Sunday, August 16, 2015


image3Ninayo Good News imenifikia mtu wangu ambayo Watanzania wengi na wakazi wa Dar es salaam tulikua tukiisubiri kwa muda mrefu ni kuhusu kukamilika kwa mradi wa Mabasi yaendayo haraka ambayo zaidi ya mwaka na nusu yaliingia kwenye headlines za kuwa yatatoa huduma hizo.
IMG_0146Habari ikufikie kuwa Mabasi hayo rasmi yanaanza kazi August 17 Jumatatu kuanzia  saa 3 asubuhi nje ya kituo cha Mabasi yaendayo Mikoani Ubungo ambako kutafanyika uzinduzi wa kuanza huduma ya mpito kisha Wananchi wataruhusiwa kupanda mabasi hayo kutoka Ubungo kwenda Kimara na kutoka Kimara hadi Kivukoni Bure.
Kwa bara la Afrika,jiji la Dar es salaam litakua la pili kutekeleza mradi huu mtu wangu baada ya Afrika Kusini na litakua jiji la kwanza kwa nchi za Afrika Mashariki,Kaskazini na Kati.
DeusiDedith Mutasingwa ambaye ni Afisa wa masuala ya fidia katika mradi wa mabasi haya yaendayo haraka yaliyo chini ya ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na serikali za mitaa,amesema yapo mabasi ya aina mbili kuna yale ya mita 18 ambayo yana uwezo wa kubeba abiria 140 na yapo yenye uwezo wa kubeba watu 80.
image1Amesema mabasi hayo pia yamezingatia watu wenye mahitaji maalum kama Walemavu na Wajawazito,pia Wafanyabiashara wanaopanga vitu vyao pembeni ya Barabara na kwenye vituo wameombwa kuviondoa na kwa wale watakaonekana kukaidi amri hiyo faini yake si chini 250,000.

Basi la Simba likiwasili uwanja wa Taifa
Basi la Simba likiwasili uwanja wa Taifa
Kikosi cha Simba SC leo kinacheza mchezo wake wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya timu ya URA kutoka Uganda ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea msimu ujao wa ligi kuu Tanzania bara 2015-2016 mchezo utakaopigwa kwenywe uwanja wa Taifa. 
Hizi ni baadhi ya picha za wachezaji wa kikosi cha Simba wakati wakiwasili uwanja wa Taifa kwa ajili ya mchezo huo.
Wachezaji wa Simba kabla ya kushuka kwenye gari
Wachezaji wa Simba kabla ya kushuka kwenye gari
Ibrahim Ajibu
Ibrahim Ajibu
Mwinyi Kazimoto
Mwinyi Kazimoto
Justice Majabvi
Justice Majabvi
Awadh Juma
Awadh Juma
Simba

Sergio Aguero akishangilia bao lake la kwanza dhidi ya Chelsea.
Mbele ya Mashabiki 54,331 Uwanjani kwao Etihad, Manchester City Leo wamewabonda Mabingwa wa England Chelsea Bao 3-0 katika Mechi ya Ligi Kuu England.
Wakati huu ni ushindi wa pili mfululizo kwa City wa 3-0 kila Mechi tangu Ligi ianze Wikiendi iliyopita, kwa Chelsea hii ni Mechi yao ya pili bila ushindi baada kuanza kwa Sare ya 2-2 huko kwao Stamford Bridge walipocheza na Swansea City.
Hii Leo City walistahili ushindi dhidi ya Chelsea ambayo kwenye Benchi lake Leo alikosekana Daktari wao Mwanamama maarufu Eva Carneiro ambae amepigwa marufuku na Meneja wa Chelsea Jose Mourinho baada kutofautiana. Ramires katiMatic na Silva wakibananBaada ya Man City kupiga hodi mara kadhaa huku wakisimamishwa na ushujaa wa Kipa wa Chelsea Asmir Begovic ambae alikuwa Golini kuchukuwa nafasi ya Kipa Nambari Wani Thibaut Courtois aliefungiwa Mechi 1 baada ya Kadi Nyekundu katika Mechi iliyopita waliyotoka 2-2 na Swansea City, Man City walifanikiwa kufunga katika Dakika ya 31.
Kweupeee 1-0
1-0Bao hilo lilitokana na pasi safi ya David Silva na kumkuta Sergio Aguero alieachia shuti la chini na kutinga.
Kipindi cha Pili kilianza kwa Chelsea kufanya kitu cha ajabu kwa kumpiga Benchi Nahodha wao John Terry na kumuingiza Kurt Zouma nah ii ni mara ya kwanza kwa Jose Mourinho kuwahi kumpumzisha Nahodha wake kwa staili hiyo.
Kepteni wa Man City, Vincent Kompany aliipa Timu yake Bao la Pili katika Dakika ya 79 kwa kichwa baada ya kuunganisha Kona ya David Silva. Akipata matibabu kutoka kwa daktari wa timu
Diego CostaDiego Costa chini!Dakika ya 84, City wakawa 3-0 mbele kwa Bao la Fernandinho aliefunga kwa shuti kutoka nje tu ya boksi.
Vincent Kompany dakika ya 79 na Fernandinho dakika ya 85Hatari tupu!! 1-0Sergio Agüero dakika ya 31aliipatia bao la kuongoza na mtanange kwenda mapumziko ukiwa 1-0 dhidi ya Chelsea.2-0 Kompany akiwachoma bao ChelseaVicent Kompany akishangilia bao lake la piliBao la pili kwa Kompany msimu huu mpya Ligi Kuu England3-0


Bao la Arsenal la kwanza limefungwa na Olivier Giroud dakika ya 16 na kipindi hicho hicho Crystal Palace walisawazisha kupitia kwa Joel Ward dakika ya 28 na kufanya 1-1. Kipindi cha pili dakika ya 55 Damien Delaney alijifunga dakika ya 55 na kuwapa bao la Ushindi Arsenal na mtanange kumalizika kwa bao 2-1 Arsenal wakiibuka washindi.
Mbele ya Mashabiki 24,732.
Mbele ya Mashabiki 24,732.


Fowadi wa Arsenal, Alexis Sanchez
Difenda Damien Delaney akijifunga!

1-1
Olivier Giroud akituma salaam dakika ya 16
Mambo safi!! Arsene Wenger akipongeza pamoja na Viongozi wengine

Kipa Petr Cech










KLABU ya Simba imeendeleza wimbi la ushindi kwenye mechi za kirafiki baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya URA ya Uganda.
Kwenye mchezo huo uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam mabao ya Simba yalifungwa na Kelvin Ndayisenga kwenye dakika ya nne ya mchezo huo na bao la pili likiwekwa kimiani na beki Juku Mushood kutoka Uganda.
Bao la la URA lilifungwa na Kalanda Frank kwenye dakika ya 19 baada ya kutokea piga nikupige kwenye lango la Simba na mfungaji kupiga mpira uliompita kipa Peter Manyika na kuzaa bao hilo.
Mchezo huo ulianza kwa kasi huku timu zote zikishambuliana kwa zamu ingawa waliwa Simba waliotangulia kufunga kwenye dakika ya nne na mchezaji wao mpya Kelvin Ndayisiyenga kuiandikia timu hiyo bao la kuongoza.
Hata hivyo bao hilo lilidumu kwa dakika 15 kwani URA walifanikiwa kusawazisha kupitia kwa mshambuliaji wake Kalanda Frank baada ya kutokea piga nikupige kwenye lango la Simba.
Baada ya bao hilo timu hizo zilishambuliana kwa zamu na dakika ya 36 Simon Sserunkuma anakosa bao la wazi lakini mpira alilopiga lilikwenda pembeni ya lango la URA kabla ya shuti dhaifu la Abdi Banda kudakwa na kipa wa URA Mwete Brian.
Kalanda Frank alikaribia kuifungia URA bao la pili lakini shuti lake liligonga mwamba na kuokolewa na mabeki wa Simba na dakika ya 42 Kagimu Fatiq alipiga mpira ulioishia mikononi mwa kipa Peter Manyika.
Kipindi cha pili kilianza kufanya mabadiliko saba kwa kuwapumzisha Awadh Juma na kuingia Said Ndemla, Abdi Banda akaingia Justice Majibva, Issa Abdallah akaingia Mwinyi Kazimoto, Emery Nimuboma akaingia Ramadhani Kessy, Samih Nuhu akaingia Mohamedi Hussein, Simon Sserunkuma akaingia Peter Mwalyanzi na Said Issa akaingia Hassan Isihaka.

Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya, Kala Jeremiah akiongea na waandishi wa habari ili kuwaelezea onyesho lao la bure wanalotarajia kulifanya Agosti 23, 2015 Jumapili kwenye viwanja vya Zakhem, Mbagala kuwahamasisha mashabiki wao kujitokeza kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na madiwani wa Oktoba 25, 2015. Pembeni ni Joseph Haule “Professa J”, Juma Kassim “Sir Nature” pamoja na Msagasumu.
 Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya, Joseph Haule “Professa J” akionyesha msisitizo mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya onyesho lao la bure wanalotarajia kulifanya Agosti 23, 2015 Jumapili kwenye viwanja vya Zakhem, Mbagala kuwahamasisha mashabiki wao kujitokeza kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na madiwani wa Oktoba 25, 2015. 
 Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya, Juma Kassim “Sir Nature” akionyesha msisitizo mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya onyesho lao la bure wanalotarajia kulifanya Agosti 23, 2015 Jumapili kwenye viwanja vya Zakhem, Mbagala kuwahamasisha mashabiki wao kujitokeza kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na madiwani wa Oktoba 25.
Tanzania Oyeeeee! Tanzania Oyeeee! ndiyo wasanii hawa walivyokuwa wakitia msisitizo.
 Baadhi ya wasanii watakaowasha moto Agosti 23, 2015 Jumapili kwenye viwanja vya Zakhem, Mbagala kuwahamasisha mashabiki wao kujitokeza kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na madiwani wa Oktoba 25, 2015.
Mwandishi wa habari wa Times Fm, akifanya mahojiano na Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya, Joseph Haule “Professa J”.
 ……………………………………………….
Na Mwandishi Wetu.

Wasanii nyota wa muziki wa kizazi kipya na baadhi ya nyota wa Bongo Movie watafanya onyesho la bure Jumapili kwenye viwanja vya Zakhem, Mbagala kuwahamasisha mashabiki wao kujitokeza kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na madiwani wa Oktoba 25.
Wasanii hao wataongozwa na Mbunge wa Mbeya mjini kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Joseph Mbilinyi “Sugu” na nyota wengine kama Juma Kassim “Sir Nature”, Joseph Haule “Professa J” na Kara Jeremiah.
Wengine ni watakaopanda jukwaani siku kuanzia saa 8.00 mchana ni Msaga Sumu, Baba Haji na waigizaji nyota wa Bongo Movie, Jacqueline Wolper na Auntie Ezekiel.
Akizungumza jijini jana, Professa J alisema kuwa sababu kubwa ya kufanya onyesho hilo ni kutoa elimu kwa mashabiki wao kuhusiana na zoezi la upigaji kura kuchagua viongozi bora wan chi hii wataodumu kwa miaka mitano.
Professa alisema kuwa wanataka kutoa mwamko kwa mashabiki wao kushiriki kwa wingi katika zoezi hilo ili kutumia demokrasia yao kumchagua kiongozi wanayemtaka.
“Tumejiandaa vilivyo kutoa elimu, lengo ni kuwahamasisha mashabiki wetu kufanya kile wanachokiona kinafaa ili kutimiza malengo yao ya kikatiba,” alisema Professa J.
Alisema kuwa mbali ya Dar es Salaam, onyesho hilo pia litafanyika katika mikoa mengine mbalimbali.
Akizungumza katika mkutano huo, Nature aliwaomba mashabiki kujitokeza kwa wingi ili kupata elimu hiyo ambayo wasanii wameamua kuitoa.
“Hii siyo kampeni ya kisiasa, sisi ni wasanii tumeamua kujitolea kufanya kazi ambayo wasanii wengi duniani wameifanya, lazima tutumie kazi yetu kutoa elimu kwa mashabiki ili wajue wajibu wao katika mambo mbali mbali pamoja na uchaguzi mkuu,” alisema Nature.

waliotembelea blog