Wednesday, May 20, 2015



Ukiachilia ustaa wao na ufundi wao wanapokua uwanjani, kuna wachezaji ambao wamekua kivutio kikubwa kwa mashabiki wao kutokana na muonekano wao kwa ujumla.
Mara nyingi wamekuwa wakitumika katika matangazo mbalimbali ya biashara lakini kuna mtandao mmoja umeweza kutaja listi ya mastaa 10 wa soka duniani ambao wana muonekano mzuri.
casu
1. Cristiano Ronaldo amekuwa na mafanikio makubwa kupitia soka, muonekano wake wa kuvutia umemfanya aingize kiasi kikubwa cha fedha kupitia matngazo anayoingia nayo mikataba kila wakati
kaka
2. Kiungo Ricardo Kaka anatokea Brazil..kwa sasa anaichezea klabu ya Sao Paulo kwa mkopo akitokea Orlando City
villa
3. Moja ya vitu vinavyomwingezea mvuto David Villa ni staili yake ya nywele ambayo hubuni mara kwa mara..pamoja na kuwa mmoja wa wachezaji wenye umri mkubwa lakini bado amekuwa na muonekano mzuri
4. Iker Cassilas ni mmoja wa makipa wenye mafanikio makubwa sana kutokana na uwezo wake akiichezea Real Madrid, amekuwa ni mmoja wa wachezaji wenye muenekano mzuri
van
5. Robin Van Persie ni Mshambuliaji wa timu ya Manchester United
nando
6. Fernando Torres Ni mshambuliaji wa klabu ya Atletico Madrid na timu ya Taifa ya Hispania
gotz
7. Mario Gotze ni kiungo mwenye umri mdogo kutoka klabu ya Taifa ya Buyern Munich ya Ujerumani, amezaliwa mwaka 1992
mes
8. Ukiachia ufundi wake uwanjani akiwa na mafanikio mengi ndani ya klabu yake ya Barcelona, Lionel Messi ameingia kwenye orodha ya wachezaji wenye muonekeano mzuri
pque
9. Gerard Pique ni mlinzi wa timu ya Taifa ya Hispania na Barcelona, amezaliwa mwaka 1987 na ni mume wa mwanamuziki Shakira
faaa
10. Cesc Fabregas ni kiungo wa timu ya Taifa ya Hispania na klabu ya Chelsea, Ni baba wa mtoto mmoja wa kike na ana amezaliwa mwaka 1987

COASTAL UNION wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini TFF limetangaza Uchaguzi Mkuu wa klabu ya Coastal Union ya jijini Tanga utafanyika tarehe 05, Julai 2015.
Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF, Wakili Melchesedek Lutema ametoa ratiba ya mchakato mzima wa uchaguzi huo, ambapo tarehe 21-22 Mei mwaka huu zitatangazwa nafasi zote zinazogombewa.
Kwa mujibu wa kalenda hiyo ya Uchaguzi, tarehe 23-30, Mei 2015 itakua ni kipindi cha uchukuaji fomu kwa wagombea wote na kuzirudisha, wakati Juni Mosi mpaka Juni 04, 2015 ni kipindi cha mchujo wa awali kwa wagombea.
Juni 05, 2015 Kamati ya Uchaguzi itatoa orodha ya awali ya wagombea, Juni 7-9, 2015 itakua ni kipindi cha kupokea na kuweka pingamizi kwa wagombea, na Juni 10-11 ni kupitia mapingamizi yote.
Julai 02 -04, 2015 ni muda wa kampeni kwa wagombea wote na uchaguzi mkuu utafanyika tarehe 05, Julai 2015.
Ratiba kamili ya mchakato wa uchaguzi wa klabu ya Coastal Union imeambatanishwa.

Jana Usiku huko England, Klabu nyingi za Ligi Kuu England zilifanya Hafla maalum kutunuku Tuzo kwa Wachezaji wao Bora wa Msimu wa 2014/15 ambao unamalizika Jumapili hii.
Huko Manchester United, Meneja wao louis van Gaal alijizolea sifa kemkem kwa spichi yake murua iliyofurahisha na kuhamasisha na kushangiliwa mno Ukumbini na kujizolea sifa kubwa katika Mitandao ya Jamii.
Katika Hafla hiyo, kwa Misimu miwili mfululizo, Kipa David De Gea alitwaa Tuzo mbili za Mchezaji Bora wa Wachezaji, inayochaguliwa na Wachezaji wenyewe, na ile ya Mchezaji Bora wa Washabiki, inayopigiwa Kura na Mashabiki.
Hivi sasa Kipa De Gea amegubikwa na uvumi wa kutaka kuhamia Real Madrid licha ya kupewa Mkataba mpya ulioboreshwa ambao hajausaini.
Tuzo za Goli Bora la Msimu ilikwenda kwa Juan Mata kwa Goli lake la pili dhidi ya Liverpool.
Tuzo ya Mchezaji Bora Kijana ilichukuliwa na Mbrazil Andreas Pereira.
Huko Liverpool, Winga machachari, Raheem Sterling alizomewa wakati akipanda Jukwaani kupokea Tuzo yake ya Mchezaji Bora Kijana wa Msimu.
Sterling alipokewa kwa shangwe iliyobadilika na kuja kuzomewa na miluzi ikiwa ni ishara ya Washabiki kuchukizwa kwa kukataa kwake kusaini Mkataba mpya akidai kuhama Klabu hiyo.
Lakini Mbrazil Philippe Coutinho ndie alieibuka Shujaa wa Liverpool kwa kutwaa Tuzo 3 za Mchezaji Bora wa Msimu, Goli Bora la Msimu, lile la Shuti la mbali dhidi ya Southampton na Tuzo ya Tukio la Uchezaji wa Ustadi.


Meneja Van Gaal akwa na mshindi tuzo mara mbili David de Gea (Tuzo mbili za Mchezaji Bora wa Wachezaji)

Van Gaal, De Gea pamoja na Steve Cross wakiwa na Kombe kama Tuzo ya Sir Matt Busby mchezaji bora wa mwaka.

waliotembelea blog