Tuesday, September 3, 2013



Kundi la watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wakiwa na bunduki, wamefunga mtaa na kupora fedha na simu za kiganjani katika maduka 11 eneo la Mvumoni Madale, kata ya Wazo na Tegeta Kibaoni, Manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Mashuhuda wa tukio hilo, wakizungumza jana na NIPASHE, walisema tukio hilo lilitokea juzi Jumapili, majira ya saa 1:30 usiku.

Hata hivyo, kumekuwa na taarifa za kukanganya kati ya wananchi walioathirika kutokana na mkasa huo ambao wanadai wameporwa simu na fedha kwa viwango tofauti katika maduka 11 huku Jeshi la Polisi likisema kuwa maduka matatu pekee ndiyo yamevamiwa na kuporwa kiasi cha Sh. 300,000.

Katika eneo la Mivumoni Madale kwenye maduka yanayofahamika kama maduka 11, majambazi hao walivamia na kupora kwenye maduka sita.

Neema Charles, muuzaji wa Super Market, alisema akiwa anahudumia wateja alishangaa baada ya watu watatu kuingia na kumrudisha mteja aliyekuwa anatoka ndani na kutoa amri ya watu wote kulala chini na kutoa fedha na simu.

“Kati ya watu watatu walioingia ndani mmoja alivaa kininja akaficha sura, alikuwa na bunduki aliyotumia kupiga watu, walipora simu, pochi, fedha za mauzo na fedha zetu binafsi…nilikuwa na Sh. 250,000 kwenye pochi zimekwenda,” alisema.

Alisema walipekua kila mahali na kupora fedha, simu na pochi huku wakiwatolea lugha ya matusi na kuwataka kila mmoja kunyamaza kimya.

Alisema wakati wanaendelea na kupekua, aliwaangalia na ndipo alichomwa na kitu chenye ncha kali karibu na bega la mkono wa kulia na baada ya kupora walikwenda kwenye maduka mengine na tukio hilo lililochukua dakika 20.

Poni Abdalah, mmiliki wa saluni ya kike, alisema alikuwa anahudumia wateja sita na watoto wanne, mara aliingia mtu mmoja na kuwataka kukaa kimya na kutotoka nje.

“Wakati anatoa amri hiyo mmoja wa wateja alikuwa na mwanaye aliyetoka nje akatoka kumfuata, alivutwa na kusukumwa ndani na tulikaa kimya baada ya kujua tumevamiwa,” alisema.

Alisema jirani yake kuna maduka ya M -pesa na Tigo-pesa nayo yaliporwa kiasi cha Sh. milioni 1.5, na kuwafungia ndani na kuondoka na funguo. Alifafanua kuwa baada ya majambazi kuondoka iliwabidi wavunje mlango ili kumtoa muuzaji aliyefungiwa ndani.

“Baada ya kuona bibi aliyekuwa mteja kwenye duka langu kaporwa simu, nilizima taa ya dukani na kukaa kimya ikawa pona yangu, baada ya dakika 20 nikatoka nje nikakutana na dada mmoja ambaye alikuwa mteja kwenye duka la dawa amenyang’anywa funguo wa gari yake na watu hao,” alisema Amos Joseph.

Katika eneo la Tegeta, mtaa wa Tegeta Ndevu, Mariamu William, alisema majambazi hayo yalifika dukani humo kama wateja na kumtaka kaka yake, Emmanuel William, muuzaji kutoa fedha huku wakiwa wamemshikia bunduki.

“Kabla ya kuamuru wenye maduka kuwapa fedha walipiga risasi mbili hewani, alivyokuwa anachelewa kuwapa walichotaka walimpiga na kitako cha bunduki,” alisema.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Kinondoni, Camillus Wambura, alithibitisha kuwapo kwa tukio hilo na kusema kuwa maduka yaliyoporwa ni matatu katika eneo la Madale mawili na moja ni eneo la Tegeta Kibaoni ambayo yaliporwa kiasi cha Sh. 300,000.

Wambura alisema hana taarifa za kuporwa maduka 11 na kuongeza kuwa polisi wanaendelea kuwasaka majambazi hayo.

MWANAMKE ABAMBWA NA SARE ZA JESHI
JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limemkamata mwanamke aliyefahamika kwa jina la Saida Mohamed (30), mkazi wa Mwasonga Kigamboni akiwa na sare za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ). Kamanda wa kanda hiyo, Suleiman Kova, alisema jana kuwa mwanamke huyo alikamatwa juzi saa 4:00 asubuhi eneo la Mwasonga Kigamboni, wilayani Temeke.

Kova alisema, mwanamke huyo alikuwa na sare za jeshi hilo ambazo ni suruali saba za kombati, mashati saba ya kombati, kofia 10 za kombati, mashati mawili mepesi, fulana mbili, kofia aina ya bereti moja, viatu jozi tatu, ponjoo moja, koti moja, begi moja la kuwekea nguo za kipolisi pamoja na mikanda miwili ya kijeshi.

Aidha, Kamanda Kova alisema mwanamke huyo anaendelea kushikiliwa na jeshi hilo kwa mahojiano.

Katika tukio lingine, watu wawili wanashikiliwa na jeshi hilo kwa kukutwa na mihuri 27 na nyaraka mbalimbali za serikali pamoja na za taasisi binafsi wakizitumia kufanyia utapeli kwa wananchi.

Kova aliwataja watu hao kuwa ni Sadraki Mwangwi (27), mkazi wa Mbagala Sabasaba na Samuel Mwangwi (38), mkazi wa Kimara Baruti.

Alisema, waliwakamata watu hao wakiwa na nyaraka hizo wakizitumia kuwatapeli wananchi wa sehemu mbalimbali jijini wakiwa wanakata risiti za serikali kama vile bima za magari, risiti za benki, manispaa na halimashauri. Aliongeza kuwa watu hao walikuwa kama mawakala wa kutoa risiti ambazo wananchi walizihitaji kwa bei yoyote ile.

Kova alisema katika msako huo walifanikiwa kuwakamata watu 120 kwa makosa mbalimbali na kusema msako huo ni endelevu.


Mhhh Aiseee Mie sisemi Kitu hapo ...Je wewe Unasemaje ....Je wewe  unaonaje wamefanana ama No?

SIKU chache baada ya tukio la wizi mkubwa wa fedha katika Benki ya Habibu mjini Dar es Salaam, siri nzito zimeanza kuvuja kuwa polisi wanadaiwa kuhusika katika tukio hilo kwa kuhujumu kamera za usalama za CCTV zinazomilikiwa na jeshi hilo. 
 
Katika tukio hilo, watu wanaodaiwa kuwa majambazi walipora dola za Marekani 20,000 ambazo ni sawa na Sh milioni 32 za Tanzania.

Katika tukio hilo, Polisi Mkoa wa Ilala inamshikilia askari mmoja kwa kosa la kuhusika katika tukio hilo kutokana na kushindwa kuchukua hatua za haraka wakati tukio linatokea.

Habari za uhakika kutokana ndani ya jeshi hilo, zinasema siku ya tukio polisi waliokuwa zamu kuongoza mitambo hiyo, kwa namna moja au nyingine wanadaiwa kufanya hujuma hiyo, kwa lengo la kupoteza mawasiliano na maeneo mengi ya polisi.

Chanzo chetu hicho, kiliongeza kuwa siku ya tukio eneo lote la mzunguko wa barabara ya Uhuru na maeneo ya jirani na Kiwanda cha Bia Tanzania (TBL), sehemu zote hazikuwa na huduma ya kamera za usalama, jambo ambalo si la kawaida kutokea.

“Hatua iliyofikia sasa ni mbaya, huwezi amini siku ya tukio kamera za CCTV zinazotumiwa na polisi zilizimwa kabisa, kitendo hiki kilisababisha polisi makao makuu wasijue nini kinachoendelea pale.

“Ndiyo maana utaona kuna askari mmoja anashikiliwa katika tukio lile, haiwezekani kituo kikuu kishindwe kubaini uwapo wa tukio hili, wakati kuna mawasiliano ya kutosha, umefika muda wa kulisafisha jeshi letu kwa kasi,” kilisema chanzo chetu.

Chanzo hicho, kilisema mitambo ya kamera hizo, ilizinduliwa na Rais mstaafu Benjamin Mkapa mwaka 2004 na imekuwa ikifanya kazi bila matatizo yoyote.

“Nimekuwapo hapa tangu mwaka 2004, kamera hizi zilipozinduliwa rasmi na hazijawahi kuharibika hata siku moja, iwe siku ya tukio zisifanye kazi,” kilihoji chanzo chetu.

Askari aliyekamatwa katika tukio hilo, anadaiwa anafanya kazi katika kituo cha Oysterbay Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Marietha Minangi, alithibitisha kukamatwa kwa askari huyo.

Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alipoulizwa na MTANZANIA jana, alisema ameipokea taarifa hiyo na wanaifanyia kazi haraka iwezekanavyo.

“Taarifa hii tumeipokea, tunaifanyia kazi haraka sana ili kupata ukweli, naomba tuwe na subira,” alisema kwa kifupi Kamishna Kova.

Alisema bado polisi wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo na kwamba watu waliokamatwa watafikishwa mbele ya vyombo vya dola.

MJADALA wa Bunge jana jioni ulitawaliwa na kauli nzito baada ya wabunge kadhaa wa Chama cha Mapinduzi (CCM), kutuhumiana kuhusika na ubadhirifu katika vyama vya ushirika nchini.

Hoja hiyo iliibuka wakati Bunge likijadili muswada wa sheria ya vyama vya ushirika wa mwaka 2013 uliowasilishwa na Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Balozi Christopher Chiza.
Aliyekuwa wa kwanza kuwasha moto huo baada ya mapumziko ya mchana alikuwa mbunge wa Busega, Dk.Titus Kamati (CCM), ambaye alisema waziwazi kuwa wanasiasa ndio wezi wa vyama vya ushirika.
Dk. Kamani alihoji ni kwa nini serikali inapata kigugumizi kuwachukulia hatua wahusika na kusisitiza kuwa hapo kuna kulegalega kumaliza ufisadi katika ushirika.
“Wanasiasa hawa kwa nafasi zao wameingia kwenye ushirika na kufanya ufisadi lakini serikali inashindwa kuwachukulia hatua.
“Huku ni kulegalega na ndio maana hata tumeshindwa kuwataja wauza dawa za kulevya, waziri anaishia kusema tunayo orodha,” alisema.
Alihoji ni kwa nini sasa serikali isiige mfano wa China wa kuwafunga na hata ikibidi kuwanyonga watuhumiwa wa ufisadi wa vyama hivyo ikithibitika bila kujali nafasi zao kwenye siasa.
Mbunge wa Mpanda Vijijini, Moshi Kakoso (CCM), ndiye aliyefuata na kuchafua hali ya hewa kwa kumtuhumu Mkurugenzi wa Bodi ya Tumbaku Nchini (TTB) kufanya ufisadi mkubwa ambao serikali inaujua lakini imeamua kuunyamazia.
Bila kumtaja kwa jina lakini alikuwa akimlenga mbunge mwenzake wa Namtumbo, Vita Kawawa, akisema kuwa anajilipa mshahara mara mbili ya ule uliopitishwa na serikali.
Alisema kuwa analipwa sh milioni mbili za mawasiliano na anachukua dola 1200 (zaidi ya sh milioni 1.8) kwa ajili nyumba badala ya sh 800,000 zilizoidhinishwa.
Mbunge huyo alisema mwenyekiti huyo anayajua mambo hayo na ndiye aliyeidhinisha.
“Nina uhakika na ninachozungumza, waziri nilishamletea taarifa juu ya jambo hili lakini amenyamaza, hivi hapa tunategemea ushirika utakuwa hai wakati mabosi wanautafuna?” alihoji.
Wakati mbunge huyo anaendelea kuzungumza, Kawawa akitaka kumpa taarifa juu ya jambo analolizungumza.
Kawawa alisema muda wake wa kuwa mwenyekiti kwenye bodi hiyo uliisha Juni 31 mwaka huu, hivyo ni vema mbunge mwenzake akatoa ushahidi wake juu ya tuhuma za watendaji wa bodi husika.
Baada ya Kawawa kumaliza, Kakosa aliendelea kuchangia ambapo alikataa taarifa hiyo kwa madai ana ushahidi wa kile kilichofanyika.
Mara baada ya Kakoso kumaliza kuchangia muswada huo, mbunge wa Kondoa Juma Nkamia alipewa fursa ya kutoa taarifa ambapo alisema tuhuma zilizotolewa na Kakoso dhidi ya Kawawa ni nzito sana na Bunge lipate fursa ya kuangalia jambo hilo pamoja na mhusika kutoa ushahidi.
Naibu Spika, Job Ndugai, alisema ofisi ya Bunge iko wazi kwa Kakoso kuwasilisha ushahidi wake juu ya kile alichosema.
Mara baada ya Ndugai kutoa ufafanuzi huo, alimpa nafasi mbunge wa Sikonge, Saidi Nkumba (CCM), ambaye alimtuhumu Kakoso kwa kushindwa kuliambia ukweli Bunge kuwa yeye ni Mwenyekiti wa Chama Kilele (APEX) ambacho kinapigiwa kelele kuwa kinawanyonya wakulima.
Alisema wakiwa Dar es Salaam kwenye vikao vya kamati za Bunge, Katibu wa Apex, aliitwa katika kamati kama mdau ambapo alipobanwa juu ya wizi unaofanyika kwenye chombo hicho alisema serikalini ikiiba kelele zinapigwa lakini APEX ikiiba kidogo kelele zinakuwa kubwa sana.
“Katibu wa Kakoso ndiye aliyetuambia hivyo. Huu ni wizi, sisi hatuwezi kukubaliana na jambo hilo, serikali haivumilii wizi, huyu Kakoso anasema APEX ni mkombozi lakini pale Tabora wamewaibia wananchi bilioni 16, hivi kweli hizi si fedha nyingi?
“Hii APEX ni lazima ifutwe, wenye tamaa ya kwenda kwenye ushirika ni vema waache siasa, na wenye ushirika ni vema wakabaki huko huko.”
Alibainisha kuwa wizi unaofanyika kwenye vyama vya ushirika unasababishwa na wanasiasa ambao wana kinga za kisiasa ndiyo maana wanaendelea kutafuna fedha za wananchi.
Mbunge wa Kasulu Mjini, Moses Machali, alisema wabunge wana taarifa za wizi wanatoa taarifa hapa bungeni lakini hakuna wanachokifanya.
“Yaani kila kukicha mnalea wizi halafu leo hii mnaanzisha tume za kuwanyonya wakulima, kule kwangu wakulima waliuza tumbaku, msianzishe vitu vya ajabu ajabu…, huu ni wizi mtu, msituletee wizi hapa kwa kubadilisha majina ya vitu,” alisema.
Tundu Lissu wa Singida Mashariki (CHADEMA) alisema sababu kubwa ya kuporomoka kwa ushirika ni serikali kuuingilia, kuudhibiti na kuuporomosha.
Alisema serikali ilianza kuvuruga mambo 1966 sheria za ushirika ilibadilishwa na msajili wa vyama vya ushirika alipewa mamlaka ambayo alianza kuyatumia vibaya ambapo mwaka 1976 alipigwa marufuku zikaja bodi za mazao.
Mwaka 1982 vilirejeshwa vyama vya ushirika lakini mamlaka yake yalikuwa yakitolewa na mrajis ambaye ni serikali.
Mbunge wa Nzenga, Andrew Kigwangalah, aliibua upya mzozo wa awali kwa kuanika nyaraka za ufisadi katika TTB kama ilivyokuwa imedokezwa awali na Kakoso.
Kingwangalah ambaye alidai kuwa hatarudi nyuma kuwataja mafisadi na wauza dawa za kulevya alisema kuwa kodi ya nyumba ya mwenyekiti wa bodi inalipiwa gahara tofauti na ile iliyoidhinishwa.
Alionyesha nyaraka kadhaa za malipo ya viongozi wa bodi hiyo na kisha kumvaa Nkumba akisema kuwa tatatizo la nchi hii si Apex bali ni rushwa, wizi, ubadhirifu halafu watu wanaona wizi wanaungalia badala ya kuchukua hatua.
“Waliobaki kwenye ushirika ni wezi watupu, wazalendo wameisha, wezi tunawajua lakini hatuwawajibishi wala kuwachukulia hatua.
“Nkumba ni msaidizi wa Kawawa katika bodi ya tumbaku anajua ukaguzi haujafanyika na ukifanyika wao hawatasalimika ndiyo maana wanaanza kuipiga vita Apex.
“Kuna watu wanatumiwa na kampuni za ubebari ambazo zilikuwa zikisafirisha tumbaku na kusambaza pembejeo, hawa sasa wanaona hatari za kampuni zao ndiyo maana zinawatumia wabunge ili APEX ifutwe, tuwe makini na wabunge waovu,” alisema.
Mzozo huo ulidumu huku Kawawa na Nkumba wakisimama kujitetea bila mafanikio hatua iliyomlazimu Naibu Spika wa Bunge kutoa nafasi kwa baadhi ya wabunge kuomba viongozi, lakini akaliahirisha Bunge hadi leo ambapo atatoa uamuzi wake.
Mapema asubuhi, wabunge walipendekeza wabadhirifu wa mali za ushirika walazimishwe kufidia hasara iliyotokea pamoja na kufilisiwa mali zao.
Pendekezo hilo limetolewa na Nkumba alipokuwa akisoma hotuba ya Mwenyekiti wa 
Kamati ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, Peter Msolla.
Nkumba alisema ushirika umewakatisha tamaa wananchi kutokana na ubadhirifu wa viongozi wake hivyo ujio wa sheria hiyo utakuwa mkombozi.
Aliongeza kuwa watuhumiwa wa ubadhirifu wa ushirika wafikishwapo mahakamani mashauri yake yamekuwa hayathibitiki licha ya taarifa za fedha kuonyesha kuwa upotevu fedha upo; ni vema kuwepo na utaratibu wa kuwabana wahusika.
Nkumba alisema vyama vya ushirika vimekuwa vikikaguliwa na Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (Coasco) ambalo halifanyi kazi zake vizuri na kuitaka serikali kuweka utaratibu mzuri ikiwemo kuhusishwa kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za serikali.
Waziri wa Kilimo, Chiza alisema kuundwa kwa sheria hiyo litakuwa suluhisho la matatizo ya ushirika nchini.
Alisema serikali inalenga kuifuta sheria ya vyama vya ushirika namba 20 ya mwaka 2003 na inaamini sheria mpya itaimarisha, kuendeleza na kuufufua ushirika.
Chiza alisema sheria ya ushirika ya mwaka 2013 ina lengo la kutekeleza sera ya maendeleo ya ushirika ya mwaka 2002, inayovitaka  vyama vya ushirika imara, endelevu na vyenye kukidhi mahitaji ya wanachama kiuchumi chini ya mazingira ya soko huria.
 Mkuu wa mkoa wa kagera akiongea na wageni waalikwa katika ufunguzi wa kiwanda cha kutengeneza nguo Endeavour group ltd kilichopo kata ya kibeta bukoba manispaa,mkuu wa mkoa amewataka wahaya wote wenye uwezo wa kuwekeza waje waitengeneze bukoba sasa,kanal massawe amesema duniani kote ukienda utamkuta muhaya, na wanauwezo mkubwa,sasa umefika wakati wa kuwekeza nyumbani,amewataka wawe na uchungu na bukoba,ambayo asilimia kubwa ya ya majengo yake yamechakaa,na nyumba nyingi mabati yamekuwa mekundu ,na hicho ni kielelezo tosha kuwa bukoba inapaswa kubadilika.
 kati ni mkurugenzi wa kiwanda akimtambulisha meneja wa kiwanda kwa mgeni rasmi kanal massawe
 mgeni rasmi akiangalia namna mashine za kushona nguo zinavyotumika ,na kufanya kazi kwa haraka zaidi na kwa muda mfupi
                                  picha ya pamoja mbele ya jengo la kiwanda cha kutengeneza nguo
 mwenye miwani mzee mashasi,mkuuwa chuo kikuu jokuko keshomshahara akiteta na mgeni rasm
 mkuu wa mkoa kagera kanal Fabian massawe akikata utepe kuzindua rasmi kiwanda cha kutengeneza nguo
                                     mkurugenzi wa kiwanda akitoa maelezo kwa mgeni rasmi
 Ndugu paskazia barongo, mmoja mwa wawekezaji bukoba maispaa akiwa na mdau wa maendeleo manispaa ya bukoba
                                mgeni rasmi akiangalia nguo mbalimbali zinazotengenezwa kiwandani hapo
 kiwnda hiki kinashona sare za shule,masuti, nguo za watoto ,wanawake na wanaume,sare za mashirika ,makampuni,mahotel, sare za viwandani nk
                                  wageni mbalimbali waliofika katika uzinduzi rasmi wa kiwanda

waliotembelea blog