Tuesday, September 22, 2015


Kocha wa zamani wa klabu ya Manchester United Sir Alex Ferguson ambaye alistaafu kuifundisha Man United baada ya kuitumikia kwa miaka 27. Ferguson alistaafu 2013 kukinoa kikosi hicho na kuendelea kusimamia miradi yake binafsi, Ferguson ameeleza sababu za Paul Pogba kuondoka Man United na kutokubali kusaini mkataba mpya.
Ferguson aliwahi kulaumiwa kwa kushindwa kumshawishi Paul Pogba abaki Man United na wengi walifikiri hakuwa katika mipango yake hivyo ndio maana alimuacha kama mchezaji huru ajiunge na Juventus 2012.  Stori hii inakuja baada ya Ferguson kueleza kwa kina nini kilipelekea hadi Paul Pogba akaondoka klabu hiyo.
pogba
Stori ni kuwa Ferguson licha ya kutozijibu lawama zake za mwanzo kuhusu Pogba wakati ule, katika kitabu chake ameeleza kuwa moja kati ya watu waliyosababisha Paul Pogba aondoke Man United ni Mino Raiola ambaye ni wakala wa Paul Pogba.


Sergio Agüero 9' PEN
Kevin De Bruyne 25'
R. Sterling 36'
V. Mannone (og) 33'
Sergio Agüero dakika ya 9 aliifungia bao la kuongoza City kwa mkwaju wa penati dhidi ya Timu ya Sunderland.


5-1Akishangilia moja ya bao zake leo usiku huu

Robert Lewandowski akishangilia baada ya kuipiga vilivyo Wolfsburg

Balaa!

Lewandowski akishangilia baada ya kuifanyia maajabu timu yake na akitokea benchi
Akitupia nyavuni
Ndani ya dakika 9 Robert L. alikuwa ameshafunga bao 5 peke yake na kuipa ushindi mnono Bayern iliyokuwa nyumba ya bao 1-0 usiku huu na kuibuka kidedea kwa bao 5-1.


Meneja wa zamani wa Manchester United Sir Alex Ferguson alitaka mshahara wake uongezwe maradufu baada ya mshahara wa Wayne Rooney kuongezwa pakubwa 2010.
Rooney alikuwa ametishia kuhama United lakini mwishowe akatia saini mkataba wa kulipwa ujira wa £250,000 kila wiki.
"Niliwaambia sikudhani ilikuwa haki kwa Rooney kulipwa mshahara mara mbili ya mshahara wangu,” Ferguson amesema kwenye kitabu kipya.
"[mwenyekiti mwenza wa United] Joel Glazer alisema: 'Nakubaliana nawe kabisa lakini tufanye nini?’ Ilikuwa rahisi. Tuliamua hakuna mchezaji anayefaa kulipwa mshahara mkubwa kunishinda.”
Kwenye kitabu chake kipya kuhusu usimamizi chenye jina Leading , Ferguson anasimulia kuhusu kipindi cha mpito alipoondoka Manchester United 2013 baada ya kuwa kwenye usukani miaka 26, akisema: "Tungeliisimamia vyema.”

Raia huyo wa Scotland, aliyeshinda mataji mawili ya Ligi ya Kilabu Bingwa Ulaya, mataji 13 ya Ligi ya Premier, vikombe vitano vya FA na vikombe vinne vya League, alirithiwa David Moyes, aliyefutwa miezi 10 baadaye.
Lakini mkufunzi huyo mwenye umri wa miaka 73 anasema alitaka pia kuzungumza na aliyekuwa kocha wa Barcelona ambaye sasa ananoa Bayern Munich Pep Guardiola kabla yake kumteua Moyes.
Anasimulia pia jinsi meneja wa Chelsea Jose Mourinho, aliyekuwa mkufunzi mkuu wa Real Madrid Carlo Ancelotti, Jurgen Klopp wa Borussia Dortmund na Louis van Gaal, ambaye ndiye mkufunzi wa sasa United, walilengwa kumrithi.


Kampuni ya StarTimes Media ya jijini Dar es salaam leo imeingia mkataba wa udhamini na TFF kudhamini Ligi Daraja la Kwanza nchini (FDL) inayoshirikisha timu 24 kutoka katika mikoa 16 ya Tanzania bara.
Akiongea na waandishi wa habari wakai uwekaji sahihi mkataba huo, Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF), Jamal Malinzi ameshukuru kituo cha Star Times kwa kuamua kuwekeza katika mpira wa miguu na hasa kwenye chimbuko la vipaji na wachezaji wengie nchini.
Malinzi amesema udhamini huo wa shilingi milioni 900 kwa kipindi cha miaka mitatu, unatarajiwa kuongezeka wiki ijayo baada ya kuingia mkataba na mdhamini mwingine wa kurusha matangazo ya ligi hiyo kwa shilingi milioni 450 na kufikia jumla ya udhamini wa shilingi bilioni 1.3.

Mgombea wa Ubunge anaekubalika na wananchi wa Masasi kupitia Mwamvuli wa Chama cha Wananchi CUF, Ismail Makombe (Maarufu Kundambada), akizungumza machache na wananchi hao waliofurika kwa wingi kwenye Uwanja wa Boma, leo Septemba 22, 2015.

Mwenyekiti Mwenza wa Ukawa, Dkt. Emmanuel Makaidi akiwa ameambatana na Mkewe, wakiwasalimia wananchi wa Mji wa Masasi, Mkoani Mtwara leo Septemba 22, 2015.

Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akizungumza jambo na Mke wa Mwenyekiti wa Chama cha NLD, Dkt. Emmanuel Makaidi (kulia), Mama Modesta Makaidi, wakati wa Mkutano wa Kampeni, uliofanyika kwenye Uwanja wa Boma, leo Septemba 22, 2015.


Sehemu ya Umati wa Wananchi wa Mji wa Masasi, Mkoani Mtwara wakiwa wamefurika kwa wingi kwenye Uwanja wa Boma, leo Septemba 22, 2015.

Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akiwahutubia wananchi wa Mji wa Masasi, Mkoani Mtwara, waliofikia kusikiliza sera zake katika Mkutano wa hadhara wa Kampeni, uliofanyika kwenye Uwanja wa Boma, leo Septemba 22, 2015.

Lowassa akiwasili uwanjani hapo.

 


Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF), Jamal Malinzi jana amefunga fainali za michuano ya kombe la Airtel Rising Stars katika uwanja Karume jijini Dar es salaam.
Akiongea wakati wa ufungaji michuano ya Airtel mbele ya halaiki ya vijana walioshirki michuano hiyo, Malinzi ameishukuru kampuni ya simu ya Airtel kwa kuendelea kudhamini michuano hiyo ambayo inawapa nafasi vijana ya kucheza mpira na kuonekana na baadae kujipatia ajira.
“Lengo la TFF ni kushirki fainali za Olimpiki za Dunia mwaka 2020 Tokyo –Japan hivyo wachezaji wenye vipaji kutoka kwenye michuano hii ya Airtel na vijana wengine wataendelea kutunzwa kwa ajili ya timu ya Taifa ya baadae” Alisema Malinzi.
Naye Mkurugenzi wa Mawasiliano wa kampuni ya simu za mkononi ya Airtel ambao ndio wadhamini wakuu wa michuano hiyo, amesema airtel wataendelea na program hiyo ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 kwa wanawake na wanaume, na kuahidi kuendelea koboresha michuano hiyo kila mwaka.

RAIS wa Shirikisho la soka nchini (TFF), Jamal Malinzi, amefunga kozi ya makocha lesseni C inayotambuliwa na Shirikisho la soka barani Afrika (CAF) na kuwataka wahitimu hao kufanyia kazi mafunzo waliyoyapata.
Akizungumza kwenye hafla fupi ya kufunga mafunzo hayo, Malinzi amesema kuwa anasikitika kuona makocha wanapata mafunzo kama hayo lakini wanaenda kuweka vyeti vyao ‘makabatini’ na kuacha kufanyia kazi walichojifunza.

“Hiki mlichokipata kwenye mafunzo haya ya wiki mbili mnatakiwa muende mkafanyie kazi kwa kutafuta timu za kufundisha na baada ya mwaka mmoja ni vizuri mkajiendeleza zaidi ya hapa,” alisema Malinzi
Aidha, amesema kuwa Shirikisho lake limepanga kuhakikisha baada ya muda litafuta utaratibu wa makocha wenye lesseni C kuwa kwenye benchi la ufundi la timu za daraja la kwanza na kuwa wasaidizi kwenye benchi la ufundi la timu za ligi kuu.
“kwa sasa hivi makocha wa ligi kuu wanatakiwa kuwa na leseni ya daraja B na wasaidizi angalau leseni daraja C, ila kuanzia msimu wa 2017-2018 mambo yatabadilika na lessen I C aizataruhusiwa kwenye mabenchi ya ufunzi kwa timu za ligi kuu, mambo yataendelea hivyo mpaka mwisho tutakuwa na leseni za daraja A,” alisema Malinzi.
 Kiungo mwenye kasi wa PSG, Angelo Di Maria amesema hatashangilia kama atafanikiwa kufunga bao wakati wakivaa Real Madrid.


Di Maria ametua PSG akitokea Manchester United ambayo ilimnunua kutoka Real Madrid ambayo sasa wako nayo kundi moja katika Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Madrid itaanza kukutana na Madrid Oktoba 21 jijini Paris, Ufaranda kabla ya kurudia Madrid Novemba 3.
 
“Nilipojua ninahamia PSG nilimueleza mke wangu hofu ya kwamba tunaweza kupangwa na Real Madrid. Nilianza kujiuliza watanipokeaje siku nikienda pale na timu nyingine.

“Tumekuwa pamoja, tulishinda makombe mengi kwa pamoja na walinionyesha heshima kubwa. Mfano baada ya kujua ninaenda Manchester United, uwanja mzima walisimama kuniaga.

“Ni watu walioonyesha upendo mkubwa kwangu, itakuwa vigumu kushangilia kama nitafunga ingawa nitacheza kwa juhudi kubwa kwa ninataka mafanikio pia nikiwa PSG, nataka kushinda makombe,” alisisitiza Di Maria.



Mshambuliaji nyota wa timu ya taifa ya wanawake ya England, Danielle Carter amepiga hat trick wakati wakishinda kwa mabao 8-0 dhidi ya Estonia.


England imeibutua Estonia kwa mabao 8-0 katika mechi ya kuwania kucheza michuano ya Euro 2017.

Katika mechi hiyo iliyopigwa katika dimba la Le Coq Arena, jana usiku, England ilionekana kutawala kila eneo na ingeweza kushinda hadi mabao 15.





RAUNDI ya 3 ya Kombe la Ligi, sasa huitwa CAPITAL ONE CUP, itarindima Jumanne na Jumatano huko England nah ii ndio Raundi ambayo Vigogo wa Ligi Kuu England huanzia. Ingawa baadhi ya Timu za Ligi Kuu England zilianza Raundi ya Pili, wale Vigogo, wakiwemo Mabingwa Watetezi, huanzia Raundi ya 3.
Jumanne zipo Mechi 16 za Raundi hii na Jumanne zipo 8 na baadhi yao ni ile Dabi ya Jiji la Birmingham kati ya Aston Villa na Birmingham City.
Pia upo mtanange wa Timu za Ligi Kuu England huko Stadium of Light kati ya Sunderland na Man City.
Jumatano Mabingwa Watetezi Chelsea wao watakuwa Ugenini kucheza na Timu ya Daraja la chini Walsall wakati Liverpool wako kwao Anfield kucheza na Carlisle.
Huko Old Trafford, Man United wataivaa Ipswish Town.

CAPITAL ONE CUP
Raundi ya 3
Jumanne Septemba 22

21:45 Aston Villa v Birmingham
21:45 Fulham v Stoke
21:45 Hull v Swansea
21:45 Leicester v West Ham
21:45 Middlesbrough v Wolves
21:45 Preston v Bournemouth
21:45 Sunderland v Man City
22:00 Reading v Everton
Jumatano Septemba 23

21:45 Crystal Palace v Charlton
21:45 MK Dons v Southampton
21:45 Newcastle v Sheff Wed
21:45 Norwich v West Brom
21:45 Tottenham v Arsenal
21:45 Walsall v Chelsea
22:00 Liverpool v Carlisle
22:00 Man United v Ipswich
MABINGWA wa Bundesliga Bayern Munich na Vinara wa Ligi hiyo Borussia Dortmund wana Mechi ngumu za Ligi hiyo ya Germany Leo Jumanne na Jumatano Usiku.
Jumanne, Bayern Munich wako kwao Allianz Arena kucheza na VfL Wolfsburg ambao wako Nafasi ya 3 baada ya kushinda Mechi 3 na Sare wakiwa na Pointi 11 zikiwa ni Pointi 4 nyuma ya Bayern ambao wako Nafasi ya Pili wakiwa na Pointi 15 sawa na Vinara Borussia Dortmund.
Msimu huu, Wolfsburg, ambao ndio waliobeba German Cup, walishaifunga Bayern Munich Mwezi Agosti baada ya kuwabwaga kwa Penati kwenye Mechi ya kufungua pazia Msimu mpya ya kugombea Super Cup.
Nao Borussia Dortmund Jumatano wapo Ugenini kucheza na Hoffenheim wakisaka ushindi wao wa 6 mfululizo kwenye Bundesliga.
BUNDESLIGA
RATIBA
Jumanne Septemba 22

21:00 Bayern Munich v VfL Wolfsburg
21:00 Hertha Berlin v Cologne
21:00 Ingolstadt v Hamburg
21:00 Darmstadt 98 v Werder Bremen
Jumatano Septemba 23

21:00 Schalke 04 v Eintracht Frankfurt
21:00 Bayer Leverkusen v Mainz
21:00 Borussia Moenchengladbach v Augsburg
21:00 Hanover 96 v VfB Stuttgart
21:00 Hoffenheim v Borussia Dortmund
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Bukoba Mjini Ndugu Hamis Sued Kagasheki akihutubia kwenye mkutano huo wa kampeni za CCM leo hii jumatatu septemba 21, 2015.Mgombea Ubunge wa Jimbo la Bukoba Mjini Ndugu Hamis Sued Kagasheki akiongea na Wananchi wa Jimbo lake la Bukoba Mjini leo. Mgombea Ubunge Bukoba Mjini. Mgombea Urais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania kupitia chama cha CCM Dkt John Pombe Magufuli akizungumza na Wananchi wa Mji wa Bukoba na Vitongoji vyake leo hii jumatatu septemba 21, 2015 kwenye Uwanja wa Gymkhana Bukoba mjini. Wananchi wa mji wa BUKOBA na vitongoji vyake wakiwa wamekusanyika kwenye uwanja wa GYMKHANA wakimsikiliza Mgombea Urais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania kupitia chama cha CCM Dkt John Pombe Magufuli Wengine waliparamia miti ili waone mkanda vyema! kati ni Mh. Mwijage Mwijage akisalimia Wananchi na kuwapa neno! Fursa kwa wote! Burudani ikishika kasi
Sehemu ya wananchi wa mji wa Bukoba waliohudhuria leo katika viwanja vya Gymkhana Bukoba mkoani Kagera wakimsikiliza Dkt John Pombe Magufuli kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni.
Diamond Platinumz akitoa Burudani kwenye Mkutano huo

Nyomi ya Watu Mwenyekiti wa ccm Mkoa Kagera Mama Buhiye akifunguka kwenye mkutano huo.
Wasafi!! Bushoke akiburudisha! Bukobaaaa Mpooo!!! Bushoke akiimba Twendeee! Viongozi meza kuu Mr. Blue akifunguka! Mh Temba na Chegge Mapanga shaaa!!

waliotembelea blog