Monday, February 13, 2017


UEFA CHAMPIONS LIGI
Raundi ya Mtoano ya Timu 16 

Mechi zote kuanza Saa 4 Dakika 45 Usiku
Mechi za Kwanza
Jumanne 14 Februari 2017

Benfica v Borussia Dortmund
Paris Saint Germain v Barcelona

Jumatano 15 Februari 2017
Bayern Munich v Arsenal
Real Madrid v Napoli

Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UEFA CHAMPIONS LIGI, UCL, inaanza Jumanne Usiku kwa Mechi mbili na Jumatano pia zipo Mechi mbili na kuendelea Wiki ijayo, zote zikiwa ni Mechi za Kwanza za Raundi hiyo.
Jumanne ni huko Portugal wakati Benfica wakiikaribisha BVB Borussia Dortmund na nyingine ni huko Jijini Paris, Paris pale Paris Saint Germain wakicheza na Barcelona.
Jumatano pia zipo Mechi 2 za Raundi hii ambapo huko Germany ni Bayern Munich na Arsenal na nyingine ni kule Santiago Bernabeu Jijini Madrid Nchini Spain kati ya Real Madrid na Napoli ya Italy.

Mechi za Kwanza za Raundi ya Mtoano ya Timu 16 za UCL zitakamilika Wiki ijayo, Jumanne na Jumatano kwa Mechi 4.

Dondoo Muhimu:
Benfica v Borussia Dortmund

Mechi hii itachezwa huko Estádio do Sport Lisboa e Benfica, Lisbon na kuchezeshwa na Refa mzoefu kutoka Italy Nicola Rizzoli.
Timu hizi zimekutana mara 2 Ulaya na kila moja kushinda mara moja.
Benfica watatinga kwenye Mechi hii wakiwakosa Andrija Zivkovic, alie Kifungoni, na Majeruhi Lisandro Lopez huku Jonas akiwa kwenye hatihati kucheza kutokana na maumivu.
Nao BVB watawakosa Majeruhi Mario Götze na Sven Bender huku hatihati ikiwa kwenye maumivu Nuri Şahin na Sebastian Rode.

Paris Saint Germain v Barcelona
Mechi hii ipo ndani ya Parc des Princes Jijini Paris Nchini France na itachezeshwa na Refa Szymon Marciniak kutoka Poland.

Katika Mechi zilizopita, PSG ilishinda mara 2, Sare 3 na Barca kushinda 4 kati yao.

PSG kwenye Mechi hii itamkosa Thiago Motta ambaye yupo Kifungoni wakati Barca watawakosa Majeruhi Arda Turan, Javier Mascherano na Aleix Vidal.

UEFA CHAMPIONS LIGI
Raundi ya Mtoano ya Timu 16

Mechi zote kuanza Saa 4 Dakika 45 Usiku 
Mechi za Kwanza
Jumanne 21 Februari 2017

Bayer 04 Leverkusen v Atlético Madrid
Manchester City v Monaco

Jumatano 22 Februari 2017
FC Porto v Juventus
Sevilla v Leicester City
 

Mechi za Pili
Jumanne 7 Machi 2017

Arsenal v Bayern Munich
Napoli v Real Madrid

Jumatano 8 Machi 2017

Barcelona v Paris Saint Germain
Borussia Dortmund v Benfica


Jumanne 14 Machi 2017
Juventus v FC Porto
Leicester City v Sevilla

Jumatano 15 Machi 2017
Atlético Madrid v Bayer 04 Leverkusen
Monaco v Manchester City


Antonio Conte amesema hapendi 'mzaha'wa Jose Mourinho baada ya Meneja huyo wa Manchester United kudai Chelsea ambao ni Vinara wa EPL, Ligi Kuu England, hawawezi kukamatika kileleni kwa sababu ni Timu 'inayojihami mno!'.
Hivi sasa Chelsea wapo Pointi 10 mbele ya Timu ya Pili Tottenham baada Jana kutoka 1-1 na Burnley huko Turf Moor.
Mourinho, ambae anasifika kwa kuchota akili za Mameneja wapinzani na kuwavuruga, Juzi alidai Chelsea haiwezi kuteleza kutoka kileleni kwa vile 'wanajihami mno' na kushinda kwa kutumia 'kaunta ataki'.
Jana Meneja wa Chelsea Antonio Conte alijibu mapigo kwa kusema: "Hiyo ni hadaa yake. Nina uzoefu kuelewa hilo!"
Mara nyingi Mourinho amekuwa akikwaruzana na Mameneja wenzake kutokana na vijembe vyake vya kuwapandisha munkari ili kushinda vita ya kisaikolojia na muhanga mkuu wa mashambulizi hayo huko nyuma akiwa Arsene Wenger wa Arsenal.

Hata hivyo Conte amegoma kuburutwa kwenye vita hiyo na kujibu: "Sipendi kujibu kuhusu Makocha wengine!" 

EPL – Ligi Kuu England
RATIBA:
Jumatatu Februari 13

2300 Bournemouth v Manchester City
Jumamosi Februari 25
1800 Chelsea v Swansea City
1800 Crystal Palace v Middlesbrough
1800 Everton v Sunderland
1800 Hull City v Burnley
Southampton v Arsenal [IMEAHIRISHWA]
1800 West Bromwich Albion v Bournemouth
2030 Watford v West Ham United
Jumapili Februari 26
1630 Tottenham Hotspur v Stoke City
Manchester City v Manchester United[IMEAHIRISHWA]
Jumatatu Februari 27
2300 Leicester City v Liverpool
Jumamosi Machi 4
1530 Manchester United v Bournemouth
1800 Leicester City v Hull City
1800 Stoke City v Middlesbrough
1800 Swansea City v Burnley
1800 Watford v Southampton
1800 West Bromwich Albion v Crystal Palace
2030 Liverpool v Arsenal
Jumapili Machi 5
1630 Tottenham Hotspur v Everton
1900 Sunderland v Manchester City
Jumatatu Machi 6
2300 West Ham United v Chelsea


Chelsea Leo wameikosa nafasi ya kwenda Pointi 12 mbele baada ya kutoka Sare na Burnley huko Turf Moor.
Chelsea sasa wako Pointi 10 mbele ya Timu ya Pili Tottenham lakini Jumatatu Usiku Manchester City wanaweza kutwaa Nafasi ya Pili na pengo lao na Chelsea kuwa Pointi 8 ikiwa wataifunga Bournemouth Ugenini.

Hii Leo Chelsea walitangulia kufunga Dakika ya 7 kwa Bao la Pedro lakini Robbie Brady akaisawazishia Burnley Dakika ya 24 kwa Frikiki kali.

Matokeo haya yanawaweka Burnley Nafasi ya 12 na kudumisha rekodi yao ya kuwa wagumu mno wakiwa kwao Turf Moor.

waliotembelea blog