Saturday, January 9, 2016


Kuna mengi huwa yanaandikwa mitandaoni na kwenye magazeti kuhusu soka mtu wangu wa nguvu, Jumamosi ya January 9 naomba nikusogezee TOP 5 ya headlines stories zilizoandikwa sana mitandaoni Jumamosi ya January 9.
Klabu ya Real Madrid ya Hispania imeingia katika mbio za kuwania saini ya beki wa klabu ya Everton ya Uingereza John Stones, beki huyo alikuwa anawaniwa na klabu ya Chelsea ya Uingereza na dirisha la usajili wa wakati wa majira ya joto Chelsea walijaribu kutuma ofa tatu kwa Everton lakini zilikataliwa.
John-Stones-592491
John Stones
Manchester United inatajwa kuwa katika mipango ya kumshawishi kocha wa klabu ya Paris Saint Germain ya Ufaransa Laurent Blanc ajiunge na klabu yao, kwani bado hawana imani sana na kocha wa sasa wa Man United Louis van Gaal ambaye mkataba wake unamalizika 2017. Blanc aliwahi kuichezea Man United katika kipindi cha mwaka 2001 hadi 2003.
Paris Saint-Germain coach Laurent Blanc gives a press conference at the Parc des Princes stadium in Paris on November 26, 2013, on the eve of the UEFA Champions League football match against Olympiakos. After failing to get the job done in their last group game, Paris Saint-Germain will seek the draw required to qualify for the Champions League last 16 when they host a Kostas Mitroglou-inspired Olympiakos. AFP PHOTO / FRANCK FIFE (Photo credit should read FRANCK FIFE/AFP/Getty Images)
Laurent Blanc
Kocha mpya wa klabu ya Real Madrid ya Hispania Zinedine Zidane ameweka wazi kuwa hawana mpango wa kumuuza staa wa kimataifa wa Ureno Cristiano Ronaldo kwenda katika klabu yoyote, hivyo hiyo ni taarifa ya kuvikatisha tamaa vilabu vya Man United na PSG vinavyohusishwa kumuhitaji nyota huyo “Ronaldo ni zaidi ya kusema hauzwi, roho yake ipo Real Madrid, ikiwa mimi nipo hapa na uhakika kuwa hawezi kwenda popote”
FILE - In this Sept. 16, 2014 file photo, Real Madrid's Cristiano Ronaldo reacts after missing a chance during a Champions League Group B soccer match against Basel at the Santiago Bernabeu stadium in Madrid, Spain. Christopher Renzi, of Rhode Island, had until November 2014, to notify the Portuguese soccer star of a lawsuit in a dispute over an underwear line, but Ronaldo's team refused to accept the legal papers. A U.S. judge has extended the deadline till March 2015. (AP Photo/Daniel Ochoa de Olza, File)
Ronaldo
Klabu ya Arsenal kupitia kwa kocha wake Arsene Wenger imetajwa kuthibitisha kuwa ipo karibu kukamilisha usajili wa kiungoa wa Basle Mohamed Elneny siku kadhaa zijazo “Bado mpango wake ni mgumu kukamilika, lakini tunaweza kukamilisha naweza kusema ndani ya siku mbili au tatu”
Mohamed-Elneny
Mohamed Elneny
Mchezaji bora wa Afrika kwa mwaka 2015 Pierre Emerick Aubameyang amemaliza uvumi wa yeye kuwa katika mpango wa kujiunga na Arsenal na kusema kuwa hana mpango wa kuondoka Borussia Dortmund kwa hivi karibuni.
Pierre-Emerick-Aubameyang-award1
Aubameyang



Mshambuliaji wa kimataifa Gabon ambaye anaichezea klabu ya Borussia Dortmund ya Ujerumani Pierre-Emerick Aubameyang ameingia kwenye headlines mara mbili tofauti. Headlines kubwa ya staa huyo ni juu ya ushindi wake wa tuzo ya mchezaji bora wa Afrika kwa mwaka 2015, lakini ya pili ni kuhusu Yaya Toure anavyoamini kuwa Pierre hakustahili tuzo hiyo.
Toure ambaye ni mshindi mara nne mfululizo wa tuzo ya mchezaji bora Afrika, alikuwa na matumaini ya kutwaa tuzo hiyo kwa mara ya tano ila anashangazwa na shirikisho la soka barani Afrika kudharau mafanikio yake ya kutwaa taji la mataifa ya Afrika na kumpa tuzo Aubameyang, kwani anaamini Kombe hilo halithaminiki.
237606
Pierre -Emerick Aubameyang akikabidhiwa tuzo na rais wa CAF
“Nimesikitishwa sana sana na jambo hili ni aibu kuona Afrika tunavyoichukulia, hatutoi kipaumbele kwa mashindano yetu ya ndani. Nafikiri tumeitia aibu Afrika. Tumeifanya Afrika isionekane muhimu mbele ya macho yetu, tunathamini mafanikio ya nje ya Afrika kuliko ndani ya bara letu”>>> Yaya Toure
Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 32 ameongea hayo baada ya kufanya mahojiano na kituo cha radio cha RFI, nakueleza kushangazwa na ushindi wa Aubameyang katika tuzo hiyo na yeye kupotezewa, licha ya kuwa ametwaa taji la mataifa ya Afrika kama nahodha wa Ivory Coast.

waliotembelea blog