Thursday, August 21, 2014


I'm out: Tim Sherwood has announced that he will not become the next Crystal Palace manager on Thursday
Mimi sipo!: Tim Sherwood jana ametangaza kuwa hatakuwa kocha Crystal Palace .

TIM Sherwood amejitoa mwenyewe katika mbio za kuwa kocha mpya wa Crystal Palace.
Kocha huyo wa zamani wa Tottenham Hotspur alikuwa anapewa nafasi kubwa ya kuteuliwa kuwa kocha mkuu wa Selhurst Park baada ya Malky Mackay kuondolewa katika kinyang'anyiro.
Lakini Sherwood hajavutiwa kurithi mikoba ya kocha aliyeondoka Tony Pulis, na hii inamaanisha Keith Millen ataendelea kuiongoza timu hiyo kwa muda katika mechi ijayo ya ligi kuu dhidi ya West Ham uwanja wa nyumbani.
No go: Sherwood is said to be uninterested in the job and has confirmed he will not take over as manager
Siendi: Sherwood anasema hajavutiwa na kazi hiyo na amethibitisha kuwa hatarithi mikoba.
"Palace ni klabu kubwa yenye utamaduni wake, lakini ipo katika hali ngumu ambayo haiwezi kuonekana kirahisi," Sherwood aliwaambia Sky Sports.
Makubaliano binafsi baina ya Sherwood na Palace yalishindwa kufikia muafaka baada ya kuripotiwa kuwa kocha huyo alitaka kuwa pamoja na wasaidizi wake wakati akiwa Spurs,  Chris Ramsey na Les Ferdinand katika dimba la Selhurst Park.
Mmiliki wa Palace, Steve Parish aligoma mapendekezo hayo na sasa anaangalia uwezekanao wa kupata kocha mpya zikisalia saa 48 tu klabu hiyo ijitupe uwanjani katika mchezo wa ligi kuu.


Na Adam Mbwana, Dar es salaam
Ilikuwa ni vita kali kati ya mafahali wawili ambao naweza kusema kila mmoja wao alikuwa na azimio tofauti kichwani mwake juu ya mwenzie. Vita hii huwezi kuifananisha na na zile za mwaka 1914 na 1939 ambazo ndio vita kubwa kuwahi kutokea duniani pale ambapo mataifa makubwa yalikuwa yalikuwa yakiwania utajiri kwa kutumia silaha kali na hatari duniani, lakini pia vita hii huwezi kuifananisha na ile maarufu ya miaka ya 1960 kati ya Urusi na Marekani wataalamu wakiita vita baridi ambayo haikutumia silaha kama sehem ya mapigano bali silaha ikitumika kama sababu kubwa ya vita hiyo
Lakini vita hii ni tofauti kabisa kwani inapiganwa katika mji ambao hauonekani kwa macho huku vyombo vya habari vikitujuza uwepo wake wakati wahusika wake wakuu wakiwa ni Romelo Lukaku na Josee Mourinho vita ambavyo havikuhitaji usuluhishi bali kuisha kwake kulihitaji mmoja wao akubali masharti ya mwenzake au kama si hivyo basi ilihitaji watu hawa kutengana kwa muda kama sio moja kwa moja.
Kocha wa Chelsea, Jose Mourinho

Wahusika hawa walikuwa na mawazo tofauti vichwani mwao, Lukaku akihitaji kuhakikishiwa namba ya kudumu katika kikosi cha kwanza cha Chelsea huku Mourinho naye akimtaka Lukaku apiganie nafasi yake katika timu mbele ya washambuliaji wengine kwenye timu kama Fernando Torres, Diego Costa na Didier Drogba. Na hapo ndipo vita iliponoga zaidi.
Tangu kusajiliwa kwake Chelsea August 2011 akitokea katika klabu ya Anderlecht ya Ubelgiji kwa paundi milion 17,  Romelo Lukaku ameshindwa kabisa kuonyesha uwezo mkubwa katika klabu hiyo ya Chelsea kama ambavyo wengi walitegemea.
 Wengi walidhania kuwa Lukaku ndiye atakuwa mrithi sahihi wa Didier Drogba katika safu ya ushambuliaji ya Chelsea kutokana na ukweli kwamba wawili hawa wanafanana sana kwa maumbo yao makubwa, staili ya kucheza kwa kutumia nguvu na hata kuwa na uwezo wa kuhimili beki zaidi ya mmoja. 
Diego Costa

Lakini hata hivyo mshambuliaji huyo mzaliwa wa Anrwerp nchinj Ubelgiji alimaliza msimu wake wa kwanza darajani akiwa mchezaji wa kikosi cha akiba.
Hali hiyo ilimfanya kupelekwa kwa mkopo msimu uliofuata wa mwaka 2012 katika timu ya Westbromwich Albiol ambapo aliweza kufunga magoli 17 na kumaliza katika nafasi ya sita ya wafungaji bora wa ligi kuu ya uingereza kwa msimu huo. Msimu uliofuata wa 2013-2014 alipelekwa tena kwa mkopo katika klabu ya Everton ambapo ambako nako alizifumania nyavu mara 15  katika mechi 31 alizocheza na kuisaidia Everton kumaliza katika nafasi ya 5 ya ligi huku akiwa na uwiano mzuri wa magoli zaidi ya washambuliaji wa chelsea Fernando Torres, Samuel Eto'o na Demba Ba ambao kwa pamoja waliweza kufunga magoli 19 tu.
Maneno yalianza kuibuka katika vyombo vya habari huku wachambuzi wa soka wakihoji nafasi ya Lukaku katika safu ya ushambuliaji ya Chelsea ambayo ilionekana kupwaya msimu uliopita chini ya kocha Josee Mourinho ambaye mara kwa mara alikuwa akiwalalamikia washambuliaji wake hao kwa kushindwa kuzifumania nyavu mara kwa mara.
Didier Drigbo amerudi Chelsea

Wachambuzi hao walimpa Lukaku sababu ya kuanza kudai nafasi ya kudumu katika kikosi cha Chelsea baada ya kumalizika kwa mkataba wake wa mkopo na Everton huku Mourinho akiweka pamba msikioni na kuendelea na mpango wake wa kumsajili mshambuliaji Diego Costa kutoka Atletico Madrid baada ya kuondoka kwa Samuel Eto'o na Demba Ba.
Kwa Lukaku hizi zilikuwa ni habari mbaya sana na ikawa ni moja ya sababu kubwa ya kuchochea vita kati yake na Mourinho kwani yeye alitegemea baada ya kuondoka kwa Etoo na Ba kungempa yeye nafasi ya kurudi kuchukua nafasi yake aliyokuwa akiisubiri kwa muda mrefu lakini badala yake akaletewa kipingamizi kingine ambaye ni Costa huku Mourinho akimpaka mafuta kwa mgongo wa chupa na kumwambia kuwa apiganie nafasi yake. Lakini kilichommaliza nguvu kabisa Lukaku na kurejea kwa Drogba klabuni hapo. Hapo ndipo Mourinho akamthibitishia Lukaku hakumuhitaji tangu mwanzo. Kwahiyo Lukaku alishuhudia makombora na vifaru vya kivita vikiingia kwenye ghala la silaha la Mourinho huku naye akishuhudia kwa macho yake.
Hatimaye Lukaku yakamshinda baada ya kuona adui yake hawezekaniki. Sasa ameamua kubwaga manyanga na kunyoosha mikono juu kama ishara ya kusalimu amri baada ya kukamilisha usajili wake wa kudumu katika klabu ya Everton wenye thamani inayotajwa kufikia paundi million 28.
Lakini suala la msingi la kujiuliza hapa ni Je, Mourinho alikuwa anataka nini cha ziada kutoka kwa Lukaku ili aweze kumpa nafasi? na Je, madai ya Mourinho kuwa Lukaku hakutaka kugombania nafasi kikosini ni ya kweli au ni kujisafisha tu mbele ya vyombo vya habari? na swali la mwisho ni Je, kwanini Torres abaki kikosini na kumuuza Lukaku ambaye msimu uliopita amefanya mambo makubwa zaidi ya Torres licha ya kuwa na umri mdogo?

Waswahili husema "funika kombe mwanaharamu apite". Hicho ndicho alichokifanya Lukaku baada ya kuamua kukubali kushindwa dhidi ya Mourinho. Ameamua kuanza maisha mapya Everton huku akimuacha Mourinho na pamba zake masikioni. Ama kweli asiyekubali kushindwa sio mshindani.

 

Mshiriki Nambari 1 (Subira Ally).
Mshiriki Nambari 2 (Hellen Eugen).
Mshiriki Nambari 3 (Rehema Jabiry).
Mshiriki Nambari 4 (Catheline Alex).
Mshiriki Nambari 5 (Dalena David).
Mshiriki Nambari 6 (Winfrida Guntram).
Mshiriki Nambari 7 (Salama Salehe).
Mshiriki Nambari 8 (Magdalena Majawa).
Mshiriki Nambari 9 (Grace John).
Mshiriki Nambari 10 (Lilian Loth).
Mshiriki Nambari 11 (Amina Salum).
Mshiriki Nambari 12 (Rebeca Mdamu).
Mshiriki Nambari 13 (Sitti Mtemvu).
Mshiriki Nambari 14 (Ellen Sule).
Mshiriki Nambari 15 (Neema Mollely).
Mshiriki Nambari 16 (Lucy Lewis).
Mshiriki Nambari 17 (Esther Mnahi).

 


Wachezaji wa Coastal Union wakiwa uwanja wa ndege Tanga wakipanda ndege kuelekea Pemba kwa ajili ya kuweka kambi ya Mazoezi kwa ajili ya maandalizi ya msimu ujao wa Ligi kuu soka Tanzania bara, safari hiyo imedhaminiwa na wafadhili wa timu hiyo
kiwanda cha Unga mkoani Tanga Pembe..


.


Competition: The signing of Rojo will add further competition to the left-back spot after Luke Shaw's arrivalCaptain: Wayne Rooney gives some advice to new boy Marcos Rojo in training
Manager: Louis van Gaal abandoned his tactics in just one half of Premier League football last weekend
Redemption: Manchester United will look to redeem themselves after losing 2-1 to Swansea last weekend
Team-mates: David De Gea and Anderson walk out to training arm in arm at Carrington
Partners: Wayne Rooney and Robin van Persie share a joke during a training session

DSC_0007-546x291
Kocha mkuu wa Simba sc Patrick Phiri akiongea na wachezaji wake


Kocha mkuu wa Yanga akiongea na msaidizi wake
Baraka Mpenja, Dar es salaam
RATIBA ya ligi kuu soka Tanzania bara msimu wa 2014/2015 utakaoanza kutimua vumbi septemba 20 mwaka huu umeanikwa hadharani na Shirikisho la soka nchini Tanzania TFF.
Afisa habari na mawasiliano wa TFF, Boniface Wambura Mgoyo katika taarifa yake amesema ratiba hiyo imezingatia michuano ya Chalenji itakayochezwa Novemba, usajili wa dirisha dogo Nov 15- Des 15, ushiriki wa klabu za Azam na Yanga kwenye mashindano ya Ligi ya Mabingwa (CL) na Kombe la Shirikisho (CC).(P.T)
Wambura alisema mechi zitachezwa wikiendi ili kuongeza msisimko/kuwapa fursa washabiki wengi zaidi kuhudhuria, na katikati ya wiki imeachwa wazi kwa ajili ya mechi za Kombe la FA (Federation Cup).
Vilevile kutakuwa na mechi Boxing Day na siku ya Mwaka Mpya.
Siku ya ufunguzi zitapigwa mechi saba katika viwanja tofauti nchini ambapo mabingwa watetezi  Azam fc wataanza kutetea ubingwa wao dhidi ya wageni Polisi Morogoro katika uwanja wa Azam Complex, Chamazi, jijini Dar es saalam.
Yanga chini ya kocha Mbrazil, Marcio Maximo wataanza ugenini katika uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro dhidi ya wakata miwa wa Mtibwa Sugar.
Timu mbili zilizopanda ligi kuu msimu huu, Stand United na Ndanda fc zitachuana katika dimba la Kambarage mkoani Shinyanga.
Mgambo JKT watakawakaribisha Kagera Sugar katika dimba la CCM Mkwakwani jinni Tanga.
Ruvu Shooting wataanza kampeni zao katika uwanja wao wa Mabatini uliopo Mlandizi Pwani dhidi ya maafande wa Tanzania Prisons.
Wagonga nyumbo wa Mbeya City fc wataanza nyumbani katika dimba la CCM Sokoine Mkoani Mbeya dhidi ya JKT Ruvu.
Wekundu wa Msimbazi Simba chini ya kocha Mzambia, Patrick Phiri wao wataanza kampeni za kuusaka ubingwa wa ligi kuu bara septemba 21 dhidi ya Coastal Union uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Raundi ya pili  itacheza septemba 27 na 28 mwaka huu ambapo timu zote zitashuka dimbani.
Septemba 27, wekundu wa Msimbazi Simba watacheza mechi yao ya pili nyumbani dhidi ya Polisi Morogoro.
Mechi nyingine siku hiyo zitakuwa baina ya Mtibwa Sugar dhidi ya Ndanda fc katika uwanja wa Manungu Turiani. Azam watawakaribisha Ruvu Shooting Chamazi, Mbeya City watachuana na Coastal Union uwanja wa Sokoine, wakati Mgambo JKT watakuwa Mkwakwani kuchuana na Stand United.
Raundi ya pili itakamilika septemba 28 ambapo JKT Ruvu watavaana na Kagera Sugar katika uwanja wa Azam Complex.
Mechi nyingine itawakutanisha Yanga sc ya Maximo dhidi ya Tanzania Prisons uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.


Maadalizi ya Miss Talents yatakayofanyika jumamosi tarehe 23 august ndani ya club kubwa ya desire 
 
 
 

Bondia Mohamed Matumla kushoto na Nassibu Ramadhani wakitunishiana misuli 
Na Mwandishi Wetu
MABONDIA Nassibu Ramadhani pamoja na Mohamed Matumla wameingia makubaliano ya kuzipiga kwa mara ya pili siku ya septemba 27 katika ukumbi wa Friends Corner Hotel Manzese Dar es salaam Akizungumzia mpambano huo mratibu wake Yassin Abdallah ‘Ostaadhi’ amesema mabondia hao wamekubaliana na kusaini mkataba wa kuzipiga siku hiyo
 mabondia hao walikutana kwa  mara ya kwanza na bondia Mohamed Matumla alimshinda kwa pointi Nassibu Ramadhani hivyo kuufanya mchezo huu kuwa mgumu zaidi kwa Matumla ili kuendeleza kipigo au Ramadhani kulipiza kisasi
hiyo Septemba 27 Mapambano  ya utangulizi yatakuwa hivi bondia Issa Omari atamkabili juma fundi.Kg 53 raundi nane. na Sadiq Momba vs Tasha Mjuaji Kg 59 raundi nane. wakati Juma Mustafa atamkabili Bakari Dunda Kg 61 raundi sita. huku kina dada Lulu Kayage akipambana na Fatma Yazidu.Kg 51 raundi nne. siku hiyo pia kutakuwa na uuzwaji wa DVD ambazo zinatoa mwanga kwa mchezaji kujua mchezo na kufahamu zaidi mbinu mpya zitumiwazo na mataifa mbali mbali Duniani.
Wakiwemo mabondia bingwa wa dunia kama Manny Paquaio,Floyd Maywether,Amir Khani, Mohamed Ali ,Mike Tayson na wengine wengi wanaotamba na waliotamba katika mchezo  wa masumbwi Duniani

1408571118014_wps_1_epa04360280_Arsenal_s_Mik 
Majanga: Kiungo wa Arsenal, Mikel Arteta atakaa nje ya uwanja kwa mechi mbili zijazo.
HABARI mbaya kwa mashabiki wa Asernal, Mikel Arteta atakaa nje ya uwanja katika mechi mbili zijazo baada ya kupata majeruhi ya kifundo cha mguu wakati wa mechi ya mtoano ligi ya mabingwa barani Ulaya jumanne ya wiki hii dhidi ya Besiktas.

1408543326669_wps_1_SAO_PAULO_BRAZIL_JULY_09_Walizinguana: Argentina Sergio Aguero na Marcos Rojo walitamkiana maneno makali katika fainali za kombe la dunia.
MECHI ya watani wa jadi nchini England baina ya Manchester United na Manchester City “The Manchester derby” itakuwa na ladha tofauti msimu huu ambapo nyota wawili wanaocheza timu ya taifa ya Argentina, Sergio Aguero na Marcos Rojo watakutana.
Wachezaji hao wawili waliocheza fainali ya kombe la dunia walisemekana kutamkiana maneno makali wakati wa mashindano ya majira ya kiangazi nchini Brazil baada ya Rojo ambaye amekamilisha kujiunga na Manchester United kwa paundi milioni 16 kutoka klabu ya Sporting Lisbon kumkaribisha rafiki yake, mkali wa muziki wa  Pop nchini Argentina, El Polaco ndani ya chumba cha kubadilishia nguo baada ya mchezo wa makundi.


Wanted: Roma have asked about the availability of Chelsea striker Fernando Torres
Anawindwa: Roma wanaitaka saini ya Fernando Torres 

ROMA wameulizia uwezekano wa kumsajili mshambuliaji wa Cheslea, Fernando Torres.
Timu hiyo ya Italia, inaitaka saini ya mshambuliaji huyo wa Hispania, na watawashawishi The Blues kumchukua Mattia Destro kama sehemu ya dili hilo.
Torres amekuwa na wakati mgumu tangu ajiunge Stamford Bridge kutokea Liverpool kwa ada kubwa ya uhamisho ya paundi milioni 50 mwezi januari 2011.
Kocha Jose Mourinho ameongeza wachezaji katika safu ya ushambuliaji majira haya ya kiangazi ambapo amemsajili Diego Costa kwa paundi milioni 32 na kumrudisha gwiji wa Chelsea, Didier Drogba.
Tayari Roma walishamsajili nyota mwingine wa zamani wa Cheslea, beki wa kushoto, Ashley Cole kama mchezaji huru.
Part of the deal: Roma are seeing whether Chelsea would be keen to take Italian frontman Mattia Destro
Sehemu ya dili: Roma wanataka kuwapatia Mattia Destro kama sehemu ya usajili wa Torres.


How it's going to be: Mario Balotelli mocked up in a Liverpool shirt in anticipation of his £16m move to Anfield
Anaenda kuwa hivi: Mario Balotelli ametengenezwa akiwa amevalia jezi ya Liverpool.

LIVERPOOL wamekubali kuilipa AC Milani ada ya uhamisho ya paundi milioni 16 ili kuinasa saini ya mshambiliaji wa Italia, Mario Balotelli.
Mwezi uliopita, Brendan Rodgers alisema Liverpool haiwezi kumsajili Balotelli, lakini amebadili moyo wake.
Mapema leo Balotelli aliwaambia Sky Italia: "Leo itakuwa siku yangu ya mwisho Milanello."
Super Mario: Balotelli left the Premier League in 2013, but now seems to be on his way back with Liverpool
Super Mario: Balotelli aliondoka ligi kuu nchini England mwaka 2013, lakini yuko njiani kurudi na safari hii anatua Liverpool 
Change of heart: Rodgers had previously said he would not be signing the Italian striker
Amebadili moyo: Rodgers awali alikataa kumsajili mshambuliaji huyo wa Italia.
Stats: Balotelli's Premier League record (via Opta)
Stats: Balotelli's Premier League record (via Opta)

Nyota huyo kurudi England kutateka hisia za mashabiki wengi wa soka wakikumbuka vituko vyake akiwa Manchester City kabla ya kuondoka mwaka 2013.
Balotelli amejihusisha na matukio mengi ya utovu wa nidhamu hususani wakati akicheza ligi kuu England 
Ndani ya uwanja, alioneshwa kadi nyekundu wakati Man City ilipochuana na Asernal mwaka 2012 na kufungwa.
Nje ya uwanja, alikuwa na matukio ya mengi ya ukutuku.
Moja ya tukio la kukumbukwa pia ni kitendo chake cha kuonesha fulana iliyoandikwa 'Why Always Me?' alipofunga goli kwenye mechi ya mahasimu wa Manchester ndani ya dimba la Old Trafford mwaka 2011.
Pia aliingia katika mgogoro na kocha wa City wakati ule, Roberto Mancini ndani ya uwanja wa mazoezi na kukunjana.
Zaidi alimchapa kibao Jerome Boateng.
Tangu aliporudi nchini Italia amefunga mabao 30 katika mechi 54, idadi sawa na aliyofunga akiwa na City katika mechi 80.
Si rahisi kusahau kuwa nyota huyu tayari ameshinda makombe manne katika mataifa mawili, ubingwa ligi na kombe la FA na Coppa Italia akiwa na umri wa miaka 24.

waliotembelea blog