Tuesday, November 17, 2015

 Mfalme mzee Yusuphy akiwa anawatumbuiza wapenzi wa bendi ya Jahazi modern taaraba Woinde Shizza,Arusha



Bendi ya muziki wa taarabu ijulikanayo kwa jina la Jahazi  modern taarab inayomilikiwa na  mfalme mzee yusuphy inatarajia kutua rasmi jijini Arusha kwa ajili ya kuitambulisha  album mpya inajulikana kwa jina la Mahaba niuee.



Akizungumza na waandishi wa habari muandaaji wa onyesho hilo ambaye ni mkurugenzi wa phide entertainment, Phidesia Mwakitalima alisema kuwa  bendi hiii ya jahazi inatarajiwa kutua jijini Arusha na kufanya onyesho lao December 11  ambapo litafanyika ndani ya ukumbi wa Triple A com lex uliopo ndani ya jiji hili.



Alisema kuwa mpaka sasa utaratibu wote umekamilika na wanangoja tu siku ya onyesho ambapo alieleza kuwa onyesho hili litakuwa rasmi kwa ajili ya kutambulisha albamu mpya ya jahazi pamoja na kutambulisha nyimbo zilizopo katika alibamu hiyo.



Aidha alitaja baadhi ya nyimbo zilizopo katika albamu hiyo na ambazo zitatambulishwa kwa wapenzi wa jahazi modern taarabu kuwa ni pamoja na nyimbo iliyobeba albamu  Mahaba niueee,alibainisha kuwa pamoja na uzinduzi huu hii pia itakuwa  ni sehemu ya ziara yao kufunga mwaka Tanzania nzima kwa bendi hii ya muziki wa Taarabu.



Phidesia aliwasihi wakazi wa mji wa Arusha pamoja na vitongoji vyake wajitokeze kwa wingi kwani wasanii wote ,waimbaji wote wacheza show wote na wake wote wa mzee yusuphy watakuwepo katika onyesho hilo.



Aliwataja baadhi ya wadhamini wa onyesho hilo kuwa ni pamoja na Geo security, kwa udhamini mkubwa wa Geo Security Arusha kampuni  bora ya ulinzi, security power fance na alarm  ambapo alisema na katika siku hiyo ya onyesho  watakuwepo pia kwa ajili ya usalama wa wapenzi wote   kuhakikisha mnarudi salama majumbani salama .

Monday, November 16, 2015


Mchezaji wa timu ya mpira wa Kikapu ya Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Ephraim Mlawa (kushoto) akichuana na Juvenary Shichose wakati Bonanza la michezo la wanafunzi wa Chuo hicho lililofanyika, mwishoni mwa wiki katika Kituo cha Michezo cha JMK Youth Park na kudhaminiwa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) kwa kutoa vifaa vya michezo kwa timu zilizoshiriki mchezo wa soka. (Picha na Francis Dande)
Timu za mpira wa kikapu kutoka Chuo cha IFM zikichuana katika Bonanza la michezo la wanafunzi wa chuo hicho.
Kikosi cha timu ya Soka ya Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), BBF kikiwa katika picha ya pamoja.



KIKOSI cha timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ inayodhaminiwa na bia ya Kilimanjaro Premium Lager kimewasili salama nchini Algeria leo jioni majira yaa 10 jioni, kabla ya kuanza safari ya kuelekea katika mji wa Bilda.
Msafara wa Taifa Stars unaongozwa na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji, Athumani Kambi, ambapo jumla ya watu 40 wapo katika mji wa Bilda wakiwemo wachezaji 21 wanaojiandaa kwa mchezo wa marudiano.
Mara baada ya kufika katika uwanja wa ndege Algiers, Stars ilipokelewa na watanzania na wanafunzi wanaoshi nchini Algeria, na kuongozana na timu mpaka katika mji wa Bilda ilipofiki timu.
Mchezaji tegemeo, Mrisho Ngassa akiwaongoza wenzake baada ya kuwasili
Stars inatarajiwa kufanya mazoezi kesho saa 1 jioni katika uwanja wa Mustapha Tchaker utakaotumika kwa mchezo wa marudiano siku ya Jumanne.
Katika mchezo wa awali uliochezwa jana jioni jijini Dar es salaam, Tanzania ilitoka sare ya mabao 2 – 2 dhidi ya Algeria, hivyo kuifanya Stars kusaka ushindi katika mchezo wa marudiano ili kuweza kusonga mbele.
Kocha wa Taifa Stars, Charles Mkwasa amesema vjana wake wote wapo katik ahali, hakuna majeruhi na wapo tayari kwa ajili ya kusaka ushindi siku ya Jumanne, na kusema makosa yaliyojitokeza katika mchezo wa jana wanayafanyia kazi yasijitokeze tena katika mchezo unaofuata.
Taifa Stars imefikia katika hoteli ya Ville Des Roses imetumia takriabn muda wa saa 1 kutoka katika uwanja wa Ndege wa Algiers mpaka katika hoteli hiyo iliyopo eneo la Bilda.



Ikiwa timu ya Taifa ya Tanzania ipo Algeria tayari kwa ajili ya mchezo wa marudiano wa kuwania kufuzu kucheza Kombe la Dunia mwaka 2018 Urusi dhidi ya timu ya taifa ya Algeria katika mji wa Blida uwanja wa Mustapha Tchaker Jumanne ya November 17, majirani zao wa Kenya bado wanaripotiwa kukwama uwanja wa ndege kwa muda sasa.
Timu hiyo ya taifa ya Kenya Harambee Stars imeshindwa kusafiri kuelekea Cape Verde na kukwama katika uwanaj wa ndege wa Wilson  baada ya kampuni ya ndege iliyokuwa inatajwa kuingia makubaliano ya kuisafirisha kugoma kuruhusu ndege hiyo iondoke hadi wakamilishiwe malipo yao yote kwani hawana imani na shirikisho la soka la Kenya KFF kama litalipa deni.
harambee-stars-have-been-drawn-to-face-rivals-uganda-in-cecafa-tournament_ss0apl92zbfu1o5xvggnmdzak
Harambee Stars ambao wanapaswa kwenda Cape Verde kucheza mchezo wa marudiano wa kuwania kufuzu fainali za Kombe la Dunia 2018 Urusi dhidi ya Cape Verde baada ya mchezo wa awali uliochezwa Kenya na Harambee Stars kuibuka na ushindi wa goli 1-0, wanakabiliwa na ukata kwa muda sasa hata awali waliripotiwa wachezaji kudai malimbikizo ya posho zao.



Staa wa FC Barcelona na timu ya taifa ya Argentina Lionel Messi November 16 ameingia katika headlines baada ya stori zake za kutaka kujiunga na Arsenal kuandikwa katika headlines za magazeti ya Ulaya, awali Lionel Messi ambaye ameichezea FC Barcelona toka akiwa mdogo aliwahi kukiri kuvutiwa kujiunga na klabu ya Arsenal ya Uingereza.
Messi-490728
Messi ambaye wengi wamewahi kumkejeli na kudhani kuwa hana uwezo wa kutamba nje ya FC Barcelona anatajwa kuwa radhi kujiunga na Arsenal ila sharti lake la mshahara ndio tatizo linalotajwa kuwa huenda hana lengo la kwenda Arsenal, Messi anatajwa kuiomba Arsenal iwe inamlipa mshahara wa pound 600000/= kwa wiki ambazo ni zaidi ya Tsh bilioni 1 za Tanzania mshahara ambao ni mgumu kwa Arsenal kumlipa hususani kwa hulka za kocha wa timu hiyo.
hi-res-2b2f4449796e8b2e48790d5220f12f0d_crop_north
Stori za Lionel Messi kuvutiwa kujiunga na Arsenal aliwahi kukiri kupenda kuichezea klabu hiyo ila November 16 habari zinazotajwa kuwa za kichunguzi kutoka katika gazeti la Star Sport zinasema Messi ameombwa kulipwa mshahara kiasi ambacho ni kigumu kwa Arsenal kukubali au kumudu kulipa, Lionel Messi kwa sasa anatajwa kulipwa mshahara usiofikia pound 300000/= kwa wiki na FC Barcelona na kwa upande wa Arsenal mchezaji anayelipwa mshahara mkubwa ni Mesut Ozil pound 140000/= kwa wiki.
CT4my_cWwAESlOf

Saturday, November 14, 2015



Jina Joseph Kimwaga sio geni katika soka la Tanzania hususani katika vilabu vya Azam FC na Simba, Kimwaga alianza kusikika katika soka akiwa katika klabu ya Azam FC kabla ya dirisha la usajili lililofungwa mwezi August 2015 kuomba kwenda katika klabu ya Simba kwa mkopo wa muda mrefu.
Kimwaga ambaye ana umri wa miaka 19 ni miongoni mwa mastaa chipukizi wa mchezo wa soka wanaofanya vizuri kwa sasa, stori za ushirikina katika soka zipo na zimewahi kumfikia Joseph Kimwaga ila yeye huwa anaamini katika dini yake ya kikristo na kuvaa rozari, licha ya kuwa rozari hukatazwa mchezaji kuvaa wakati wa mechi Kimwaga huwa anaifunga katika bukta yake ili refa asijue kwa imani yake anaamini inamlinda.
IMG_20151113_215912
Staa huyo ambaye amewahi kuingia katika headlines baada ya kufunga goli la ushindi kwa klabu yake ya Azam FC dhidi ya Yanga amepewa rozari hiyo iliyotoka kwa Papa kutoka Italia na padri wake, ndio aliompatia hivyo kwa sababu imebarikiwa na Papa sio rahisi kwa vitu vya imani za giza kumpata Kimwaga.
“Kuna majaribu ambayo yanatokea katika soka kiukweli ila kama una roho fupi unaweza ukaacha lakini ni vitu ambavyo mimi na imani kwa sababu nikikumbuka tu msemo mmoja nilioambiwa na paroko kuwa ukiingia tu katika imani ndio majaribu yatakavyozidi kwa hiyo mimi na imani na ndio maana navaa rozari muda wote” >>> Joseph Kimwaga



Mshindi wa shindano la Trace Music Stars Africa, Mtanzania Nalimi Mayunga anaziandika headlines za leo kwenye kurasa za Bongo Fleva. Baada ya kushinda shindano hilo kubwa la kusaka vipaji, Mayunga aliondoka na mkataba wa kurekodi na Universal Studio wenye thamani ya dola 500,000 ambayo kwa pesa ya sasa inagonga mpaka Tzs bilion 1!
MAYUNGA2
Good news kwako mtu wangu, mtu wetu Mayunga anatarajiwa kuondoka Tz siku ya Jumatatu tarehe 16 November 2015 kwenda Marekani kwa ajili ya mafunzo ya muziki pamoja na kurekodi single yake na Akon ambaye kwenye shindano la Trace Music Stars Africa alikuwa miongoni wa majaji.
MAYUNGA3
Akiongea na CloudsFM radio leo kupitia kipindi cha XXL, Mayunga aligusia pia kuhusu safari yake ya Marekani
>>> “Marekani naenda Jumatatu na ninachoenda kukifanya kule ni kile kinachoongelewa kwenye media, kuwa naenda kwa ajili ya mafunzo, kufanya wimbo, na vilevile kushoot video ya wimbo nitakaoenda kuurekodi… japo kusema kweli sijajua wimbo huo utakuaje kwa sababu mpaka sasa bado sijaupata na wala sijausikia. Dili ni kwamba Akon anakuandikia wimbo mwenyewe, sema sijaupata ili niweze kujipanga, so nahisi kama anataka kunipima aone uwezo wangu…” Mayunga.
MAYUNGA

waliotembelea blog