Wednesday, February 11, 2015

Mkurugenzi wa masoko wa Airtel bw. Levi Nyakundi (kushoto) akimkabidhi mmoja kati ya washindi wa promosheni ya Yatosha Zaidi bi. Mwajabu Omary leo katika makabidhiano yaliyofanyika katika ofisi za makao makuu ya Airtel Tanzania. Anayeshuhudia (katikati) Mkurugenzi wa wa kitengo cha Mawasiliano bi Beatrice Singano Mallaya .Airtel imekabidhi magari matatu katika hafla hiyo.
KAMPUNI Ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania leo asubuhi imekabidhi magari kwa washindi watatu wa kwanza wa promoseni ya Yatosha Zaidi.
Hafla hiyo fupi ya kuvutia ilifanyika Makao Makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam na kushuhudiwa na waandishi wa habari, wafanyakazi wa Airtel na wageni waalikwa kadhaa.
Mkurugenzi wa Masoko wa Airtel Levi Nyakundi aliwaomba washindi kuendelea kutumia mtandao wa Airtel kwani kwa sasa wao ni sehemu ya familia ya kampuni hiyo.

Mario Balotelli akituma akituma salaam baada ya kuipatia ushindi Liverpool kwenye Uwanja wa nyumbani Anfield. Mtanange huo ukimalizika kwa bao 3-2 dhidi ya Spurs. Mtanange huo pia umeshuhudiwa na Mmiliki wa Klabu hiyo Bw. John Henry sambamba akiwa na mkewe Bi. Linda Pizzuti. Ushindi huu umewatuliza Liverpool nafasi ya 7 wakiwa na pointi 42 huku Spurs wakiwa juu yao nafasi ya 6 wakiwa na pointi 43 wakipishana pointi 1 moja tu kwa sasa.Nyumba ikiungua ya Spurs!Mario Balotelli ndie kaipatia Ushindi Liverpool wa bao 3-2.Mario Balotelli aliingizwa kipindi cha pili dakika ya 74 kwa kuchukua nafasi ya Daniel Sturridge na kuipa bao la ushindi Liverpool dakika za mwishoni dakika ya 83 na kufanya Liverpool kuongoza kwa bao 3-2 dhidi ya Spurs katika mtanange uliochezwa kwa kasi na nguvu Uwanjani Anfield.3-2 Mario kamaliza mchezo!!!2-2 Dembélé alisawazisha dakika ya 61 kipindi cha pili.
2-1 Steven Gerrard aliongeza bao la pili kipindi cha pili dakika ya 53, Bao hilo halikuweza kudumu sana Spurs dakika ya 61 M. Dembélé alisawazisha bao hilo na kufanya 2-2Steven Gerrard akishangilia bao lake la pili kwa Liverpool
Mashabiki wa Spurs wakimpongeza Harry Kane baada ya kusawazisha bao kipindi cha kwanza dakika ya 261-1 Hadi mapumzikoHarry Kane dakika ya 26 kipindi cha kwanza hicho hicho aliisawazishia bao Spurs na kufanya 1-1 dhidi ya Wenyeji Liverpool.Lazar Markovic akishangilia bao lake.Akipongezwa!!!Lazar Markovic dakika ya 15 kipindi cha kwanza alitangulia kuziona nyavu za Spurs na kuwapatia bao Liverpool katika kipindi cha kwanza.Lazar Markovic opened the scoring for Liverpool against Tottenham with a low left-footed strike during the first half1-0VIKOSI:
Liverpool:
Mignolet, Can, Skrtel, Sakho, Markovic, Henderson, Gerrard, Moreno, Ibe, Coutinho, Sturridge.
Liverpool Akiba: Johnson, Lovren, Lambert, Lallana, Allen, Balotelli, Ward.
Tottenham Hotspur: Lloris, Walker, Dier, Vertonghen, Rose, Bentaleb, Mason, Lamela, Eriksen, Dembele, Kane.
Spurs Akiba: Paulinho, Soldado, Vorm, Townsend, Fazio, Chadli, Davies.
Mwamuzi: Phil Dowd
Sturridge kuanza kwa Liverpool



Bao la pili lilifungwa na Theo Walcott dakika ya 41 baada ya kumalizia mpira uliotemwa na kipa wa Leicester City.
Andrej Kramaric aliipatia bao Leicester City kipindi cha pili dakika ya 61 na mtanange kumalizika kwa dakika 90 kwa 2-1 Arsenal wakiibuka na ushindi. Ushindi huu wa Arsenal umemshusha Man United nafasi ya tano nao Gunners kushika nafasi ya nne kwa muda wakiwa na pointi zao 45 na Man United wakishinda kesho watamshusha pia kwani wanacheza kesho Jumatano na Timu ya Burnley usiku.
Laurent Koscielny aliipachikia bao la kwanza Arsenal kipindi cha kwanza dakika ya 27 akipata mpira kutoka kwa Mesut Özil.RATIBA/MATOKEO
Jumanne Februari 10

Hull 2 vs 0 Aston Villa
Sunderland 0 vs 2 QPR
Arsenal 2 vs 1 Leicester
Liverpool 3 vs 2 Tottenham 
Taswira Emirates Stadium



Rais wa Ivory Coast  Alassane Ouattara na Nahodha wa  Ivory Coast  Yaya Toure jana Jumatatu

Maelfu ya mashabiki wa soka nchini Ivory Coast wamefika kuwapokea mabingwa wa mataifa ya Afika Ivory Coast baada ya kuifunga Ghana kwa njia ya penati na kunyakua kombe hilo.
Maelfu ya mashabiki walitanda mitaani ili kuwalaki wachezaji na viongozi kwa ushindi huo,Rais wa Ivory Coast Alassane Ouattara amewapongeza wachezaji na kusema ushindi wa Ivory Coast utaleta umoja na amani kwa nchi.
Polisi ilibidi kuamuru watu kubaki majumbani kwao sababu ya usalama baada ya uwanja uliokuwa umeandaliwa kwa ajili ya kuwalaki wachezaji na viongozi baada ya ushindi wa kihistoria wa kushinda kombe la mataifa ya Afrika huko Guinea ya Ikweta.

Rais wa Ivory Coast Alassane Ouattara akiwa na Nahodha Yaya Toure wakati wakilitembeza Kombe kwa Mashabiki
Wachezaji wa Ivory Coast wakishangilia ushindi huku wakilindwa na Wanajeshi
Yaya Toure akionesha Kombe Juu wakati wanashuka kwenye Ndege Mjini Abidjan
Karibu karibu..Ongera!!

Ushindi huo ulifanya Nchi ya Ivory Coast jana siku ya Jumatatu kuwa ni siku ya Mapumziko Nhini humo na kuweza kuhudhuria kwa Wingi mapokezi hayo na kuweza kuliona Kombe hilo waliloshinda Nchini Guinea wlipoifunga kwa Mikwaju ya Penati 9-8 Ghana.

Wakitembeza Kombe kwa Mashabiki

Mchezaji wa Ivory Coast Nahodha na ambaye pia anacheza Ligi Kuu England kwenye Klabu ya  Manchester City  Yaya Toure aliiongoza Timu hiyo na kupigana Mpaka mwisho na Kuibuka Na Ubingwa wa AFCON 2015 dhidi ya Ghana.

Yaya Toure na wenzake wakishangilia baada ya kuibuka Kidedea dhidi ya Ghana.

waliotembelea blog