Bieber amefunguliwa mashtaka ya kumpiga dereva wa gari la kifahari la kukodisha mwezi Disemba mwaka uliopita.
Bwana Bieber aliye na umri wa miaka 19 alikaribishwa katika katika kituo cha polisi cha Toronto na kikosi kikubwa cha wapiga picha za televisheni pamoja na unyende wa mashabiki wake chipukizi.
Amefunguliwa mashtaka chini ya juma moja baada ya kukamatwa mjini Florida marekani kwa shutuma za kuendesha gari akiwa mlevi na mashtaka mengine.
Mwanasheria wa Marekani anayemwakilisha mwimbaji huyo amesema mteja wake hana makosa.
Kwa mujibu wa polisi wa Toronto, yapata saa 02:50 saa za Canada tarehe 30 Disemba, gari la kifahari liliwasili kumchukuwa bwana Bieber na wenzake watano katika kilabu moja ya starehe ili kuwarejesha katika chumba chao cha hoteli.
Na wakati walipokuwa njiani, dereva huyo pamoja na mmoja wa abiria wake, aliyetajwa kama bwana Bieber, wanasemekana kuanza kufokeana maneno makali.
Abiria huyo "alimgonga dereva wa limousine hiyo kwenye kisogo mara kadhaa", polisi wamesema.
Dereva huyo anasemekana kusimamisha gari lake na kisha kutoka nje na kuwaita polisi. Mshukiwa 'alichana mbuga' kabla ya polisi kuwasili.
Bwana Bieber alijisalimisha kwa polisi Jumatano. Anatarajiwa kufikishwa kizimbani tarehe kumi mwezi Machi.
Justin Bieber amekuwa na 'vituko' katika siku za hivi karibuni
Howard Weitzman, wakili wa Bwana Bieber mjini California, amesema msanii huyo hana hatia na kwamba anatarajia kesi hiyo itachukuliwa kama kosa dogo tu.
Kuendesha gari akiwa mlevi
Kadhalika siku ya Jumatano, ombi la kutaka bwana Bieber atimuliwe nchini marekani lilipata sahihi laki moja.
Ombi hilo liliwasilishwa kwenye mtandao mmoja wa Ikulu ya White House na raia mmoja wa Marekani.
Rais wa Marekani hana madaraka ya kuamuru mtu kuondolewa kwa lazima nchini Marekani, na haijabainika iwapo Ikulu ya White House itajibu ombi hilo.
Bwana Justin Beiber amejikuta matatani mara kadhaa na maafisa wa polisi katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita.
Mapema asubuhi Alhamisi iliyopita, bwana Bieber alikamatwa kwenye Ufukwe wa Miami baada ya afisa mmoja wa polisi kumfumania akiendesha kwa kasi gari la kukodi aina ya Lamborghini rangi ya njano kwenye barabara ya umma.
Akimshuku kuwa alikuwa mlevi afisa huyo alimtia mbaroni.
Kadhalika alifunguliwa mashtaka ya kupinga kukamatwa na pia kuendesha gari akiwa na leseni iliyopita muda wa matumizi.

Mshambulizi Sergio Aguero wa Man City
Klabu ya Manchester City imechupa hadi kileleni mwa ligi kuu ya soka nchini England baana ya kuonesha soka safi dhidi ya klabu ya Tottenham katika uga wa White Hart Lane.
Kikosi cha kocha Manuel Pellegrini kilihitaji ushindi dhidi ya Spurs ili kuwapiku Arsenal kwenye jedwali la msimamo wa ligi hiyo, na matumaini hayo yalianza kuonekana mapema wakati Aguero alipovuna bao la kwanza, hii ikiwa ni mara ya nane mfululizo akiifungia City katika mechi nane mfululizo.
Yaya Toure aliiweka Man City kifua mbele kwa bao la pili, dakika ya tano kipindi cha pili kupitia mkwaju wa penalti uliozua utata ambapo mlinda ngome wa Spurs Danny Rose alitimuliwa uwanja kwa kulishwa kadi nyekundu japo alionekana kuugusa mpira kwanza kabla ya kuadhibiwa kwa kumchezea rafu Edin Dzeko.
Dzeko aliongeza bao la tatu na ingawa Etienne Capoue alifunga bao la kufuta machozi kwa Spurs, bado kulikuwa na fursa kubwa kwa Man City kuendelea kuinyeshea Spurs mvua ya magoli kupitia mchezaji wa akiba Stevan Jovetic aliyefunga bao lake la kwanza katika ligi kuu tangu uhamisho wake wa pauni £22m kutoka klabu ya Fiorentina ya Italia.
Aguero afunga mabao 50
Baada ya mechi hiyo Sergio Aguero sasa ameandikisha rekodi ya kufunga takriban mabao 50 ya ligi kuu baada ya mechi 81, na kuibuka kuwa mtu wa tano kufunga kiasi hicho cha mabao, baada ya Andy Cole, Alan Shearer, Ruud van Nistelrooy na Fernando Torres.
Kisha City ikaongeza maumivu zaidi kwa Spurs baada ya kile kipigo cha mabao 6-0 mwezi November mwaka uliopita, pale Vincent Kompany alipokamilisha kibarua kwa kufunga bao la tano na la ushindi.
Kwenye matokeo ya mechi nyinginezo Chelsea ilipata pigo kwenye harakati zake za kutafuta uongozi kwenye jedwali baada ya kulazimika kutoka sare ya kutofungana na West Ham katika uwanja wa nyumbani Stamford Bridge.
Kwingineko Aston Villa iliishinda West Brom mabao 4 - 3 nayo Sunderland ikainyuka Stoke 1-0.

Hii ndiyo orodha ya saba bora tarehe 30-01-2014:
1 Man City 53
2 Arsenal 52
3 Chelsea 50
4 Liverpool 46
5 Tottenham 43
6 Everton 42
7 Man Utd 40



Wabunge wa Ukraine
Bunge la Ukraine limeidhinisha sheria inayotoa msamaha kwa waandamanaji waliozuiliwa wakati wa vurugu zilikumba taifa hilo katika siku za hivi karibuni.
Vyama vya upinzani vilisusia kura hiyo kulalamikia kifungu katika mswada wa sheria hiyo ambacho kinasema msamaha utatolewa tu ikiwa waandamanaji watasalimisha majengo ya serikali ambayo wameteka katika siku za hivi karibuni.
Waandamanaji katika baarabara za mji mkuu wa Kiev kadhalika wamekatalia mbali hatua hiyo.
Maandamano hayo yalianza mwezi Novemba mwaka uliopita baada ya rais Viktor Yanukovych kubatili uamuzi wa kusaini mkataba wa kibiashara kati ya Ukraine na umoja wa ulaya.
Kisha baadaye akatia saini mkataba wa mkopo wa takriban dola bilioni 15 na Urusi.
Maandamano bado yanaendelea nchini Ukraine
Hapo jana jumatano, mkuu wa sera za za kigeni katika umoja wa Ulaya Catherini Ashton alisema kuwa amegutushwa na vurugu zilizosababisha maafa katika mji wa mkuu wa Kiev na maneo mengine ya taifa hilo.
" Ni lazima nisema kuwa nimegutushwa sana anasema Bi. Ashton, na ripoti na ripoti ambazo nimepata kuhusu hali ilivyo na bila shaka mojawepo wa maswala muhimu tunayopaswa kushugulikia ni kuzuia vurugu na vitisha. Nina wasiwasi kuhusu watu ambao inaonekana wametoweka. Kuna gumzo kali kwamba ukijadili hili na watu wengi, kuhusu watu kuwa katika hali iliyo sawa na mateka na mengine yanayotokana na vurugu ni sharti yakome. Ni swala lenye umuhmu mkubwa,'' anasema Bi Catherine Ashton
Catherine Ashton - ambaye yuko mjini Kiev kufanya mazungumzo na bwana Yanukovych pamoja na makundi ya upinzani amesema Ukraine inahitaji suluhu ya kisiasa itakayopatikana kwa haraka na kumshirikisha kila mmoja.
Hapo jana jioni mswada huo wa kutoa msamaha ulipitishwa kwa kura 232 dhidi ya 11, huku chama cha Bwana Yanukovych cha Party of the Regions kilicho na idadi kubwa ya wabunge kikiunga mkono.
Lakini wabunge 173 hawakupiga huku wabunge wa upinzani wakipiga mayowe kupinga kura hiyo.

 

Mwenyekiti wa Chama cha Demokreasia na Maendeleo (CHADEMA) na Mbunge wa Kawe, Halima Mdee wakiondoka baada ya kuhutubia mkutano wa Operesheni M4C Pamoja Daima, uliofanyika mjini Ifakara jana.

  Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe akimtambulisha mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya, Afande Sele, wakati wa mkutano wa Operesheni M4C Pamoja Dama, uliofanyika katika Kata ya Tungi mjini Mororgoro jana.

  Afande Sele akiwahutubia wananchi wa Kata ya Tungi mjini Morogoro jana, katika mkutano wa hadhaa wa Operesheni M4C Pamoj Daima, ambao pia ulihutubia na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe.
  wakazi wa mji wa Ifakara, wakitawanyika baada ya mkutano wa Operesheni M4C Pamoja Daima, ambao ulihutubiwa na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe jana.
 Mbunge wa Kawe, Halima Mdee akiwahutubia maelfu ya wakazi wa mji wa Mtibwa,
 Baadhi ya wa mji wa Ifakara wakiwa wamebeba mabango yenye ujumbe mbalimbali, wakati wa mkutano wa Operesheni M4C Pamoja Daima, ambao ulihutubiwa na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe jana.


 Mwenyekiti wa Chama ch Demokrasia na Mendeleo (Chadema), Freeman Mbowe akiwahutubia


 .Maelefu ya wakazi wa mkji wa Ifakara,


 


 

 Kocha wa Manchester City akijionea mwenyewe wenzao bao 5-1 kwao White Hart Lane.

 
 Bao la nne kwa City limefungwa na Stevan Jovetic katika dakika ya 78, Huku Spurs wakicheza pungufu wakiwa 10. Spurs Mchezaji wao alifanya makosa na hatimaye Kompany akawashona bao la tano na kufanya 5-1 dhidi ya wenyeji Spurs.
Yaya Toure na Dzeko wakipongezana baada ya kupata bao.

Yaya Toure akifunga mkwaju wa penati
 
 
 
 

 
 Kocha wa Spurs akitoa maelekezo kwa wachezaji baada ya kuona wanapitiwa kimchezo na kufungwa fungwa katika kipindi cha pili.




Samuel Eto'o akiachia shuti kali

J




Jose Mourinho akipagawa na kulalamikaLosing ground: Chelsea failed to get three points at home, losing ground to Man City in the title raceJoseakicheki mechi


 


waliotembelea blog