Monday, September 1, 2014


FalcaoManchester United imekubaliana na AS Monaco ya France kumsaini Straika wa Colombia Radamel Falcao kwa Mkopo na wakati huo huo Straika wao Javier Hernandez anahamia Real Madrid ya Spain pia wa Mkopo.
Falcao anatarajiwa kuwasili Jijini Manchester kupimwa afya yake na tayari Chicharito nae yuko huko Madrid kupimwa afya.
Falcao alijiunga na AS Monaco Mei 2013 kwa Dau la Pauni Milioni 50 kutoka Atletico Madrid na kufunga Bao 11 katika Mechi alizoichezea.

Msimu huu Falcao amefunga Bao 2 katika Mechi 3.
Dili ya Falcao kwenda Man United pia ina makubaliano kuwa wanaweza kumnunua moja kwa moja kwa Dau la Pauni Milioni 43.5.

Mwezi Januari Falcao aliumia vibaya Goti lake na kumfanya alikose Kombe la Dunia.
Meneja wa Manchester United Louis Van Gaal tayari ameshawasaini Luke Shaw, Marcos Rojo, Ander Herrera na Angel Di Maria huku Mchezaji wa Netherlands Daley Blind akiwa njiani kujiunga.

Javier Hernandez ni dole tuu!! Baada ya kutua Real! mambo super!

Hernandez anaenda Real kuongeza ujuzi akitokea  Manchester United kwa mkopo!

Hernandez alikuwa akisugua benchi pale United na sasa ameenda Real kuona kama namba ya kudumu atapata ya kikosi cha kwanza.

Hernandez alipofika Real na tayari kwa kutambulishwa Klabuni hapo jana jumatatu

Hernandez kuonesha kiwango chake hapo  Real Madrid

Hernandez akitabulishwa na atavaa jezi no. 14

Hernandez  akitabasamu mbele ya makombe  Bernabeu

Chicharito'akiwa na  Perez  Bernabeu

Hernandez tayari kwa kuichezea  Real Madrid baada ya vipimo kwenda safi jana jumatatu!

Akiwamwagia wino mashabiki!

Safi! Chicharito amefurahia kutua Real

Javier Hernandez alipokuwa na Daktari



Gari ya Polisi iliyoibuka kumuokoa Diamond kufuatia sakata la mashabiki wake kupandwa na jazba
Sehemu ya ukumbi ulioharibiwa vibaya na washabiki mjini stuttgart,ujerumani
Stuttgart,Ujerumani,
Usiku wa Jumamosi ya Tarehe 30.Augost 2014, majira ya saa 10 alfajiri
Mwanamuziki nyota wa Bongo Flaver Nasib Abdul aka Diamond Platnumz alijikuta katika hali ya hatari hadi kuokolewa na Polisi mjini Stuttgart,ujerumani,baada ya washabiki waliokuwa na hasira kuchoka kusubiri show,washabiki hao waliokuwa wamelipa ticket euro 25 kwa kiingilio waliahidiwa kuwa show ingeanza saa 4.00 usiku,lakini walijikuta wakisubiri hadi majira ya saa10 usiku au alfajiri ndipo mwanamuziki Diamond alipoletwa jukwaani na promota wake raia wa Nigeria anajiita kama Britts Event.
Hapo ndipo washabiki walipoona kuwa hawakutendewa haki walianza kurusha chupa na kutaka kumvamia mwanamuziki Diamond na promota wake,Kilichowakera zaidi washabiki ni pamoja na vyombo vibovu vilivyofungwa katika ukumbi huo kitu ambacho kiliwafanya washabiki kuvunja hadi vyombo vya muziki ma-Djs walishambuliwa na wapo Hosptalini kwa sasa.

Mmoja wa Djs hao alipoteza Lap top yake ,mwanadada DJ Flor alipatwa shock mshtuko wa moyo na kukimbizwa hosptali, washabiki hao walimpa kipigo DJ Drazee naye yupo hoi hospatal.
Polisi nchini ujerumani wanamesema tukio hili la aibu halijawahi kutokea,kuwa msanii kuchelewa kufika jukwaani kwa ujerumani ni kitu cha hatari kwani washabiki wa ujerumani wanaheshimu sana muda wao.
mpaka sasa polisi wanamsaka mwandaaji wa onyesho hilo na wamesema kuwa wanachunguza thamani ya hasara hiliyosababishwa na ghasia hizo na pia itamfungulia mashataka promoter huyo raia wa Nigeria,ambaye pia anachunguzwa kwa kusemekana anajihusisha na mtandao fulani wa biashara.


KLABU ya Manchester United imeshinda mbio za kuwania saini ya mshambuliaji Radamel Falcao kutoka Monaco kwa mkopo wa mwaka mmoja.
Mpachika mabao huyo ataigharimu klabu hiyo ya Old Trafford Pauni Milioni 12 kwenda kuungana na Angel di Maria, Daley Blind, Luke Shaw, Ander Herrera na Marcos Rojo katika orodha ya wachezaji wapya kwenye kikosi cha Louis van Gaal.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Colombia mwenye umri wa miaka 28 tayari ameafiki kulipwa mshahara wa Pauni 200,000 kwa wiki na anatarajiwa kutua Manchester wakati wowote kwa ndege binafasi kukamilisha taratibu. 
REKODI YA FALCAO.
River Plate (2005-2009): Mechi 105 mabao 45
Porto (2009-2012): Mechi 87 mabao 72
Beki wa kati wa klabu ya Arsenal Laurent Koscielny ameondolewa katika kikosi chake cha cha timu ya taifa kwa sababubu ya majeraha ya kichwa yaliyompata baada ya hapo jana kugangana na mchezaji wa klabu ya Leicester City,Jeffrey Schlupp katika mchezo uliofanyika dimani King Power na timu zote kutoka sare ya goli 1-1.

View image on Twitter
Koscienly akipoke matibabu uwanjani mara baada ya kugongana kichwa na mshambuliaji wa Leicester City,Jeffrey Schlupp(hayupo katika picha) dimbani King Power ambapo timu zote zilitoka sare ya goli 1-1. 

Koscienly alipata jeraha hilo mnamo dakika ya 26 ya mtanange huo ambao nafasi yake ililazimika kuchukuliwa na Calum Chambers
Taarifa katoka shirikisho la soka nchini Ufaransa zimedhibitisha kuwa beki huyo kwa sasa hayupo katika hesabu ya wachezaji wa kikosi cha timu ya taifa kinachotarajia kucheza michezo miwili ya kirafiki siku za karibuni kati Hispania na Serbia.
Nafasi ya Koscienly kwa sasa katika kikosi cha timu ya taifa ya Ufaransa inaonekana kuchukuliwa na beki anayekipiga kunako klabu ya Barcelona Jeremy Mathieu.

Mathieu, amejiunga na Wakatalunya msimu huu akitokea Valencia na amekwisha fanikiwa kucheza michezo miwili ya kimataifa.

Kitengo cha utabibu ya klabu ya Arsenal kimesema kinaendelea na uchunguzi wa jeraha hilo kisha watasema rasmi ni kwa muda gani beki huyo atakuwa nje ya dimba akiuguza jeraha lake.


Wachezaji Liverpool wakishangilia ushindi
Ligi kuu ya England ambayo imendelea jumapili kwa timu sita kujitupa uwanjani katika michezo mitatu.
Katika mechi ya kwanza Meneja wa Liverpool Brenden Rodgers alitimiza mechi yake 100 tangu aichukue usukani wa kuifundisha liverpool kwa kushuhudia timu yake ikiisambaratisha Tottenham Hotspur kwa jumla ya magoli 3 kwa 0.
Liverpool walianza kuonja ushindi katika dakika ya 8 kwa goli lililofungwa na Raheem Sterling.
Baadae Nahodha wa timu hiyo Steven Gerrald katika dakika 49 akafunga goli la pili kwa mkwaju wa penalty baada ya Joe Alllen kudondoshwa kwenye kisanduku cha 18 kwenye goli la Tottenham.
Goli la tatu la Liverpool lilifungwa na Alberto Moreno Perez baada ya kuwatoka mabeki wa Tottenham na kufunga goli la tatu katika dakika 60.
Hadi mechi hiyo inamalizika Tottenham 0 Liverpool 3
Nayo Aston Villa ambao waliiadhibu Hull City magoli 2 na Hull City 1.
Aston Villa ndio walioanza kufunga goli lililofungw Gabriel Agbonlahor katika dakika ya 14.
Aston villa wakaandika goli la pili ambalo lilifungwa na Andreas Weimann katika dakika ya 36.
Nao Hull City walipata goli moja la kufutia machozi lililofungwa na Nikica Jelavic.
Mechi ya mwisho iliyomalizika usiku ilikuwa ni kati ya Leicester City na Arsenal na matokeo ni kwamba Leicester goli 1 na Arsenal wamepata goli 1.
Kwa matokeo hayo sasa Chelsea ndio wanaoongoza msimamo wa ligi ya England kwa pointi 9 wakifuatiwa na Swansea iliyoshika nafasi ya pili nayo ikiwa na pointi 9 ila ikiwa na toufuti ya magoli Aston Villa ya tatu, Manchester City ya nne, Liverpool ya tano, Tottenham ya sita, Arsenal ya saba na Manchester United ikishika nafasi ya kumi na nne.

waliotembelea blog