Tuesday, September 15, 2015




Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van der Pluijm amesema ana imani na kikosi chake kuendelea kufanya vizuri ingawa kuna mambo kadhaa hajaridhika sana.


“Katika soka kila unapocheza, linaibuka jambo jipya. Mkirekebisha na kucheza mechi nyingine, linaibuka jambo ambalo linahitaji marekebisho tena.

“Huo ndiyo mpira, tulitengeneza nafasi nyingi dhidi ya Coastal. Tunachotakiwa ni kuzitumia zaidi,” alisema.

“Lakini kuna makosa kadhaa tulifanya, bado tutayafanyia kazi zaidi.”

Yanga imeanza kutetea kombe lake kwa kuichapa Coastal Union kwa mabao 2-0.


Mechi inayofuata Yanga itacheza na Prisons amnayo ilianza ligi hiyo kwa kipigo cha mabao 2-1 ktoka kwa Azam FC.


NAFTAL (KATIKATI) AKIFANYA YAKE LIGI KUU KENYA

Beki wa zamani wa Simba, David Naftal ameendelea kung’ara katika kikosi cha Kenya Revenue Authority (KRA) na sasa amepania kuhakikisha wanamaliza Ligi Kuu Kenya wakiwa katika nafasi tano za juu.



Kutoka Kenya, akizungumza na SALEHJEMBE, Naftal amesema amekuwa akipambana na sasa ana uhakika wa namba katika kikosi cha kwanza, lakini kwa pamoja KRA wanataka nafasi hizo tano za juu.

“Tupo katika nafasi ya saba ya ligi. Tumebakiza mechi nne, sasa tunapambana kumaliza katika top 5.

“Huku Kenya mkimaliza top 5, mnapata nafasi ya kucheza michuano ya Top 8 ambayo bingwa wake hucheza michuano ya Shirikisho,” alisema Naftal.

Kwa sasa amekuwa akicheza nafasi ya kiungo mkabaji nan dye tegemeo katika kikosi hicho cha wakusanya kodi wa Kenya.

Wakati Staa wa Barcelona Lionel Messi akijitayarisha kucheza Mechi yake ya 100 kwenye UEFA CHAMPIONS LIGI, UCL, Kocha wake, Luis Enrique, Jumatano anapambana na Klabu yake ya zamani AS Roma katika Mechi yao ya kwanza ya Kundi E.
Luis Enrique, Mchezaji wa zamani wa Kimataifa wa Spain, aliwahi kuwa Kocha wa AS Roma katika Msimu wa 2011/12 na kuondoka Klabuni hapo baada ya kushindwa kuiingiza Mashindano ya Klabu Ulaya.
Lakini Enrique, ambae Timu yake Barca Jumatano ipo Stadio Olimpico kucheza na AS Roma, amesema kuwa uzoefu aliopata huko Italy na Klabu ya AS Roma ndio unampa mafanikio.
Msimu uliopita, Enrique aliiongoza Barca kutwaa Trebo ikiwa ni Ubingwa wa La Liga, Copa del Reay na UCL.
Gemu hii ya Barca na AS Roma pia itamfanya Lionel Messi apige hatua nyingine katika maisha yake ya Soka kwa kufikisha Mechi 100 za UCL.
Messi ndie anaeshika Rekodi ya Ufungaji Bao nyingi kwenye Mashindano hayo.
Mwezi Agosti, Barca, ambao ndio Mabingwa Watetezi wa Ulaya, waliichapa AS Roma 3-0 katika Mechi ya Kirafiki ya Joan Gamper.
Mara ya mwisho kwa Barca kuivaa AS Roma kwenye UCL ni Februari 2002 Mechi ambayo walitoka 1-1 na Luis Enrique aliichezea Barca kama Kiungo.
Wakati Messi akitaka kupiga hatua, nae Gwiji wa AS Roma,Francesco Totti, anawania kuifungia Timu yake Bao lake la 300.

RATIBA
kuanza Saa 3 Dakika 45 Usiku
Jumatano 16 Septemba 2015

KUNDI E
Bayer Leverkusen v BATE Borislov
AS Roma v Barcelona

KUNDI F
Dinamo Zagreb v Arsenal
Olympiakos v Bayern Munich

KUNDI G
Chelsea v Maccabi Tel Aviv
Dynamo Kiev v FC Porto

KUNDI H
KAA Gent v Lyon
Valencia v Zenit St Petersburg



Meneja wa Chelsea Jose Mourinho akiteta jambo leo wakati akiwa kwenye mahojiano na Wahandishi wa Habari leo.
Wakati Chelsea ikikanusha kuwepo na ngumi kati ya John Terry na Diego Costa, zipo habari kuwa Meneja wao Jose Mourinho atacharuka na ‘kuwapiga shoka’ Mastaa Watatu kutoka Kikosi cha Kwanza.
Huku wakigubikwa na habari za kuwepo mzozo kati ya Kepteni wao John Terry na Straika wao Diego Costa kufuatia Timu yao kuanza vibaya Ligi Kuu England katika Miaka 29 baada ya Juzi kuchapwa 3-1 na Everton, zipo habari nzito Jose Mourinho atawatoa Wachezaji Watatu kutoka Kikosi cha Kwanza katika Mechi yao ya Jumatano ya UEFA CHAMPIONS LIGI na Maccabi Tel Aviv.
Katika Mechi 5 za Ligi walizocheza Msimu huu ili kutetea Taji lao la Ubingwa, Chelsea wamefungwa Mechi 3 na wapo Nafasi ya 17 wakiwa Pointi 11 nyuma ya Vinara Manchester City.
Mechi hiyo ya Uefa Champions ligi itachezwa kesho jumatano dhidi ya timu ya Meccabi Tel AvivJose Morinho
Cesc Fabregas, Branislav Ivanovic na Diego Costa ndio ambao wanatajwa kuwa watalivaa shoka la Mourinho kwenye Mechi yao ya kwanza ya Kundi lao la UEFA CHAMPIONS  LIGI Uwanjani Stamford Bridge.
Fabregas na Costa wamenyooshewa kidole kuwa uchezaji wao Msimu huu ni chini ya kiwango wakati Ivanovic amebebeshwa lawama kubwa ya kuwa uchochoro kwenye Difensi ya Chelsea ambayo Msimu uliopita ilisimama imara.
Mbali ya Mechi hii ya Jumatano, Chelsea Jumamosi wapo kwenye Dabi ya London dhidi ya Arsenal katika Mechi ya Ligi Kuu England itakayochezwa Stamford Bridge
Mapacha wawili kutoka kundi la Psquare wamerudi tena kwenye headlines baada ya kununua nyumba katika moja ya ya majengo huko Atlanta.
Katika jengo hilo Peter, Paul pamoja na meneja wao ambaye ni kaka yao Jude Okoye kila mmoja ana sehemu yake ya kukaa.
psq

psq2
psq3
psq4
psq5

Kocha wa klabu ya Chelsea Jose Mourinho ambaye ni mtaalam wa kucheza na saikolojia za makocha na wachezaji wa timu pinzani ili aweze kushinda, kwa sasa yupo katika wakati mgumu na klabu yake ya Chelsea kwani bado haijafanya vizuri katika michezo ya Ligi Kuu.
Licha ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Uingereza msimu uliyopita, klabu ya Chelsea chini ya kocha Jose Mourinho imecheza mechi 5 za Ligi Kuu Uingereza na kushinda moja, sare moja na kupoteza mechi tatu. Hivyo September 15 katika Press Conference na waandishi wa habari, Jose Mourinho ameongea kuhusu hali ilivyo katika vyumba vya kubadilishia nguo.
481302717-467652
” Hili ni swali ambalo limeendelea kuulizwa mara kwa mara lakini jibu ambalo utataraji ni lile lile, hali za wachezaji katika vyumba vya kubadilishia nguo ni kuwa kuna wakati wa kutabasamu na kutaniana nafikiri hilo ni jibu la msingi. Kama watu hawapati mafanikio unatakiwa mpambane ili mfanikiwe nakuahidi tunafanya kazi kwa bidii”>>> Mourinho
“Tatizo pekee tulionalo ni mfululizo wa kutopata matokeo mazuri tunajua na hatufurahishwi na hii hali, ila unaweza kuniuliza kwa nini makocha wengine hawapo katika wakati mgumu licha ya kutofanya vizuri kwa miaka mitano, saba au kumi? lakini mimi bado ni bingwa wa Ligi Kuu Uingereza kwa nni nipate wakati mgumu”>>> Mourinho
MADRID, SPAIN - APRIL 30:  Jose Mourinho, coach of Real Madrid looks on during the La Liga match between Real Madrid and Real Zaragoza at Estadio Santiago Bernabeu on April 30, 2011 in Madrid, Spain.  (Photo by Julian Finney/Getty Images)
Hayo ni baadhi ya majibu ya kocha wa Chelsea Jose Mourinho ambaye amejibu kuhusu yeye kuwa na wakati mgumu kwa sasa, hizo ni kauli zilizotoka wakiwa wanaelekea kucheza mechi yao ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Maccabi Tel Aviv September 16.

Mashindano ya maarufu ya urembo duniani, Miss Universe, sasa yatakuwa chini ya kampuni ya kusaka, kuendeleza vipaji na masoko ijulikanayo kwa jina la WME/IMG. 
Awali mashindano hayo yalikuwa yakiendeshwa kwa ushirika baina ya kampuni hiyo na kampuni inayojishughulisha na masuala ya habari na burudani ya NBCUniversal na mtangazaji maarufu wa vipindi vya televisheni, mwanasiasa na mfanyabiashara, Donald J Trump. 
Akizungumza jijini jana, Mwandaaji wa mashindano ya Miss Universe Tanzania, Maria Sarungi Tsehai alisema kuwa wamepokea taarifa kuhusiana na kampuni mpya hiyo ambayo pia inaandaa mashindano ya Miss USA na Miss Teen Usa. 
Maria ambaye pia ni mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Compass Communications alisema kuwa wamepokea mabadiliko hayo na wataendelea kufanykazi na mmiliki huyo mpya ili kuendeleza vipaji vya wasichana nchini. 
Alisema kuwa mashindano ya Miss Universe ni moja kati ya matukio makubwa ya burudani duniani ambayo usaidia wasichana kutoka nchi zaidi ya 190 zinazoshiriki kila mwaka na watu zaidi ya nusu bilioni kufuatilia mashindano hayo kwa njia mbalimbali ikiwemo mitandao na televisheni. 
“Kwa sasa tupo katika maandalizi ya kufanya mashindano ya Miss Universe Tanzania, tunaamini kuwa mabadiliko haya yatatupa changamoto zaidi kwa lengo la kufika mbali na zaidi kuhakikisha tunatwaa taji baada ya matokeo mazuri ya Flaviana Matata ya mwaka 2007 ambapo aliingia hatua ya 10 bora,” alisema Maria. 
Afisa Mkuu wa kampuni ya WME/IMG, Mark Shapiro ameahidi kuyaendeleza mashindano hayo kufika ngazi ya juu kabisa ikiwa pamija na washindano bora. 
"Najisikia faraja kuendshs mashindano haya, tutayaendeleza kwa kiwango kikubwa na kuhakikisha umaarufu wake unaongezeka, naamini mashabiki wengi zaidi kwa sasa watafuatilia mashindano yetu kwa njia ya mbalimbali,” alisema Shapiro.
Maria Mwandaaji wa mashindano ya Miss Universe Tanzania, Maria Sarungi Tsehai alizungumza katika mashindano yaliyopita.
Miss Universe Tanzania 2014 Caroline Bernard akitoa elimu ya afya kwa wanafunzi wa kike katika shule ya msingi Msimbazi Mseto



Marais wengi wa Afrika wamekuwa wakikaa kwa muda mrefu madarakani hali inayochangia baadhi ya nchi kuingia katika machafuko wa kisiasa.
Ukongwe wao kwenye siasa umewafanya wengi wao kujikuta wakikaa miaka mingi zaidi na kuvunja rekodi ya kukaa madarakani kwa muda mrefu.
Hapa nimekuwekea list ya Marais wa Afrika wenye umri mkubwa zaidi ya wengine…
rais
1. Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe ana miaka 91, ndiye Rais mzee kuliko wote, ameshinda urais kwa muhula wa saba

tuni
2. Beji Caid Essebsi-Ana miaka 88, amekua Rais wa Tunisia tangu Desemba 31 2014

biya
3. Rais Paul Biya wa Cameroon ana miaka 82,ameingia madarakani tangu mwaka 1982

alge
4. AbdelAziz Boeteflika ni Rais wa Algeria toka April 1999, ana miaka 78

gine
5. Rais wa Guinea Alpha Conde ana miaka 77, amekua madarakani tangu Desemba 2010

da
6. Rais wa visiwa vya Sao Tome Manuel Pinto da Costa ana miaka 77, aliingia madarakani tangu mwaka 2011

lib
7. Rais wa Liberia Ellen Johnson Sirleaf ana miaka 76, aliingia madarakani tangu Januari 2006

muth
8. Rais wa Malawi Peter Mutharika ana miaka 74, aliingia madarakani May 2014

ivoo
9. Rais wa Ivory Coast Alassane Quattara  ana miaka 73, aliingia madarakani tangu mwaka 2011

zzzzz
10. Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma ana miaka 73, aliingia madarakani tangu May 9, 2009



.
.
Ni stori ya kisiasa ambayo ilianza kuchukua headlines kwenye mitandao mbalimbali kuhusu wasanii wawili wa Bongo Movies, Aunt Ezekiel na Vicent Kigosi aka Ray kuondoka UKAWA na kuhamia chama cha Mapinduzi.
Baada ya taarifa hizo kuchukua nafasi kubwa kwenye mitandao sasa ripota wa millardayo.com amezungumza na  Steve Nyerere ambaye ni mwenyekiti wa kampeni ya Mama ongea na Mwanao…’Ndugu zetu wakina Vicent Kigosi na Aunt Ezekiel walitoroka wamerudi CCM  kabla hawajatangaza lakini watatangaza wamerudi kwa kishindo kikubwa wanaamini bila hapo walipofika bila nguvu ya Mh Jakaya Mrisho Kikwete wasingiweza kufika‘ – Steve Nyerere
.
.
‘Kwa hiyo nataka kuwaambia watanzania kuwa hao watu wamerudi katika chama cha mapinduzi na wala msidanganywe pilika pilika za huku na kule hawa watu ni wanachama wa CCM hai walitoroka na sifa ya kutoroka ni kukosa nidhani kwa sisi wazazi ambao tuna watoto , mtoto akitoroka unatakiwa umpe adhabu ili siku nyingi afahamu njia ya sahihi na njia sahihi ni chama cha Mapinduzi ambacho kina Dkt John Pombe Magufuli na Mama Samia Suluhu’ – Steve Nyerere


Mchezaji Matata wa Man United Martial Taswira kamili Wachezaji wa Man United wakifanya Mazoezi kabla ya kukutana na  PSV EindhovenMeneja wa Man United Van GaalBastian, Shaw, Carrick, Young, Depay Juan Mata akiteta jambo na RojoDepay na ShawWakipasha wakati wa mazoezi kabla ya kukutana na PSV leo usikuFellaini nae ndaniKipa David De GeaBastian David De Gea aliyeongeza mkataba wa miaka minne na Kabu ya Man United.


MSIMAMO ULIVYO KWA SASA:
Barclays Premier League
PosLogo &TeamPWDLGDPts
1Manchester CityManchester City220066
2Leicester CityLeicester City220036
3LiverpoolLiverpool220026
4Manchester UnitedManchester United220026
5EvertonEverton211034
6Swansea CitySwansea City211024
7Crystal PalaceCrystal Palace210113
8West Ham UnitedWest Ham United210113
9Norwich CityNorwich City210103
10Aston VillaAston Villa210103
11ArsenalArsenal2101-13
12WatfordWatford202002
13Stoke CityStoke City2011-11
14Tottenham HotspurTottenham Hotspur2011-11
15Newcastle UnitedNewcastle United2011-21
16ChelseaChelsea2011-31
17SouthamptonSouthampton2011-31
18West Bromwich AlbionWest Bromwich Albion2011-31
19BournemouthBournemouth2002-20
20SunderlandSunderland2002-40

waliotembelea blog