Monday, November 17, 2014






























Taifa Stars leo huko Mjini Mbabane, Swaziland Uwanjani Somhlolo imetoka Sare ya Bao 1-1 na Timu ya Taifa ya Swaziland, Sihlangu, katika Mechi ya Kimataifa ya Kirafiki.

Sihlangu waliongoza Kwa Bao 1-0 hadi Mapumziko na Taifa Stars kusawazisha kwa Bao la Thomas Ulimwengu Dakika ya 51.
Lakini Ulimwengu aliikosesha Stars ushindi baada ya kukosa Penati katika Dakika ya 72.
Sihlangu waliongoza Kwa Bao 1-0 hadi Mapumziko na Taifa Stars kusawazisha kwa Bao la Thomas Ulimwengu Dakika ya 51.
Lakini Ulimwengu aliikosesha Stars ushindi baada ya kukosa Penati katika Dakika ya 72.



MWANAMICHEZO ambaye anacheza kwa kutumia pikipiki Bian Capper kutoka nchini Afrika kusini ametoa wito kwa watanzania kucheza mchezo huo ambao mbali ya kufurahisha pia unatumia akili na kukufanya uwe mkakamavu wakati wote.

Akizungumza jana kabla kuonesha umahiri huo mchezaji wa pikipiki ambaye ni raia wa Afrika Kusini anayefanya ziara katika nchi za Afrika kwa udhamini wa kinywaji cha Redbull atakuwa nchini kwa ziara za ya maonesho ya kuonesha namna ya kucheza na pikipiki kwa siku tatu.


Onyesho la kwanza lilianza jana kwenye viwanja vya Coco beach , leo Jumapili atakuwa Mlimani City na kesho Jumatatu atakuwa katika eneo la Ubungo Tanesco ambako litakuwa onyesho lake la mwisho.

Capper amesema kwamba amefurahia kuweza kufika nchini pia tayari ameshafanya maonyesho yake katika nchi za Kenya na Uganda.



Wakati huohuo Rais wa Tanzania Motorcross Acrobatic Club Blagina Mwihava alisema kwamba wamemleta mwanamuchezo huyo ambaye wana imani kubwa ataleta msisimko mkubwa kwa vijana wa kitanzania kuweza kupata hamasa ya kucheza mchezo huo wenye mvuto. 



www.bukobasports.com
Hatimaye ile Filamu iliyokuwa ikisubiriwa sana na Wadau pamoja na Wapenzi wa Filamu Nchini ambayo Imechezwa na Wasanii kutoka Nchini Tanzania wakiwemo Slim Omary, Hashim Kambi, Irene Paul na Staa wa Filamu Kutoka Nchini Ghana Van Vicker iitwayo NEVER GIVE UP iliyochezwa Nchini Tanzania tayari imeshaingia Sokoni na Sasa inapatika katika Maduka yote ya Kuuza Filamu hapa Nchini. Vilevile ni filamu ambayo inatarajiwa kufanya vizuri sana katika Soko la Filamu Nchini na Nje ya Nchi.

Filamu ya NEVER GIVE UP ni filamu nyingine kutoka Kampuni ya Proin Promotions ambayo imeingia Sokoni Huku ikiwa imetanguliwa na Filamu mpya ya Lulu iitwayo MAPENZI YA MUNGU ambayo ipo sokoni wiki ya tatu sasa huku ikiendelea kufanya vizuri sana. Kabla hata ya FIlamu ya NEVER GIVE UP kuingia Sokoni tayari Kampuni ya Proin Promotions Ltd ilishapokea oda ya Nakala zisipongua Elfu 30 kutoka sehemu mbalimbali ndani ya Nchi ya Nje Ya Nchi.

Na Kama wewe pia unahitaji Filamu hii kwa bei ya Jumla unaweza kupiga Simu 0712 390 200 na Kufanya Oda yako

EURO 2016: ENGLAND 3 vs 1 SLOVENIA, ROONEY NA DANNY WELBECK WAIPA USHINDI ENGLAND! ROONEY ACHEZA MECHI YA 100, AFUNGA BAO!


Wayne Rooney akishangilia bao lake la mkwaju wa penati baada ya kusawazisha bao na kuweka 1-1 kwa bao walilokuwa wamejifunga wao wenyewe kupitia kwa Jordan Henderson usiku huu tarehe 15.11.2014 na Mtanange huo kumalizika kwa 3-1, England wameibuka Kidedea. 
Wayne Rooney Usiku huu Uwanjani Wembley amecheza Mechi yake ya 100 wa England na pia kuwanasua toka Goli 1 nyuma na kusawazisha walipocheza na Slovenia Mechi ya Kundi E na hatimae kushinda Bao 3-1.
England fans show their support of Wayne Rooney
Kabla ya Mechi kuanza, Rooney alikabidhiwa Kofia ya Dhahabu na Sir Bobby Charlton ikiwa ni Tuzo kwa kuichezea England Mechi 100.
England's Wayne Rooney before the game with sons Klay and Kai as he celebrates his 100th cap for EnglandMapema kabla ya mechi Wayne Rooney alitinga Uwanjani hapo na Wanae Klay na KaiEngland's Wayne Rooney before the game with son Kai as he is presented with his 100th cap for England by Sir Bobby CharltonAlipewa kofia ya DhahabuEngland's team shotKikosi cha England.Slovenia's Ales Mertelj celebrates scoring their first goal Wachezaji wa Slovenia wakipongezana baada ya kupata bao.England manager Roy Hodgson with assistant manager Ray Lewington and coach Gary NevilleViongozi wa England na wachezaji wa Akiba
Jordan Henderson alijifunga bao dakika ya 57' na kuwapa zawadi ya bao Slovenia ya bao 1-0 lakini baadae England walisawazisha kupitia kwa Wayne Rooney katika dakika ya  59 na kufanya 1-1 baada ya kwenda 0-0 kipindi cha kwanza.

Danny Welbeck aliwaongezea bao la pili England na kufanya 2-1 katika kipindi cha pili hiho hicho katika dakika ya 65.Danny Welbeck akifanya yake..
Danny Welbeck alifunga bao lake la pili tena na kufanya 3-1 katika dakika ya 72. Ushindi huu umeifanya England ipae kileleni ikiwa na Pointi 12 ikifuatiwa na Lithuania na Slovenia zenye Pointi 6 kila moja.Danny Welbeck baada ya kuziona nyavu za SloveniaDanny Welbeck of England scores the 3rd goal 3-1 Danny Welbeck akitupia..England's Danny Welbeck scoring the third goal Danny Welbeck akimchungulia kipa wa SloveniaDanny Welbeck akishangilia na wenzake bao.Roy Hodgson akiwa karibu na Kocha msaidizi wake Ray Lewington (kulia).Danny Welbeck scores to make it 2-1 and is congratulated by team-matesWachezaji wa England wakishangilia..England's Danny Welbeck celebrates scoring the third goal with Raheem Sterling Danny Welbeck akipongezwa na Sterling baada ya kuifungia Timu bao la tatu na kufanya 3-1 dhidi ya Slovenia.

waliotembelea blog