Wednesday, April 15, 2015


Mabingwa Watetezi wa International Champions Cup, Manchester United, Mwezi Julai huko USA watakuwa na kazi ya kutetea Taji lao walilotwaa Mwaka Jana wakati Mashindano haya yatakapochezwa tena yakishirikisha Vigogo wa Ulaya.
Zipo Timu 10, wakiwemo Mabingwa Man United, ambazo zitashiriki na nazo ni Barcelona, Chelsea, PSG, Porto na Fiorentina, kutoka Ulaya pamoja na Klabu ya Mexico, Club America, na Klabu za Marekani New York Red Bulls, LA Galaxy na San Jose Earthquakes.

Mashindano hayo ya ICC yanatarajiwa kuanza Julai 11 na kumalizika Agosti 5 kabla tu ya Misimu mipya ya 2015/16 kuanza huko Ulaya.
Mwaka Jana kwenye Mashindano haya, Mechi kati ya Man United na Real Madrid, ambayo Man United walishinda 3-1, iliweka Rekodi huko Michigan, USA kwa kuhudhuriwa na Washabiki wengi mno ambapo Watu zaidi ya 109,000 walisheheni Uwanjani.
Mwaka Jana, chini ya Kocha mpya Louis van Gaal, Man United iliitwanga Liverpool 3-1 kwenye Fainali na kubeba Kombe.
Kwenye Fainali hiyo, Liverpool walitangulia kwa Penati ya Steven Gerrard lakini Man United wakajibu kwa Bao 3 za Wayne Rooney, Juan Mata na Jesse Lingard.
Kwa kuelekea Fainali, Man
United walizibwaga Klabu za Italy, AS Roma na Inter Milan, na kisha kuitwanga Real Madrid.

TIMU ZITAKAZOSHIRIKI:
Chelsea
Manchester United
Barcelona
Club America
Fiorentina
LA Galaxy
New York Red Bulls
Paris Saint-Germain
Porto
San Jose Earthquakes



Kipindi cha pili dakika ya 67 Luis Suarez alipenyeza kwa mapeki n kuachia shuti na kumfunga kipa wa PSG baada ya kupenyezewa mpira na Martín Montoya na kufanya 2-0 dhidi Bayern Munich ya Ujerumani. 3-1...suarez akipongezwa baada ya kufunga bao mbili peke yake usiku huuBao la Tatu lilifungwa tena na Luis Suarez dakika ya 78 na kufanya 3-0. Bao la PSG lilifungwa na Gregory Van Der Wiel dakika ya 82 mpira ukitenguliwa njia na Javier Mascherano na kufanya 3-1.Neymar akishangilia bao lake la dakika ya 18 baada ya kuitangulizia bao Barcelona kwa kufanya 1-0 dhidi ya PSG katika kipindi cha kwanza. Neymar akishangilia bao lake la nne kwa msimu huu wa Klabu Bingwa Ulaya kwenye mechi nane alizocheza.Neymar akipongezwa na Lionel Messi baada ya kufunga bao, Neymar alipewa pasi na Messi kisha kufunga bao hilo la kipindi cha kwanza.Neymar akimkumabtia staa MessiLaurent Blanc wa PSG akipagawaDavid Luiz akijificha Uso!1-0VIKOSI:
PSG: Sirigu, van der Wiel, Thiago Silva, Marquinhos, Maxwell, Rabiot, Cabaye, Matuidi, Lavezzi, Cavani, Pastore.
Akiba: Douchez, Camara, Lucas Moura, Bahebeck, Digne, Luiz, Kimpembe.
Barcelona: Ter Stegen, Montoya, Pique, Mascherano, Jordi Alba, Rakitic, Busquets, Iniesta, Messi, Suarez, Neymar.
Akiba: Bravo, Xavi, Pedro, Rafinha, Bartra, Adriano, Mathieu.
Referee: Mark Clattenburg


Martinez celebrates putting Porto into a commanding 3-1 lead as Bayern have a night to forget in PortugalFC Porto walipata bao la kwanza kupitia kwa Ricardo Quaresma dakika ya 3 kwa mkwaju wa penati na bao la pili dakika ya 10 kupitia kwa mchezaji huyo huyo Ricardo Quaresma. Bao la Bayern Munich lilifungwa na Thiago Alcantara dakika ya 28 kipindi hicho cha kwanza na kufanya 2-1. 
Kipindi cha pili Jackson Martínez wa FC Porto alipewa pasi safi na Alex Sandro na kukatiza kwa mabeki na kumkaanga kipa wa Bayern na kumfunga bao la tatu na kufanya 3-1 dhidi ya Bayern Munich.
Jackson Martínez anafikisha bao 6 kwenye michezo 7 aliyocheza ya Klabu Bingwa Ulaya Msimu huu.
Porto earned an impressive 3-1 Champions League first leg victory against Bundesliga champions Bayern Munich on Wednesday night
Porto wameshinda 3-1 dhidi ya Vinara wa Ligi ya Ujerumani
Bayern goalkeeper Manuel Neuer brings down Porto striker Jackson Martinez to concede a third minute penalty 
Bayern kipa Manuel Neuer akimwangusha chini straika wa Porto Jackson Martinez
The Bayern players surround referee Carlos Velasco Carballo following his decision to award Porto a spot-kick
Wakimznga Mwamuzi
The 31-year-old forward had   
1-0
German star Neuer dives in the wrong direction as Quaresma calmly slot away the spot-kick with just three minutes on the clock
Kipa Neuer akifungwa bao na  Quaresma
Bayern boss Pep Guardiola looks perplexed as his side fall two goals behind during the early stages of the Champions League clash
Meneja wa Bayern Pep Guardiola kichwa chini baada ya kupigwa bao 3-1Porto's head coach Julen Lopetegui (left) shouts instructions to his team during the Champions League first-leg
Kocha wa FC Porto Julen Lopetegui akitafuta pointi
FC Porto vs Bayern Munich
VIKOSI:

Porto: Fabiano, Danilo, Maicon, Martins Indi, Alex Sandro, Herrera, Casemiro, Torres, Quaresma, Martinez, Brahimi.
Akiba: Helton, Quintero, Reyes, Evandro, Hernani, Ruben Neves, Aboubakar.

Bayern Munich: Neuer, Rafinha, Boateng, Dante, Bernat, Lahm, Alonso, Thiago, Muller, Lewandowski, Gotze.
Akiba: Reina, Pizarro, Gaudino, Rode, Badstuber, Weiser, Lucic.
Refa: Carlos Velasco Carballo


Kocha wa Klabu ya Bundesliga ya Germany Borussia Dortmund, Jurgen Klopp, ametangaza kuachana na Klabu hiyo inayosuasua Msimu huu.Kocha huyo ambae Mkataba wake ulikuwa unamalizika 2018 amesema ataondoka Klabuni hapo mwishoni mwa Msimu. Klopp, mwenyevMiaka 48, alijiunga na Dortmund Mwaka 2008 na kuiwezesha kutwaa Ubingwa wa Bundesliga Mwaka 2011 na 2012 ikiwa na pamoja na kutwaa Dabo akiweka rekodi ya kuwa Meneja wa kwanza wa Dortmund kufanya hivyo.
Pia Klopp aliiwezesha kufika Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI ambayo walifungwa 2-1 na Bayern Munich.
Hivi sasa Dortmund wako Nafasi ya 10 kwenye Bundesliga wakiwa Pointo 37 nyuma ya Mabingwa na Vinara wa Ligi hii ya Germany, Bayern Munich.Mchezaji wake Mats Hummels amehusishwa kutimkia Ligi kuu England kwenye Klabu ya Manchester United msimu ujao.
Ilkay Gundogan nae hivyo hivyo kwenda England
Jurgen Klopp confirmed in a press conference he is to leave Borussia Dortmund this summer
Jurgen Kloppkwenye mkutano na Waandishi wa Habari leo
An emotional Klopp said he believed Dortmund needed a change of manager 
Klopp kuondoka kwake kunahitaji Dortmundkufanya mabadiliko kwa kuweka meneja mpya ili waweze kurudi kwenye hali yao kama walivyokuwa na hatimae kucheza Klabu Bingwa.
Klopp will officially cease to be Dortmund manager on June 30
Klopp kuiacha Klabu hiyo June 30



Mabingwa Watetezi wa Ligi Kuu Vodacom, Azam FC, Leo wako huko Tanga kucheza na Mgambo JKT Uwanjani Mkwakwani wakiwania ushindi na kupunguza pengo la Pointi 8 kati yao na Vinara Yanga.
Yanga wanaongoza Ligi wakiwa na Pointi 46 wakifuatiwa na Azam FC, waliocheza Mechi 1 pungufu, wakiwa na Pointi 38.
Wikiendi iliyopita, Azam FC walipata pigo la kutetea Ubingwa wao baada ya kutoka Sare ya 1-1 na Mtibwa Sugar huko Manungu, Morogoro na sasa inabidi washinde Mechi zao zote zilizobaki, ambazo ni pamoja na dhidi ya Yanga na Simba, ikiwa watataka kutwaa tena Ubingwa waliotwaa kwa mara ya kwanza Msimu uliopita..
Hata hivyo, Mgambo JKT ni Timu ngumu kwa Vigogo hasa wakicheza kwao Mkwakwani na Leo Azam FC wanatinga Mechi hii wakiwa na hatari ya kuwakosa Nyota wao kadhaa wenye maumivu ambao ni pamoja na John Bocco, Abdallah Heri, Kipre Tchetche, Aggrey Morris na David Mwantika ambae ana matatizo ya Kifamilia.
Mechi nyingine hii Leo iko huko Manungu, Morogoro wakati Mtibwa Sugar wataikaribisha Tanzania Prisons.

LIGI KUU VODACOM
RATIBA
Jumatano Aprili 15

Mgambo JKT vs Azam FC
Mtibwa Sugar vs Tanzania Prisons


Baada ya Mechi za kwanza za Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI kuchezwa Jumanne Usiku kwa Mechi mbili, Jumatano Usiku pia zipo Mechi nyingine mbili.
Huko Uwanja wa Parc des Princes, Paris, France, Paris Saint-Germain wataivaa FC Barcelona.www.bukobasports.com
VIKOSI VINATARAJIWA:
PSG:
Sirigu; Van der Wiel, Marquinhos, Thiago Silva, Maxwell; Matuidi, Cabaye, Rabiot; Pastore, Lavezzi, Cavani.
-Hawatacheza: Ibrahimovic, Verratti na Aurier: Wote wapo Kifungoni
-Hatihati: David Luiz (Musulizya Pajani), Thiago Motta (Paja)
Barcelona: Ter Stegen; Adriano, Mathieu, Piqué, Alba; Busquets, Iniesta, Rakitić; Suárez, Messi, Neymar.
-Hawatacheza: Alves (Kifungo), Vermaelen (Musuli za Pajani)

Huko Portugal, Mjini Porto, kwenye Uwanja wa Estádio do Dragão, Wenyeji FC Porto watakutana na Vigogo wa Germany, Bayern Munich.

UEFA CHAMPIONS LIGI
Robo Fainali-Mechi za Kwanza
Mechi zote kuanza Saa 3 Dakika 45 Usiku

Jumatano Aprili 15
Paris Saint-Germain vs Barcelona

Refa: Marc Clattenburg [England]– Uwanja: Parc des Princes, Paris, France
FC Porto vs Bayern Munich
Refa: Carlos Velasco Carballo [Spain] – Uwanja: Estádio do Dragão, Porto, Portugal

Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari wa Airtel Tanzania, Frank Filman (kulia), akikabidhi mfano wa funguo za gari jipya aina ya Toyota IST, kwa mmoja wa washindi wa droo ya mwisho ya promosheni ya ‘Airtel Yatosha Zaidi’, Lilian Festo Mjimba katika hafla iliyofanyika Makao
Makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam jana. Wanaoshuhudia ni washindi wengine wa droo hiyo.

Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari wa Airtel Tanzania, Frank Filman (kulia), akikabidhi mfano wa funguo za gari jipya aina ya Toyota IST, kwa mmoja wa washindi wa droo ya mwisho ya promosheni ya ‘Airtel Yatosha Zaidi’, Lilian Festo Mjimba katika hafla iliyofanyika Makao Makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam jana.

Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari wa Airtel Tanzania, Frank Filman (kulia), akikabidhi mfano wa funguo za gari jipya aina ya Toyota IST, kwa mmoja wa washindi wa droo ya mwisho ya promosheni ya ‘Airtel Yatosha Zaidi’, Mama lishe Efgenia Mathew Mushi katika hafla iliyofanyika Makao Makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam jana. Wanaoshuhudia ni washindi wengine wa droo hiyo.

Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari wa Airtel Tanzania, Frank Filman (kulia), akikabidhi mfano wa funguo za gari jipya aina ya Toyota IST, kwa mmoja wa washindi wa droo ya mwisho ya promosheni ya ‘Airtel Yatosha Zaidi’, Kinyozi Juma Ally Songoro katika hafla iliyofanyika
Makao Makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam jana.

Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari wa Airtel Tanzania, Frank Filman (kulia), akikabidhi mfano wa funguo za gari jipya aina ya Toyota IST, kwa mmoja wa washindi wa droo ya mwisho ya promosheni ya ‘Airtel Yatosha Zaidi’, Kinyozi Juma Ally Songoro katika hafla iliyofanyika
Makao Makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam jana.

Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari wa Airtel Tanzania, Frank Filman (kulia), akikabidhi mfano wa funguo za magari mapya aina ya Toyota IST, kwa washindi wa droo ya mwisho ya promosheni ya ‘Airtel Yatosha Zaidi’, (kutoka kushoto), Subeti Salim Subeti, Kuruthumu Seleman Forogo, Juma Ally Songoro, Liliani Festo Mjimba, Christone Edick Mbalamula, Efgenia Mathew Mushi na Obel Samwel Mwamugiga katika hafla iliyofanyika Makao Makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam jana.

Mmoja wa washindi wa droo ya mwisho ya promosheni ya ‘Airtel Yatosha Zaidi’, Subeti Salim Subeti akionyesha kwa waandishi wa habari (hawapo pichani), funguo ya gari jipya aina ya Toyota IST, baada ya kukabidhiwa na Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari wa Airtel Tanzania,
Frank Filman (kushoto), katika hafla iliyofanyika Makao Makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam jana. Wanaoshuhudia ni watoto wa mshindi huyo.

Mmoja wa washindi wa droo ya mwisho ya promosheni ya ‘Airtel Yatosha Zaidi’, Kuruthumu Seleman Forogo akionyesha kwa waandishi wa habari (hawapo pichani), funguo ya gari jipya aina ya Toyota IST, baada ya kukabidhiwa na Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari wa Airtel
Tanzania, Frank Filman (kushoto), katika hafla iliyofanyika Makao Makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam jana. Anayeshuhudia ni kaka wa mshindi huyo, Yasin Juma.

waliotembelea blog