Tuesday, March 10, 2015


Kipindi cha pili dakika ya 52 Karim Benzema na kufanya 3-2 nao Schalke 04 kusawazisha bao kupitia kwa Leroy Sane dakika ya 57 na kufanya 3-3 Agg ikiwa 5-3 kiujumla. Dakika ya 84 Klaas Jan Huntelaar aliifungia bao la nne Schalke 04 na kufanya bao kuwa 4-3 Agg kuwa 5-4.Ronaldo akiwa aamini kile kilichotokea Uwanjani baada ya kufungwa bao 4-3 na bao la Ugenini kuwabeba!Wachezaji wa Schalke 04 wakishangilia moja ya bao lao dhidi ya Real kwenye Mchezo wa Marudiano.Bao..Klaas Jan HuntelaarCristiano Ronaldo alipoisawazishia bao dakika ya 45Klaas Jan Huntelaar aliwapachikia Schalke 04 bao la pili dakika ya 40 kisha Ronaldo tena akaisawazishia bao dakika ya 45 kwenye dakika za majeruhi za kipindi cha kwanza na mtanange kwenda mapumziko zikiwa nguvu sawa ya 2-2.

Cristiano Ronaldo anaisawazishia bao Real Madrid bao kwa kichwa baada ya kupigwa kona katika dakika ya 25 kipindi cha kwanza.Schalke 04 ndio walioanza kutangulia kupata bao mapema dakika 20 ya kupitia kwa Christian Fuchs kwa kupiga shuti kali lililomfanya kipa Real Casillas kuupangulia nyavuni baada ya kumzidi nguvu.VIKOSI:
Real Madrid wanaoanza XI:
Casillas, Coentrao, Varane, Pepe, Arbeloa, Khedira, Kroos, Isco, Bale, Ronaldo, Benzema

Akiba: Navas, Marcelo, Hernandez, Nacho, Modric, Jese, Illarramendi
Schalke wanaoanza XI: Wellenreuther, Howedes, Matip, Nastasic, Hoger, Neustadter, Fuchs, Barnetta, Meyer, Choupo-Moting, Huntelaar

Akiba: Wetklo, Uchida, Kaan Ayhan, Sobottka, Goretzka, Sane, Kehrer Toni Kroos and Cristiano Ronaldo hand over a cheque to the Red Cross before kick-off
Mashabiki wakiingia Uwanjani Bernabeu tayari kwa kipute


Mshindi wa tatu wa Miss Tanzania 2014,Doris Mollel akishiriki zoezi la uchangiaji damu katika ikiwa ni sehemu ya kusherehekea Siku ya wanawake Duniani,iliyofanyika Buguruni Chama jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Kushoto Ofisa Muuguzi kutoka Benki ya Damu Salama,Selina Joseph. Zoezi hilo la uchangiaji damu liliandaliwa na Mrembo huyo. 

Katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani,mrembo Doris Mollel ambaye ni Miss Tanzania namba tatu kwa mwaka 2014 ameongoza mamia ya watanzania katika zoezi la kizalendo la kuhamasisha kuchangia damu kwa watanzania kwa ajili ya wagonjwa mbalimbali,zoezi ambalo limefanyika jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki. 

Zoezi hilo ambalo lilikuwa linaongozwa na mpango wa taifa wa damu salama kwa udhamini wa kampuni ya METL lilikuwa na lengo la kupata damu kwa ajili ya kuokoa maisha ya Mama na Mtoto kwani matatizo ya damu katika hospitali za Tanzania yamekuwa yakiongezeka siku hadi siku,jambo lililompelekea mrembo huyo kuamua kujitoa kuhamasisha watanzania kujitokeza kwa wingi katika zoezi hilo. 

Zoezi hilo lilifanyika Machi 8 mwaka huu katika maeneo ya Buguruni Chama kwa muda wa siku nzima,ambapo jumla ya uniti 65 za damu zimepatikana kiwango ambacho kimetajwa kuwa kinatia matumaini kwa mrembo huyo kufanikiwa katika kuwahamasisha watanzania kujitokeza kwa wingi. 
Akizungumza na wanahabari kuhusu kitu kilichomsukuma kuendesha zoezi hilo,Doris alisema kuwa ameamua kufanya hivyo baada ya kugundua kuwa wakina mama wengi pamoja na watoto hufariki dunia wakati wa kujifungua kutokana na kukosa damu ya kuongezewa,jambo ambalo amesema ni lazima watanzania kuungana kwa pamoja kutafuta damu ya kutosha katika kila hospitali ili kuiondoa hali hiyo ambayo inaweka hatarini maisha ya mama na mtoto wa kitanzania. 

Amesema kuwa swala la kujitolea damu ni swala la kizalendo zaidi na moyo wa kujitoa kwa kuwa kila mtanzania anaweza kuwa na uhitaji wa damu muda wowote hivyo ni lazima watanzania wawe na utamaduni wa kuchangia damu mara kwa mara kwani itasaidia endepo kutatokea uhitaji wa damu katika mahospitali yetu.

Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa kanda ya Mbeya, Dk. Mpoki Ulisubisya akiwaongozwa Wakuu wa Mikoa ya Mbeya na Rukwa kuelekea Wodini kumjulia hali Mtoto Baraka aliyekatwa kiganja cha mkono wa kulia na watu wasiojulikana kijijini kwao juzi.
Mtoto Baraka aliyekatwa kiganja cha mkono wa kulia na watu wasiojulikana kijijini kwao juzi akiwa amelala kitandani akiendelea kupatiwa matibabu.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stellah Manyanya akiwa anamwangalia kwa jicho la huruma Mtoto Baraka aliyekatwa kiganja cha mkono wa kulia na watu wasiojulikana na kutokomea nacho akiwa amelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya.
Wakuu wa Mikoa ya Mbeya na Rukwa wakimjulia hali Mtoto Baraka aliyekatwa kiganja cha mkono wa kulia na watu wasiojulikana kijijini kwao juzi.
Wakuu wa Mikoa ya Mbeya na Rukwa sambamba na viongozi wa Chama cha Albino Mkoa wa Mbeya wakiwa wameinamisha nyuso zao huku wakisali kuwaombea watu wenye ulemavu wa ngozi ili wasipate madhara baada ya kumtembelea Mtoto Baraka aliyekatwa kiganja cha mkono wa kulia na watu wasiojulikana kijijini kwao juzi.
Mama mzazi wa mtoto Baraka,Prisca Shabani akiwa na jeraha kichwani baada ya kupigwa na watu waliomkata kiganja mtoto wake, akiwa anawasikiliza wakuu wa mikoa ya Mbeya na Rukwa waliomfika kuwajulia hali katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya wanakopatiwa matibabu.
.Waandishi wa habari wakichukua maelezo kutoka kwa wahanga wa tukio la kukatwa kiganja kwa mtoto mwenye ulemavu wa ngozi (albino).

Kaimu meneja Acacia Buzwagi Simon Sanga akikabidhi zawadi.

Wanawake wa mgodi wa Acacia Buzwagi kupitia mfuko wa maendeleo wa mgodi huo  wameshiriki siku ya wanawake kwa kutoa misaada mbalimbali kwenye vituo viwili vya kulelea watoto yatima wilayani Kahama mkoani Shinyanga.


Wanawake hao kupitia kwa makamu meneja wa Acacia Buzwagi Simon Sanga wamekabidhi Misaada hiyo katika vituo vya kulelea watoto yatima vya Muvuma kilichopo Nyasubi pamoja na kituo cha Peace Orphanage Center kilichopo mtaa wa Nyihogo.

Wafanyakazi wa Mgodi wa Buzwagi wakiwa na watoto wakati wa kutolewa kwa zaiwadi hizo.

Akikabidhi misaada hiyo makamu meneja wa Acacia Buzwagi Simon Sanga amesema wameamua kutoa misaada hiyo kwa kutambua uwepo wa jamii inayozunguka mgodi na kuongeza kuwa wataendelea kushirikiana na jamii ikiwa ni moja ya wajibu wao kuwasadia wananchi.


Wakipokea misaada hiyo kwa nyakati tofauti viongozi wa vituo hivyo wameshukuru Acacia Buzwagi kwa kutambua uwepo wa watoto yatima ambao wanahitaji misaada toka kwa wananchi na wadau mbalimbali wanaoguswa na makundi yasiyojiweza katika jamii wakiwemo yatima.

Picha ya Pamoja ya wafanyakazi wa mgodi wa Buzwagi na watoto Yatima.

Mkurugenzi wa Peace Orphanage Center Halima Hamza akipokea msaada huo amewashukuru wanawake wa Acacia Buzwagi kwa kukumbuka kundi la yatima katika siku ya wanawake na wakaamua kushiriki kwa kutoa misaada na amewaomba waendelee kufanya hivyo.
Naye mmoja wa watoto wanaolelewa katika kituo cha kulelea watoto yatima Muvuma Jacquline Pius kwa niaba ya wenzake amewashukuru wanawake wa Acacia Buzwagi kwa kujitoa na kuwakumbuka na amewakaribisha kushiriki katika masuala mengine katika kituo hicho.

Wafanyakazi wa Buzwagi wakishiriki michezo mbalimbali na watoto hao.
Misaada iliyotolewa katika vituo hivyo na wanawake wa Acacia kupitia mfuko wa maendeleo wa mgodi huo ni pamoja na Magodoro,Shuka,Vitanda 6,unga,vifaa vya mashuleni,Mafuta ya kula,na sabuni ambavyo vinathamani ya milion11 na nusu.

Pia kuna picha za chakula cha pamoja cha mchana na watoto hao,,kuna picha pia za michezo mbalimbali ambazo wafanyakazi wa Mgodi wa Acacia walishiriki michezo hiyo na watoto yatima






Freeman Mbowe akiongozana na viongozi wenzake kuelekea eneo la Mwakata wilayani Kahama



Mheshimiwa Freeman Mbowe akisalimiana na mkuu wa mkoa wa Shinyanga Ally Rufunga,wa kwanza kulia ni mkuu wa wilaya ya Kahama Benson Mpesya
Mheshimiwa Freeman Mbowe (mwenye miwani kushoto) na viongozi wengine wa CHADEMA Taifa wakijadiliana jambo kabla ya kukabidhi msaada kwa wahanga wa mvua kubwa ya mawe, kushoto kwa Mbowe ni mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Ally Rufunga.

 
Sehemu ya umati wa wafuasi wa CHADEMA walioongozana na mwenyekiti wao wa Taifa Freeman Mbowe wakati wa kukabidhi msaada wa wahanga wa mvua ya mawe iliyosababisha vifo vya watu 47.
 
Mwenyekiti wa CCM mkoani Shinyanga, Khamis Mgeja akijiandaa kukabidhi msaada wa fedha kwa niaba ya waziri mkuu mstaafu, Edward Lowassa.

Tafadhali pokea msaada huu kwa niaba ya mheshimiwa Edward Lowassa kwa ajili ya waathirika wote waliobomolewa nyumba zao kutokana na mvua kubwa ya mawe pamoja na rambirambi kwa waliofiwa na  jamaa zao, ndivyo anavyoeleza, Khamis Mgeja (kulia)


Maskini mtoto huyu hajui kitu gani kilichowasibu hadi kuwa katika hiyo ya maisha.

Haya ndiyo makazi ya muda kwa sasa kwa wakazi wa kijiji cha Mwakata Kahama - Shinyanga.
 
VIONGOZI wawili wa kisiasa nchini wameungana na watanzania wengine katika kuwapa pole na kuwafariji wahanga wa mvua kubwa ya mawe iliyonyesha na kubomoa nyumba kadhaa za wakazi wa kijiji cha Mwakata wilayani Kahama mkoani Shinyanga na kusababisha vifo vya watu 47 huku familia 450 zikibaki bila makazi.

Viongozi hao ni pamoja na mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe na waziri mkuu mstaafu Edward Lowassa ambao kwa ujumla wao walikabidhi msaada wa fedha jumla ya shilingi milioni 15.
Akikabidhi msaada kwa niaba ya familia ya waziri mkuu mstaafu, Edward Lowassa, mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoani Shinyanga, Khamis Mgeja alisema mara baada ya kutokea kwa maafa yaliyotokea, waziri mkuu mstaafu na familia yake waliguswa na tukio hilo na hivyo kuona umuhimu wa kuwasaidia wahanga wa maafa hayo.

“Mheshimiwa mkuu wa mkoa wa Shinyanga na wakazi wote wa kijiji cha Mwakata, kwa niaba ya familia ya waziri mkuu mstaafu Edward Lowassa, naomba nikabidhi msaada wa shilingi milioni tano kwa ajili ya wahanga waliokumbwa na tatizo hili ikiwa ni pole na rambirambi kwa familia ya watu waliopoteza maisha,”

“Binafsi yeye mwenyewe alikuwa aje lakini kutokana na majukumu aliyonayo ameniomba mimi mjumbe mwenzake wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) nifikishe salaam za pole na mchango wa kusaidia matatizo yaliyojitokeza hapa, pia ameniomba niwaeleze kuwa anaungana na watanzania wote kutoa pole zake za dhati kwa janga hili lililotokea,”

“Anasema yeye yuko pamoja nanyi na anaungana na watanzania wengine wote na kwamba janga hili siyo lenu peke yenu bali ni la watanzania wote na ameahidi kuendelea kushirikiana nanyi kwa hali na mali mpaka pale hali zenu zitakaporejea kuwa za kawaida, na pia anatoa pole kwa uongozi wa serikali mkoani Shinyanga,” alieleza Mgeja.
Kwa upande wake mwenyekiti wa CHADEMA wa Taifa Freeman Mbowe mbali ya kukabidhi msaada wa shilingi milioni 10 kwa niaba ya chama chake aliwataka watanzania wote hasa viongozi wa CCM kutochanganya mambo ya siasa pale panapotokea janga lolote la kitaifa na kwamba tukio la Mwakata ni janga la Taifa.
Mbowe alisema kwa kawaida maafa yanapotokea hayana itikadi ya chama chochote cha siasa na kwamba si vizuri kwa viongozi wa vyama vya kisiasa kugeuza maafa ya kitaifa kuwa mashindano ya kisiasa na hakuna sababu yoyote ya kushindana kuona nani katoa zaidi katika kuwafariji wahanga.

“Ndugu zangu sisi CHADEMA tumeguswa sana kwa tukio hili, kwa hali hiyo tumeona tutoe kitu kidogo ili kuwasaidia wenzetu walioathiriwa na mvua hii kubwa, kwa sasa tutatoa shilingi milioni 10 ambazo hata hivyo tutaomba mtueleze ni vitu gani mnavyohitaji, kama ni vifaa au vyakula mtueleze,”

“Tunasema hivi kwa sababu tunaweza kuja na unga hapa kumbe kinachohitajika ni mafuta ya kula, au tukaja na maharagwe kumbe wengine wameishaleta ya kutosha na kinachohitajika ni mabati au mifuko ya saruji, hivyo baada ya msaada huu wa leo, tunatarajia kufanya mkutano mkubwa mjini Kahama kwa ajili ya kuchangia wahanga,” alieleza.

Akipokea misaada hiyo mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Ally Rufunga aliwapongeza waziri mkuu mstaafu Lowassa na Mbowe kwa jinsi walivyoonesha kuguswa na tukio hilo na kwamba misaada waliyoitoa itasaidia kupunguza makali ya matatizo yaliyojitokeza baada ya mvua kubwa iliyoleta madhara kwa wakazi wa Mwakata.

“Kwa niaba ya mkoa wa Shinyanga tunawashukuru wote walionesha moyo wa upendo wa kuwasaidia wahanga hao, na kwa upande wa mheshimiwa Mbowe nikupongeze binafsi kwa jinsi ulivyoamua kuweka kando masuala ya kisiasa na kutanguliza mbele uzalendo, tunakushukuru sana, mpaka sasa tunaendelea kupokea misaada mbalimbali kwa ajili ya kaya 649 zilizoathiriwa na mvua hiyo,” alieleza Rufunga.

Mpaka Machi 9, mwaka huu idadi ya watu waliokufa kutokana na mvua kubwa ya mawe iliyopewa jina la Tornado iliyonyesha hivi karibuni ilifikia watu 47 baada ya majeruhi mwingine aliyekuwa amelazwa katika hospitali ya serikali mjini Kahama kufariki dunia juzi.  Majeruhi wanne walikuwa wakiendelea na matibabu katika hospitali rufaa ya Bugando jijini Mwanza.


Mkurugenzi wa Uendeshaji wa NSSF, Cresentius Magori (wa tatu kulia) akishiriki kwenye mbio za Kilimanjaro.Baadhi ya wafanyakazi wa NSSF- Kilimanjaro wakishiriki kwenye mbio za Kilometa 5.Baadhi ya Wafanyakazi wa NSSF - Kilimanjaro wakimalizia kukimbi mbio za kilometa 5.

MFUKO wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umeshiriki kwenye Mbio za nyika za zinazoendelea kuwa maarufu mwaka hadi mwaka Kilimanjaro ambazo zimefanyika kwa mwaka wa 13 mfululizo. NSSF ilishiriki ikiwa kama mdhamini wa mbio za KM 5 ambazo zilishirikisha washiriki zaidi ya 3500. Pamoja na udhamini huo NSSF ilipata nafasi ya kutoa elimu kwa wakazi mbalimbali wa Mkoa wa kilimanjaro walioshiriki na kutembelea kwenye banda lao.


MECHI za Marudiano za Raundi ya Mtoano ya Timu 16 za UEFA CHAMPIONS LIGI zinaanza kuchezwa Jumanne Usiku Machi 10 kwa Mechi mbili.
Huko Santiago Bernabeu, Mabingwa Watetezi wa Ulaya, Real Madrid, wako kwao kurudiana na Schalke ya Germany ambayo waliitandika Bao 2-0 katika Mechi yao ya kwanzo huko Nchini Ujerumani.

Real wako kwenye nafasi murua kuwa Timu ya kwanza kutua Robo Fainali ya Mashindano haya kwani Mechi nyingine inayochezwa Jumanne Usiku ipo huko Ureno kati ya FC Porto na FC Basel ambazo zilitoka 1-1 katika Mechi yao ya kwanza huko Uswisi.
Jumatano Usiku, Machi 11, pia zipo Mechi 2 za Marudiano za Raundi hii kati ya Bayern Munich na FC Shakhtar Donetsk, zilizotoka 0-0 huko Ukraine, ambayo itachezwa Allianz Arena Jijini Munich Nchini Germany na nyingine ni ile itakayochezwa Stamford Bridge Jijini London kati ya Wenyeji Chelsea FC na Paris Saint-Germain ambazo zilitoka 1-1 huko Paris, France. Mechi za Marudiano za Raundi ya Mtoano ya Timu 16 za UEFA CHAMPIONS LIGI zitakamilika Wiki ijayo kwa Mechi 4, mbili Jumanne Machi 17 na mbili Jumatano Machi 18.
RAUNDI YA MTOANO TIMU 16
RATIBA
MARUDIANO
Jumanne 10 Machi 2015

FC Porto vs FC Basel 1893 [1-1]
Real Madrid CF vs Schalke 04 [2-0]

Jumatano 11 Machi 2015

Bayern Munich vs FC Shakhtar Donetsk [0-0] 

Chelsea FC vs Paris Saint-Germain [1-1]



Mchezaji wa Liverpool  Philippe Coutinhowakati wa Mchezo wao wao na Timu ya  Blackburn
Bradford waliwaondosha  Chelsea na wanategemea kati yake na  Reading kucheza na Arsenal kutokana na Droo iliyochezeshwa punde..-BRADFORD/ READING vs ARSENAL
-ASTON VILLA vs BLACKBURN/LIVERPOOL


Dakika 90 zimemaliza Arsenal wakiwa na Ushindi wa bao 2-1, bao la Ushindi likifungwa na Danny Welbeck mchezaji wa zamani wa Timu ya Manchester United katika dakika ya 61 baada ya Valencia kufanya makosa ya kurudisha mpira nyuma.2-1Ushindi!!Umetupa bao!!Umerudi na kuua!!.Danny Welbeck baada ya kutupia nyavuni bao la pili.
Arsenal walitangulia kufunga kwa Bao la Dakika ya 25 la Nacho Monreal na Wayne Rooney kusawazisha Dakika ya 29 lakini Welbeck kuipa ushindi Arsenal katika Dakika ya 61. Nje!! Di MariaMan United walimaliza Mechi hii Mtu 10 baada ya Angel Di Maria kulambwa Kadi za Njano mbili na kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu.
Huu ulikuwa Usiku mwema kwa Arsenal ambao wameendelea kutetea vyema Kombe la FA CUP ambalo wao ni Mabingwa Watetezi na pia wamekuwa wakiteswa na Man United kwa kufungwa Mechi 11 kati ya 15 zilizopita.
Unamvuta Mwamuzi jezi???Mhhh !! Hii ni La Liga EPL??Kaa mbali kwanza!Unakosea Di Maria ...tulia!! Rooney akituliza Jazba!!Pia kwenye Droo ya Nusu Fainali ya FA CUP, iliyofanyika maraa baada ya Mechi hii, Arsenal watacheza na Mshindi kati ya Bradford City au Reading ambao Juzi walitoka 0-0 kwenye Mechi yao ya Robo Fainali.
Nusu Fainali nyingine itakuwa kati ya Mshindi wa Liverpool na Blackburn Rovers, ambao nao walitoka 0-0, dhidi ya Aston Villa.
Kipindi cha pili Danny Webeck mchezaji wa zamani wa Man United aliipa bao la pili Arsenal katika dakika ya 61 na kufanya 2-1. Rooney akisawazisha bao kipindi cha kwanzaRooney  baada ya kuisawazishia United bao kwa kufanya 1-1 dhidi ya Arsenal katika kipindi cha kwanza. Mpaka mapumziko kipindi cha kwanza Manchester United 1-1 Arsenal.1-1Nacho Monreal dakika ya 25 kipindi cha kwanza kaifungia bao Arsenal nao Man United walifufuka na dakika ya 29 Wayne Rooney aliisawazishia bao Manchester United kwa kichwa na kufanya 1-1.Mzee Ferguson akishuhudia kipute Old TraffordMhh!!VIKOSI:
Man United 11: De Gea, Valencia, Smalling, Rojo, Shaw, Blind, Herrera, Di Maria, Fellaini, Young, Rooney
Akiba: Valdes, Rafael, Jones, Carrick, Januzaj, Mata, Falcao


Arsenal 11: Szczesny, Bellerin, Mertesacker, Koscielny, Monreal, Coquelin, Cazorla, Oxlade-Chamberlain, Ozil, Sanchez, Welbeck
Akiba: Martinez, Gibbs, Chambers, Ramsey, Giroud, Walcott, Akpom 
Man United vs Arsenal

waliotembelea blog