Wednesday, February 11, 2015



Rais wa Ivory Coast  Alassane Ouattara na Nahodha wa  Ivory Coast  Yaya Toure jana Jumatatu

Maelfu ya mashabiki wa soka nchini Ivory Coast wamefika kuwapokea mabingwa wa mataifa ya Afika Ivory Coast baada ya kuifunga Ghana kwa njia ya penati na kunyakua kombe hilo.
Maelfu ya mashabiki walitanda mitaani ili kuwalaki wachezaji na viongozi kwa ushindi huo,Rais wa Ivory Coast Alassane Ouattara amewapongeza wachezaji na kusema ushindi wa Ivory Coast utaleta umoja na amani kwa nchi.
Polisi ilibidi kuamuru watu kubaki majumbani kwao sababu ya usalama baada ya uwanja uliokuwa umeandaliwa kwa ajili ya kuwalaki wachezaji na viongozi baada ya ushindi wa kihistoria wa kushinda kombe la mataifa ya Afrika huko Guinea ya Ikweta.

Rais wa Ivory Coast Alassane Ouattara akiwa na Nahodha Yaya Toure wakati wakilitembeza Kombe kwa Mashabiki
Wachezaji wa Ivory Coast wakishangilia ushindi huku wakilindwa na Wanajeshi
Yaya Toure akionesha Kombe Juu wakati wanashuka kwenye Ndege Mjini Abidjan
Karibu karibu..Ongera!!

Ushindi huo ulifanya Nchi ya Ivory Coast jana siku ya Jumatatu kuwa ni siku ya Mapumziko Nhini humo na kuweza kuhudhuria kwa Wingi mapokezi hayo na kuweza kuliona Kombe hilo waliloshinda Nchini Guinea wlipoifunga kwa Mikwaju ya Penati 9-8 Ghana.

Wakitembeza Kombe kwa Mashabiki

Mchezaji wa Ivory Coast Nahodha na ambaye pia anacheza Ligi Kuu England kwenye Klabu ya  Manchester City  Yaya Toure aliiongoza Timu hiyo na kupigana Mpaka mwisho na Kuibuka Na Ubingwa wa AFCON 2015 dhidi ya Ghana.

Yaya Toure na wenzake wakishangilia baada ya kuibuka Kidedea dhidi ya Ghana.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog