Tuesday, November 3, 2015



JoseJose MourinhoMENEJA wa Chelsea Jose Mourinho amekanusha kwamba kuna maasi ya Wachezaji ndani ya Timu yao.
Mapema Leo Kiungo wa Chelsea Cesc Fabregas aliibuka na kukana ripoti kuwa yeye ndio ameandaa maasi kwenye Timu.
Chelsea, ambao ni Mabingwa Watetezi wa Ligi Kuu England, hivi sasa wamekumbwa na matokeo mabovu baada ya kufungwa Mechi 6 kati ya 11 za Ligi Msimu huu.
Akiongea hii Leo, Mourinho alisema: “Ni tuhuma za kuhuzunisha, unamtuhuma Mchezaji au Wachezaji, kutokuwa waaminifu.”
Nae Nahodha wa Chelsea, John Terry, akihojiwa na kuulizwa ikiwa ni kweli yupo Mchezaji wa Chelsea alietamka kwamba ‘wapo tayari kufungwa kuliko kushinda chini ya Mourinho’, alijibu: “Katika maisha yangu yote ya Soka sijasikia Mchezaji atoke na kusema hivyo. Nakuhakikishia sisi tupo Asilimia 100 nyuma ya Meneja.”
Terry aliongeza: “Tuko pamoja, yeyote alieona Gemu zetu 4 au 5 zilizopita aliona tulikosa sana bahati. Tutageuza mambo. Tutabaki pamoja.”
Chelsea, ambao Msimu uliopita waliotwaa Ubingwa walipoteza Mechi 3 tu za Ligi kwa Msimu mzima, wapo Pointi 14 nyuma ya Vinara Manchester City.


Mshambuliaji wa timu ya Taifa ya Wanawake ya Tanzania ‘Twiga Stars’ Estha Chaburuma ‘Lunyamila’ ataagwa rasmi katika mchezo wa kirafiki kati ya timu ya Taifa ya Tanzania ya Wanawake ‘Twiga Stars’ dhidi ya timu ya taifa ya wanawake ya Malawi utakaochezwa siku ya jumamosi katika uwanja wa Azam Complex Chamazi jijini Dar es salaam.
Chaburuma amekua ni miongoni mwa wachezaji waanzilishi wa Twiga Stars ambapo amekua akiitumikia timu hiyo tangu kuanzishwa kwake mpaka sasa timu inapojiandaa na mchezo dhidi ya Malawi.
Mwenyekiti wa Kamati ya Soka la Wanawake ya TFF, Amina Karuma amesema wameamua kutumia mchezo huo wa kirafiki kwa ajili ya kumuaga Chabruma ambaye amekua ni chachu ya maendeleo ya mpira wa miguu kwa wanawake, kutokana na kuwafanya wanawake wengi kujitokeza kucheza mchezo huo.
Naye kocha wa timu hiyo, Rogasian Kaijage amesema vijana wake wapo katika hali nzuri, wananadelea na maandalizi ya mchezo huo wa jumamosi, ambapo anaimani watautumia vizuri katika kumuaga mchezaji mwenzao wa siku nyingi.


Rooney akishangilia bao lake la pekee baada ya kuipa bao Man United katika dakika ya 79 kipindi cha pili.Ushindi huu umewapaisha kileleni Man United kwa kupata pointi 7, anayefuata ni PSV ana pointi 6, Wolfsburg nae 6 na wa mkiani ni SCKA anazo pointi 4 katika grupu lao BRooneyJesse Bastian akiendesha mpira Meneja wa Man United Van Gaal Mlinda mlango wa Man United De GeaMartial akichomoka na mpiraWayne Rooney Chris Smalling akikacha na mpiraRooney  na AlanJesse akiachia shuti kaliIgor na Wayne RooneyAnthony Martial Jesse kenye patashika na kipa wa CSKA MoscowVIKOSI
Manchester United:
De Gea, Young, Smalling, Blind, Rojo, Schweinsteiger, Carrick, Lingard, Mata, Martial, Rooney.
Akiba: Romero, Jones, Darmian, Pereira, Ander Herrera, Depay, Fellaini.
CSKA Moscow: Akinfeev, Fernandes, Ignashevich, A. Berezutski, Schennikov, Wernbloom, Z. Tosic, Dzagoev, Milanov, Natcho, Musa.
Akiba: Chepchugov, Vasin, Nababkin, Golovin, Panchenko, Doumbia
Walipo Man United


Nacho dakika ya 35 kafunga baoChupuchupu!1-0 Real wanaongoza kipindi cha kwanza...likifungwa na Nacho dakika ya 35
VIKOSI:
Real Madrid:
Navas, Danilo, Sergio Ramos, Varane, Marcelo, Modric, Casemiro, Kroos, Jese, Ronaldo, Isco.
Akiba: Casilla, Pepe, Nacho, Rodriguez, Kovacic, Lucas, Cheryshev.

PSG: Trapp, Aurier, Thiago Silva, Luiz, Maxwell, Verratti, Thiago Motta, Matuidi, Di Maria, Ibrahimovic, Cavani.
Akiba: Sirigu, Stambouli, Lucas Moura, Kurzawa, Lavezzi, van der Wiel, Rabiot.

Real Madrid vs PSG


Sevilla 1-3 Manchester City: Raheem Sterling nets first Champions League goal as Manuel
VIKOSI:

Sevilla XI: Sergio Rico, Coke, Rami, Kolodzieczak, Tremoulinas, Iborra, Krychowiak, Vitolo, Banega, Konoplyanka, Llorente

Manchester City XI: Hart; Sagna, Kompany, Otamendi, Kolarov; Fernando, Fernandinho; Navas, Toure, Sterling; Bony



Jana CAF imetoa 10 Bora ya Wagombea wa Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwaka kwa Afrika kwa Makundi yake Mawili na Straika mahiri wa Tanzania, Mbwana Samatta, yumo.
Samatta, ambae huchezea Klabu ya Congo DR TP Mazembe ambayo ameifikisha Fainali ya CAF CHAMPIONS LIGI, yumo kwenye 10 Bora ya Wachezaji wanaogombea Tuzo hii kwa Wachezaji wanaocheza ndani Afrika.

Samatta ndie anaongoza Listi ya Wafungaji Bora wa CAF CHAMPIONS LIGI akiwa na Bao 7 baada ya Majuzi kufunga Bao la ushindi wakati TP Mazembe inaichapa 2-1 USM Alger huko Algeria kwenye Mechi ya Kwanza ya Fainali ya CAF CHAMPIONS LIGI.
Timu hizo zitarudiana huko Lubumbashi Jumapili inayokuja.
Washindi wa Tuzo hii huamuliwa kwa Kura za Makocha wa Timu za Taifa za Nchi Wanachama wa CAF.
Washindi hao watatangazwa Alhamisi, Januari 7, 2016 huko Abuja, Nigeria.


MCHEZAJI BORA WA MWAKA – WANAOCHEZA NDANI YA AFRIKA:
Abdeladim Khadrouf (Morocco & Moghreb Tetouan)
Baghdad Bounedjah ( Algeria & Etoile du Sahel)
Felipe Ovono (Equatorial Guinea & Orlando Pirates)
Kermit Erasmus (South Africa & Orlando Pirates)
Mbwana Aly Samatta (Tanzania & TP Mazembe)
Mohamed Meftah ( Algeria & USM Alger)
Mudather Eltaib Ibrahim ‘Karika’ (Sudan & El Hilal)
Robert Kidiaba Muteba ( DR Congo & TP Mazembe)
Roger Assalé (Cote d’Ivoire & TP Mazembe)
Zineddine Ferhat (Algeria & USM Alger)


MCHEZAJI BORA WA MWAKA:
André Ayew (Ghana & Swansea)
Aymen Abdennour (Tunisia & Valencia)
Mudather Eltaib Ibrahim ‘Karika’ (Sudan & El Hilal)
Mohamed Salah (Egypt & Roma)
Pierre-Emerick Aubameyang (Gabon & Borussia Dortmund)
Sadio Mané (Senegal & Southampton)
Serge Aurier (Cote d’Ivoire & Paris Saint Germain)
Sofiane Feghouli (Algeria & Valencia)
Yacine Brahimi ( Algeria & Porto)
Yaya Touré (Cote d’Ivoire & Manchester City)

waliotembelea blog