Friday, March 14, 2014

United Robin van Persie
Mshambulizi wa Manchester United Robin van Persie amesema kuwa yuko tayari kuongeza muda wa mkataba wake.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka thelathini amekuwa akihusishwa na madai ya kutaka kukihama klabu hiyo kwa kuwa hana uhusiano mwema na kocha wa David Moyes na kumekuwa na fununu kuwa huenda akaondoka mwishoni mwa wa msimu huu.
Lakini mchezaji huyo kutoka Uholanzi amesema kuwa anaridhika kucheza chini ya Moyes.
Katika michuano ya kuwania kombe la Uropa, Tottenham itakuwa na kibarua kigumu kufunga zaidi ya magoli mawili wakati wa mechi yake ya raundi ya pili, baada ya kufungwa magoli matatu kwa moja na Benfica, katika uwanja wa White Hart Lane.
Emmanuel Adebayor
Mchezaji wa zamani wa Bolton Rodrigo aliifungia benfica bao lake la kwanza kabla ya Luisao kuongeza magoli mawili katika mechi hiyo.
Emmanuel adebayor alipoteza nafasi nyingi za kufunga.
Tottenham ilipata bao lake la kuvutia machozi kupitia kwa nyota wake Christian Eriksen.
Benfica, ambayo ilishindwa na Chelsea kwa magoli 2-1 to katika fainali ya mwaka uliopita itakuwa na nafasi nzuri ya kufuzu kwa raundi ijayo wakati itakapocheza nyumbani.
 
Uli Hoeness
Mahakama nchini Ujerumani imemhukumu rais wa
 klabu bingwa Ulaya, Bayern Munich, Uli Hoeness, kifungo cha miaka mitatu na miezi sita jela kwa kukwepa kulipa kodi.
Nyota huyo wa zamani mwenye umri wa miaka 62 alikiri kuitapeli mamlaka ya kutoza ushuru ya Ujerumani mamilioni ya Euro huku akiweka akiba ya fedha zake kisiri kwenye akaunti ya benki ya Uswizi.
Licha ya wakili wake kuiomba mahakama kutomwadhibu Bw Hoeness kwa sababu ya kujisalimisha kwake, mahakimu waliafikia kwamba Hoeness hakukiri kikamilifu.
Hapo awali Hoeness alishtakiwa kwa kukwepa kulipa ushuru wa euro milioni 3.5 (£2.9m; $4.9m) lakini baadaye akakiri kuwa hajawahi kulipa milioni nyingine 15.
Hatimaye Alhamisi, korti ilibaini kuwa alikosa kulipa ushuru wa jumla ya euro milioni 27.2.
Upande wa utetezi umesema kwamba utakata rufaa dhidi ya uamuzi huo.
Hata hivyo Hoeness atabakia kuwa huru hadi uamuzi wa mwisho kabisa utakapotolewa.

waliotembelea blog