Saturday, May 17, 2014


Jose Chameleone akiwa meneja wake mpya.
Jose Chameleone akiwa meneja wake mpya.
Msanii aliyejinyakulia tuzo ya wimbo bora wa Afrika Mashariki akitokea Uganda Jose Chameleone ameamua kuajiri meneja mpya katika kazi zake za sanaa.
Kwa mujibu wa Jose Chameleone Meneja mpya anaitwa Robert Jackson Nkuka. Meneja mpya amechukua nafasi ya aliyekuwa maeneja wake anayeitwa Sam Mukasa

Kikosi cha TP Mazembe
Kikosi cha TP Mazembe
Klabu ya soka ya TP Mazembe ya nchini Congo jana imechezea kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa El Hilal Omdurani ya Sudan katika mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa barani Afrika.
El Hilal walianza kutibua mipango ya Mazembe katika dakika ya 51 baada ya Salah Al Jizoli kuandika bao la kuongoza kufuatia kumalizia pasi nzuri ya Bakri Babeker.
Kipigo hicho cha bao 1-0 kimewafanya Mazembe kuanza vibaya michuano hiyo na sasa watahitaji kufanya vizuri mchezoz unaofuata, huku wakiwa katika kundi A pamoja na wapinzani wao wakubwa AS Vita.
Washambuliaji wote wawili wa Tanzania wa TPM walicheza, Mbwana Samatta akianza na Thomas Ulimwengu akitokea benchi dakika ya 66 kwenda kuchukua nafasi ya Rainford Kalaba.
Samatta na Ulimwengu wanatarajiwa kuondoka asubuhi kuja Dar es Salaam kujiunga na timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars kwa ajili ya mchezo wa Jumapili dhidi ya Zimbabwe, kuwania hatua ya makundi ya kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Mataifa ya Afrika mwakani nchini Morocco

Mb Doggy msanii anayetamba na wimbo wa baby mbona umenuna hivi sasa.
Mb Doggy msanii anayetamba na wimbo wa baby mbona umenuna hivi sasa.
Mwanamuziki wa kizazi kipya, Mbwana Mohamed Mb Doggy amekamilisha video ya wimbo wake mpya inayokwenda kwa jina la ‘Baby Mbona Umenuna’.
Video ya wimbo huo imetengenezwa na Abby Kazi, ambapo imekamilika wiki hii.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Qs Mhonda J Entertainment, Joseph Mhonda, amesema kwamba video ya wimbo huo imeandaliwa kwa kiwango cha juu ili kuwapatia burudani kamili wadau na mashabiki wa Bongo Fleva.


Rais wa shirikisho la kandanda ulimwenguni, FIFA, Sepp Blatter, amethibitisha ilikuwa kosa kuchagua Quatar kuwa mwenyeji wa kombe la dunia la mwaka wa 2022. Katika mahojiano na televisheni nchini Uswisi, Sepp Blatter aliulizwa iwapo kuiruhusu Qatar kuwa mwenyeji wa kombe hilo ambalo huchezwa kati ya mwezi Juni na Julai ilikuwa kosa, hasa ikizingatiwa kuwa hali ya hewa katika nchi hiyo hufikia hadi nyuzi joto 50 wakati huo. Alijibu kwa kukiri na kuongeza kuwa kila mtu hukosea maishani. Alipinga madai kwamba taifa hilo lilikuwa limelipia michezo hiyo. Aliongeza kuwa kamati inayojumuisha maafisa wa FIFA walikuwa wamekubali uwezekano wa taifa hilo kuwa mwenyeji ijapokuwa walikuwa wamepokea taarifa kuhusu vipimo vya juu vya joto. Alisema kwamba michezo hiyo badala yake inaweza kusogezwa hadi miezi ya mwisho wa mwaka, wakati vipimo vya joto vitakuwa vimepungua.

waliotembelea blog