Friday, September 25, 2015


Zile stori za viongozi wa shirikisho la mpira wa miguu duniani FIFA kutuhumiwa kula rushwa na kutumia madaraka vibaya, bado zinazidi kuchukua nafasi katika vyombo vingi vya habari duniani, September 25 kutoka mtandao wa dailymail.co.uk umetangaza kuwa ofisi ya mwanasheria mkuu Uswiss imemfungulia mashitaka Rais wa FIFA Sepp Blatter.
2CC2AECE00000578-3249145-image-m-26_1443193310410
Rais wa shirikisho la soka barani Ulaya UEFA Michel Platini
Taarifa kutoka ofisi ya mwanasheria mkuu inamtuhumu Blatter kwa makosa kadhaa ikiwemo ya utawala mbovu, kuingia mikataba mibovu ya haki za matangazo ya TV akiwa pamoja na aliyekuwa Rais wa mpira wa miguu wa CONCACAF  Jack Warner mwaka 2005. Blatter pia anatuhumiwa kumlipa pound milioni 1.3 kinyume na taratibu Rais wa Shirikisho la soka barani Ulaya (UEFA) Michel Platini mwaka 2011 ikiaminika kuwa zilitumika kwa kampeni.
2CA1AFBD00000578-3249145-image-a-27_1443193328413
Rais wa zamani wa CONCACAF Jack Warner
Ofisi ya mwanasheria mkuu Uswiss imeripoti kumfungulia mashitaka Sepp Blatter September 24. Ofisi ya Rais wa FIFA Sepp Blatter imechunguzwa mchana wa September 25 mjini Zurich Uswiss kama sehemu ya kuendelea kufanya uchunguzi kwa mamlaka husika.
2CC1FBBE00000578-3249145-image-a-5_1443191725765
Hawa ndio waandishi wa habari waliokuwa wamejitokeza katika mkutano ambao Blatter alipanga kufanya lakini ulihairishwa.

Mshambuliaji wa kimataifa wa Ureno na klabu ya Real Madrid ya Hispania Cristiano Ronaldo ambaye ni baba wa mtoto mmoja wa kiume aitwaye Cristiano Ronaldo Junior, September 25 amepiga picha nakuiweka katika account yake ya Instagram huku akiwa na tabasamu la furaha linalotafsiriwa kuwa ni furaha yake ya kukaribia kuweka rekodi ya kuwa mfungaji bora wa Real Madrid wa muda wote.
2CBEFBE300000578-0-image-a-39_1443175044026
moja kati ya picha zake alizopost Ijumaa katika account yake ya Instagram
Cristiano Ronaldo anatajwa kuwa, huenda akaingia katika rekodi ya ufungaji bora wa muda wote wa klabu ya Real Madrid endapo atafanikiwa kufunga hat trick katika mchezo wa September 26 dhidi ya Malaga katika uwanja wao wa nyumbani Santiago Bernabeu. Rekodi ya ufungaji wa muda wote kwa sasa inashikiliwa na Raul  ambaye ana magoli 323.
2CB10F9A00000578-3248839-Ronaldo_did_not_score_as_Real_Madrid_secured_a_hard_fought_2_1_a-a-55_1443177400612
Uwezekano wa Cristiano Ronaldo kuvunja rekodi hiyo Jumamosi ya September 26 upo licha ya kuwa hadi sasa amefunga goli nane katika mashindano yote kwa msimu huu ila bado hajafunga goli lolote katika uwanja wao wa Santiago Bernabeu msimu huu. Ronaldo alifunga goli tano katika mechi ya Laliga dhidi ya Espanyol na alifunga hat trick katika mechi ya UEFA dhidi ya Shakhtar Donetsk.
Kabla ya dirisha la usajili halijafungwa mwezi August mwaka huu, barani Ulaya kulikuwa na stori tofauti tofauti kuhusiana na baadhi ya wachezaji nyota kuhusishwa kutaka kuvihama vilabu vyao na kujiunga na timu nyingine. Moja kati ya mastaa waliokuwa wanahusishwa kuhama timu zao ni Neymar ambaye alitajwa kuwa katika mipango ya Man United.
September 25 mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Brazil anayekipiga katika klabu ya FC Barcelona ya Hispania, amefunguka kuhusiana na mpango huo wa yeye kutaka kuhamia Man United katika dirisha la usajili lililofungwa mwezi August mwaka huu.
IwWEj
“Ni kweli tulikuwa na mazungumzo ya awali, lakini hakukuwa na nia ya dhati katika hili, awali nilisikia kuwa kulikuwa na ofa kwa ajili yangu lakini hakuna kilichofanyika kwangu”>>> Neymar
Afisa mtendaji mkuu wa klabu ya Man United Ed Woodward alisafiri mapema mwezi August kwenda Barcelona kwa ajili ya kukamilisha usajili wa Pedro Rodriguez kabla ya nyota huyo kujiunga na Chelsea ila Ed Woodward inaripotiwa jumuisha mipango ya kumtaka Neymar.

 


Kocha wa klabu ya Chelsea ambaye amekuwa akiingia katika headlines mara kadhaa kutokana na tabia yake ya kupenda kulumbana na kuwatoa mchezoni wapinzani wake kwa maneno yake ya kejeli. September 25 Mourinho amenukuliwa na vyombo vya habari akitoa kauli bila kutaja jina lakini waandishi wanajua alimlenga kocha wa Arsenal Arsene Wenger.
Kauli ya Mourinho inakuja ikiwa ni siku kadhaa zimepita toka klabu ya Chelsea iifunge klabu ya Arsenal kwa goli 2-0  Mourinho bado anaendeleza kauli zake ambazo ni kama ishara ya kumkejeli Wenger licha ya kuwa hakumtaja moja kwa moja ila kauli hii inatafsiriwa kumlenga Wenger. 2C80C82400000578-3249035-image-a-25_1443187316818
“Kila kocha wa Ligi Kuu Uingereza ana presha na Ligi, Steve McClaren, Pellegrini na  Brendan Rodgers wote wana presha na mechi za Ligi na tunalazimika kuyafikia malengo, kiukweli nawaonea huruma kwa sababu ni kazi ngumu. lakini kuna mmoja ambaye hayupo katika hiyo list lakini yeye anajisikia vizuri na wala hana presha”>>> Mourinho





 
 LIGI KUU ENGLAND
RATIBA:
Jumamosi Septemba 26
14:45 Tottenham vs Man City
17:00 Leicester vs Arsenal
17:00 Liverpool vs Aston Villa
17:00 Man United vs Sunderland
17:00 Southampton vs Swansea
17:00 Stoke vs Bournemouth
17:00 West Ham vs Norwich
19:30 Newcastle vs Chelsea
 
Jumapili Septemba 27
18:00 Watford vs Crystal Palace
Jumatatu Septemba 28
22:00 West Brom vs Everton
 


Barabara zote za Jiji la Dar es Salaam zitaelekea Uwanja wa Taifa kushuhudia Klabu kongwe Nchini Tanzania, Simba na Yanga, zenye Makao Makuu yao Eneo la Kariakoo Jijini humo, zikipambana katika pambano la Ligi Kuu 


LIGI KUU VODACOM
RATIBA
Jumamosi Septemba 26

Simba vs Yanga
Coastal Union vs Mwadui
Tanzania Prisons vs Mgambo Shooting
JKT Ruvu vs Stand United (Uwanja wa Karume, Dar es salaam)
Mtibwa Sugar vs Majimjaji
Kagera Sugar vs Toto Africans (Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, Tabora)

Jumapili Septemba 27
Azam FC vs Mbeya City
African Sports vs Ndanda FC 

Kiiza apania kuifunga Yanga Sc
 Mfanyaakzi wa Airtel, (kulia), akijaza fomu ya kujiunga na mpango wa uchangiaji wa hiari (Wote Scheme), wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, wakati wa ufunguzi wa wiki ya Wafanyakazi wa Airtel, makao makuu ya kampuni hiyo ya simu za mikononi, jijini Dar es Salaam, Septemba 26, 2015.
 Wafanyakazi wa Airtel, wakipatiwa maelezo juu ya huduma mbalimbali zitolewazo na PPF, wkati wa wiki ya wafanyakazi wa kampuni hiyo ya simu makao makuu ya Airtel, Morocco jijini Dar es Salaam, Septemba 26, 2015.
 Meneja Masoko wa PPF, Elihuruma Ngowi, (kulia), akizungumza jambo na Meneja Uhusiano wa Airtel, Jackson Mbando, wakatyi wa ufunguzi wa wiki ya Wafanyakazi wa Airtel



 
 
 
 MSIMAMO ULIVYO KWA SASA:
Barclays Premier League
PosLogo &TeamPWDLGDPts
1Manchester CityManchester City65011015
2Manchester UnitedManchester United6411413
3West Ham UnitedWest Ham United6402612
4Leicester CityLeicester City6330412
5ArsenalArsenal6312010
6EvertonEverton623139
7Swansea CitySwansea City623129
8Crystal PalaceCrystal Palace630319
9Tottenham HotspurTottenham Hotspur623119
10WatfordWatford623109
11Norwich CityNorwich City6222-18
12West Bromwich AlbionWest Bromwich Albion6222-28
13LiverpoolLiverpool6222-38
14BournemouthBournemouth6213-17
15ChelseaChelsea6213-37
16SouthamptonSouthampton6132-16
17Aston VillaAston Villa6114-34
18Stoke CityStoke City6033-43
19Newcastle UnitedNewcastle United6024-62
20SunderlandSunderland6024-72








































































































































































MSIMAMO ULIVYO KWA SASA'
La Liga
PosLogo &TeamPWDLGDPts
1Real MadridReal Madrid54101313
2Celta de VigoCelta de Vigo5410813
3VillarrealVillarreal5410713
4Atlético de MadridAtlético de Madrid5401712
5BarcelonaBarcelona5401312
6EspanyolEspanyol5302-59
7Deportivo de La CoruñaDeportivo de La Coruña522128
8EibarEibar522128
9Rayo VallecanoRayo Vallecano5212-37
10Valencia CFValencia CF513106
11Real SociedadReal Sociedad512215
12Las PalmasLas Palmas512205
13Sporting de GijónSporting de Gijón5122-15
14Real BetisReal Betis5122-55
15Athletic ClubAthletic Club5104-43
16LevanteLevante5032-43
17GetafeGetafe5104-53
18Granada CFGranada CF5104-73
19MálagaMálaga5023-32
20SevillaSevilla

waliotembelea blog