Thursday, January 12, 2017


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa Barabara ya Mwigumbi-Maswa (Km 50.3) katika Wilaya ya Maswa mkoani Simiyu. Wengine katika picha ni Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Antony Mtaka watatu kutoka kulia Waziri wa Ujenzi Profesa Makame Mbarawa wakwanza kulia pamoja na viongozi wengine.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na viongozi wengiene  akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Mitambo itakayotumika katika ujenzi wa mradi wa Barabara ya Mwigumbi-Maswa (Km 50.3).
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisikiliza maelezo ya mradi wa ujenzi wa Barabara ya Mwigumbi-Maswa (Km 50.3) kutoka kwa Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini TANROADS  Mhandisi Cristianus Ako kabla ya kuweka jiwe la msingi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wananchi wa Maswa kabla ya kuweka jiwe la msingi ujenzi wa wa Barabara ya Mwigumbi-Maswa (Km 50.3), mkoani Simiyu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Waziri wa Ujenzi Profesa Makame Mbarawa mara baada ya kuwasili Wilayani Maswa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimsikiliza mkuu wa mkoa wa Simiyu Antony Mtaka mara baada ya kuwasili Wilayani Maswa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Waziri wa TAMISEMi na Kazi maalumu kutoka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Haji Omari Heri kabla ya kuweka jiwe la msingi ujenzi wa barabara hiyo ya Mwigumbi-Maswa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na Waziri wa TAMISEMi na Kazi maalumu kutoka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Haji Omari Heri wakimwagilia maji mti mara baada ya kuupanda baada ya uwekaji wa jiwe la msingi ujenzi wa barabara ya Mwigumbi-Maswa (Km 50.3), mkoani Simiyu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiweka saini kwenye Ubao kwa kutumia Chaki zinazotengenezwa na Kiwanda cha Chaki cha Maswa Mkoani Simiyu. Rais Dkt. Magufuli aliwapongeza wenye kiwanda hicho na kuwashauri kukipanua zaidi ili kiweze kuwafikia Watanzania wengi wenye mahitaji ya Chaki.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwahutubia Wakazi wa Maganzo mkoani Shinyanga mara baada ya kumaliza ziara yake ya siku mbili mkoani Simiyu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwahutubia Wakazi wa Maganzo mkoani Shinyanga mara baada ya kumaliza ziara yake ya siku mbili mkoani Simiyu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na wakazi mbalimbali wa Maswa mara baada ya kumaliza kuwahutubia Wilayani humo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na wakazi mbalimbali wa Maswa mara baada ya kumaliza kuwahutubia Wilayani humo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mkuu wa mkoa wa Simiyu Antony Mtaka wakiangalia utengenezwaji wa Chaki katika kiwanda cha Chaki cha Maswa mkoani Simiyu.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein akiongea na wananchi wakati wa sherehe za miaka 53 ya mapinduzi ya Zanzibar ambapo alisema mbali za jitihada zilizofanywa na serikali hiyo katika kuinua maisha ya wazanzibar ameahidi kuendelea kusimamia rasilimali ili zitumike kwa maslahi ya wananchi wote.
PINDU 2
2-Makamo wa Pili wa Rais Zaznzibar Balozi Seif Ali Idd akiongea na wananchi wakati wa sherehe za miaka 53 ya mapinduzi ya Zanzibar ambapo alisema serikali ya mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kuweka jitihada ili kuendelea kujenga uchumi za Zanzibar kwa maslahi ya wananchi.
PINDU 3
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein akiwasalimia wananchi walijitokeza katika sherehe za miaka 53 ya mapinduzi ya Zanzibar zilizofanyika katika uwanja wa Amani, Zanzibar.
PINDU 5
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein akiimba wimbo wa Taifa katika sherehe za miaka 53 ya mapinduzi ya Zanzibar zilizofanyika katika uwanja wa Amani, Zanzibar.
PINDU 6
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein akikagua gwaride katika sherehe za miaka 53 ya mapinduzi ya Zanzibar zilizofanyika katika uwanja wa Amani, Zanzibar.
PINDU 7
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein akisalimiana na viongozi wastaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika sherehe za miaka 53 ya mapinduzi ya Zanzibar zilizofanyika katika uwanja wa Amani, Zanzibar.
PINDU 8
Vikundi mbalimbali, Asasi za Kiraia,Vyama vya Siasa,Mikoa,Wizara na Taasisi za Serikali wakipita mbele Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein katika sherehe za miaka 53 ya mapinduzi ya Zanzibar zilizofanyika katika uwanja wa Amani, Zanzibar.
PINDU 13
Vikosi mablimbali vya Jeshi la Polisi vikipita mbele Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein katika sherehe za miaka 53 ya mapinduzi ya Zanzibar zilizofanyika katika uwanja wa Amani, Zanzibar.
PINDU 14
Vijana vya halaiki wakiwa katika umbo linaloonesha miaka 53 ya mapinduzi ya Zanzibar katika sherehe zilizofanyika katika uwanja wa Amani, Zanzibar.
PINDU 16
Kikosi cha Kwata la KimyaKimya wakionesha onesho wakati wa sherehe za miaka 53 ya mapinduzi ya Zanzibar zilizofanyika katika uwanja wa Amani, Zanzibar.
PINDU 18
Komando wa Jeshi la Wananchi Tanzania akishuka katika kamba katika sherehe za miaka 53 ya mapinduzi ya Zanzibar zilizofanyika katika uwanja wa Amani, Zanzibar.
PINDU 19
Kikosi cha Makomandoo wa Jeshi la Wananchi Tanzania wakionesha onesho wa namna ya kuakibiana na vikwazo mbalimbali wawapo kazini katika sherehe za miaka 53 ya mapinduzi ya Zanzibar zilizofanyika katika uwanja wa Amani, Zanzibar.
PINDU 20
Askari wa Kikosi cha Mbwa, akionesha namna mbwa anavyoweza kuruka vikwazo mbalimbali katika kukabiliana na wahalifu katika sherehe za miaka 53 ya mapinduzi ya Zanzibar zilizofanyika katika uwanja wa Amani, Zanzibar.
………..

ZANZIBAR imeadhimisha miaka 53 ya Mapinduzi Matukufu huku ikiwa imepiga hatua mbalimbali za kimaendeleo na utoaji wa huduma bora za kijamii.
Hayo yamebainishwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein wakati akihutubia wananchi katika sherehe za maadhimisho ya Mapinduzi leo katika uwanja wa Amani, Unguja, Zanzibar.
Dkt. Sein amesema kuwa siku ya Mapinduzi ni muhimu sana katika historia ya Zanzibar kwani ndiyo siku ambayo Wazanzibar walipokuwa huru katika nchi yao na kuweza kufanya shughuli mbalimbali za kujiletea maaendeleo.
“Tukiwa tunasherehekea miaka 53 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ni vyema tukajivunia maendeleo yaliyopatikana na yanayoendelea kupatikana.”Alisema Dkt. Shein.
Akitaja baadhi ya mafanikio yaliyopatikana tangu Mapinduzi Matukufu yatokee tarehe 12 Januari 1961, Dkt. Shein amesema kuwa mafanikio makubwa yamepatikana katika sekta za elimu kwa kuwa na ongezeko la shule kutoka shule 752 mwaka 2015 hadi kufikia 843 mwaka 2016.
Ongezeko hilo limeenda sambamba na ongezeko la udahili wa wananfunzi ambapo umeongezeka kutoka wanafunzi 384,000 hadi kufikia 424,000 mwaka 2016.
Katika sekta ya afya kumekuwa na mafanikio ya kuongezeka kwa vituo vya afya kwa asilimia 13.4 ambapo mwaka 2015 kulikuwa na Vituo vya Afya 134 hadi kufikia sasa jumla ya Vituo 152 vimepatikana.
Mafanikio mengine ni pamoja na upatikanaji wa ajira 2658 zilizotokana na miradi mbalimbali iliyozindulia katika kipindi hiki cha maadhimisho ya siku ya Mapinduzi, kukua kwa Sekta ya Utalii kwa ongezeko la watalii kwa asilimia 13 huku ikichangia pato la taifa kwa asilimia 27.
Huduma za kijamii zimezidi kuboreshwa huku upatikanaji wa maji safi na salama umeendelea kutatuliwa ambapo miradi ya maji imeekuwa ikitekelezwa ikiwemo kuchimba visima vipya 9 na kuvifanyia ukarabati visima vya zamani.
Kwa upande wake Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd amesema kuwa Mapinduzi haya yamekuwa chachu ya kuleta maendeleo kwa kuwa yamewaweka Wazanzibar kuwa huru katika kutekeleza shughuli zao za kujiletea maendeleo.
Zanzibar imeadhimisha miaka 53 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar huku ikiwa imepiga hatua kubwa za kimaendeleo ambapo katika shamra shamra za maadhimisho haya jumla ya miradi 32 ya maendeleo imezinduliwa huku mingine 16 ikiwekwa jiwe la msingi tayari kwa utekelezaji wake, hayo yote ni matunda yatokanayo na Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ambayo baadaye yalizaa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.


 Makomandoo wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania  wakionyesha uwezo wao wa kupigana bila silaha katika Maadhimisho ya miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar kwenye wawnja wa Aman Januari 12, 2017. (Picha na ofisi ya Waziri Mkuu)
  Makomandoo wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania  wakionyesha  jinsi matofari yanavyoweza kuvunjwa juu ya kichwa katika maadhimisho ya miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar kwenye uwanja wa Aman, Januari 12, 2017. (Picha na ofisi ya Waziri Mkuu)
 Komandoo wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania akiwa  amelala  juu ya misumari  huku wenzake wakipita juu yake ikiwa ni moja ya maonyesho ya ukakamavu yaliyoonyeshwa na Makomandoo hao katika maadhimisho ya  miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar kwenye uwanja wa Aman Januari 12. 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
  Rais wa  Zanzibar Dkt. Ali Mohammed Shein  akihutubia katika kilele cha Maadhimisho ya miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar kwenye uwanja wa Aman   Januari 12, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

 Rais Mstaafu wa Zanzibar, Aman Karume akiteta na  Rais Mstaafu wa Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete katika maadhimisho ya miaka  53 ya Mapinduzi  ya Zanzibar  zilizofanyika kwenye uwanja wa Aman Zanzibar Januari 12, 2017.  
  Baadhi ya waandamanaji wakishangilia  wakati walipopita mbele ya Rais wa Zanzibar, Dkt. Ali Mohammed  Shein katika maadhimisho ya  miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar kwenye uwanja wa Aman, Zanzibar Januari 12, 2017.
 Mmoja wa wananchi wa Zanzibar akimsikiliza kwa makaini Rais wake, Dkt. Ali Mohammed Shein  wakati alipohutuba katika Maadhimisho ya  miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar  kwenye uwanja wa Aman Januari 17, 2017.
 Rais wa Zanzibar, Dkt. Ali Mohammed Shein, Makamu wa Rais, Samia Suluhu, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Sif Idd wakifuatilia kwa makini gwaride  la Maaddhisho ya miaka 53  ya Mapinduzi ya Zanzibar kwenye uwanja wa Aman, Januari 12, 2017
 Askari wa Kikosi cha Zimamoto na Uokozi cha Zanzibar akipita   kwa ukakamavu mbele ya  mgeni rasmi Rais wa Zanzibar, Dkt. Ali Mohammed Shein  katika gwaride la kuadhimisha miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar Januari 12, 2017.


Barcelona defeated Athletic Bilbao 3-1 on Wednesday.BAO za Suarez, Neymar na Messi zimewapeleka Mabingwa Watetezi FC Barcelona Robo Fainali ya Copa del Rey, Kombe la Mfalme wa Spain, walipoifunga Athletic Bilbao 3-1 huko Nou Camp hapo Jana.

Wakiwa wamefungwa 2-1 katika Mechi ya Kwanza, Barca walitangulia kufunga Dakika ya 36 kwa Bao la Luis Suarez likiwa Bao lake la 100 katika Mechi 120 za Barca.

Neymar aliongeza Bao la Pili Dakika ya 47 na Bilbao kupiga Bao lao moja Dakika ya 51 kupitia Saborit na kufanya Gemu iwe Sare 3-3 kwa Mechi 2 lakini Messi akapiga Bao la 3 Dakika ya 70 na kuwapa Barca ushindi wa 3-1 na 4-3 kwa Mechi Mbili.


Southampton imeifunga Liverpool 1-0 huko Saint Mary hapo Jana katika Mechi yao ya Kwanza ya Nusu Fainali ya EFL CUP, ambalo ndio Kombe la Ligi huko England.
Juzi, kwenye Mechi nyingine ya Kwanza ya Nusu Fainali nyingine iliyochezwa Old Trafford, Manchester United iliichapa Hull City Bao 2-0 kwa Bao za Juan Mata na Marouane Fellaini.
Bao la ushindi la Southampton, ambao ni maarufu kama ‘Watakatifu’, hapo Jana lilifungwa na Nathan Redmond baada kupokea Pasi ya Jay Rodriguez katika Dakika ya 20. Van Dijk blocks a shot from Roberto FirminoSouthampton wamgeweza kupata Bao nyingi kama si ushujaa wa Kipa wa Liverpool Loris Karius alieokoa Mipira mingi na hasa mara 2 kufuta kwenye chaki ya Goli Mipira ya Nathan Redmond.
Daniel Sturridge battles for the ball with Vigril van DijkNusu Fainali hizi huchezwa kwa Mikondo Miwili ya Nyumbani na Ugenini na hivyo Marudiano ya Mechi hizi yatakuwa hapo Januari 25 na 26 huko Anfield na KCOM Stadium. Lucas and Jay Rodriguez battle for the ball in the first halfEFL CUP
Nusu Fainali
MARUDIANO
Jumatano Januari 25

23:00 Liverpool v Southampton [0-1]
Alhamisi Januari 26
22:45 Hull City v Manchester United [0-2]

waliotembelea blog