Thursday, July 17, 2014




Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
Imechapishwa Julai 18, 2014, saa 2:41 asubuhi
WAGONGA nyundo wa Mbeya, Mbeya City fc wapo katika mkakati mzito wa kurejea na nguvu mpya kwenye michuano ya ligi kuu, msimu wa 2014/2015 unaotarajia kuanza kushika kasi septemba 20 mwaka huu.
Klabu hiyo inayonolewa na kocha maarufu nchini na kocha bora wa msimu uliopita, Juma Mwambusi ina nia ya kutwaa ubingwa msimu ujao baada ya kumaliza nafasi ya tatu katika msimu wake wa kwanza.
Ikiwa ni sehemu ya kujiweka sawa, Mbeya City fc itacheza mechi za kirafiki za kimataifa nchini Malawi na Zambia .
Mwenyekiti wa klabu hiyo, Mussa  Mapunda alisema wanatarajia kucheza angalau mechi mbili za kirafiki za kimataifa nchini Zambia kabla ya kwenda Malawi kwa maandalizi zaidi.
“Malengo yetu ni kutwaa ubingwa msimu ujao. Nina uhakika tutaweza kufanikiwa”. Alisema Mapunda.
Mapunda alisema maamuzi ya kuweka kambi nchi jirani  yamechagizwa na kitendo cha shirikisho la soka Tanzania kusogeza ligi mbele mpaka septemba 20 mwaka huu.
Kocha wa Mbeya City fc, Juma Mwambusi (kushoto)
Kwa upande wake, kocha Juma Mwambusi alisema amepanga programu nzuri ya mazoezi kwa vijana wake, na anaamini watafanya kazi nzuri msimu ujao.
Mwambusi alisema kikosi chake hakijabadilika sana kwasababu karibu wachezaji wote wamebaki, achilia mbali wachache walioongezwa akiwemo Them Ferlix `Mnyama` kutoka klabu ya Kagera Sugar.
“Malengo yetu ni kufanya vizuri zaidi ya msimu uliopita. Tunajiandaa vizuri ili kukabiliana na changamoto iliyopo mbele yetu”. Alisema Mwambusi.
Msimu uliopita, Mbeya City ilimaliza katika nafasi ya tatu kwa kujikusanyia pointi 49. Walifungwa michezo mitatu tu.

Walifungwa bao 1-0 na Yanga katika dimba la Taifa, wakafungwa 2-0 na Coastal Union, Mkwakwani Tanga na mechi ya mwisho kufungwa ni dhidi ya mabingwa Azam fc ambapo walilala mabao 2-1 katika uwanja wao wa nyumbani wa kumbukumbu ya sokoine jijini Mbeya.


Announcement: Arsenal made the transfer public on their twitter with a picture of the new signing
Tangazo rasmi: Arsenal walitangaza hadharani usajili huo kupitia mtandao wake wa Twita ambapo waliweka picha na ujumbe.
Imechapishwa Julai 18, 2014, saa 1:45 asubuhi

KLABU ya Arsenal imemsajili beki wa kulia wa Ufaransa Mathieu Debuchy kutokea  klabu ya Newcastle.
Debuchy, mwenye miaka 28, amesajiliwa kwa nia ya kuziba pengo la beki wa kulia, Mfaransa mwenzake, Bacary Sagna aliyetimka Emirates na kujiunga na mabingwa wa ligi kuu, Manchester City majira haya ya kiangazi mwaka huu.
Asernal alitweet picha ya Debuchy ikisindikizwa na ujumbe uliosomeka #Karibu Debuchy.
Pedigree: Debuchy played four of France's five World Cup matches as Les Bleus impressed in Brazil
Jembe jipya: Debuchy aliichezea Ufaransa mechi nne kati ya tano za kombe la dunia nchini Brazil na alionesha kiwango cha juu. 
Welcome: Arsenal's official Instragram posted a picture of the Frenchman's new shirt
Karibu: Pia Arsenal iliposti picha ya jezi ya mfaransa huyo kwenye mtandao wake rasmi wa  Instragram.

Debuchy alijivunia usajili huo na akasisitiza kuwa umuhimu wa ligi ya mabingwa ndio kichocheo cha yeye kujiunga na Asernal.
"Najivunia kujiunga na klabu kubwa kama hii na kuvaa rangi zake, ni moja ya klabu kubwa zaidi duniani," beki huyo wa kulia aliuambia mtandao wa Asernal.com.
"Naangalia mbele nikiwa na Aserne Wenger na kuisaidia timu kuendeleza mafanikio ya msimu uliopita ya kutwaa kombe la FA".
"Kucheza tena ligi ya mabingwa ni fuaraha kubwa kwangu na nitajitahidi kadiri ya uwezo wangu kuisaidia Asernal kushindania kombe"
Replacement: Debuchy arrives at Arsenal to replace Bacary Sagna who he has displaced in the France side
 Debuchy amewasili  Arsenal kurithi mikoba ya Bacary Sagna ambaye hakuonesha kiwango kikubwa katika fainali za kombe la dunia akiwa na Ufaransa.
Striking a pose: Debuchy said he was excited to be playing Champions League football again
Pozi bab kubwa!: Debuchy alisema amefurahi kucheza ligi ya mabingwa tena. 
Looking up: The new signing will be Arsenal's first choice right-back after Sagna joined Manchester City
Ametokelezea: Nyota huyu atakuwa chaguo la kwanza katika nafasi ya beki wa kulia baada ya kuondoka kwa Sagna aliyejiunga na Manchester City
Welcome: Arsene Wenger highlighted Debuchy's top-level experience as a key reason for signing the Frenchman
Karibu: Arsene Wenger aliweka wazi kuwa uzoezi mkubwa wa Debuchy ndio sababu ya msingi ya kumleta kikosini beki huyo Mfaransa


Official: Rio Ferdinand joins QPR on one-year deal
Imechapisha Julai 18, 2014, saa 1:00 asubuhi

NAHODHA wa zamani wa Manchester United na England, Rio Ferdinand amesaini mkataba wa mwaka mmoja katika klabu ya QPR, klabu hiyo mpya iliyopanda daraja imethibitisha.
Mtandao wa Goal.com uliripoti mwezi juni mwaka huu kuwa klabu hiyo iliyopanda ligi kuu ilikuwa na nia ya kumsaini Ferdinand baada ya kumaliza mkataba na klabu yake ya Man United.
Ferdinand alithibitisha kuondoka Old Trafford mwezi mei mwaka huu baada ya kuitumikia timu hiyo kwa miaka 12 ambapo alicheza mechi 454 na alishinda makombe sita ya ligi kuu na ligi ya mabingwa (UEFA) mwaka 2008.
“QPR ni klabu ya kwanza inayocheza ligi  kunisajili mimi. Ni kumbukumbu kubwa kwangu-na kwa familia yangu,” aliuambia mtandao wa klabu hiyo.
“Nilizungumza kwa kirefu na Harry na (mwenyekiti) Mr (Tony) Fernandes. Nadhani wote walionekana kunikubali na wakaona bado kuna kitu naweza kufanya-hiyo ndio ilinifanya niwe na hamu ya kuja hapa na kucheza mpira”.

“Nilikuwa na ofa nyingi duniani kote-baadhi ya sehemu zilikuwa nzuri kuliko hapa. Lakini malengo yangu yalikuwa kucheza ligi kuu ya England na kurudi hapa ambapo ilianzia”.

Harry Redknapp alifanya kazi na Ferdinand wakati beki huyo alikuwa kijana mdogo katika klabu ya West Ham na kocha huyo wa QPR imefurahi kuungana tena na mkongwe huyo.
“Nimefurahi sana,” aliongeza. “Rio ni mchezaji mkubwa na waajabu.
Nimefurahi kwasababu tumeweza kumleta hapa”.
“Nilimsajili Rio akiwa na miaka 14. Muda wote akiwa ndani na nje ya uwanja alipenda kujifunza, ameendelea kufanya hivyo katika maisha yake yote ya mpira”.

“Wakati anacheza Manchester United,  alikuwa ndiye beki bora barani Ulaya, kama sio dunia nzima”.




Viongozi wa klabu ya Azam Fc Mwenye Kiti Saidi Muhamed, Katibu Mkuu Nassoro Idrisa pamoja na Meneje Jemedali Saidi walipo watembelea Majeruhi Joseph Kimwaga pamoja na Frank Domayo Katika Hostel za Azam Complex iliyopo chamazi.
Wachezaji hao kwa hivi sasa wanaendelea vizuri baada ya kupatiwa matibabu Afrika ya kusini.


Staying put: Louis van Gaal says he will find roles for Paul Scholes and Phil Neville
Mtabakia: Louis van Gaal amesema atawatafutia kazi Paul Scholes na Phil Neville.

Imechapishwa Julai 17, 2014, saa 12:36 jioni

LOUIS van Gaal ameahidi kuwajumuisha Paul Scholes na Phil Neville katika benchi la ufundi la Manchester United.
Mholanzi huyo aliyeanza kazi rasmi United wiki hii amesema atawatafutia kazi ya kufanya katika benchi lake.
Ryan Goggs tayari alishateuliwa kuwa msaidizi wa pili wa Van Gaal na Nicky Butt alibaki kuwa kocha wa timu za vijana.
Kocha huyo wa zamani wa Uholanzi amethibitisha kuwa Neville na Scholes ambao kwa pamoja walikuwa wachezaji wa kikosi cha mwaka 1992 kilichoshinda kombe la FA, watapatiwa kibarua cha kufanya.
Alisema: "Nicky Butt tayari anatusaidia. Tutatafuta kazi ya Paul Scholes na Phil Neville. Hicho ndicho tunataka".
"Tunatakiwa kurithi ubora wa watu hawa na tutazungumza na kila mtu binafsi na tusubiri na kuona"
The new team: Van Gaal will be assisted by Ryan Giggs
Timu mpya: Van Gaal atasaidiwa na Ryan Giggs
Getting his points across: Van Gaal speaks to the media for the first time as Manchester United manager
Van Gaal akizungumza na waandishi wa habari kwa mara ya kwanza katika klabu ya  Manchester United.

Neville aliletwa Old Trafford na kocha aliyefukuzwa kazi, David Moyes kama msaidizi wake wa timu ya kwanza na alibakishwa baada ya Giggs kuteuliwa kuiongoza Man United kwa muda katika mechi nne za mwisho za msimu uliopita.
Inafahamika kuwa United walitaka kumbakisha Neville kwa pointi kuwa mchezaji huyo wa kikosi cha 1992 ni muhimu katika klabu hiyo, lakini kutokana na ujio wa Van Gaal majukumu ya kocha huyo yanaweza kupunguzwa zaidi ukilinganisha na msimu uliopita.

article-2696004-1FB0265200000578-757_634x503Bosi mpya: Louis van Gaal alifanya mkutano wake wa kwanza na waandishi wa habari leo tangu ajiunge na Manchester United.
LOUIS van Gaal amesema Manchester United ni klabu kubwa duniani, lakini inatakiwa kujijenga upya baada ya kuvurunda msimu uliopita.
Van Gaal amefanya mkutano wake wa kwanza na waandishi wa habari tangu ajiunge na Man United baada ya kumaliza nafasi ya tatu ya kombe la dunia akiwa na timu ya Taifa ya Uholanzi.
Mholanzi huyo ameisifu klabu ya United kuwa ni kubwa katika ulimwengu wa soka, lakini aliwakumbuksha mashabiki kuwa maboresho ya haraka yanahitajika ili kuepukana na majanga waliyokumbana nayo msimu uliopita.
article-2696004-1FB9622500000578-188_634x356 
Gwiji wa zamani na gwiji ajaye? Louis van Gaal akitambulishwa kwa waandishi wa habari na  Sir Bobby Charlton.
“Msimu uliopita mlikuwa wa saba, kwahiyo ninyi sio klabu kubwa. Mnatakiwa kujithibitsha wenyewe,” alisema.


demba_fadeb.jpg
Usajili mpya na mikataba mipya kwa wachezaji vinara ndio shughuli kuu inayoendelea sasa kabla msimu mpya wa michuano kuanza.
Pamoja na kasheshe zinazomuandama, Suarez sasa yuko Bacelona 100% baada ya kuihama Liverpool, nae Demba Ba tayari amewasili Uturuki anakotarajiwa kukamilisha uhamiaji wake kutoka Chelsea hadi Besiktas kwa gharama ya £8m.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa mika 29 ameyathibitisha hayo katika mtandao wa Twitter akionekana tayari kavalia jesi ya Besi-ktas. "amesema yaliyobaki ni kukamilisha ukaguzi wa kiafya na kuweka saini mkataba.
Demba Ba amewahi kuifungia Chelsea angalau mabao 14.
Hivyo Chelsea wamejibu kwa kumshawishi Filipe Luis aihame Atletico Madrid ingaje Mbrazil huyo yuko katika safu ya ulinzi.
Msimu uliopita Luis alishiriki mechi zaidi ya 40 na kilele ikawa Atletico kushinda la liga kwa mara ya kwanza tangu 1996 na pia wakafikia fainali ya Champions League.(E.L)



Ujerumani imechukua namba moja katika msimamo wa Fifa kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka 24. Mabingwa hao mara nne, wamechukua nafasi iliyokuwa inashikiliwa na Spain. Argentina ni ya pili, na Uhoanzi ni ya tatu. Spain imeporomoka hadi namba nane. Ureno namba 11, Italy 14 na England ni ya 20.
Msimamo ni kama ifuatavyo, pamoja na timu kutoka Afrika Mashariki. Nafasi ilizopanda au kushuka kwenye mabano.

1. Ujerumani (+1)
2. Argentina (+3)
3. Uholanzi (+12)
4. Colombia (+4)
5. Ubelgiji (+6)
6. Uruguay (+1)
7. Brazil (-4)
8. Spain (-7)
9. Uswisi (-3)
10. Ufaransa (+7)


AFRIKA MASHARIKI NA KATI
87. Uganda (-1)
95. Kenya (+13)
96. DRC (-12)
106. Tanzania (+7)
109. Rwanda (+7)
126. Burundi (+2)




Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Lina Kessy ameteuliwa kuwa Ofisa Michezo wa Umoja wa Afrika (AU).

Uteuzi huo umefanywa na Mwenyekiti wa Kamisheni ya AU, Nkozasana Dlamini-Zuma, na Lina atatumikia nafasi hiyo kwa mkataba wa miaka mitatu katika makao makuu ya AU yaliyopo Addis Ababa, Ethiopia.

Lina ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu wa Wanawake Tanzania (TWFA) amewashukuru wote ambao kwa michango yao ya hali na mali imemwezesha kufika hapo.

Ameishukuru TFF kwa kumlea na kumjenga. Shukrani nyingine amezitoa kwa Serikali kupitia Kurugenzi ya Michezo, Baraza la Michezo la Taifa (BMT) na Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC).

TFF inampongeza kwa uteuzi huo, na tunaamini ataipeperusha vyema bendera ya Tanzania ikiwemo kuwa chachu ya maendeleo ya michezo kwa Tanzania na Afrika kwa ujumla.

BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO

SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)


Na Boniface Wambura, Dar es salaam


Timu ya Taifa ya Msumbiji (Mambas) inawasili Dar es Salaam kesho (Julai 18 mwaka huu) kwa ajili ya mechi ya michuano ya Afrika dhidi ya Taifa Stars itakayochezwa Jumapili, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
 Mambas itatua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) saa 7.30 mchana kwa ndege ya LAM ikiwa na msafara wa watu 37 ambapo kati ya hao, 25 ni wachezaji.
 Wachezaji kwenye msafara huo ni Almiro Lobo, Apson Manjate, Bone Mario Uaferro, Dario Ivan Khan, Edson Sitoe, Eduardo Jumisse, Gelicio Aurelio Banze, Helder Pelembe, Josemar Machaisse, Elias Pelembe, Isac Carvalho na Jeffrey Constatino.
 Wengine ni Manuel Fernandes, Manuel Uetimane, Mario Sinamunda, Momed Hagi, Reginaldo Fait, Reinoldo Mandava, Ricardo Campos, Saddan Guambe, Simao Mate Junior, Soares Victor Soares, Stelio Ernesto, Vando Justino na Zainadine Junior.
 Timu hiyo itafikia kwenye hoteli ya Accomondia, na itaondoka Jumapili mara baada ya kumalizika kwa mechi hiyo itakayochezeshwa na mwamuzi Mahmoud Ashour.


Na Boniface Wambura, Dar es salaam

Imechapishwa Julai 17, 2014, saa 8:43 mchana

Kocha Mkuu wa Serengeti Boys, Hababuu Ali Omari amesema morali ya wachezaji wake ipo juu kwa ajili ya mechi dhidi ya Afrika Kusini (Amajimbos) itakayochezwa kesho (Julai 18 mwaka huu). 
Mechi hiyo ya kwanza ya raundi ya pili ya michuano ya Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 itafanyika kwenye Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi jijini Dar es Salaam kuanzia saa 10 jioni. 
Akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari kwenye ofisi za TFF jijini Dar es Salaam leo, Kocha Hababuu amesema nia ya kikosi chake ni kuhakikisha wanafika kwenye fainali za Afrika zitakazofanyika mwakani nchini Niger. 
“Tunaiheshimu Afrika Kusini, lakini hatuiogopi. Morali ya wachezaji ipo juu na wanajiamini. Kimsingi wanajua kuwa hii ndiyo njia ya wao kutokea kwenye mpira wa miguu, kwa hiyo lengo ni kushinda,” amesema Kocha Hababuu. 
Naye Kocha wa Afrika Kusini, Molefi Ntseki amesema anaziheshimu timu za Tanzania, na changamoto aliyonayo ni kuhakikisha kuwa anashinda mechi hiyo kwani mara ya mwisho kwa timu yake kushiriki fainali za Afrika ilikuwa miaka sita iliyopita.


Kiingilio katika mechi hiyo ni sh. 2,000 na tiketi zitapatikana uwanjani kwenye magari maalumu.


Mwinyi Kazimoto Mwitula (kulia) akifanya vitu vyake kwenye moja ya mechi za Taifa Stars siku za nyuma

Na Boniface Wambura, Dar es salaam

Imechapishwa Julai 17, 2014, saa 8:27 mchana

Kikosi cha Taifa Stars kimerejea jijini Dar es Salaam leo kutoka Mbeya ambapo Jumapili (Julai 20 mwaka huu) kitapambana na Msumbiji (Mambas) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Benchi la Ufundi la Taifa Stars pamoja na wachezaji kesho (Julai 19 mwaka huu) saa 5 asubuhi watakuwa na mkutano na waandishi wa habari kwenye hoteli ya Protea Courtyard iliyopo Upanga Seaview jijini Dar es Salaam.


Imechapishwa Julai 17, 2014, saa 8:23 mchana

Timu ya Azam Fc leo imepata ushindi wa magoli mawili kwa moja Dhidi ya Jkt Ruvu katika mchezo wa kirafiki uliochezwa kwenye Uwanja wa chamazi Complex uliopo chamazi.
Azam ndio walioanza kufunga magoli hayo kupitia kwa Kavumbagu na Kipre Tchetche kipindi cha kwanza wakati bao la JKT ruvu likifungwa na Ally Bilali.
Katika Mchezo huo Kocha wa Azam Fc Joseph Omog aliwatumia wachezaji wa timu ya Vijana ya Azam kuangalia viwango vyao.
Kocha Omog bado amesema anahitaji mechi za kirafiki zaidi ili kukitengeneza kikosi chake huku akiwasubili wachezaji waliopo kwenye majukumu ya timu ya tafa.
Wachezaji wa Azam Fc waliopo kwenye Timu ya Taifa ni Tisa ambao ni Aishi Manula, Agrey Moris, Shomari Kapombe, Saidi Morad, Erasto Nyoni, Himid Mao, Mcha Hamis, Kelvin Friday pamoja na John Bocco


 Meneja wa Kilimanjaro Premium Lager, George Kavishe akimkabidhi vifaa Makamu wa Rais wa Simba SC, Geoffrey Nyange. (Picha: Executive Solutions).
 Meneja wa Kilimanjaro Premium Lager, George Kavishe akimkabidhi vifaa Mkurugenzi wa Masoko wa Yanga, George Simba. Anayeshuhudia ni Hafidh Saleh, Meneja wa Yanga. (Picha: Executive Solutions). 
Meneja wa Kilimanjaro Premium Lager, George Kavishe akiwakabidhi vifaa Makamu wa Rais wa Simba SC, Geoffrey Nyange pamoja na Mkurugenzi wa Masoko wa Yanga George Simba (Picha: Executive Solutions).
  Ikiwa ni sehemu ya udhamini wake, bia ya Kilimanjaro Premium Lager imekabidhi vifaa vya michezo kwa klabu maarufu za Simba SC na Young Africans SC kwa ajili ya msimu wa 2014/15 wa Ligi Kuu inayotarajiwa kuanza mwezi ujao. Meneja wa bia ya Kilimanjaro Premium Lager, George Kavishe alisema “Tunawapatia vifaa mapema kabla ya ligi kuanza ili wapate muda wa kutosha kujiandaa kwa ajili ya msimu wa 2014/15 ambayo bila shaka itakuwa na changamoto kubwa kwa timu hizi mbili na pia tunaamini kuwa siri ya mafanikio katika michezo ni maandalizi mazuri. Ni matumaini yetu kuwa wachezaji wapya waliosajiliwa Simba na Yanga wataiwakilisha Kili vizuri na kufurahia kuzichezea klabu hizi kongwe.” Kavishe aliongeza kuwa Vifaa ambavyo leo tunatoa ni pamoja na mipira, viatu, soksi, shin guards, nguo za mazoezi, nguo za kawaida, gloves na vitu vingine vingi ambavyo vitawezesha timu hizi za Simba na Yanga kucheza wakifurahia kuvaa vifaa vyenye ubora wa hali ya juu. Kilimanjaro Premium Lager kama mdhamini mkuu wa Simba na Yanga, na kinywaji kinachoongoza katika udhamini wa soka hapa nchini tunadhani kwamba uhusiano wetu na klabu hizi ni kiungo muhimu sana katika kuendeleza mpira wa miguu hapa Tanzania. Tutaendelea kutimiza wajibu wetu kwa klabu hizi na kama ilvyo kawaida yetu, tutahakikisha tunalifikisha soka la Tanzania kwenye kilele cha mafanikio. Kavishe alisema kuwa udhamini wa Kilimanjaro Premium Lager kwa Simba na Yanga umelenga kukuza soka la Tanzania, kuleta msisimko, na kuvutia mashabiki wengi wa mpira wakati na vilevile kuwaweka wachezaji wa Tanzania katika nafasi nzuri ya kimataifa. Tunawashukuru viongozi wa Simba na Yanga, mashabiki wote, vyombo vya habari na wadau wote wa mpira kwa ushirikiano mzuri tunaoendelea kupata kwenye udhamini wetu na hiyo ndio siri ya mafanikio ya uhusiano wetu na klabu hizi mbili maarufu. “Tunawaomba mashabiki wa Simba na Yanga waendelee kuiunga mkono bia yao ya Kilimanjaro Premium Lager kwani tunafanya kila jitihada kuwapa burudani na kufikisha soka la Tanzania kwenye kilele cha mafanikio.”


Go west: Rio Ferdinand is set to join QPR after leaving Manchester United
Anaenda Magharibi: Rio Ferdinand anatarajia kujiunga na QPR baada ya kuondoka Manchester United.

Imechapishwa Julai 17, 2014, saa 6:46 mchana

BEKI mkongwe, Rio Ferdinand hatarithi mikoba ya unahodha wa Clint Hill katika klabu ya QPR mara atakapokamilisha uhamisho wake.
Ferdinand anamalizia taratibu za kujiunga na klabu hiyo ya Magharibi mwa London na anatarajiwa kusaini mkata muda wowote kutoka sasa.
Nahodha huyo wa zamani wa Manchester United na timu ya Taifa ya England yupo katika hatua ya mwisho ya makubaliano ya mkataba mwa mwaka mmoja na QPR baada ya kuondoka Old Trafford mwishoni mwa msimu uliopita.
New chapter: Ferdinand is set to join QPR
Ukurasa mpya: Ferdinand anataka kujiuna na QPR

Uhamisho huo utamkutanisha na kocha Harry Redknapp, ambaye alimsajili kwa mara ya kwanza akiwa mdogo katika klabu ya West Ham miaka 21 iliyopita.
 Redknapp alisema:"Ni dili kubwa. Rio atakuwa mchezaji mkubwa kwetu kutokana na maarifa na uzoefu wake katika  mchezo wa soka".
Licha ya uzoefu wake uwanjani, Redknapp hatampa unahodha klabuni hapo.


 MARIO Gotze, maisha yanamwendea safi kabisa.
Akitokea kushinda  kombe la dunia na nchi yake ya Ujerumani baada ya kufunga bao la dakika za nyongeza, mshambuliaji huyo wa Bayern Munich ameanza likizo akiwa na demu wake kipenzi,  Ann-Kathrin Brommel maeneo ya Ibiza.
Wawili hao wamepigwa picha wakifurahia maisha kwenye jua tamu  juu ya boti.
Angalau nyota huyo mwenye miaka 22 anastahili kufanya hivyo baada ya kutoa mchango wake wa kuwafanya Ujerumani wawe mabingwa wa dunia nchini Brazil.
Winning: Germany World Cup winner Mario Gotze and his model girlfriend Ann-Kathrin Brommel relax
Mshindi: Nyota aliyewapa Ujerumani kombe la dunia,Mario Gotze akila bata na mpenzi wake, mwanamitindo, Ann-Kathrin Brommel.
Relaxing: Gotze and his model girlfriend Brommel chill on their boat in the sunshine
Bata batani!: Gotze na demu wake Brommel wakiwa wametulia juani juu ya boti yao
Time to relax: Brommel joins her boyfriend as Gotze sunbathes on the boat in Ibiza
Muda wa kupunga upepo: Brommel akiwa na basha wake maeneo ya Ibiza
Peckish? Gotze and Brommel share some grapes on board the boat as they relax after a hectic summer
Chukua bebii? Gotze na Brommel wakifurahi pamoja.
Lavish: The pair were taking a break after all the excitement of winning the World Cup
Nifunike `hanii`: wawili hao wakila bata baada ya kushinda kombe la dunia majira haya ya kiangazi nchini Brazil
Proud: Brommel was on holiday with Gotze after the Germany midfielder won the 2014 World Cup
Anajivunia kidume: Brommel yupo likizo na Gotze baada ya kiungo huyo wa Ujerumani kushinda kombe la dunia.
That's how to celebrate: Brommel was seen on the pitch in Brazil after Germany won the World Cup
Brommel alionekana uwanjani nchini Brazil baada ya Ujerumani kutwaa `ndoo` ya dunia
Well earned: Gotze was relaxing in Ibiza, Spain, after scoring the decisive goal in the World Cup final
 Gotze akipumzika maeneo ya  Ibiza, Hispania, baada ya kufunga bao zuri lililowapa ubingwa Ujerumani
Spotted: Gotze was taking time off before returning to Bayern Munich after winning the World Cup
Gotze akiwa mapumzikoni kabla ya kurudi kuungana na Bayern Munich
Celebrations: Match winner Gotze said the German players would enjoy a great party after the World Cup
Shangwe: Mshindi wa mechi,  Gotze alisema wachezaji wa Ujerumani wanatakiwa kufurahia pati `bab kubwa` baada ya kushinda kombe la dunia. 
Victory: The forward scored the only goal after the 1-0 extra-time win against Argentina
Champions: Gotze and Andre Schurrle celebrate Germany's World Cup win on their return to Berlin
Mabingwa: Gotze na Andre Schurrle wakishangilia ubingwa wa Ujerumani mjini Berlin

waliotembelea blog