Monday, August 18, 2014


http://www.foxsportsasia.com/servlet/file/Football%20News-%20Real%20Madrid%20Luis%20Figo.jpg?ITEM_ENT_ID=810803&COLLSPEC_ENT_ID=10&ITEM_VERSION=1
Na Abdallah H.I Sulayman 'Msuni'

Wachezaji waliowahi kutamba na mabingwa wa ulaya Real Madrid wanatarajiwa kuanza kuwasili nchini wakati wowte katika juma hili kwa ajili ya ziara nchini ikiwemo kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya mastaa wa Tanzania waliomaliza soka lao (Walio staafu).

Hivi sasa katika kila kona ya nchini ziara hii ya nyota hao ambao wanakubalika vilabu mbalimbali ulaya na duniani kwa jumla imekuwa gumzo na mashabiki wa soka nchini wanangoja kwa hamu agosti 23 ifike wakawashuhudie katika uwanja wa taifa.

Kwa muda mrefu toka ziara ya magwiji hao wa soka ianzwe kuzungumza, nimekuwa nikijiuliza ni ipi faida tutakayo ipata sisi wapenda soka la bongo kwa ujio huo wa magwiji wa soka nchini.

Kwa muda mrefu tumekuwa tunalia na kulalama juu ya matokeo mabovu ya timu yetu ya taifa na mara nyingi tulikuwa tunakimbilia kutoa sababu ya kukosa wachezaji wanao cheza ligi ya ushindani katika timu yetu ya taifa kama nchini nyingine za bara letu la Afrika.

Ni dhahiri kuwa ni vigumu kumvuta wakala ama mwakilishi wa kilabu toka kwenye ligi yenye ushindani kuja nchini kuangalia vijana wetu, na hata katika michuano ambayo vilabu na mawakala wanayotolea macho, timu zetu zimekuwa ndoto kupata nafasi ya kushiriki.

Je wenye dhamana na soka letu wanaitumiaje ziara hii, kwa faida ya soka letu, ama ni yale yale ya kuja kusimulia wajukuu kuwa nimesmshuhudia mchezaji bora wa dunia akicheza katika uwanja wetu wa Taifa.

Nikosa kubwa kama magwiji hao wa soka duniani kumaliza ziara yao nchini bila ya kushuhudi mechi walau moja ya vijana wakitanzania chini ya miaka 15 au 17.

Ni imani yangu kwa vipaji tuliovyo jaaliwa watanzania katika wachezaji wa 25 watakao cheza katika mechi hiyo, magwiji hao wasoka hawato kosa wachezaji walau watano wa kwenda kuwazungumzia huko mbeleni na walau siku moja tunaweza kushuhudia mawakala wakipiga hodi, Tanzania kuja kuangalia vipaji ambavyo walivyo visikia toka kwa magwiji hao.

Tanzania tumekosa wabalozi kwenye soka huko kwenye ligi za ushindani ambao, kwa uwezo wao uwanjani wanaweza kuwavutia mawakala kuja kuangalia madini yaliyopo Tanzania.

Tutakuwa kwenye hasara kama ujio wa Magwiji hao, utakuwa ni wakuja na kuondoka bila kuacha athari katika soka letu.

Kama bado hakuna mchezo wowote ulioandaliwa ni wakati wa ratibu wa ziara, TFF, vilabu na akademik kutumia fursa hii ya kuwanadi vijana wetu kwa magwiji hao wa dunia.


LOUIS VAN GAAL ameambiwa ni lazima aende Sokoni kusaka Wachezaji Wanne wazuri kabla Dirisha la Uhamisho halijafungwa hapo Septemba Mosi.
Huo ndio msimamo wa Kocha wa zamani wa Manchester United chini ya Sir Alex Ferguson, Mholanzi Rene Meulensteen, ambae ametoboa Kikosi cha sasa si imara katika mbio za Ubingwa.
Jumamosi Uwanjani Old Trafford kwenye Mechi ya kwanza kabisa ya Msimu mpya wa Ligi Kuu England, Man United ilichapwa Bao 2-1 na Swansea City, Gemu ambayo pia ilikuwa ya kwanza kabisa ya Ligi kwa Meneja mpya Van Gaal.

Akihojiwa na Wanahabari kwenye Kipindi Maalum cha TV, Meulensteen alisema Timu hiyo inahitajika kujengwa upya.
Ameonya: “Hamna njia fupi. Bado wana Wiki mbili na lazima waende Sokoni kununua Wachezaji kwenye Kipindi hiki na kijacho cha Uhamisho cha Januari!”

Kocha huyo mahiri ambae mafanikio makubwa ya Man United yanasemwa ni mchango wake mkubwa ameongeza: “Tunahitaji kuimarisha Difensi, lazima tuongeza nguvu Kiungo na hayo ndio maeneo makubwa yanayotakiwa kutazamwa kwanza na haraka. Kwa maoni yangu, wanahitajika Wachezaji Wanne wa kiwango cha juu!”Kuhusu Van Gaal kutumia Mfumo mpya wa 3-5-2, Meulensteen ameeleza: “3-5-2 inaweza kufanya kazi. Mfumo wowote unawezekana ukiwa na Wachezaji sahihi na Wachezaji wakauelewa Mfumo huo. Ni mtirirko wa muda mrefu na walianza vizuri kwenye Mechi za kujipima kabla Msimu kuanza. Itachukua muda hadi wafikie kile kiwango cha ile Man United inayotawala, inayocheza


Mechi ya kugombea Gamper Trophy dhidi ya Club Leon ya Mexico, Barcelona wameichakaza timu hiyo bila huruma ambapo Magoli ya Barva yamefungwa na Lionel Messi bao la mapema dakika ya 3  aliyefuata kufunga ni kijana matata Neymar aliyetokea kwenye kujiuguza majeraha yake dakika ya 12 na dakika ya 44 akifunga bao mbili.
Bao la tatu lilifungwa kipindi cha pili dakika 55 na Munir El Haddadi  na akiongeza tena bao lake la pili katika dakika ya 78.
Dakika ya 86 aliyemalizia bao ni Sandro Ramírez hivyo Mtanange kumalizika kwa bao 6-0 Club Leon wakimaliza mchezo huo bila hata bao la kufutia machozi!!!

Suarez ametambulishwa leo mbele ya mashabiki wa Barca ambapo pia wamecheza mechi ya kirafiki na kushinda bao 6-0

Suarez akisalinia Mashabiki wa Barca leo walipokuwa wakijiandaa kucheza na timu ya Mexico Club  Leon

Mambo safi!!! Luis Suarez ametambulishwa Rasmi leo jumatatu mbele ya Mashabiki wa Barcelona

Suarez (wa tatu kulia) wakiwa mbele ya Mashabiki wao leo

Suarez akiwapungia mkono Mashabiki
Majembe mapya!!! Thomas Vermaelen na Suarez katikati wakipata picha mbele ya Mashabiki wao leo huko Nou Camp.


Diego Costa akishangilia bao lake...Andre Schürrle akipongezana na Diego Costa baada ya kufunga bao. Chelsea waliongoza kipindi hicho cha kwanza kwa kuwabamiza Wenyeji Burnley bao 3-1. Kipindi cha pili hakuna aliyeliona lango la Mwenzake licha ya timu zote mbili kushambuliana kwa zamu!Kipindi cha kwanza Dakika 14 Burnley walitangulia kufunga bao kupitia kwa Scott Arfield baada ya kutuliza vyema pasi ya Matthew Taylor ndani ya box na dakika 16 Chelsea wakasawazisha kupitia kwa Diego Costa...
Dakika ya 21 Chelsea waliongeza bao la pili kupitia kwa Andre Schürrle akilishwa mpira na Cesc Fàbregas. Bao la tatu lilifungwa na Branislav Ivanovic katika dakika ya 34 akipewa pasi tena na Cesc Fàbregas na kufanya 3-1 dhidi ya Wenyeji Burnley. VIKOSI: 
Burnley: Heaton, Trippier, Duff, Shackell, Mee, Taylor, Marney, Jones, Arfield, Ings, Jutkiewicz.
Subs: Wallace, Kightly, Sordell, Gilks, Long, Barnes, Dummigan.
Chelsea: Courtois, Ivanovic, Cahill, Terry, Azpilicueta, Fabregas, Matic, Schurrle, Oscar, Hazard, Costa.
Subs: Cech, Luis, Zouma, Torres, Drogba, Mikel, Willian.
Referee: Michael Oliver (Northumberland)
Mourinho akiteta jambo leo muda mfupi kabla ya MtanangeMourinho na Viongozi wenzake wakijiuliza jambo


Klabu ya Arsenal itajielekeza nchini Uturuki jumanne wiki hii kuchuana na klabu ya Besiktas katika michuano ya ligi ya mabingwa. Besiktas haijawahi kucheza na Arsenal barani Ulaya.
Mechi zingine zitakazochezwa jumanne wiki hii katika mzunguko wa kwanza ni pamoja na FC Copenhague kumenyana na Bayer Leverkusen, huku Naples ikiwa na kazi kubwa dhidi ya Athletic Bilbao.
Mwaka jana Arsenal iliishinda Fenerbahçe kwa mabao (3-0) na (2-0) katika mchuano wa marudio. Arsenal imekua ikishinda katika viwanja vya Uturuki. Klabu hiyo haijafungwa katika michuano 7 iliyocheza nchini Uturuki, huku ikifungwa mabao mawili dhidi ya mabao 12 iliyofunga timu za taifa hilo.

Arsenal ikichezea nyumbani ilishindwa kufanya vizuri juzi Jumamosi dhidi ya Crystal Palace na kulazimika kwenda sare ya kufungana bao moja kwa moja, baada ya kufunga bao la kusawazisha katika dakika ya 90 ya mchezo.

Wenger huenda akafanya mabadiliko katika klabu yake baada ya kumkosa kwa muda mrefu Walcott. Monreal huenda akacheza upande wa kushoto wa ulinzi. Naye Giroud huenda akawekwa mbele kwenye nafasi ya Sanogo.

Mechi hizo za mzunguko wa kwanza zitachezwa jumanne na jumatano wiki hii. Mechi za marudio zimepangwa kuchezwa jumanne na jumatano wiki kesho.


Manchester United wanajiandaa kuwekeza kitita cha kutosha ili kuinasa saini ya Angel Di Maria kutoka Real Madrid. 
MASHETANI wekundu, Manchester United wanajiandaa kumwaga paundi milioni 100 kumshawishi Angel di Maria kutua Old Trafford wakati huu klabu inahitaji kujiboresha ili kushindania ubingwa wa ligi kuu England.
Kocha mkuu wa United, Louis Van Gaal anahitaji kusajili wachezaji wa kiwango cha dunia kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili barani ulaya na tayari ameshaonja machungu ya kufungwa ambapo alilala mabao 2-1 dhidi ya Swansea jumamosi iliyopita uwanjani Old Trafford.
Mkurugenzi mkuu wa United, Ed Woodward amemuunga mkono Van Gaal na yupo tayari kufanya lolote lile ili mradi Di Maria atue Man United.
Inafahamika kuwa United imemuambia Muargentina huyo kwamba kwa kiwango chake cha sasa itamlipa mshahara wa paundi laki mbili kwa wiki.
Kwa mkataba wa miaka mitano anaotarajiwa kupewa, United itawezekeza paundi milioni 100 ikijumuisha mshahara wake na ada ya uhamisho.



Baadhi ya wana Bongo dansi wakiwa katika picha ya pamoja na bendi ya vijana Jazz wakati wa kusherehekea mwaka mmoja wa kundi hilo tangu lianzishwe kwenye mtandao wa kijamii wa fecebook ambapo kundi hilo mpaka sasa lina wanachama 3,086 mashabiki wa bendi mbalimbali za mziki ya dansi nchini. picha na www.burudan.blogspot.com

Baadhi ya wanachama maarufu wa Bongo dansi kushoto ni Abdulfareed Hussein , Senetor Mwinyi na William Kaijage walipokutana katika sherehe za mwaka wa kundi hilo zilizofanyika vijana kinondoni Dar es salaam. picha na www.burudan.blogspot.com

wafulumusha magitaa wa bendi ya Vijana Jazz wakiwajibika wakati wa sherehe za kutimiza mwaka mmoja kwa kundi la Bongo Dansi ambao ni mashabiki wa mziki wa dansi nchini wanaokutanishwa katika mtandao wa kijamii wa fecebook kushoto ni Shomari Ally na Said Kizunga picha na www.burudan.blogspot.com

Wasanii wa bendi ya Vijana Jazz wakiserebuka

Mpiga tumba wa bendi ya vijana jazz Ally Rajabu kushoto na Mpiga drams wa bendi hiyo Samata Hassani wakiwajibika wakati wa onesho lao

Waimbaji wa bendi wa Vijana Jazz kutoka kushoto ni Saburi Athumani,Julius Mwesiwa,Abdallah Mgonahanzeru na Husein Boom wakitoa burudani


Waimbaji wa bendi ya vijana Jazz wakitoa burudani kwa kundi la Bongo Dansi kutoka kushoto ni Julius Mwesiwa na Komweta Maneti picha na www.burudan.blogspot.com

Baadhi ya wana Bongo Dansi wakiwa katika meza wakiendelea kupata burudani za vijana jazz

Mwimbaji wa bendi ya Vijana Jazz Komweta Maneti kushoto akiserebuka na wana bongo Dansi wakati wa onesho lao

















waliotembelea blog