Tuesday, June 16, 2015


Mlinzi wa Borussia Dortmund na Ujerumani, Mats Hummels amefunga pingu za maisha na mpenzi wake wa muda mrefu, Cathy Fischer.
Ndoa ya mshindi huyo wa kombe la dunia ambaye miezi ya karibuni amekuwa akihusishwa kujiunga na Manchester United alifunwga jana mjini Munich.
Hummels mwenye miaka 26 alipigwa picha akiwa na mapambo yenye rangi ya jezi ya Borussia kwenye suti yake maridadi kabisa.
Ripoti nchini Ujerumani zinasema kuwa wapenzi hao walianza mahusiano tangu Hummels alipokuwa na miaka 19.


Mlinzi huyu mwenye miaka 26 ametupia suti yenye mapambo yenye rangi ya jezi ya Dortmund

Hummels amefunga ndoa ya kiserikali katika mahakama ya Mandelstrasse, mjini Munich


Timu ya taifa ya soka ya Uganda yenye wachezaji wanaocheza soka nyumbani imeanza maandalizi ya michuano ya mzunguko wa kwanza kufuzu kwa michuano ya Afrika CHAN itakayofanyika mwakani nchini Rwanda.
Uganda inajiandaa kuchuana na Tanzania siku ya Jumamosi mchuano utakaochezwa katika visiwa vya Zanzibar.
Kocha Milutin ‘Micho’ Sredojevic anasema baada ya mchuano wa mwishoni mwa juma lililopita wa kufuzu katika fainali za mataifa bingwa barani Afrika mwaka 2017, kazi kubwa iliyo mbele yao ni kuikabili Tanzania.
Siku ya Jumanne, kikosi cha Micho kinaendelea na maandalizi yake katika taasisi ya mafunzo ya kiufundi ya Njeru ili kupata uzoefu katika uwanja wa bandia.
Kikosi kamili:
Makipa: Alitho James, Ochan Benjamin, Bwete Brian
Mabeki: Okoth Denis, Ntambi Julius ,Ochwo Brian, Musisi Farouk, Waswa Hassan, Bakaki Shafiq, Kiyemba Ibrahim, Okello Silvester
Viungo wa Kati: Bukenya Deus, Tekkwo Derrick, Mugerwa Yasser, Kizito Keziron, Mutyaba Muzamil, Eturude Abel, Kyeyune Saidi, Miya Farouk, Kiiza Martin
Washambuliaji: Sekisambu Erisa, Semazi John, Kalanda Frank, Ssentongo Robert, Fahad Muhamed Hassan

Shirikisho la soka nchini Tanzania TFF, limempa kocha wa Stars Mart Nooij raia wa Uholanzi nafasi ya mwisho ya kuhakikisha kuwa kikosi chake kinafuzu katika michuano hii, la sivyo ajiuzulu.
Uamuzi huu ulitolewa na uongozi wa soka nchini humo baada kumalizika kwa michuano ya Kusini mwa mataifa ya Afrika COSAFA mwezi mmoja uliopita walikofungwa michuano yao yote.
Tanzania iliwahi kucheza katika michuano hii ya CHAN mwaka 2009 wakati makala ya kwanza ya michuano hii ilipofanyika nchini Cote Dvoire.
Kikosi cha Tanzania:
Salum Swedi, Kelvin Yondani, Amir Maftah, Juma Jabu, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Shadrack Nsajigwa na Erasto Nyoni, huku viungo ni Nizar Khalfan, Shaaban Nditi, Mwinyi Kazimoto, Godfrey Bonny, Athuman Idd ‘Chuji’, Nurdin Bakary na Henry Joseph. Safu ya ushambuliaji ilikuwa chini ya Abdi Kassim ‘Babi’, Haruna Moshi ‘Boban’, Kigi Makassy, Mrisho Ngassa, Jerson Tegete, Mussa Hassan Mgosi.


    Kiungo wa zamani wa klabu ya Manchester United, Cleverley mchana wa leo alifunga pingu za maisha na mchumba wake wa muda mrefu Georgina Dorsett katika shughuli ya kifahari iliyofanyika huko Claridge.
  Ndoa hiyo ilihudhuriwa na mastaa wengi wa soka akiwemo nahodha wa klabu ya Manchester United na England Wayne Rooney ambaye pia aliongozana na mkewe Coleen, Chris Smalling wa Man United, Danny Welbeck na wachezaji wengine, pia alikuwepo muimbaji wa band ya The Saturdays, Rochelle Humes.
Cleverley na Mkewe wakiwa wanatoka kanisani

   
Mchezaji wa Arsenal – Danny Welbeck
Wayne na Coleen Rooney Harusini


Mshindi wa mbio za Acacia Tufanikiwe Pamoja Lake Zone Cycle Challenge, Masunga Duba aliyeinua mikono akishangilia mara baada ya kumaliza mbio hizo akiwa mbele ya wenzake. Mshindi huyo anatoka mkoa wa Shinyanga.

Makamu wa rais wa Kampuni ya Uchimbaji wa dhahabu ya Acacia, Deo Mwanyika (wa kwanza kushoto) akifurahia jambo na Afisa Mkuu wa Uendeshaji wa kampuni ya Acacia, Mishel Ash, (wa pili kutoka kushoto) ambaye pia ni kaimu Meneja Mkuu wa Mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu

Washindi wa mbio za wanawake (kilometa 80). Aliyesimama katikati ni Martha antony ambaye ndio aliibuka mshindi wa kwanza, akifuatiwa na Laulensia Luzuba, (mwenye mtoto) aliyekuwa mshindi wa pili na Veronica Saimon (wa kwanza kushoto) aliyejinyakulia nafasi ya Tatu.

Washiriki wa mbio za Acacia tufanikiwe pamoja lake zone cycle challenge wakimenyana vikali wakati wa mashindano hayo.
Afisa mkuu wa uendeshaji wa kampuni ya Acacia Mishel Ash akimvisha medali mshindi wa mbio hizo Martha Antony wakati wa Hafla ya Kutoa zawadi kwa washindi.

Mmoja wa washiriki wa mbio hizo akinywa maji wakati wa mashindano hayo.
………………………………….
Na Mwandishi wetu
Washiriki wa mbio za baiskeli zijulikanazo kama “Acacia Tufanikiwe Pamoja Lake Zone Cycle Challenge” kutoka mikoa ya Shinyanga na Mwanza wameendelea kuudhihirisha umma wa wakazi wa kanda ya ziwa na watanzania kwa ujumla kuwa mpaka sasa hawana mpinzani baada ya washiriki wa mbio hizo kuibuka kidedea katika fainali za kumtafuta mshindi wa kanda hiyo.
Washiriki wa mikoa hii miwili wamejinyakulia nafasi zote za juu na hivyo kuwashinda wenzao wa mikoa mingine ya Kanda ya ziwa ikiwemo Kagera, Mara, Geita na Simiyu.

Katika mbio za wanaume za umbali wa kilometa 156.6 kutoka Kahama mpaka Tinde na kisha Kurejea Kahama, mshindi wa mwaka jana Masunga Duba (Mwanza) aliibuka tena kidedea huku nafasi ya pili ikichukuliwa na Lupilya Hamis(Shinyanga) na nafasi ya tatu ikimuendea Kulwa Tuki(Shinyanga), washindi hawa wamejinyakulia kitita cha pesa taslimu Sh1,500.000/- kwa mshindi wa kwanza, Sh1,200.000/= mshindi wa pili na Sh800,000/= kwa mshindi wa tatu.

Kwa upande wa mbio za wanawake za umbali wa kilometa 80, kutoka Kahama mpaka Mwakata Kisha kurejea Kahama, timu ya mkoa wa Mwanza imedhihirisha kuwa wao bado ni mabingwa kwa kuibuka tena washindi wa mbio hizo, huku mshindi wa mbio za Mwaka jana Martha Antony, akiibuka mshindi wa kwanza akifuatiwa na Laulensia Luziba na nafasi ya tatu ikienda kwa Veronica Simon. Washindi hao wamepata zawadi ya pesa taslimu Sh1,200.000/= kwa mshindi wa kwanza, Sh800,000/= mshindi wa pili na Sh600,000/= mshindi wa tatu.

Mbio hizo ambazo zimeandaliwa na Chama cha Baiskeli Tanzania (CHABATA) kwa udhamini wa kampuni ya uchimbaji wa Madini ya Acacia, inayomiliki migodi ya North Mara, Bulyanhulu na Buzwagi, yote ikiwa mikoa ya kanda ya ziwa, kupitia mpango wake wa Tufanikiwe Pamoja ikiwa ni mara ya pili sasa ambapo mashindano ya mwaka huu yameonyesha mafanikio makubwa kutokana na maandalizi mazuri yaliyofanyika.
Akizungumza na washiriki wa mashindano hayo Mkuu wa wilaya ya Kahama Benson Mpyesa, ambaye alikua mgeni rasmi wa fainali hizi, amesema ana imani kuwa mashindano hayo yatasaidia kuibua vipaji ambavyo vitauletea sifa mkoa wa Shinyanga, Kanda ya ziwa na hata taifa kwa ujumla kwani baiskeli kwa maeneo hayo ndiyo jadi yao.
Awali akimkaribisha Mkuu wa wilaya kuzungumza na washiriki hao, Makamu wa Rais wa Acacia Deo Mwanyika amesema kampuni ya Acacia imekuwa ikifanya shughuli za uchimbaji unaojali na ndio maana iliona vyema kuweka udhamini wake pia katika mchezo wa baiskeli, “toka tuanze huu sasa ni mwaka wa pili na tunayaona mafanikio makubwa kwani hata maeneo ambapo mchezo huu ulikuwa hauchezwi sasa unachezwa, hali ambayo imeongeza hamasa na idadi ya washiriki.”
Aidha Makamu wa Rais huyo wa Acacia amesema mipango ya kampuni kwa sasa ni kuona pia inashiriki katika kuendeleza michezo mingine ikiwemo na soka.


Ratiba ya Msimu mpya wa 2015/2016 wa Ligi Kuu England itatolewa Kesho Jumatano Saa 5 Asubuhi.
Pamoja na Ratiba hiyo ya Ligi ya juu England pia zitatolewa Ratiba za Ligi za chini yake kwa Msimu huo mpya ambao unahusisha jumla ya Timu 92 kwa Madaraja yake yote.
Chelsea ndio Mabingwa wa Ligi Kuu England walipotwaa Ubingwa wakiwa Pointi 8 mbele ya Timu ya Pili Manchester City waliofuatiwa na Arsenal na Manchester United na Timu zote hizi 4 zitacheza UEFA CHAMPIONS LIGI Msimu ujao.

Timu zilizoshika Nafasi ya 5 na 6 ni LIverpool na Tottenham ambazo zitacheza UEFA EUROPA LIGI pamoja na West Ham walioingizwa kwa Tiketi ya Mchezo wa Haki.
Timu mpya kwenye Ligi Kuu England, ambazo zimepanda Daraja kutoka Daraja la Championship, ni Bournemouth, inayoshiriki kwa mara ya kwanza, na Watford na Norwich ambazo zishawahi kucheza Ligi hii ya juu.

Timu hizo 3 zitabadiliwa huko Championship na Hull, QPR na Burnley baada ya kuporomoka Daraja kutoka Ligi Kuu England.
LIgi Kuu England itaanza Agosti 8 na kumalizika Mei 7, 2016 lakini Mechi ya kufungua pazia Msimu, ya kugombea Ngao ya Jamii, kati ya Mabingwa Chelsea na waliobeba FA CUP, ARsenal, itachezwa Uwanjani Wembley JIjini London hapo Agosti 2.


Premier League Fixtures 2015-16 – Important Dates
 DETAILS  DATES
Premier League Fixtures Release Date 17th June 2015 @ 09:00 UK Time
EPL Season Start Date (confirmed) 08 August 2015
EPL Season End Date (not confirmed yet) 07 May 2016
First Set of Changes in EPL Fixtures  Within two weeks of fixtures announcement
Second set of changes After champions league fixtures announced
Community Shield Match 01 August 2015
Capital One Cup Final  28 February 2016
FA Cup Final  15 May 2016
table seperater

AC Milan wamemteua Kocha wa zamani wa Serbia Sinisa Mihajlovic baada kumtimua Filippo Inzaghi.
Mihajlovic, ambae ni Beki wa zamani mwenye Miaka 46, amesaini Mkataba wa Miaka Miwili na kibarua chake cha mwisho kama Kocha kilikuwa huko Sampdoria ambako aliondoka mwanzoni mwa Mwezi huu.
Flippo Inzaghi, mwenye Miaka 41, alikuwa Mchezaji wa zamani wa AC Milan aliyoichezea kuanzia 2001 hadi alipostaafu 2012.
Inzaghi aliteuliwa kuwa Kocha wa AC Milan Mwezi Juni Mwaka Jana kuchukua nafasi ya Mchezaji mwenzake wa zamani Klabuni hapo Clarence Seedorf.
Lakini AC Milan, chini ya Inzaghi, haikufanya vyema na ilimaliza Nafasi ya 10 kwenye Ligi Serie A ikiwa Pointi 35 nyuma ya Mabingwa Juventus.
Akiwa Mchezaji, Mihajlovic alizichezea AS Roma, Sampdoria, Lazio na Inter Milan katika kipindi cha Miaka 20 ya maisha yake ya uchezaji na pia kuichezea Timu ya Taifa ya Nchini kwao Mechi 63.
Baada kustaafu kama Mchezaji akiwa na Inter Milan, Mihajlovic alianza kama Kocha hapo hapo akiwa Msaidizi wa Roberto Mancini na kisha kuziongoza Klabu za Bologna, Catania na Fiorentina na Aprili 2012 kuteuliwa kuwa Kocha wa Serbia.


Kenya 


Bingwa mtetezi wa voliboli ya wanawake barani Afrika,Kenya, Wameishinda Algeria kwenye mechi yake ya pili huku Senegal wakizidi kuwika katika mashindano ya voliboli ya kombe la mataifa ya Afrika yanayoendelea jijini Nairobi Kenya.
Nahodha wa Kenya Praxidis Agala alicheza kufa na kupona na kuongoza Kenya kuibwaga Algeria kwa seti 3-0 katika mashindano ya voliboli ya wanawake ya kuwania ubingwa wa mataifa ya Afrika.
Agala alionana vyema na seta Jane Wacu na kunyamazisha Algeria 25-20 seti ya kwanza, na ya pili Kenya ikashinda 25-22.
Kenya ilikamilisha kivuno hicho cha alama kwa kuichabanga alama 25-19 .
Huu ni ushindi wa pili kwa Kenya baada ya kuicharaza Mauritius seti 3-0 katika mechi yao ya kwanza Ijumaa.
Kenya inawania kushinda taji hili mara ya nane na kujikatia tiketi ya kushiriki mashindano ya kombe la dunia itakayoandaliwa baadaye mwaka huu nchini Japan.
 null
Mshindi wa mashindano haya ataiwakilisha Afrika katika kombe la dunia litakaloandaliwa huko Japan
Senegal nayo inazidi kuwika kinyume na matarajio ya wengi.
Katika mechi ya kwanza Senegal ilishinda Cameroon seti 3-1 na leo hii ikanyamazisha Tunisia seti 3-2.
Katika matokeo mengine, Botswana ilishinda Mauritius seti 3-1 na Cameroon ikaizaba Morocco seti 3-0.
Jumatatu, Tunisia inapambana na Cameroon, Kenya dhidi ya Botswana, Morocco inamenyana na Senegal na Algeria dhidi ya Mauritius.







TIMU ya soka ya taifa, Taifa Stars leo imerejea nchini kutoka Misri ilipokwenda kucheza mechi ya kuwania kufuzu fainali za Kombe la Mataifa Afrika mwishoni mwa wiki iliyopita na kufungwa mabao 3-0.
Kwa muda mrefu Stars haijapata matokeo mazuri kwenye mechi za kimataifa hali iliyofanya wachezaji wake kutoka uwanja wa ndege kwa mafungu huku wengine wakikwepa kuzungumza na vyombo vya habari.
Timu hiyo iliwasili kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere saa 7:30 mchana na wachezaji wake kuanza kutoka mmoja mmoja wakiongozwa na Juma Abdul, kisha akafuata Salum Telela, Amri Kiemba, Aggrey Moris na Jonas Mkude.
Tofauti na siku za nyuma, mashabiki hukusanyika kuipokea timu hiyo pamoja na viongozi mbalimbali, leo hali ilikuwa tofauti hakukuwa na kiongozi yeyote uwanjani hapo si kutoka Shirikisho la soka Tanzania (TFF) wala kwa wadau wa soka.
Kila mchezaji alipotoka, madereva taxi wa uwanja wa ndege  walisema: “Eeh watalii mmerudi, watalii mmerudi,”.
Akizungumza uwanjani hapo, mchezaji wa kimataifa anayecheza TP Mazembe ya Congo DR, Mbwana Samatta alisema hakuna ubishi kwamba walicheza na timu bora na kilichobaki ni kujipanga upya.
“Ni kweli mechi ilikuwa ngumu sana kama mlivyoona… tulifungwa sababu muda mwingi tulikuwa tunazuia, sasa unategemea nini? si unachoka,” alisema Samatta.
Naye nahodha wa timu hiyo Nadir Haroub alisema anajua watanzania wanaumizwa na matokeo hayo lakini wasikate tamaa, wanaahidi watafanya vizuri kwenye mechi dhidi ya Uganda Jumamosi ( Kuwania kufuzu fainali za mataifa kwa wachezaji wa ndani, CHAN)  ili kurudisha imani.

1
Jokate (kushoto) akizungumza katika mkutano wa jukwaa la sanaa. Katikati ni katibu mkuu wa Chama cha  Waandishi wa Habari za Sanaa na Utamaduni nchini, (CAJAtz), Hassan Bumbuli na mbunifu mkongwe wa mavazi, Asia Idarous.
2
Mbunifu mkongwe wa mavazi nchini, Asia Idarous (kulia) akisisitiza jambo katika mkutano wa jukwaa la sanaa. Katikati ni Katibu mkuu wa Chama cha  Waandishi wa Habari za Sanaa na Utamaduni nchini, (CAJAtz), Hassan Bumbuli na msichana mwenye vipaji vingi, Jokate Mwegelo.
3
Katibu mkuu wa Chama cha Waandishi wa Habari za Sanaa na Utamaduni nchini, (CAJAtz), Hassan Bumbuli (Katikati) akizungumza katika mkutano wa jukwa la wasanii, kulia ni Mbunifu mkongwe, Asia Idarous na msichana mwenye vipaji vingi, Jokate Mwegelo.
4
Katibu mkuu wa na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) Godfrey Mngereza akifafanua jambo katika mkutano huo.
5
Msanii mkongwe wa maigizo na filamu nchini, Mzee Jangala akifuatilia mkutano wa jukwaa la sanaa.
6
Katibu mkuu wa na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) Godfrey Mngereza akionyesha kipaji chake cha kupiga zeze na kuimba kwa kushirikiana na wasanii wengine waliohudhuria mkutano wa Jukwaa la Sanaa.

Msichana mwenye vipaji lukuki nchini, Jokate Mwegelo amewataka wasanii kuwa wabunifu ili kupata mafanikio katika sanaa na shughuli zao za kila siku.
Jokate alitoa wito huo wakati akitoa mada katika Jukwaa la Sanaa la lililoandaliwa na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) kwa kushirikiana na chama cha  Waandishi wa Habari za Sanaa na Utamaduni nchini, (CAJAtz).
Alisema kuwa sanaa ina wigo mpana sana na kila msanii anatakiwa kuwa mbunifu ili kujiweka tofauti  na msanii mwingine na kujipatia fedha kwa kutumia ubunifu wake.
Kwa mujibu wa Jokate, yeye aliamua kupitia kwenye fani ya urembo na mwaka 2006 alifanikiwa kushika nafasi ya pili katika mashindano ya Miss Tanzania. Alisema kuwa aliamua kutumia umaarufu wake kujipatia maendeleo pamoja na ukweli kuwa alisomea mambo ya siasa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
“Elimu yangu ya mamo ya siasa haina nafasi kwangu, nilianza kuwa mshehereshaji (MC) katika shughuli mbalimbali, nikaingia katika fani ya ubunifu wa mabavi (Kidoti Fashion), nikaanzisha kidoti club ili kupata marafiki ambao tutazungumza lugha moja,” alisema Jokate.
Mrembo huyo hakuishia hapo kwa kuingia katika fani ya utangazaji wa vipndi hasa Chanel O, uigizaji wa filamu, utengenezaji wa nywele, ndala na sasa mwanamuziki.
 “Hii yote ni kutafuta ‘chaneli’ za kupata fedha, nimefanikiwa na sasa nina makubaliano yenye thamani ya Sh 8.5 bilioni na kampuni ya Kichina, Rainbow Shell Craft Company Limited kwa ajili ya kuzalisha na kuuza bidhaa mbalimbali za lebo yake ya Kidoti,” alisema.
Mbali ya Jokate, mbunifu maarufu nchini, Asia Idarous naye aliwataka wasanii kuwa waaminifu na kujitangaza katika shughuli zao ili kupata maendeleo.
Idarous  alisema kuwa msanii ambaye atakuwa mbunifu na kipaji cha hali ya juu, hataweza kupata maendeleo kama atakosa sifa ya uaminifu ambayo mara nyingi uendana na nidhamu katika kazi.
“Mimi nilianza kazi ya ubunifu wa mavazi miaka ya 1980, mpaka leo nafanya kazi hii, wabunifu wengi (hata Jokate) amepitia kwangu, siri kubwa ya mafanikio haya ni uaminifu na nidhamu katika kazi, nimefanikiwa kuanzisha Vazi la Khanga nchini Marekani na Lady in Red, leo hii ni maarufu,” alisema Idarous.
Katibu Mkuu wa Chama cha  Waandishi wa Habari za Sanaa na Utamaduni nchini, (CAJAtz), Hassan Bumbuli alitoa wito kwa wasanii chipukizi kufuata nyayo za Jokate na Idarous ili kuweza kufanikiwa katika kazi zao za sanaa.
Bumbuli alisema kuwa ni vigumu kupata mafanikio katika sanaa bila kuweka wazi kipaji chako hadharani na hapo ndipo vyombo vya habari vitakuona na kuanza kuandika habari zao.


Wakala wa Fowadi wa Hoffenheim Roberto Firmino amethibitisha kuwa Mchezaji huyo anahamia England kwa ajili ya Msimu ujao.
Roger Wittmann, ambae anamwakilisha Nyota huyo mpya anaewika kutoka Brazil mwenye Miaka 23, amekataa kutoboa waziwazi ni Klabu ipi Mchezaji wake huyo atakwenda ingawa hivi karibuni amehusishwa na kujiunga na Manchester United.
Akiongea na Gazeti la Ujerumani, Bild, Wittmann amesema: "Ninachoweza kusema ni kuwa anahamia England!"
Hivi sasa Firmino yuko huko Nchini Chile akiwa na Timu ya Taifa ya Brazil inayocheza Fainali za Copa America, Kombe la Mataifa ya Marekani ya Kusini.


Mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu (kushoto), akiwa na Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo, Dk.Fenellah Mukangala (kulia) aliyekuwa mgeni rasmi katika fainali za mashindano ya Mtemvu CUP yaliyofikia tamati viwanja vya Mwembe Yanga Dar es Salaam jana. Timu zilizoingia ingia fainali hiyo ni Miburani Kata ya 15 na Kata ya 14 ambayo iliibuka kidedea kwa ushindi wa bao 1-0.
Mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu (kushoto), akiwa na Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo, Dk.Fenellah Mukangala (kulia), wakati akizungumza na wananchi baada ya kumalizi kwa fainali hizo.

Nahodha wa Timu ya Kata 14,Uhuru Selemani akiwa ameinua kombe baada ya kukabidhiwa na mgeni rasmi Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo, Dk.Fenellah Mukangala baada ya kuibuka washindi.

Mashabiki wakiwa kwenye fainali hizo.



Mchuano ukiendelea.

Hapa ni kazi tu kwa kwenda mbele.


Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, Akifurahia mara baada ya kutua Bukoba na tayari kuwahutubia wakazi wa mji wa Bukoba leo wakati wa mkutano wa hadhara kwenye Uwanja wa Mashujaa/Uhuru Platform Bukoba leo Jumatatu tarehe 15 june, 2015. Kiongozi huyu ambaye amefuatana na viongozi wenzake wa juu wa chama hicho, yuko kwenye ziara ya kukitangaza chama na sera mpya ya azimio la arusha lenye usasa. Picha na Faustine Ruta, BukobaUmati wa Watu wengi waliudhuria mkutano huo leo Jumatatu katika Uwanja wa Mashujaa mjini Bukoba
Kwa mara ya kwanza Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe ameteta na Wakazi wa Bukoba leo tangu ajiunge na Chama cha ACT.
Wimbo wa Taifa uliimbwa


Kulia ni msanii mkongwe wa Bongo Fleva nchini, Seleman Msindi 'Afande Sele' nae aliambatana na msafara huo mjini Bukoba.
Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo Samson Mwigamba, akiwahutubia wakazi wa Mji wa Bukoba leo wakati wa mkutano wa adhara kwa mara ya kwanza mjini Bukoba leo

MSANII mkongwe wa Bongo Fleva nchini, Seleman Msindi 'Afande Sele' akiteta na Wananchi mjini Bukoba wakati wa mkutano huo wa adhara katika uwanja wa Uhuru Platform

Wananchi waliunga mkono jambo hapa!


Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo, Anna Mghira, akiwahutubia wakazi wa mji wa Bukoba leo wakati wa mkutano wa hadhara kwenye Uwanja wa Uhuru Platform leo Jumatatu juni 15, 2015 Picha na Faustine Ruta, Bukoba



Wakazi wa mji wa Bukoba wakifuatilia mkutano huo wa hadhara kwa makini


Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe akiongea na wakazi wa Mji wa Bukoba leo Jioni jumatatu ya juni 15, 2015

Neno likakolea!

Wakazi wa mji wa Bukoba wakifuatilia mkutano  huo kwa makini
Kwa makini wakimsikiliza Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe

waliotembelea blog