Mahrez, Mzaliwa wa France mwenye Miaka 25, aliisaidia mno Leicester City kutwaa Ubingwa wa England Mwezi Mei kwa mara ya kwanza katika Historia yao na hilo limempa Tuzo hii maarufu na inayosifika ya BBC, Shirika la Utangazaji la Uingereza.
Mapema Mwaja huu, Mahrez alitunukiwa Tuzo ya PFA ya Mchezaji Bora wa Mwaka kwa England baada ya kuifungia Bao 17 na kutoa Msaada wa Bao 11 kwenye EPL, Ligi Kuu England, na kuwa Mchezaji wa Kwanza kutoka Afrika kuwahi kushinda Tuzo hiyo ya PFA, Professional Footballers Association, ambacho ni Chama cha Kutetea Maslahi ya Wanasoka wa Kulipwa.
Mahrez, ambae alijiunga Leicester Mwaka 2014 akitokea Klabu ya France Le Havre kwa Dau la Pauni 400,000, sasa anaungana na kina Didier Drogba na Staa wa Liberia George Weah ambao waliwahi kushinda Tuzo hii.
0 maoni:
Post a Comment