Saturday, July 11, 2015


Mfahamu Bernard Kamilius Membe, mmoja wa wagombea watano. Ni mbunge wa jimbo la Mtama (2000 - 2015), na waziri wa mambo ya nje Tanzania (2007-2015). Mhe. Membe amesomea Sayansi ya Siasa katika Chuo Kikuu Cha Dar-es-salaam na Mahusiano ya Kimataifa katika chuo cha Johns Hopkins, na amepitia mafunzo ya kijeshi (nationa service) kwa mwaka mmoja katika kambi la kijeshi la Oljoro (Arusha) #KaribuDodoma UMOJA NI USHINDI!Mfahamu John Pombe Magufuli, mmoja wa wagombea watano. Ni mbunge wa jimbo la Biharamulo Mashariki Tanzania, na ni waziri wa ujenzi (2010-2015). Amesomea shahada ya uzamivu ya Kemia katika chuo kikuu cha Dar-es-salaam. #KaribuDodoma UMOJA NI USHINDI!

Mfahamu Asha-Rose Migiro, mmoja wa wagombea watano. Ni Mbunge wa kuteuliwa katika bunge, na waziri wa sheria na katiba Tanzania. Mhe. Migiro amesomea sheria katika Chuo Kikuu Cha Dar-es-salaam na shahada ya uzamivu yake katika chuo cha Konstanz (Ujerumani). Kabla ya kujiunga na siasa, alikua mhadhiri mkuu wa mafunzo ya sheria Chuo Kikuu Cha Dar-es-salaam. Pia aliwahi kuwa naibu katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa (2007-2012) #KaribuDodoma UMOJA NI USHINDI!

Mfahamu Amina Salum Ali, mmoja wa wagombea watano. Aliwahi kuwa waziri wa Fedha (Zanzibar; 1990-2000), na ni balozi wa Umoja wa Mataifa ya Afrika nchini Marekani (2007-2015). Amesomea uchumi katika chuo cha Delhi na pia ana MBA ya Masoko kutoka chuo cha Pune. #KaribuDodoma UMOJA NI USHINDI!
Mfahamu January Makamba, mmoja wa wagombea watano. Ni Mbunge wa Bumbuli (2010-2015), na naibu waziri wa mawasiliano, sayansi, na teknolojia Tanzania (2012-2015). Amesomea shahada ya uzamivu katika diplomasia na usuluhishi wa migogoro katika chuo cha George Mason, kabla ya kuwa msaidizi wa Rais Jakaya Kikwete. #KaribuDodoma UMOJA NI USHINDI!


valdes-ronaldinho-and-etoo-1436557439755
.
Wachezaji wa zamani wa Fc Barcelona ya Hispania Ronaldinho Gaucho na Victor Valdes uwenda wakaungana na mchezaji mwenzao wa zamani wa klabu hiyo Samuel Eto’o nchini Uturuki.
Story inayovutia wapenzi wa soka duniani kuhusu hawa ma star sio kucheza tena pamoja ila ni timu wanayo kwenda kuichezea Antalyaspor ya nchini Uturuki ambayo ndio imepanda daraja msimu huu. Ni nadra sana kukuta ma star wanao maliza muda wao katika soka kwenda kucheza timu inayopanda daraja na ipo katika ligi ya kawaida.
Uwenda ingekuwa kawaida kukuta ma star hawa wanacheza timu iliyopanda daraja katika ligi zinazotajwa kuwa bora zaidi duniani kama Hispania,Uingereza, Ufaransa na hata Ujerumani.
ETOO
.
Eto’o tayari amesha saini mkataba wa miaka mitatu klabuni hapo na Ronaldinho bado ana jadili ofa hiyo licha ya kuthibitisha kupitia mitandao ya kijamii kuwa anaenda Uturuki. Lakini sasa Antalyaspor bado wanamtaka Valdes licha ya kuwa anatazamiwa na Manchester United kama mbadala wa David Degea ambae ana husishwa na kuhamia Real Madrid.
Eto’o, Valdes na Ronaldinho wamewahi kucheza Fc Barcelona katika misimu ya 2003-2004 na 2007-2008 chini ya kocha Frank Rijkard na kuisaidia klabu kutwa taji la pili la klabu bingwa barani ulaya.
Klabu ya Manchester United imekubaliana kimsingi na mabingwa wa Bayern Munich juu ya usajili wa kiungo wa timu ya taifa ya Ujerumani Bastian Schweinsteiger.
  Bastian, mwenye umri wa miaka 30, aliomba mwenyewe klabu ya Bayern Munich kutompa mkataba mpya na angependa kwenda sehemu nyingine.
Mkurugenzi mkuu wa Bayern Karl-Heinz Rummenigge ameongea na waandishi wa habari muda mfupi uliopita na kusema: “Marafiki zangu wa pale Manchester United tumekuwa na mawasiliano kwa muda kidogo. Tumefikia makubaliano juu ya uhamisho wa Bastian.
Schweinsteiger ameshaichezea Bayern Munich mechi 536 tangu alipovaa jezi ya timu hiyo kwa mara ya kwanza mwaka 2002.
 
Inamaanika kwamba Bastian amevutiwa kujiunga na Manchester United kutokana na kuwa na mahusiano mazuri na kocha Louis van Gaal ambaye alimfundisha soka wakati alipokuwa kocha wa Bayern Munich.
Ada ya uhamisho iliyolipwa kumsajili Schwesteiger inaaminika kuwa karibia kiasi cha £8m na mshahara wake utakuwa kiasi cha £7m kwa mwaka.



.
.
Baada ya chama cha Mapinduzi kupitisha majina matano kwenye tano bora ya Wagombea CCM nafasi ya Urais 2015 kupitia chama hicho.
Sasa kiongozi wa Chama Cha ACT Wazalendo, Mh Zitto Kabwe leo amefunguka kuhusu chama chake kumteua mgombea au kuunga mkono mgombea cha chama kingine.
Kupitia kwenye ukurasa wake wa twitter amewahabarisha wananchi kwa kusema…’Chama chetu kitateua mgombea au kuunga mkono mgombea wa chama kingine kwa maamuzi ya VIKAO vya chama. Kama Kiongozi wa chama sina mamlaka yeyote yale kutangaza mtu kuwa mgombea wetu’ – @zittokabwe
.
.
Hivi sasa Uongozi mzima wa Chama upo kwenye retreat ili kujipanga na uchaguzi. Hatuna mazungumzo wala makubaliano na mtu yeyote kutoka chama kingine kuhusu nafasi ya Urais. Mgombea wetu atapatikana kwa kupitia vikao vya chama chetu…’  -@zittokabwe
 

Ads Separator
.
.
Baada ya jina la katibu Mkuu wa Chadema Dk Wibroad Slaa likiwa limeteuliwa na UKAWA kuwa mgombea wake wa nafasi ya Urais katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba.
Dakika chache zilizopita kwenye ukurasa  wa @twitter wa Dr Slaa kathibitisha kuteuliwa na UKAWA.
.
.
Nashukuru UKAWA kwa imani kubwa. Kazi ya mabadiliko iliyoanza 1992 kwa vyama vingi imebakiza miezi michache kushinda. Kura yako ni ukombozi –  @willibrordslaa
Nashukuru UKAWA kwa imani kubwa. Kazi ya mabadiliko iliyoanza 1992 kwa vyama vingi imebakiza miezi michache kushinda. Kura yako ni ukombozi.

Pichaz zilianza kusambaa mitandaoni, baadae ikaja stori kuhusu Wagombea walioteuliwa kwenye Urais kupitia CCM.
Muda unavyozidi kwenda ukweli wa hii stori unachukua nafasi zaidi, kwenye ukurasa wa @Twitter wa Rais JK kathibitisha majina haya matano kupitishwa na Kamati Kuu ya CCM Dodoma.
“Kamati Kuu imefanya kazi ya kwanza. Majina matano ya awali ni: Bernard Membe John Magufuli Asha Rose Migiro Januari Makamba Amina S. Ali“– @


CCM II
Unahitaji chochote nachokipata kikufikie? jiunge na mimi kwenye Twitter, Facebook na Instagram www.denbazita.com

waliotembelea blog