Friday, December 9, 2016

RAIS MAGUFULI KUENDELEZA JITIHADA ZA MARAIS WALIOPITA KUWALETEA MAENDELEO WANANCHI.

mako4
Rais John Magufuli akiwapungia wananchi waliofurika kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam wakati alipoingia kwenye uwanja huo kuongoza sherehe  za miaka 55 ya Uhuru Desemba 9, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
mako5
Rais John Magufuli akikagua gwaride katika sherehe za miaka 55 ya uhuru kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es salaam Desemba 9, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
mako2
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiteta na Rais wa Zanzibar, Dkt. Ali Mohammed Shein katika sherehe za miaka 55 ya uhuru kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam Desemba 9, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
mako3 mako4
Makamu wa Rais, Samia Suluhu akisalimiana na  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam kuhudhuria sherehe za miaka 55 ya Uhuru jijini Dar es salaam Desemba 9, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 
mako6
Rais Joh Magufuli akisalimiana na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam kuongoza sherehe za miaka 55 ya Uhuru jijini Dar es salaam Desemba 9, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
mako7 mako8
Makomando wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania wakionyesha  uwezo wao wa kukabiliana na adui bila kutumia silaha za moto katika  maadhimisho ya miaka 55 ya uhuru kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam Desemba 9, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
mako1
Makomando wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania wakionyesha  uwezo wao wa kukabiliana na adui bila kutumia silaha za moto katika  maadhimisho ya miaka 55 ya uhuru kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam Desemba 9, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
……………………………………………………………………..
Na Beatrice Lyimo-MAELEZO-Dar es Salaam
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Tano itaendeleza jitihada zilizoachwa na Serikali za awamu zilizopita   ili kuzidi kuwaletea maendeleo Watanzania.
Ameyasema hayo leo Jijini Dar es Salaam wakati wa maadhimisho ya sherehe za miaka 55 ya Uhuru wa Tanzania bara yaliyofanyika katika uwanja wa uhuru Jijini Dar es Salaam.
Rais Magufuli alisema kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imeanza jitihada za kuboresha huduma za maendeleo ya jamii, ambapo katika bajeti ya mwaka 2016/17 imeamua kutenga asilimia 40 ya bajeti  katika miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo umeme, miundombinu, afya, elimu.
“Mbali na kujiwekea vipaumbele mbalimbali kwa maendeleo ya nchi, kumekuwa na changamoto kadha wa kadha zinazozikabili nchi ikiwemo ufisadi, rushwa ndani ya baadhi ya watendaji” alisema Rais Magfuli
Aidha Rais Magufuli alisema juhudi zinazoendelea kufanywa na Serikali ni kuboresha maslahi kwa watanzania kwa kuchukua hatua mbalimbali za kuwawajibisha wale wote wanaojihusisha na vitendo vya rushwa na ufisadi.
Akifafanua zaidi Rais Magufuli aliwataka watanzania kudumisha amani na kulinda muungano uliyopo kwani amani ni msingi wa maendeleo ya nchi bila amani hakuna maendeleo.
Rais Magufuli pia alitoa wito kwa wantanzania kuendelea kufanya kazi kiwa bidii kwani kila mwananchi ana haki ya kufanya kazi, na kusema kuwa waasisi wa nchi walileta uhuru kwa maendeleo ya nchi kwani Uhuru ni kazi.
“Serikali ya Tanzania imejipanga kufanya kazi, tutafanya kazi kwelikweli, watendaji niliowachagua wanafanya kazi hivyo watanzania kwa ujumla mnatakiwa kuonesha ushirikiano kwao kwa maendeleo ya nchi yetu” alisema Rais Magufuli.
Mbali na hayo Rais Magufuli alisema kuwa ndani ya miaka 55 ya Uhuru Tanzania imepata mafanikio makubwa ambapo Tanzania imelinda Uhuru wa nchi, sambamba na kulinda mipaka iliyopo.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wananchi waliojitokeza katika sherehe za miaka 55 ya Uhuru wa Tanzania Bara katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia wananchi waliohudhuria sherehe za miaka 55 ya Uhuru wa Tanzania Bara katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam mara baada ya kuwasili.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amesimama wakati wimbo wa Taifa ulipokuwa ukipigwa uwanjani hapo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. John Pombe Magufuli akikagua gwaride katika sherehe za miaka 55 ya Uhuru wa Tanzania Bara katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Vikosi mbalimbali vya Majeshi vikipita mbele ya mgeni Rasmi kwa mwendo wa pole na Haraka katika sherehe za miaka 55 ya Uhuru wa Tanzania Bara katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
Kikosi cha Maadhimisho cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania kikionesha gwaride la kimyakimya mbele ya Amiri Jeshi mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika uwanja wa Uhuru.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Mama Fatma Karume mara baada ya kumaliza kuhutubia katika uwanja wa Uhuru.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na wananchi katika uwanja wa Uhuru mara baada ya kumalizika kwa sherehe hizo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitembea pamoja na Askari Polisi ambao huongoza misafara ya viongozi VIP riders mara baada ya kuwasili Ikulu wakati wakitokea katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Rais Mstaafu wa Awamu ya pili Mzee Ali Hassan Mwinyi mara baada ya Kuwasili katika uwanja wa Uhuru.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda mara baada ya kuwasili. 
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akisalimiana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu,Sera,BungeKazi,Ajira,Vijana na Wenyeulemavu Jenister Muhagama mara alipowasili katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam kushiriki nkatika sherehe za Miaka 55 ya Uhuru wa Tanzania bara 


 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akisalimiana na  Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman  alipowasili katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam kushiriki nkatika sherehe za Miaka 55 ya Uhuru wa Tanzania bara

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam katika sherehe za Miaka 55 ya Uhuru wa Tanzania bara zilizofanyika leo

Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri  ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli akiwasili  katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam kuhudhuria katika sherehe za Miaka 55 ya Uhuru wa Tanzania bara zilizofanyika leo


 Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri  ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli akikagua gwaride maalum la Vikosi vya Ulinzi na Usalama mara alipowasili katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam kuhudhuria katika sherehe za Miaka 55 ya Uhuru wa Tanzania bara zilizofanyika leo


Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri  ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli akikagua gwaride maalum la Vikosi vya Ulinzi na Usalama mara alipowasili katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam kuhudhuria katika sherehe za Miaka 55 ya Uhuru wa Tanzania bara zilizofanyika leo
.
Amiri Jeshi Mkuu  na Rais wa Jamhuri  ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli (katikati) akitembea kikakamavu  na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Jenerali Devis Mwamunyange baada ya kukagua gwaride maalum la Vikosi vya Ulinzi na Usalama  katika sherehe za Miaka 55 ya Uhuru wa Tanzania bara zilizofanyika leo katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU


Waamuzi waliochezesha mchezo namba 49 kati ya Yanga na Simba, Martin Saanya na Samweli Mpenzu wametolewa kwenye ratiba ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, huku suala lao likipelekwa kwenye Kamati ya Waamuzi ili ishughulikie tatizo lao kitaalam.

Maamuzi hayo yamefanyika baada ya Kikao cha Kamati ya Usimamizi na Uendeshaji ya Bodi ya ligi, kuwaita na kuwahoji na kuangalia mkanda wa mchezo husika. Kamati imebaini mapungufu mengi ya kiutendaji yaliyofanywa na waamuzi hao, na hivyo kuitaka kamati ya waamuzi ishughulikie.
Pia Mwamuzi Rajabu Mrope aliyechezesha mchezo namba 108 kati ya Mbeya City na Yanga naye ametolewa kwenye Ratiba ya Ligi Kuu ya Vodacom msimu 2016/2017 na kurudishwa kwenye Kamati ya Waamuzi ili waweze kumpangia daraja lengine la uamuzi.

Mrope alitiwa hatiani kwa kosa la kutojiamini mchezoni na kwenye uamuzi wake na kushindwa kuudhibiti mchezo.

Miongoni mwa matatizo ya mwamuzi huyo ni kukubali goli, kisha kukataa na mwisho kukubali tena hali iliyoonyesha kutokujiamini na kusabisha mtafaruku mkubwa katika mchezo huo.

Katika ligi ya Daraja la kwanza, Mwamuzi Thomas Mkombozi aliyechezesha mechi namba 15B kati ya Coastal Union na KMC ameondolewa kwenye orodha ya waamuzi kutokana na kushindwa kuudhibiti mchezo na kutoshirikiana na wasaidizi wake.

Adhabu hiyo ametolewa baada ya Kamati ya usimamizi na uendeshaji wa ligi kuwaita waamuzi wa mchezo huo na kufanya mahojiano nao na kugundua Mkombozi alikuwa na maamuzi mengi bila umakini na hakushirikiana kiufundi na wasaidizi wake. Kutokua makini kulisababisha mchezo huo kumalizika kwa vurugu.

Pia Klabu ya Coastal Union imepewa adhabu ya kucheza bila ya mashabiki kwa mechi mbili za nyumbani na mechi moja ya nyumbani kuchezwa uwanja wa ugenini kwa kosa la mashabiki wa timu hiyo kumshambulia Mwamuzi Thomas Mkombozi na kumsababishia majera ha maumivu makali.
Soma Zaidi Hapa »


EPL, LIGI KUU ENGLAND
RATIBA:
Jumamosi Desemba 10
15:30 Watford vs Everton
18:00 Arsenal vs Stoke City
18:00 Burnley vs Bournemouth
18:00 Hull City vs Crystal Palace
18:00 Swansea City vs Sunderland
20:30 Leicester City vs Manchester City

Jumapili Desemba 11
15:00 Chelsea v West Bromwich Albion
17:15 Manchester United v Tottenham Hotspur
17:15 Southampton v Middlesbrough
19:30 Liverpool v West Ham United

Jumanne Desemba 13

2245 Bournemouth v Leicester City
2245 Everton v Arsenal

Jumatano Desemba 14
2245 Middlesbrough v Liverpool
2245 Sunderland v Chelsea
2240 West Ham United v Burnley
2300 Crystal Palace v Manchester United
2300 Manchester City v Watford
2300 Stoke City v Southampton
2300 Tottenham Hotspur v Hull City
2300 West Bromwich Albion v Swansea City

Jumamosi Desemba 17
1530 Crystal Palace v Chelsea
1800 Middlesbrough v Swansea City
1800 Stoke City v Leicester City
1800 Sunderland v Watford
1800 West Ham United v Hull City
2030 West Bromwich Albion v Manchester United

Jumapili Desemba 18
1630 Bournemouth v Southampton
1900 Manchester City v Arsenal
1900 Tottenham Hotspur v Burnley

Jumatatu Desemba 19
2300 Everton v Liverpool

waliotembelea blog