Sunday, October 11, 2015


John Banda dakika ya 41 anaipa bao Malawi kwenye Uwanja wa Kamuzu Stadium, Blantyre.
Mpaka dakika 90 zinamalizika Malawi 1-0Tanzania (Agg:1-2)
Ushindi wa Nyumbani wawabeba Taifa stars leo Ugenini kwenye Uwanja wa Kamuzu Stadium, Blantyre - Malawi.

Tanzania wamefanikiwa sasa kuvuka na wanasonga mbele kwenye Raundi ya Pili watakwaana na Algeria ambao wanaanzia hatua hii ya raundi ya pili.
Washindi wa Raundi ya Pili wataingizwa kwenye Droo ya kupanga Makundi 5 ya Timu 4 kila mmoja ambapo Washindi wake wataenda Fainali Russia moja kwa moja.

Katika Mechi ya Kwanza iliyochezwa Jumatano iliyopita Tanzania iliichapa Malawi 2-0 kwa Bao za Maprofeshanali Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu ambao wote hucheza huko Congo DR kwenye Klabu ya Lubumbashi TP Mazembe.

Leo, Wamalawi walicharuka na kutawala, hasa Kiungo, dhidi ya Kikosi cha Tanzania chini ya Kocha Charles Boniface Mkwasa na kupata Bao lao la pekee la Mechi hii katika Dakika ya 41 kupitia kwa Banda.
Tanzania sasa watacheza Raundi ya Pili na Algeria ambao wanaanzia hatua hiyo ambayo Mechi zake zimepangwa kuchezwa Jijini Dar es Salaam Novemba 9 na Marudiano huko Algiers hapo Novemba 17.

Washindi wa Raundi ya Pili wataingizwa kwenye Droo ya kupanga Makundi 5 ya Timu 4 kila mmoja ambapo Washindi wake wataenda Fainali Russia moja kwa moja.

KOMBE LA DUNIA 2018 
MATOKEO
Afrika-Raundi ya Awali- Marudiano
Jumapili Oktoba 11
 

Malawi 1 v 0 Tanzania - Agg:[1-2]Tanzania win
Ethiopia 3 v 0 Sao Tome And Principe - Agg [3-1]
Kenya 0 v 0 Mauritius [5-2]

Mshindi wa Shindano la Bongo Star Search 2015 (BSS), Kayumba Juma (katika), akiwa ameshikilia fedha zake muda mfupi baada ya kuibuka kidedea kwenye fainali hizo zilizokuwa zikifanyika usiku wa kuamkia leo katika Ukumbi wa King Solomoni uliopo Namanga jijini Dar es Salaa.
Jaji Mkuu wa mashindano hayo, Madam Rita (wa pili kutoka kushoto), akimtangaza mshindi huyo.
Washiriki waliongia kwenye 6 bora ya mashindano hayo wakiwa jukwaani kabla ya mchujo huo kuanza
Mmoja wa Majaji wa shindano hilo (kulia), Master Jay akiingia ukumbini hapo huku akiwa ameongozana na mpenzi wake ambaye ni msanii wa Bongo fleva Shaa.

Majaji wakiwa kwenye meza yao ya kuratibia mashindano hayo.
Peter Msechu akiwa katika pozi kwenye Red Carpet.

Wasnii wanaounga kundi la Navy Kenzo wakipagawisha jukwaani hapo.

Msanii kutoka nchini Nigeria, Run Town anayetamba na kibao chake cha Gallardo, akipagawisha jukwaani hapo.

Mmoja wa washiriki waliokuwa wakichuana jukwaani hapo, Angel Marykato akisaka milioni 50.

Vijana wanaounda kundi la Yamoto Bendi wakitoa burudani kwenye fainali hizo.

Msanii wa Dansi Christiani Bella akitunza na mashabiki wake wakati akitumbuiza kwenye fainali hizo.

Bosi anayesimamia lebo ya Mkubwa na Wanawe, Saidi Fella akishuhudia kwa makini fainali hizo.

Mshiriki wa Shindano hilo kutoka Arusha, Frida Amani akipagawisha jukwaani hapo kuwania kitita cha shilingi milioni 50.
Kala Jeremiah akikumbushia enzi zake katika mashindano hayo.

Msanii wa Bongo Fleva, Estelina Sanga ‘Linah’ akiwa katika pozi kwenye red Carpet ya mashindano hayo.
Ben Poul akiwa katika pozi na mmoja wa mashabiki zake.

Baadhi ya washiriki waliyotolewa mapema kwenye kinyang’anyiro hicho wakihojiwa muda mfupi baada ya kuwasili ukumbini hapo.
Msanii wa Filamu, Muna Alphonce akiwa katika ubora wake kwenye tamasha hilo.

Kayumba akitunzwa na mashabiki wake kabla ya kutangazwa kuwa mshindi.

Madam Rita akifuta machozi muda mfupi baada ya kumkabidhi mshindi kitita cha shilingi milioni 50.

Madam Rita akiwa kwenye pozi.

Mmoja ya kikundi cha kudansi kikitumbuiza jukwaani hapo.

Mpiga picha Musa Mateja (kushoto), akihojiwa mara baada ya kuingia ukumbini hapo.

Baadhi ya mashabiki waliohudhuria ukumbini hapo wakifuatilia burudani hizo kwa makini.
Kayumba Juma wa jijini Dar es Salaam juzi usiku aliibuka mshindi wa shindano la kusaka vipaji vya muziki la Bongo Star Search (BSS) kwa mwaka 2015 baada ya kuwabwaga washiriki wengine watano waliofika hatua ya fainali, hivyo kutwaa kitita cha Sh50 milioni. Mbali na kuondoka na fedha hizo, kijana huyo amepewa bima ya afya ya mwaka mzima kutoka kwa kampuni ya Jubilee Insurance.

Juma aliibuka kidedea katika fainali hizo zilizofanyika katika Ukumbi wa King Solomon Hall, Kinondoni jijini Dar es Salaam zilizopambwa na wasanii mbalimbali wa muziki.

Mshindi huyo aliwabwaga washiriki wengine watano ambao walifika hatua ya fainali; Frida Amani, Nassib Fonabo, Jacqueline Kayengi, Angel Mary Kato na Kevin Gerson. Licha ya kushindwa kutwaa taji hilo washiriki hao watano walitoa ushindani mkubwa na kuwapa burudani mashabiki waliohudhuria kwenye ukumbi huo.
Sambamba na burudani kutoka kwa washiriki hao, pia wapo baadhi ya wasanii waliolipamba jukwaa la fainali hizo ikiwa ni pamoja na Kala Jeremiah, Peter Msechu, Christian bella, Yamato Band pamoja na msanii kutoka Nigeria, Runtown.

Jaji kiongozi wa mashindano hayo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Benchmark, Rita Poulsen alimtangaza mshindi huyo baada ya washiriki wote sita kuchuana jukwaani na kubaki wawili.

Baada ya wawili hao, Kayumba Juma akiwakilisha Dar es salam na Nassib Fonabo kutoka Arusha ambao waliingia katika hatua ya mbili bora na kutupa karata yao ya mwisho kwa kuimba muziki wa mwisho, mashabiki walipiga kura na muda mfupi baadae Jaji huyo maarufu kwa jina la Madam Rita alipanda jukwaani na kumtangaza mshindi.
“Mnamjua mshindi…? Sina maneno mengi maana kazi yangu ni kumtangaza mshindi wa mashindano ya BSS msimu wa 8 (season eight), mshindi ni.. ni.. Kayumba Juma’’ alitangaza Madam Ritah huku mashabiki wakishangilia kutokana na burudani aliyotoa mshindi huyo. Mashindano hayo yanayoandaliwa na Kampuni ya Benchmark Production 360 yalianza mwaka 2006 kwa kusaka vipaji vya vijana wa Kitanzania kila mwaka lakini mwaka jana mashindano hayo hayakufanyika tofauti na ilivyozoeleka.
Baadhi ya washindi wa BSS kwa miaka tofauti toka shindano lianzishwe ni pamoja na; Jumanne Iddi, Kala Jeremiah, Peter Msechu, Walter Chilambo na Emmanuel Msuya.
Mshambuliaji wa kimataifa wa Uingereza na nahodha wa Manchester United Wayne Rooney ambaye kwa hivi karibuni alikuwa na majukumu ya kuitumikia timu yake ya taifa ya Uingereza sambamba na tukio la kupewa kiatu cha dhahabu baada ya kuweka rekodi ya kuwa mfungaji bora wa muda wote wa Uingereza.
Wayne Rooney ambaye ni baba wa watoto wawili wa kiume Kai na Klay aliyowapa akiwa na mkewe Coolen, ameonekana akiwa pamoja na familia yake licha ya kuwa busy wiki hii, Rooney alikuwa na majukumu ya timu ya taifa ya Uingereza pamoja na tukio la kuzawadiwa kiatu cha dhahabu na FA kwa kuweka rekodi ya ufungaji.
Man United striker Wayne Rooney at a football event with sons Kai and Clay at The Trafford Centre along with wife Coleen who is expecting their third child. Kai Rooney who was taking part in the 6 monthly event at the sports centre. 10/10/2015 ***EXCLUSIVE ALL ROUND***
Staa huyo wa Man United alikabidhiwa kiatu cha dhahabu na Bobby Charlton baada ya kuwa mfungaji bora wa muda wote wa timu ya taifa ya Uingereza kwa kufunga jumla ya goli 50, goli alilofunga mwezi uliyopita dhidi ya Switzerland limefanya kuvunja rekodi ya Bobby Charlton na kutimiza magoli 50.
England-v-Estonia



Bado uhamisho wa mshambuliaji wa zamani wa FC Barcelona ya Hispania na timu ya taifa ya Hispania Pedro Rodriguez kujiunga na Chelsea unaendelea kuwaumiza wachezaji wenzake wa zamani, baada ya Daniel Alves kusema kuwa ni bora nyota huyo angeendelea kubakia FC Barcelona kuliko kujiunga na Chelsea.
“nilimwambia Pedro asiondoke FC Barcelona lakini kulikuwa na watu wengi waliohusika katika hili, kama angebakia FC Barcelona angeendelea kuwa na furaha hapa, lakini hatukuwa katika nafasi ya kufanya maamuzi kuhusiana na mpango huo kama tungekuwa na nafasi ya kufanya hivyo ningependa abaki hapa kwa miaka mingi zaidi”>>> Alves
Pedro-611359
Pedro Rodriguez aliamua kuhama na kujiunga na klabu ya Chelsea ya Uingereza kwa dau la pound milioni 22, baada ya kupoteza nafasi ya kucheza katika kikosi cha kwanza cha FC Barcelona. Pedro ilimlazimu kuondoka kutokana na nafasi yake ya kucheza kuwa finyu kutokana na uwepo wa Luis Suarez, Lionel Messi na Neymar kuwa wanafanya vizuri wakicheza pamoja.

KOCHA Mkuu wa Tanzania, Charles Boniface Mkwasa amechagua kumuanzisha kinda Farid Malik Mussa badala ya mkongwe Mrisho Khalfan Ngassa katika mchezo wa leo dhidi ya Malawi.
Taifa Stars inamenyana Malawi kuanzia Saa 8:00 mchana Uwanja wa Kamuzu katika mchezo wa marudiano hatua ya kwanza ya mchujo kuwania kupangwa kwenye makundi ya kuwania tiketi ya Fainali za Kombe la Dunia mwaka 2018 Urusi.
Na Mkwasa ‘Master’ ameanzisha viungo watatu, mmoja zaidi kutoka mchezo wa kwanza Dar es Salaam ambao alishinda 2-0 Jumatano.
Himid Mao Mkami na Said Hamisi Ndemla walianza peke yake Dar es Salaam na leo katika kuiongezea uimara safu hiyo ambayo Wamalawi waliitawala mchezo wa kwanza, ameongezeka Mudathir Yahya Abbas.
Kwa ujumla kikosi cha Stars kitakuwa sawa na kile kilichoanza katika ushindi wa 2-0 Dar es Salaam, kasoro Ngassa tu amempisha Mudathir.
Langoni kama kawaida, ‘TZ One’ Ally Mustafa Mtinge ‘Barthez’ atalindwa na Shomary Salum Kapombe kulia, Mwinyi Hajji Mngwali kushoto, Kelvin Patrick Yondan na Nadir Haroub Ally ‘Cannavaro’ katikati.  
Viungo Himid Mao Mkami, Said Hamisi Ndemla na Mudathir Yahya Abbas, wakati washambuliaji ni Farid Malik Mussa, Mbwana Ally Samatta na Thomas Emmanuel Ulimwengu.
Ulimwengu na Farid watakuwa wanacheza pembeni zaidi, wakati Samatta atacheza mbele ya lango la wapinzani.
Leo kutakuwa na mechi tatu za marudiano na nyingine 10 Jumanne na washindi wa jumla wataungana na timu nyingine 27 kwa mechi za mwisho za mchujo Novemba na Tanzania ikiitoa Malawi itamenyana na Algeria.

Golikipa wa klabu ya Arsenal Peter Cech ambaye kwa sasa anatajwa kuwa ni golikipa bora Uingereza kwa mujibu wa takimu fupi za hivi karibuni kutoka katika mtandao wa metro.co.uk. Takwimu hizo ni kulingana na hatari alizookoa golini kwake katika mechi za Ligi Kuu Uingereza msimu wa 2015/2016.
Golikipa huyo wa zamani wa Chelsea amezungumza mtazamo wake kutokana na mwenendo wa klabu yake ya zamani ya Chelsea. Cech anaamini Chelsea wananafasi ya kuwania ubingwa msimu huu, licha ya kuwa wameanza vibaya msimu wa 2015/2016.
“Kiwango chao kwa msimu huu kinanishangaza kwa sababu Chelsea ni moja kati ya vilabu bora katika Ligi Kuu Uingereza. Hata hivyo sipo tena katika klabu ya Chelsea hivyo ni ngumu kujua nini kinaendelea, ligi bado ndefu lakini Chelsea bado ni timu nzuri machoni mwangu”>>> Peter Cech
key
Takwimu zilizoandikwa na mtandao wa metro.co.uk October 8
Peter Cech ambaye msimu uliyopita alicheza katika klabu ya Chelsea na kufanikiwa kuisaidia timu hiyo kutwaa Ubingwa wa Ligi Kuu Uingereza, alijiunga na Arsenal katika dirisha la usajili lililofungwa mwezi August 2015  akitokea klabu ya Chelsea kwa ada ya uhamisho wa pound milioni 11.


Wales wamefanikiwa kutinga Fainali yao ya kwanza ya Mashindano makubwa tangu Mwaka 1958 baada ya Jana kufuzu kuingia Fainali za Kombe la Mataifa ya Ulaya, EURO 2016, licha ya kuchapwa 2-0 Ugenini na Bosnia.
Wales wamefuzu kutoka Kundi B la EURO 2016 pamoja na Belgium ambao Jana waliinyuka Andorra 4-1 kutokana na Cyprus kuichapa Israel 2-1 katika Mechi nyingine ya Kundi hilo.
Italy nao wamefuzu kutoka Kundi H baada ya kushinda Ugenini walipoichapa Ugenini Azbeijan Bao 3-1.
Hadi sasa Timu 12, pamoja na Wenyeji France, zimeshatinga Fainali za EURO zikibakisha Nafasi 12 ambazo 8 zitajazwa kwa Mechi kati ya Leo na Jumanne na 4 zitatokana na Mechi 4 za Mchujo zikishirikisha Washindi wa 3 Bora wa Makundi ambazo zitachezwa Mwezi Novemba.
Kutoka Kundi A, hali ni tete kwa Netherlands ambao Jana waliifunga Ugenini Kazakhstan 2-1 lakini wapo hatarini kuikosa Nafasi ya 3 kwa vile Turkey nao walishinda Ugenini kwa kuichapa Czech Republic 2-0.

Toka Kundi A, Iceland na Czech Republic tayari zimefuzu na nafasi inayogombewa ya kwenda Fainali ni kupitia Tiketi ya Mshindi wa 3 ambayo Turkey watainasa wakitoka Sare na Iceland huko Uturuki Jumanne.
Bao za Holland hapo Jana zilifungwa na Georginio Wijnaldum na Wesley Sneijder huku Straika wa zamani wa Manchester United akiingizwa Kipindi cha Pili kuichezea Holland Mechi yake ya 100.


Katika Mechi ya mwisho hapo Jumanne, Holland watakuwa Wenyeji wa Czech Republic.

 
TIMU ZILIZOFUZU HADI SASA [9 bado 15]:
-France [Wenyeji]
-KUNDI A: Iceland, Czech Republic
-KUNDI B: Belgium, Wales
-KUNDI C: Spain
-KUNDI D:
-KUNDI E: England, Switzerland
-KUNDI F: Northern Ireland
-KUNDI G: Austria
-KUNDI H: Italy
-KUNDI I: Portugal
EURO 2016
RATIBA
Saa za Bongo
Jumapili Oktoba 11
1900 Armenia vs Albania
1900 Faroe Islands vs Romania
1900 Finland vs Northern Ireland
1900 Greece vs Hungary
1900 Serbia vs Portugal
2145 Germany vs Georgia
2145 Gibraltar vs Scotland
2145 Poland vs Republic of Ireland
Jumatatu Oktoba 12
1900 Austria vs Liechtenstein
1900 Russia vs Montenegro
1900 Sweden vs Moldova
2145 Belarus vs Macedonia
2145 Estonia vs Switzerland
2145 Lithuania vs England
2145 Luxembourg vs Slovakia
2145 San Marino vs Slovenia
2145 Ukraine vs Spain
Jumanne Oktoba 13
2145 Belgium vs Israel
2145 Bulgaria vs Azerbaijan
2145 Cyprus vs Bosnia and Herzegovina
2145 Italy vs Norway
2145 Latvia vs Kazakhstan
2145 Malta vs Croatia
2145 Netherlands vs Czech Republic
2145 Turkey vs Iceland
2145 Wales vs Andorra


Timu ya Taifa ya Tanzania Leo hii inajitupa Uwanja wa Kamuzu Banda huko Blantyre kurudiana na Wenyeji Malawi katika Raundi ya Kwanza ya Kanda ya Afrika ya Mchujo wa Kombe la Dunia ambazo Fainali zake zitafanyika huko Russia Mwaka 2018.
Katika Mechi ya Kwanza iliyochezwa Jumatano iliyopita Tanzania iliichapa Malawi 2-0 kwa Bao za Maprofeshanali Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu ambao wote hucheza huko Congo DR kwenye Klabu ya Lubumbashi TP Mazembe.
Kikosi cha Tanzania huko Malawi kipo chini ya Kocha Charles Boniface Mkwasa.
Ikiwa Tanzania watafanikiwa kuvuka kigingi hiki cha Malawi basi kwenye Raundi ya Pili watavaana na Algeria ambao wanaanzia hatua hiyo.
Washindi wa Raundi ya Pili wataingizwa kwenye Droo ya kupanga Makundi 5 ya Timu 4 kila mmoja ambapo Washindi wake wataenda Fainali Russia moja kwa moja.



KOMBE LA DUNIA 2018
RATIBA:
Afrika-Raundi ya Awali- Marudiano
Jumapili Oktoba 11

15:00 Malawi v Tanzania [0-2]
16:00 Ethiopia v Sao Tome And Principe [0-1]
16:00 Kenya v Mauritius [5-2]

Jumanne Oktoba 13
14:30 Madagascar v Central African Republic [3-0]
16:00 Burundi v Seychelles [1-0]
17:00 Sierra Leone v Chad [0-1]
18:00 Namibia v Gambia [1-1]
18:00 Niger v Somalia [2-0]
19:00 Lesotho v Comoros [0-0]
19:00 Guinea-Bissau v Liberia [1-1]
20:00 Botswana v Eritrea [2-0]
20:00 Swaziland v Djibouti [6-0]
20:00 Mauritania v South Sudan [1-1]


Sunderland imemteua Sam Allardyce kuwa Meneja wao mpya kwa Mkataba wa Miaka Miwili.
Sunderland wamekuwa hawana Meneja tangu Jumapili iliyopita baada ya Dick Advocaat kutimka akiiacha Klabu hiyo ikiwa Nafasi ya Pili toka mkiani mwa Ligi Kuu England.
Advocaat, Raia wa Holland mwenye Miaka 68, aliteuliwa kushika wadhifa wa Umeneja wa Sunderland Mwezi Machi wakati Timu ikiwa hatarini kushuka Daraja Msimu uliopita.
Baada ya kuinusuru kutoshuka Daraja, Advocaat alikuwa ndio amemaliza Mkataba wake lakini akaongeza Mkataba wa Mwaka mmoja ambao ungembakisha hadi mwishoni mwa Msimu huu wa 2015/16.
Katika Kipindi cha Miaka Minne, Sunderland wameajiri Mameneja 6.

Mameneja waliopita katika kipindi hicho ni Steve Bruce, alietimuliwa Novemba 2011, Martin O'Neill, Paolo di Canio, Gus Poyet, Advocaat na sasa Sam Allardyce.
Allardyce, mwenye Miaka 60 na maarufu kama Big Sam, amekuwa hana kazi tangu mwishoni mwa Msimu uliopita baada ya Mkataba wake na West Ham kumalizika.
Mara baada kutua Sunderland, Allardyce alikiri ana kazi ngumu kwa kusema: “Ni wazi ni kazi yenye changamoto kubwa. Lakini nategemea kuirekebisha Timu na kuleta mafanikio anayotaka kila Mtu.”
Big Sam ashawahi kuichezea Sunderland kati ya Mwaka 1980 na 1981 na sasa ameweka Historia ya kuwa Mtu wa Kwanza kuwahi kuwa Meneja wa Klabu mbili zenye upinzani wa Jadi, Sunderland na Newcastle.
Mechi ya kwanza kwa Allardyce kama Meneja wa Sunderland ni Ugenini na West Bromwich Albion hapo Oktoba 17 na ya kwanza Uwanja wa Nyumbani Stadium of Light ni hapo Oktoba 25 dhidi ya Newcastle.


Sam Allardyce:Kazi ya Umeneja
1989–1991 West Bromwich Albion (Msaidizi)
1991–1992 Limerick (Meneja Mchezaji)
1992 Preston North End (Meneja wa Muda)
1994–1996 Blackpool
1997–1999 Notts County
1999–2007 Bolton Wanderers
2007–2008 Newcastle United
2008–2010 Blackburn Rovers
2011–2015 West Ham United
2015– Sunderland

waliotembelea blog