Tuesday, December 17, 2013

 Kila mtu anaithamini na kuipenda tarehe ya siku 
yake ya kuzaliwa,ni siku ambayo baadhi yetu huifurahia kwa
 mitindo tofauti tofauti kulingamna 

na nafasi aliyonayo mtu husika,lakini hebu
 jiulize how it feels ndani ya hiyo siku mhimu kabisa 
unapofanyiwa kitu kizuri na cha pekee na mtu
 mhimu maishani mwako,inapendeza siyo?hivyo ndivyo
 nilivyojiskia siku ya jana baada ya 
kufanyiwa suprise ya  birthday party
 na kipenzi changu,Penniel pamoja
 na Mama yangu mpenzi,dada yangu Esma,Halima kimwana 
na familia yangu kwa ujumla.
checkout picha zikijieleze zenyewe........
Ilikuwa ni baada ya kutoka kwenye  uzinduzi wa Coke studio,kufika nyumbani  alipokelewa kwa bashasha na  Queen Darlin(aliyeshikilia cake)







,Queen Darlin na Diamond




ilivyokuwa chumbani sasa . wooow!!











Picha ya pamoja na family

Habari zimetujia sasa hivi zinasema abiria kadhaa akiwemo Waziri Mkuu mstaafu na mbunge wa Monduli  Mh Edward Lowassa wamenusurika kifo, baada ya ndege waliyokuwa wakisafiria kuwa pasuka matairi yote manne ya nyuma wakati ilipokuwa ikitua katika uwanja wa Arusha leo mchana. 
Ndege hiyo ya shirika la ndege la precision aina ya ATR ilipata ajali hiyo wakati ikitua, ambapo Matairi yote manne ya nyuma yalipasuka na kusababisha taharuki kubwa kwa abiria.
"Yaani Mungu ni mkubwa kwa kweli, ametunusuru maisha yetu na kiongozi kipenzi chetu Lowassa...Mungu atamlinda jamani...siamini" alisikika akisema mama mmoja miongoni mwa abiria hao wakati akishuka.
 Mh Lowassa ni mbunge wa Monduli, jimbo ambalo anatoka Waziri Mkuu aliyekuwa kipenzi Cha mwalimu Nyerere na watanzania hayati Edward Moringe Sokione.Sokoine aliyefariki katika ajali ya gari mwaka 1994.
 UPDATES KUTOKA ABIRIA MWINGINE:Nikiwa mmoja wa abiria tuliosafiri na PW kurudi Arusha leo, ndege ya shirika hilo yenye usajili No 5HPWI imepata kizaazaa wakati wa kutua baada ya tairi mojawapo kupasuka kwa kishindo, likufuatiwa na mengine yote ya nyuma ambapo yalipasuka pia na kuacha vipandevipande kwenye njia ya kurukia.

Waliookota vipande hivyo wamesema kuwa wamekuta viraka(pechi, watu wa magari wananielewa zaidi hapa), kitu ambacho si kawaida kwenye usafiri wa jamii hii!

Rubani wa ndege hiyo amejitahidi kuitoa ndege hiyo nje ya njia ili kutozuia ndege nyingine kuruka, japokuwa mwishowe ilimgomea kabisa na kubaki ikisota pembeni mwa njia hiyo.

Kikubwa ni kwamba hakuna madhara yaliyowapata abiria, akiwemo Bwana Lowassa.

Mwanamuziki Fid Q akizikonga nyoyo za mashabiki wa Mwanza
 

Young Killer
Young Killer akifanya makamuzi ya nguvu ndani ya CCM Kirumba jana.
H-Baba akikamua katika Tamasha kubwa la Ujasiriamali uko mwanza
...H-baba akiwasalimia mashabiki
Msanii Jitaman  akifanya yake jukwaani jijini mwanza
Mkurugenzi wa Global Publishers na Street University, Eric Shigongo 

 

Mbunge wa (Chadema), Mheshimiwa Joseph Mbilinyi 'Sugu', akiwafundisha wananchi wa Mwanza.
 
 
 

Joseph Mbilinyi 'Sugu' akipozi na H-Baba.
Tamasha kubwa la Ujasiriamali lililofikia tamati jana jioni katika Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza lilitawaliwa na elimu pamoja na burudani kali kutoka kwa wasanii Fid Q, H-Baba, Young Killer na Jitta Man. Kwa upande wa injili, burudani hizo ziliongozwa na Martha Mwaipaja na Emmanuel Mgaya 'Masanja Mkandamizaji. Walimu wa ujasiriamali nchini, Eric Shigongo na James Mwang'amba wakiwa sambamba na Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Mhe. Joseph Mbilinyi 'Sugu' walitoa elimu ya ujasiriamali kwa wakazi wa Mwanza na kuwaacha wakiwa wameiva kwenye masuala hayo.


Chelsea na Manchester City leo zimeshinda Mechi zao za Ligi Kuu England walizocheza Nyumbani na kuikaribia Arsenal ambao wapo kileleni na pia kuishusha Liverpool iliyokuwa Nafasi ya Pili na kuitupa Nafasi ya 4.
Wakati Liverpool hii leo ikichapwa Bao 3-1 na Hull City, Chelsea ilishinda kwake Stamford Bridge kwa kutoka nyuma kwa Bao 1-0 hadi Haftaimu na kuifunga Southampton Bao 3-1.
Bao za Chelsea zilifungwa na Gary Cahill, John Terry na Demba Ba, alieingizwa Kipindi cha Pili.
Bao la Southampton, lililofungwa katika Dakika ya Kwanza tu, lilipachikwa na Rodriguez.
Huko Etihad, Bao la Negredo na mbili za Samir Nasri, ziliwapa Manchester City ushindi wa Bao 3-0 walipoichapa Swansea City.

Ushindi wa leo umeifanya Chelsea ikamate Nafasi ya Pili ikiwa Pointi 4 nyuma ya Vinara Arsenal na Nafasi ya Tatu imeshikwa na Man City walio Nafasi ya Tatu na wapo Pointi 2 nyuma ya Chelsea.
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
  

waliotembelea blog