Friday, November 21, 2014

JUMAMOSI KESHO HAPATOSHI!! ARSENAL v MAN UNITED - VAN GAAL ATAJA KIKOSI CHAKE CHA KUIUA GUNNERS EMIRATES!! KIPA DE GEA NDANI!

 
Meneja wa Manchester United Louis van Gaal ameongea na Wanahabari kuhusu Mechi yao ya Jumamosi na Arsenal huko Emirates na hasa hali ya Wachezaji wake Majeruhi ambao mwanzoni mwa Wiki walifikia 12 toka Timu ya Kwanza.
Akiongea huko Aon Training Complex, Carrington Jijini Manchester, Van Gaal alitoboa kuwa Angel Di Maria, David De Gea na Michael Carrick wako fiti kuivaa Arsenal.
Alisema: “Ni ngumu kusema kama wote wamerudi kwa sababu inabidi tusubiri hadi Mazoezi ya Ijumaa na kuamua. Falsafa yangu ni kuwa ufanye Mazoezi si chini ya Wiki moja na Kikosi kizima, vizuri hasa ni Wiki 2. Lakini kwa hali yetu, inabidi tuwaingize Wachezaji hao Kikosini hivi sasa.”Alifafanua: “Di Maria amefanya mazoezi kawaida tu, hamna tatizo hapo lakini Shaw lipo. De Gea safi, hamna tatizo. Kwa Carrick inabidi tusubiri kidogo lakini yupo tayari kucheza.”
Kuhusu kuumia kwa Kiungo Daley Blind ambae alipata tatizo la Goti akiichezea Nchi yake Netherlands, Van Gaal amesema amewekewa sapoti kwenye Goti na atapimwa baada ya Siku 10 lakini hayupo katika hali mbaya kama ilivyofikiriwa.Angel di Maria (left) took part in Manchester United training on Friday after recovering from a foot injury
Arsenal wataingia kwenye Mechi hii ya Jumamosi wakiwa Nafasi ya 6 Pointi 1 tu mbele ya Man United ambayo iko Nafasi ya 7.
Michael Carrick (left) was pictured all smiles as he looks to regain full fitness after hurting his groin
Mara ya mwisho Arsenal kuifunga Man United ni Mei Mosi Mwaka 2011 Bao 1-0 Uwanjani Emirates kwenye Mechi ya Ligi na tangu wakati huo wamecheza Mechi 6 na kutoka Sare 2 tu na zote zilizobaki Man United kushinda ukiwemo ushindi wa kishindo wa Bao 8-2 hapo Tarehe 28 Agosti 2012.
The news of the quartet's return to fitness will be a boost to boss Louis van Gaal (right) ahead of their clash against ArsenalVan Gaal akiteta jambo na Vijana wake leo IjumaaManchester United captain Wayne Rooney (centre) will be hoping to lead the Red Devils to victory on SaturdayWachezaji wa United wakijifua leo tayari kwa mchezo wao na Arsenal Emirates.Rooney (left) needs one more goal against Arsenal to become the highest Premier League goalscorer against Arsene Wenger's sideKazi ipo kesho!Van Gaal (right) and assistant manager Ryan Giggs share a joke as they watch the session unfold at the Aon Training ComplexVan Gaal na msaidizi wake GiggsBelgium international duo Adnan Januzaj (centre) and Marouane Fellaini will both be hoping to start against Arsenal on SaturdayNi sisi na Arsenal kesho!Midfield duo Juan Mata (bottom left) and Antonio Valencia (bottom right) are put through their paces on FridayAnders Lindegaard (left) could make his first Premier League appearance of the season if De Gea fails to recover from his injury


Diamond Platinumz wakati akitambulisha ngoma yake mpya iitwayo Ntapata Wapi leo hii kwenye kipindi cha Leo Tena cha Clouds FM.Hapa akichagua barua za wale waliotuma kwa ajili ya watoto wao wanaompenda Diamond na atakayeshinda atatembelewa na msanii huyo nyumbani kwake.
You might also like:

www.bukobasports.com

Jumamosi hii tukutane Jembe Beach Malimbe Mwanza kwani kuna bonge la Show la Hiphop toka kwa WEUSI, siunajua makamuzi yao si yakitoto mazee ama nini.

waliotembelea blog