Saturday, February 25, 2017


Image may contain: 2 people, stadium and outdoorDabi ya Kariakoo uliochezwa Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam, Leo ulishuhudia Mtu Simba ikitoka nyuma kwa Bao 1-0 na kuichapa Yanga 2-1.
Yanga walifunga Bao lao Dakika ya 5 kwa Penati ya Simon Msuva iliyotolewa baa Fowadi wao Obrey Chirwa kuangushwa na Beki Novatus Lufunga.

Image may contain: 8 people, people standing, stadium, grass and outdoorDakika ya 55 Simba walibaki Mtu 10 baada ya Mchezaji wao Janvier Besala Bokungu kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu baada ya kulambwa Kadi za Njano 2.
Simba wakasawazisha Bao Dakika ya 66 kupitia Laudit Mavugo aleingizwa Kipindi cha Pili na kufunga Bao la Pili na la ushindi Dakika ya 81 Mfungaji akiwa Shiza Kichuya.
VPL, inayoshirikisha Timu 16, sasa inaongozwa na Simba wenye Pointi 54 kwa Mechi 23 na Yanga ni wa Pili wakiwa na Pointi 49 kwa Mechi 22 huku Azam FC ni wa 3 wakiwa na Pointi 41 kwa Mechi 23.
VIKOSI:
SIMBA:
Daniel Agyei, Janvier Bokungu, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Novaty Lufunga [Shiza Kichuya, 51’], Abdi Banda, James Kotei, Ibrahim Hajib, Muzamil Yassin, Juma Luizio [Said Ndemla, 27’], Laudit Mavugo, Mohammed ‘Mo’ Ibrahim [Jonas Mkude, 57’].

YANGA:
Deogratius Munishi ‘Dida’, Juma Abdul, Mwinyi Haji, Andrew Vincent, Kevin Yondan, Justine Zulu [Juma Mahadhi, 78’], Simoni Msuva, Thabani Kamusoko [Said Juma ‘Makapu’, 45’], Amisi Tambwe [Deus Kaseke, 70’], Obrey Chirwa, Haruna Niyonzima.

REFA:
Mathew Akrama [Mwanza]
WASAIDIZI: Mohammed Mkono [Tanga] na Hassan Zani [Arusha]

Tuesday, February 21, 2017



Kocha wa Man United Jose Mourinho kuelekea mchezo wao wa marudiano wa Europa League dhidi ya St Etienne ya Ufaransa, ameulizwa maswali kuhusu hatma ya nahodha wa Man United Wayne Rooney kama ataondoka katika timu hiyo au atabaki.
Jose Mourinho ambaye inaaminika ndio anaweza akafanya Rooney aondoke mwisho wa msimu kama inavyoripotiwa au akabaki, ameshindwa kuweka wazi kama ataondoka staa huyo au atabaki, lakini amekiri kuwa hawezi kumlazimisha mchezaji kuhama.
“Kuhusu kuondoka unaweza kumuuliza mwenyewe kwa sababu hata mimi siwezi kukuhakikishia kama nitakuwa hapa wiki ijayo, sasa nawezaje kukuhakikishia kuwa mchezaji ataendelea kuwepo msimu ujao, kama Rooney ataamua kuondoka sio kwa sababu mimi nataka aondoke”

“Hicho ndio ninachoweza kukuhakikishia sitaweza kulazimisha legend wa Club hii kwenda sehemu nyingine, hivyo unaweza kumuuliza Rooney mwenyewe kama angependa kumaliza soka lake katika timu hii? lakini mimi nina furaha kuwa nae katika timu”

Wednesday, February 15, 2017


Jana huko Parc des Princes Jijini Paris Nchini France Mabingwa wa huko Paris St Germain waliifumua Barcelona 4-0 katika Mechi ya Kwanza ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UCL, UEFA CHAMPIONS LIGI.
Kwenye Mechi nyingine ya Raundi hiyo Benfica iliichapa Borussian Dortmund 1-0.
Katika Mechi ya PSG na Barca, Bao za PSG zilipigwa na Angel Di Maria, Dakika za 18 na 55, Julian Draxler, 40', na Edinson Cavani, 71'.
PSG walitawala Mechi hii na Barca kupooza mno huku Mastaa wao Lionel Messi, Luis Suarez na Neymar 'wakijificha'.
Kipigo hiki kinaiweka Barca pagumu kufuzu kwenda Robo Fainali na wakishindwa hilo hii itakuwa mara ya kwanza kwao kutotinga Robo Fainali katika Miaka 10.


Jana huko Parc des Princes Jijini Paris Nchini France Mabingwa wa huko Paris St Germain waliifumua Barcelona 4-0 katika Mechi ya Kwanza ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UCL, UEFA CHAMPIONS LIGI.
Kwenye Mechi nyingine ya Raundi hiyo Benfica iliichapa Borussian Dortmund 1-0.
Katika Mechi ya PSG na Barca, Bao za PSG zilipigwa na Angel Di Maria, Dakika za 18 na 55, Julian Draxler, 40', na Edinson Cavani, 71'.
PSG walitawala Mechi hii na Barca kupooza mno huku Mastaa wao Lionel Messi, Luis Suarez na Neymar 'wakijificha'.
Kipigo hiki kinaiweka Barca pagumu kufuzu kwenda Robo Fainali na wakishindwa hilo hii itakuwa mara ya kwanza kwao kutotinga Robo Fainali katika Miaka 10.

Monday, February 13, 2017


UEFA CHAMPIONS LIGI
Raundi ya Mtoano ya Timu 16 

Mechi zote kuanza Saa 4 Dakika 45 Usiku
Mechi za Kwanza
Jumanne 14 Februari 2017

Benfica v Borussia Dortmund
Paris Saint Germain v Barcelona

Jumatano 15 Februari 2017
Bayern Munich v Arsenal
Real Madrid v Napoli

Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UEFA CHAMPIONS LIGI, UCL, inaanza Jumanne Usiku kwa Mechi mbili na Jumatano pia zipo Mechi mbili na kuendelea Wiki ijayo, zote zikiwa ni Mechi za Kwanza za Raundi hiyo.
Jumanne ni huko Portugal wakati Benfica wakiikaribisha BVB Borussia Dortmund na nyingine ni huko Jijini Paris, Paris pale Paris Saint Germain wakicheza na Barcelona.
Jumatano pia zipo Mechi 2 za Raundi hii ambapo huko Germany ni Bayern Munich na Arsenal na nyingine ni kule Santiago Bernabeu Jijini Madrid Nchini Spain kati ya Real Madrid na Napoli ya Italy.

Mechi za Kwanza za Raundi ya Mtoano ya Timu 16 za UCL zitakamilika Wiki ijayo, Jumanne na Jumatano kwa Mechi 4.

Dondoo Muhimu:
Benfica v Borussia Dortmund

Mechi hii itachezwa huko Estádio do Sport Lisboa e Benfica, Lisbon na kuchezeshwa na Refa mzoefu kutoka Italy Nicola Rizzoli.
Timu hizi zimekutana mara 2 Ulaya na kila moja kushinda mara moja.
Benfica watatinga kwenye Mechi hii wakiwakosa Andrija Zivkovic, alie Kifungoni, na Majeruhi Lisandro Lopez huku Jonas akiwa kwenye hatihati kucheza kutokana na maumivu.
Nao BVB watawakosa Majeruhi Mario Götze na Sven Bender huku hatihati ikiwa kwenye maumivu Nuri Şahin na Sebastian Rode.

Paris Saint Germain v Barcelona
Mechi hii ipo ndani ya Parc des Princes Jijini Paris Nchini France na itachezeshwa na Refa Szymon Marciniak kutoka Poland.

Katika Mechi zilizopita, PSG ilishinda mara 2, Sare 3 na Barca kushinda 4 kati yao.

PSG kwenye Mechi hii itamkosa Thiago Motta ambaye yupo Kifungoni wakati Barca watawakosa Majeruhi Arda Turan, Javier Mascherano na Aleix Vidal.

UEFA CHAMPIONS LIGI
Raundi ya Mtoano ya Timu 16

Mechi zote kuanza Saa 4 Dakika 45 Usiku 
Mechi za Kwanza
Jumanne 21 Februari 2017

Bayer 04 Leverkusen v Atlético Madrid
Manchester City v Monaco

Jumatano 22 Februari 2017
FC Porto v Juventus
Sevilla v Leicester City
 

Mechi za Pili
Jumanne 7 Machi 2017

Arsenal v Bayern Munich
Napoli v Real Madrid

Jumatano 8 Machi 2017

Barcelona v Paris Saint Germain
Borussia Dortmund v Benfica


Jumanne 14 Machi 2017
Juventus v FC Porto
Leicester City v Sevilla

Jumatano 15 Machi 2017
Atlético Madrid v Bayer 04 Leverkusen
Monaco v Manchester City


Antonio Conte amesema hapendi 'mzaha'wa Jose Mourinho baada ya Meneja huyo wa Manchester United kudai Chelsea ambao ni Vinara wa EPL, Ligi Kuu England, hawawezi kukamatika kileleni kwa sababu ni Timu 'inayojihami mno!'.
Hivi sasa Chelsea wapo Pointi 10 mbele ya Timu ya Pili Tottenham baada Jana kutoka 1-1 na Burnley huko Turf Moor.
Mourinho, ambae anasifika kwa kuchota akili za Mameneja wapinzani na kuwavuruga, Juzi alidai Chelsea haiwezi kuteleza kutoka kileleni kwa vile 'wanajihami mno' na kushinda kwa kutumia 'kaunta ataki'.
Jana Meneja wa Chelsea Antonio Conte alijibu mapigo kwa kusema: "Hiyo ni hadaa yake. Nina uzoefu kuelewa hilo!"
Mara nyingi Mourinho amekuwa akikwaruzana na Mameneja wenzake kutokana na vijembe vyake vya kuwapandisha munkari ili kushinda vita ya kisaikolojia na muhanga mkuu wa mashambulizi hayo huko nyuma akiwa Arsene Wenger wa Arsenal.

Hata hivyo Conte amegoma kuburutwa kwenye vita hiyo na kujibu: "Sipendi kujibu kuhusu Makocha wengine!" 

EPL – Ligi Kuu England
RATIBA:
Jumatatu Februari 13

2300 Bournemouth v Manchester City
Jumamosi Februari 25
1800 Chelsea v Swansea City
1800 Crystal Palace v Middlesbrough
1800 Everton v Sunderland
1800 Hull City v Burnley
Southampton v Arsenal [IMEAHIRISHWA]
1800 West Bromwich Albion v Bournemouth
2030 Watford v West Ham United
Jumapili Februari 26
1630 Tottenham Hotspur v Stoke City
Manchester City v Manchester United[IMEAHIRISHWA]
Jumatatu Februari 27
2300 Leicester City v Liverpool
Jumamosi Machi 4
1530 Manchester United v Bournemouth
1800 Leicester City v Hull City
1800 Stoke City v Middlesbrough
1800 Swansea City v Burnley
1800 Watford v Southampton
1800 West Bromwich Albion v Crystal Palace
2030 Liverpool v Arsenal
Jumapili Machi 5
1630 Tottenham Hotspur v Everton
1900 Sunderland v Manchester City
Jumatatu Machi 6
2300 West Ham United v Chelsea


Chelsea Leo wameikosa nafasi ya kwenda Pointi 12 mbele baada ya kutoka Sare na Burnley huko Turf Moor.
Chelsea sasa wako Pointi 10 mbele ya Timu ya Pili Tottenham lakini Jumatatu Usiku Manchester City wanaweza kutwaa Nafasi ya Pili na pengo lao na Chelsea kuwa Pointi 8 ikiwa wataifunga Bournemouth Ugenini.

Hii Leo Chelsea walitangulia kufunga Dakika ya 7 kwa Bao la Pedro lakini Robbie Brady akaisawazishia Burnley Dakika ya 24 kwa Frikiki kali.

Matokeo haya yanawaweka Burnley Nafasi ya 12 na kudumisha rekodi yao ya kuwa wagumu mno wakiwa kwao Turf Moor.

Sunday, February 5, 2017



Usiku wa February 5 ndio siku ambayo mchezo wa fainali ya mataifa ya Afrika maarufu kama AFCON 2017 ulichezwa,  mchezo wa fainali ya AFCON 2017 ulikuwa unazikutanisha timu za Misri dhidi ya Cameroon, lakini Cameroon wamefanikiwa kufuta uteja kwa kufungwa fainali mbili na Misri.

Cameroon wamefanikiwa kupata ushindi wa goli 2-1, Nicolas N’koulou alifunga goli la kusawazishia Cameroon dakika ya 58 baada ya Mohamed Elneny kuifungia Misri goli la uongozi dakika ya 22, Vincent Aboubakar ndio alizima ndoto za Misri baada ya dakika ya 88 kufunga goli la ushindi.

Ushindi huo unakuja baada ya Cameroon kufumgwa fainali mbili za AFCON na Misri, alifungwa fainali ya AFCON 2008 goli 1-0 Mohamed Aboutrika akifunga goli hilo, lakini walipoteza fainali ya AFCON 1986, Cameroon wanakuwa wamechukua taji lao la tano la AFCON wakati Misri wanabakia na rekodi yao ya kuchukua mataji nane ya AFCON.

Rekodi nyingine zilizowekwa katika AFCON na Cameroon ni kuwa inakuwa timu ya kwanza kuwahi kuifunga Misri goli katika fainali za AFCON baada ya Ethiopia, huku kocha wa Misri Hector Raul  Cuper akiendeleza rekodi yake mbovu kwa kupoteza fainali yake ya sita katika soka akiwa kama kocha wa timu tofauti.


Ibra akishangilia bao lake MANCHESTER UNITED imewatandika Mabingwa wa England Leicester City 3-0 wakiwa kwao King Power Stadium kwenye Mechi ya EPL, Ligi Kuu England.
Ushindi huu umewabakiza Man United Nafasi ya 6 lakini sasa wapo Pointi 1 nyuma ya Timu ya 5 Liverpool, Pointi 2 nyuma ya Timu ya 4 Arsenal, Pointi 4 nyuma ya Timu ya 3 Man City na Pointi 5 nyuma ya Timu ya Pili Spurs huku Chelsea wakiwa kileleni Pointi 14 mbele ya Man United.

Man United walipata Bao lao la kwanza Dakika ya 41 baada ya Kichwa cha Chris Smalling kuwahiwa na Mkhitaryan kabla Beki wa Leicester Huth kuukuta Mpira na kumtoka Beki mwingine wa Leicester Morgan na kumchambua Kipa Schmeichel.

Sekunde 87 baada ya Bao hilo Man United walikuwa 2-0 mbele kwa Bao la Zlatan Ibrahimovic alieunganisha Krosi ya Valencia.
Hadi Mapumziko Leicester 0 Man United 2.

Kipindi cha Pili kuanza Timu zote zilifanya mabadiliko kwa Leicester kuwaingiza King na Gray kuwabadili Musa na Okazakina huku Man United wakimtoa Marcos Rojo na kumwingiza Daley Blind.
Man United walifunga Bao la 3 Dakika ya 49 kufuatia ushirikiano mwema wa Ibrahimovic na Mkhitaryan kumfungulia Juan Mata kupiga Bao.



http://a1.espncdn.com/combiner/i?img=%2Fphoto%2F2017%2F0205%2Fr178232_1296x518_5%2D2.jpg&w=1006&h=402&scale=crop&cquality=80&location=originBao la Egypt lilifungwa na Mohamed Elneny dakika ya (22')

Huku Nicolas N'Koulou akiisawazishia bao dakika ya (59') kipindi cha pili na dakika za lala salama Vincent Aboubakar aliipa bao dakika ya (88') na mtanange kumalizika kwa 2-1.



Friday, February 3, 2017


MSIMAMO WA LIGI KUU ENGLAND ULIVYO KWA SASA:
PosLogo &TeamPWDLGDPts
1ChelseaChelsea2318233256
2Tottenham HotspurTottenham Hotspur2313822947
3ArsenalArsenal2314542647
4LiverpoolLiverpool2313732446
5Manchester CityManchester City2314451946
6Manchester UnitedManchester United2311931242
7EvertonEverton2310761037
8West Bromwich AlbionWest Bromwich Albion23968233
9Stoke CityStoke City23788-629
10BurnleyBurnley239212-829
11West Ham UnitedWest Ham United238411-1128
12SouthamptonSouthampton237610-527
13WatfordWatford237610-1227
14BournemouthBournemouth237511-926
15MiddlesbroughMiddlesbrough234910-721
16Leicester CityLeicester City235612-1421
17Swansea CitySwansea City236314-2421
18Crystal PalaceCrystal Palace235414-919
19Hull CityHull City234514-2717
20SunderlandSunderland234415-2216


EGYPT wametinga Fainali ya AFCON 2017, Kombe la Mataifa ya Afrika, nah ii ni mara yao ya 9 kufanya hilo na kuikuta Rekodi ya kucheza Fainali nyingi baada ya Jana huko
Stade de I'Amitie, Libreville Nchini Gabon kuibwaga Burkina Faso 4-3 kwa Mikwaju ya Penati Tano Tano kufuatia Sare ya 1-1 katika Dakika 120.
Kipa Vterani wa Egypt, Essam El Hadary, mwenye Miaka 44, ndie alikuwa Shujaa kwa kuokoa Penati ya Bertrand Traore na kuwapa Egypt ushindi.

Katika Mechi hiyo, Egypt walitangulia kufunga kwa Bao la Dakika ya 65 la Mohamed Salah na Burkina Faso kusawazisha Dakika ya 72 kupitia Aristide Bance.
Kwenye Fainali, Egypt watapambana na Mshindi kati ya Ghana na Cameroon wanaopambana Leo huko Libreville, Gabon.
VIKOSI:
BURKINA FASO:
Koffi, Yago, Dayo, B. Koné, Y. Coulibaly, Kaboré, I. Touré, R. Traoré (Diawara 80'), B. Traoré, Bancé (A.Traore 102'), Nakoulma.

EGYPT:
El-Hadary, El Mohamady (Gaber 106'), Hegazy, Gabr, Fathy, Hamed, M. Salah, I. Salah, Said, Trezeguet (Sobhi 85'), Kahraba (Warda 76')

AFCON 2017

RATIBA
Robo Fainali
Jumamosi Januari 28

Burkina Faso 2 Tunisia 0 [RF 1]
Senegal 0 Cameroon 0 [Penati 4-5] [RF 2]

Jumapili Januari 29

Congo DR 1 Ghana 2 [RF 3]
Egypt 1 Morocco 0 [RF 4]
Nusu Fainali
Jumatano Februari 1
Burkina Faso 1 Egypt 1
Alhamisi Februari 2
2200 Cameroon v Ghana
Mshindi wa 3
Jumamosi Februari 4
2200 Burkina Faso v Aliefungwa NF 2
Fainali
Jumapili Februari 5

2200 Egypt v Mshindi NF 2

NCHI ZILIZOWAHI KUTWAA UBINGWA WA AFRIKA:
-Egypt-Mara 7
-Cameroon, Ghana-Mara 4
-Nigeria-Mara 3
-Congo DR-Mara 2
-Zambia, Algeria, Congo, Ethiopia, Ivory Coast, Morocco, South Africa, Sudan, Tunisia-Mara 1


2-1Stefan Savic is proving a problem at the back for Atletico MadridMabingwa Watetezi wa Kombe la Mfalme wa Spain, Copa del Rey, Barcelona usiku  wameichapa Atletico Madrid Bao 2-1 huko Estadio Vicente Calderon Jijini Madrid katika Mechi ya Kwanza ya Nusu Fainali.
Timu hizi zitarudiana Wiki ijayo huko Nou Camp na Mshindi kucheza na Mshindi wa Nusu Fainali nyingine kati ya Deportivo Alaves na Celta Vigo ambao Leo wanacheza Mechi yao ya Kwanza.

Atletico forward Antoine Griezmannheads to score a goalKwenye Mechi ya Jana, Luis Suarez ndie aliifungia Barca Bao la Kwanza katika Dakika ya 7 alipokokota Mpira toka Mstari wa Kati na kufunga kilaini.
Barcelona's Lionel Messi celebrates a goal with Luis Suarez
Dakika ya 33 mzinga wa Lionel Messi kutoka nje ya Boksi uligonga Posti na kutinga na kuwapa Barca Bao la Pili.
Dakika ya 59, Antoine Griezmann akaipa matumaini Atletico baada ya kufunga Bao pekee kwao.
Barcelona's Luis Suarez scores their first goalLA LIGA
Copa del Rey – Nusu Fainali
Jumatano Februari 1

Atletico Madrid 1 Barcelona 1

Alhamisi Februari 2

2300 Celta Vigo v Deportivo Alaves

Mechi za Pili
[Kwenye Mabano Matokeo Mechi ya Kwanza]
Jumanne Februari 7

2300 Barcelona v Atletico Madrid [2-1]

Jumatano Februari 8
2300 Deportivo Alaves v Celta Vigo

waliotembelea blog