Tuesday, April 22, 2014


UEFA CHAMPIONS LIGI, LEO Jumanne na Jumatano Usiku zitakuwa na Mechi zake za Kwanza za Nusu Fainali huko Jijini Madrid Nchini Spain.
LEO Jumanne, ndani ya Estadio Vicente Calderon, Vinara wa La Liga, Atletico Madrid, wataikaribisha Chelsea ya Engand.
Siku ya Pili yake, yaani Jumatano Usiku, huko Santiago Bernabaeu, Real Madrid watakuwa Wenyeji wa Mabingwa Watetezi wa UCL, Bayern Munich.



ATLETICO MADRID v CHELSEA:
Jose Mourinho ameshawahi kuifikisha Chelsea mara 2 Nusu Fainali ya UCL, Mwaka 2005 na 2007, na kutolewa na Liverpool.

Lakini safari hii wapo Uwanja wa Vicente Calderon ambao Atletico Madrid hawajafungwa hata Mechi moja ya La Liga Msimu huu na wanaongoza Ligi hiyo ya Spain wakiwa Pointi 4 mbele ya Barcelona.
Chelsea watatinga kwenye Mechi hii bila ya Fulbeki wao Branislav Ivanovic ambae amefungiwa na hili linaweza kumrudisha Kikosini Mkongwe Ashley Cole ambae amepoteza namba kwa Cesar Azpilicueta ambae atapelekwa Fulbeki ya Kulia na Cole kucheza kushoto.



Hatimaye kocha Manchester United David Moyes amefukuzwa kazi, miezi 10 baada ya kumrithi Sir Alex Ferguson.
United jana waligoma kuthibitisha kuhusu ripoti kwamba Moyes angefukuzwa mwishoni mwa msimu.
Moyes, 50, alichaguliwa na Sir Alex Ferguson kumrithi wakati kocha huyo mwenye 72, alipoamua kustaafu baada ya miaka 26 mwaka jana baada ya ligi kuisha.
Moyes aliondoka Everton na kusaini mkataba wa miaka sita na mabingwa ya Premier league.
Kwenye taarifa rasmi, klabu ilisema: “Tungependa kumshukuru kwa kazi nzuri aliyoifanya, uaminifu wake aliokuwa nao kwenye kazi yake”.
Ryan Giggs kwa pamoja na Nicky Butt watashika majukumu ya ukocha mpaka mwishoni mwa msimu.

Mashabiki wa United wakiwa wachache Uwanjani wakati wa malumbano ya hapa na pale kabla ya mtanange huku wakishinikiza baongo la  'Chosen One' kuondolewa uwanjani hapo..

Moyes akiwa amebeba kombe la Ngao ya Jamii (Community Shield) baada ya Man  United kuifunga Wigan bao 2-0 kwenye uwanja wa  Wembley mwezi wa Nane kipindi cha nyuma.

waliotembelea blog